Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Zito ni mnafiki sana na anataka kukiharibu chama..kwanza nchi imeyumba sana maisha ni magumu sana mafisadi wanaitafuna nchi ,,huyu kibaraka zitto yeye anakuja na stori ili watu waache kujadili mambo ya maana .nchi imeharibika sana jk keshaishindwa na 100% zitto sio mkombozi wetu huyu katumwa ama anataka kuiharibu nchi.zitto ana uroho wa madaraka na hatutaki watu kama hawa an huyu kijana inabidi avuliwe madaraka kwenye chama.ni mnafiki hana lolote ..watu wanataabika sana nchi inatafunwa yeyemiudenda inamtoka eti anautaka urais.
huyu ni mtu hatari sana kuweni makini na nina uhakika 100% huyu akiingia madarakani lazima aibadili katika ili akae hadi azeeke madarakani.
sio hivyo tu chadema mkimpitisha zito mjue chama ndio kimekufa hivyo kwani huyu jamaa ametumwa na mafisadi.
mimi binafsi SITAMPA KURA YANGU
kwa sababu kule twitter aliuliza swali na kijana mmoja yeye akajibu kuwa eti kura moja hana haja nayo..kumbe hajui kuwa sio kura moja tu ya yule kijana ni kura za wengi kwa sababu wengi tulikuwa tunasubiri ajibu lile swali,,sasa mntaka kuniambia ni rais gani huyu mwenye nyodo?
huyu hafai na huu ulikuwa sio muda wa kuja kujitangaza uroho wake wa madaraka hapa hata kama katiba inaruhusu.

kipanya_20111207_2001492155.jpg
 
Zitto umeiona hii!!?
Jipange upya!! Sio kwamba hufai kuwa raisi NO, bali hujakomaa kiasi cha kuwa Raisi. Zitto acha kulewa misifa utapotea!!
Uraisi unatakiwa uonwe sio ujione kuwa unafaa kuwa Rais!!
Jengeni chama huku Bukoba vijijini hamjaonekana!!
 
Wanajf ebu tupevuke, tutakosa thamani ya kuwa great thinkers, hakuna anayemwonea wivu zito, so what ila huu ndo ukweli, zito analewa sifa, kiongozi wa watu hajioni anafaa ila huonekana anafaa na kuambiwa afanye nini. Zito you have lost my brother naomba ufuate ushauri wa huyu mwandishi na wanajf tuache ulimbukeni tuseme ukweli na si kushambuliana kwa matusi ila tujadili hoja, tukiwa hivi jf haitakuwa tofauti na Facebook.
 
Mimi siyo mwana usalama kama wewe nitapata wapi nafasi ya kuongea na rais?

Mkuu kweli wewe upo kwenye ligi ya kubisha na kutetea,swali kwako-je jk tangu awe raisi ameongea na wana usalama tu??!! (kip in mind that he has been a good friend of Zito na pia alishamshauri agombee uraisi),na je Zito naye pia ni miongoni mwa wanausalama??
Hivi leo hii kwa wafuatiliaji wa siasa wakisema kwamba Zitoanaihujumu CDM kwani kwa kuwa amekuwa anakuja na mada za kujipambanua yeye anasitahili zaidi na ni bora zaidi katika timing ambayo sio muafaka itakuwa watu wamekosea ??
 
Zitto umeiona hii!!?
Jipange upya!! Sio kwamba hufai kuwa raisi NO, bali hujakomaa kiasi cha kuwa Raisi. Zitto acha kulewa misifa utapotea!!
Uraisi unatakiwa uonwe sio ujione kuwa unafaa kuwa Rais!!
Jengeni chama huku Bukoba vijijini hamjaonekana!!

Hivi yule kiongozi wa Korea Kaskazini ana umri gani vile...??
 
Hivi yule kiongozi wa Korea Kaskazini ana umri gani vile...??
Achana na hao wakorea mkuu! Hao hawana demokrasia, Zitto angejenga chama kwanza, kiingie kwenye utawala, apate uwaziri harafu hatua kwa hatua atajikuta keshawin kila kona!! Sasa ni mapema mno! sawa, anayo haki ya kufanya hivyo kwakuwa katiba tutaichakachua muda si mrefu!!.
 
Kweli Zitto kiboko. Anawanyima watu usingizi. Zitto ana haki ya kutoa maoni yake kama wengine.
 
Chee-le
Haya uliyopaste Hapo yameibwA HAPA JF, TAZAMA POST ZA MAJI YA MTUNGI na wengine
 
Wana jf hii nimeinasa kwenye blog iitwayo yerickonyerere.wordpress.com

Nimeshangaa kuona kumbe wengi wanamuogopa zito kiasi cha kusema sana.

25 Mar 2012


Zitto bado hajafikia kuwa kiongozi wa juu zaidi kitaifa ndani ya chama chake achilia mbali kuwa rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Urais unahitaji hekima, Zitto hana kwa sasa, Urais unahitaji busara, Zitto hana kwa sasa, Urais ujasiri wa kweli Zitto hana kwa sasa,Urais unahitaji mtu wa kutafakuri, Zitto hana kwa sasa, Urais hauhitaji mtu mnafiki, Zitto kwa sasa ni mnafiki, Kwa ujumla Urais unahitaji mtu aliyepevuka, na Zitto bado hajapevuka

Mwono wako unaonyesha wazi ni chuki au wivu........sijui umempima huyu Zito kwa kutumia vipimo gani?.....kama kuungombania urais basi ni haki yake ya Kikatiba.......mbona Nyerere alipochukua nchi alikuwa na umri mdogo na alikuwa hajakomaa kisiasa na aliwza kuongoza nchi hii kwa muda mrefu tu.
 
Zitto
Nimeisoma tena hii thread na kupitia Comments karibu zote na nimepata ujumbe mkubwa kwamba wengi wa wanachama wa CDM hawana imani na wewe Zitto.Ni ukweli mchungu lakini ni lazima nisema.Nimegundua wasichokipenda wanachama wa CDM ni majivuno ya Zitto na kujiona yeye pekee ndiye anayefaa na wengine wote hawana maana.Wapo baadhi hawajafurahishwa na pale uliposema Mnyika alikuwa haipendi CDM na wewe ndiye ulimlazimisha kujiunga.Kwa kusema hivyo wenzako wametafsiri una bifu la chinichini na Mnyika.Zitto nakushauri ukitaka kudumu katika siasa acha papara.Haraka haraka haina baraka na Subira yavuta heri.Nakumbuka baada ya uchaguzi mkuu ulikimbilia kwenye vyombo vya habari na kutangaza kwamba wewe ndiye unafaa kuwa kiongozi wa upinzani bungeni.Ulisababisha vurumai kubwa ambalo lilikuwa la kipuuzi kabisa.Mbowe alipoulizwa alijibu kwa busara kubwa kwamba vikao ndio vitaamua.Baada ya vikao Mbowe ndiye akaonekana kuwa na hekima ya kupewa nafasi ile.Sasa kwa mfano huu ukiwa kama mdogo wangu nakushauri tuliza akili na chapa kazi.Urais unakuja tu wenyewe.Urais haupatikani kwa kukashifu wengine na kujiona wewe ni bora zaidi hapana.Wala urais hauji kwa kutuma watu kwenye mitandao ya kijamii kukashifu viongozi wako wanaoheshimika.Niendelee kukushauri kwamba kwa papara unazozionyesha ukipewa uenyekiti wa chama basi CDM kitasambaratika ndani ya muda mfupi sana kwa sababu ya kudharau wengine na kujiona bora sana.Zitto usiwe kama Mrema aliyejiona yeye ni kila kitu akaisambaratisha NCCR.Mwisho kabisa fahamu kitu kimoja kwamba bado sana wewe kujilinganisha na Slaa au Mbowe.Unahitaji si chini ya miaka kumi kujijenga kufikia upeo ujasiri na uaminifu wa Dr Slaa.

Mkuu wangu salute!
Na ndicho nimekuwa nikipigia kelele hapa kwamba kukimbilia Ikulu ni sifa moja ya kuwa disqualified! Nilibahatika kushuhudia mapokezi ya Dr Slaa alipowasili Arumeru.Hakika magazeti hayakukosea kusema alilakiwa kama mfalme.Yalikuwa ni mapokezi makubwa kuwahi kushuhudiwa jimboni Arumeru tangu Uhuru kama wazee wa kule wanavyosema.Njia yote Slaa alitwaa Rais.....Rais....Sasa nikajiuliza ni lini Slaa amejitangaza Rais au ni lini Slaa ameropoka nataka kugombea urais 2015? Kwa hiyo nawaambia wale waroho wa madaraka kwamba Urais unakuja wenyewe na wala hauji kwa mbinu chafu na ovu za kuwachafua watu wengine.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom