Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Lakini kusema kwa Kabwe kuhusu hamu yake ya kuwa rais ina ubaya gani? Kila mtu anayo ndoto yake, wengine hukaa kimya na ndoto zao na wengine huropoka hadharani. Hata aliyeko madarakani alikuwa na ndoto ya urais, ndio maana baba wa taifa alimnyamazisha baada ya kuona anasemasema kuutaka urais wakati huo baba wa taifa alishaona muda bado na kumbe ni kweli, si mnaona anachofanya sasa? Ni rafiki yake sana Kabwe, kwa hiyo akiukwaaa urais sitaona tofauti na aliyepo sasa, watabaki kulindana na kuhamasishana utundu wa kuchanga karata za kuiona siku inapita hata kama kwa mazingaombwe.

Kama alivyotumia haki yake kuongea Kabwe, huyo Yeriko naye katumia haki yake kutoa uchambuzi juu ya mambo yaliyoanikwa na Kabwe ili yachambuliwe kwa faida ya walaji ambao ni umma. Wabaya sio wanaoomba bali wabaya ni wale wawapao waombaji ambao wanaonekana wazi kwamba hawahitajiki kupewa sasa. Urais sio kuwa msomi ingawa inasaidia, lakini wapo wasomi wengi wanavurunda kila kukicha. Tusipendelee kusikia yale tunayoyataka tu, siasa ni pamoja na kuvumiliana kwa kusikia yanayotuumiza. Cha msingi ni kujenga hoja na kuhakikisha hoja yako yenye mshiko inapita.
 
Mimi sina tatizo na uhuru wa mawazo. Sina tatizo kabisa na kauli ya zito. Ni haki yake kikatiba na nina heshimu mawazo yake. TATIZO KUBWA NILILOKUWA NAO NI MUDA ZITTO ANAOTUMIA KUTOA MAWAZO YAKE. Chunguza utaliona hili. Zitto anapenda kutoa kauli zake kipindi ambacho chama chake kipo kwenye harakati fulani. ALIWAHI PIA KUTOA KAULI YA URAISI KWENYE JIMBO LAKE WAKATI BADO UCHAGUZI WA RAISI UNAENDELEA 2010. kwa hili watu wote wenye kupenda kuchambua na kuangalia vitu kwa undani si walaumi kwa KUMUITA HUYU JAMAA MNAFIKI. Angalia hata kampeni za uraisi 2010 alishiri kwa kiasi gani?


ndio maana nikasema anapayuka alfajiri sana.....achilia mbali kauli aliyotoa kipindi cha uchaguzi 2010..kuna ile nyinge alitoa wakati wa msiba wa regia....na hii ya sasa.....anautaka uraisi huku akiwanga wengine ..eti mnyika alikuwa haipendi chadema kabisa na hata kujiunga nayo alikuwa hataki......haya si maneno mazuri ya kusema......mrafi tu
 
cdm wanatakiwa walishike kwanza bunge wawe nusu au zaidi wataweza kurun system kiasi
 
ndio maana nikasema anapayuka alfajiri sana.....achilia mbali kauli aliyotoa kipindi cha uchaguzi 2010..kuna ile nyinge alitoa wakati wa msiba wa regia....na hii ya sasa.....anautaka uraisi huku akiwanga wengine ..eti mnyika alikuwa haipendi chadema kabisa na hata kujiunga nayo alikuwa hataki......haya si maneno mazuri ya kusema......mrafi tu

Nimewahi kusikia kwamba Zitto anadhani Mnyika anaandaliwa kuchukua nafasi kubwa ndani ya chama kwenye uchaguzi wa ndani.Sasa huenda hili ni shambulio dhidi ya Mnyika kuonyesha watu kwamba huyu Mnyika anayepigiwa chapuo ni adui wa chama.Anapenyeza sumu mbaya kwa wanachama dhidi ya Mnyika.
 
Zito unataka urais utetelekeze kama unavyofanya kwa mwanao Baraka pale Kigogo. Tunza mwanao kulingana na status yako na aspirations zako. Mtoto umemtupa shule ya Msingi kigogo hana hata viatu, leo unatulete habari za kuwa Rais? Jiangalie kwanza na linda kwanza cha kwako ndio tuamini hata sisi pia utatulinda ukiwa Rais.
 
Hallo Mods,
Hoja kama hizi zinafaa kuwekwa kwenye sticky..ifanyiwe marekebisho kidogo and then iwekwe pale watu waisome.Mawazo haya ndiyo niliyokuwa nafikiria.Zitto ni mwanasiasa kijana asiyetaka ushauri.Kauli zake zimekuwa ni tatizo si kwa chama tu bali hata kwa taifa..nadhani mnakumbuka hoja ya mitambo ya DOWANS..nadhani ni wakati muafaka sasa kwa Zitto kuchukua maoni hapa JF na kuyafanyia kazi.Atambue kuwa tangu ameanza kuwa katika medani za siasa za Tanzania umaarufu wake na kuaminika kwake hasa kwa vijana wapenda mabadiliko umeshuka sana na unazidi kushuka kila iitwapo leo.Mfano mzuri ni hapa JF...wengi wamepoteza imani na Zitto.Na kama kaka Zitto akitaka kujifanya kama hajali vile hakika anguko lake kwa level ya taifa laja muda si mrefu,asije akashangaa siku moja akipita mitaani anazomewa.Zitto huyu si yule wakati nasoma pale MZUMBE UNIVERSITY MIAKA YA 2005-2008 tulimualika lakini VC akasema anamfahamu Zitto akifika pale mawazo yetu yatabadilika,walikuwa wanamfahamu vyema,sio Zitto wa BUZWAGI huyu...Sio Zitto aliyekuwa akisimama kuchangia bungeni watu wanaacha kazi zao na kusogea kwenye TV kumisikiliza.HAKIKA ZITTO AMEPOTEZA MVUTO
 
LaBDA ningependa niulize swali ambalo linaweza kuwa la kibaguzi lakini si nia yangu kuleta ubaguzi bali kuna kitu huenda nikajulishwa inawezekana sifahamu!!......
Hivi ni kwa nini Aman Walid Kaborou, David Kafulila na Zitto Kabwe hawa wote ni kutoka kigoma? Hapa naona naladhimika kuamini kuna tatizo hapa, maana sitaki kwenda mbali nitalazimika kuhoji mpaka kabila zao na asili za koo zao zilitoka nchi gani maana Watanzania tunafahamiana tabia zetu ni watu wa kiasi.
 
Mimi sina tatizo na uhuru wa mawazo. Sina tatizo kabisa na kauli ya zito. Ni haki yake kikatiba na nina heshimu mawazo yake. TATIZO KUBWA NILILOKUWA NAO NI MUDA ZITTO ANAOTUMIA KUTOA MAWAZO YAKE. Chunguza utaliona hili. Zitto anapenda kutoa kauli zake kipindi ambacho chama chake kipo kwenye harakati fulani. ALIWAHI PIA KUTOA KAULI YA URAISI KWENYE JIMBO LAKE WAKATI BADO UCHAGUZI WA RAISI UNAENDELEA 2010. kwa hili watu wote wenye kupenda kuchambua na kuangalia vitu kwa undani si walaumi kwa KUMUITA HUYU JAMAA MNAFIKI. Angalia hata kampeni za uraisi 2010 alishiri kwa kiasi gani?

Ukiwaeleza ukweli wanakuona unachuki na Zitto
 
idadi ya kina nyerere inazd kushamiri tu.
Nafikili 2015 tutakuwa na akina mushumbushi nyerere.
 
huwezi kuamka asubuhi kabla hata hujapiga mswaki unaanza kupayuka..''mimi ni mpole''mimi ni mtu mwema sana, ninafaa.. nimekijenga chama toka nina miaka 16..mimi ndio nimekifikisha hapo kilipo ...ni mimi na mbowe tu ndio tuliokuwa tunakesha...nafaa jamani...wanaokuona ndio wanaweza kusema hivyo kama wewe ni mpole au mkali, jasiri au muoga......kama zitto anafaa hakuna haja ya kusimama kwenye kingo za barabara juu ya kilima alfajiri yote hii na kuanza kupayuka kuwa yeye ni mtu mwema na anafaa kuwa rais wa nchi......

hizi ni dalili za urafi ulipindukia...zitto hufai kuwa rais...take it or leave it

Mkuu wangu.Kwa andiko lake viongozi wote wa chama na wapiganaji wote waliopigania chama hiki hawana maana yoyote kwake na hawana msaada wowote kwa chama.Eti kwa sababu ni yeye tu na Mbowe waliojenga chama.Shame!!! Mbona simsikii Mbowe akijigamba?? Maandiko matakatifu yanasema ajikwezae lazima atashushwa.Wanachadema waliopigana kufa na kupona kupigania chama hiki wanahitaji matusi gani zaidi ya haya???? Eti kina Ndesamburo,Mtei,Makani,Marehemu Ngwilulupi na Slaa hawana mchango wowote ndani ya chama.Ni yeye tu na Mbowe waliojenga chama.Kauli hii inaweza kutolewa tu na mlevi wa kupindukia.
 
Lakini kusema kwa Kabwe kuhusu hamu yake ya kuwa rais ina ubaya gani? Kila mtu anayo ndoto yake, wengine hukaa kimya na ndoto zao na wengine huropoka hadharani. Hata aliyeko madarakani alikuwa na ndoto ya urais, ndio maana baba wa taifa alimnyamazisha baada ya kuona anasemasema kuutaka urais wakati huo baba wa taifa alishaona muda bado na kumbe ni kweli, si mnaona anachofanya sasa? Ni rafiki yake sana Kabwe, kwa hiyo akiukwaaa urais sitaona tofauti na aliyepo sasa, watabaki kulindana na kuhamasishana utundu wa kuchanga karata za kuiona siku inapita hata kama kwa mazingaombwe.

Kama alivyotumia haki yake kuongea Kabwe, huyo Yeriko naye katumia haki yake kutoa uchambuzi juu ya mambo yaliyoanikwa na Kabwe ili yachambuliwe kwa faida ya walaji ambao ni umma. Wabaya sio wanaoomba bali wabaya ni wale wawapao waombaji ambao wanaonekana wazi kwamba hawahitajiki kupewa sasa. Urais sio kuwa msomi ingawa inasaidia, lakini wapo wasomi wengi wanavurunda kila kukicha. Tusipendelee kusikia yale tunayoyataka tu, siasa ni pamoja na kuvumiliana kwa kusikia yanayotuumiza. Cha msingi ni kujenga hoja na kuhakikisha hoja yako yenye mshiko inapita.


ile kusema hivi ''NDIO NAUTAKA URAIS'' ni ishara ya urafi wa madaraka.....
 
Huyu yericko naye ni mmoja wa wanafamilia ya nyerere?
 
- Ninaamini ni haki ya Zitto kikatiba kugombea anything, msiomataka Zitto mnapwaya sana kwenye hoja wengi wenu mnajikita kwenye kujali chama kuliko Taifa, that is very sad kama hatuwezi kutenganisha Taifa na Vyama vya siasa, then hili taifa tutakwama daima. Simfahamu vizuri Zitto ila siamini kwamba hawezi kuaminika na Taifa, miswaada yake yote bungeni ni masilahi ya Taifa tu na hasa wananchi, I mean wananchi wa jimbo lake wanaiamini naye sana which is the most important ishu of all.

- Zitto, kuwa rafiki na Viongozi wa CCM siamini kwamba ni ishu ya kumfanya asiwe Rais mzuri, unless kuna something else hakisemwi hapa, kwamba ana tamaa ya madaraka labda mtuambie kiongozi gani Duniani asiye na tamaa ya madaraka zaidi ya aliyonayo, mtajeni mmoja tu!

- Kwamba ni Raifiki wa Rostam, unless kama hutumiii cell phone za bongo, wewe sio rafiki wa Rostam, ila kama unatumia any of them basi wewe automatically unashirikana na Rostam vile vile, ni hoja haina mshiko kwamba anaigawa CDM then huko CDM mtakuwa wanafiki wa Dunia, jinsi mnavyoweza kuweka smilling face to the public huku mnamchukia kama mnavyojisema hapa kwenye hii thread.

- Ninasema hivi, simjui sana Zitto on a personal level, lakini wale mnao-claim kumjua so far mnashindwa kuweka hoja nzito za kutushawishi tusimjua kwa karibu kwamba hafai kuwa Rais, mnajaribu sana kuonyesha hana royalty kwa chama, hapo ndipo mnajiharibia sana maana mnathibitisha kwamba CDM kuna unafiki Zitto is good kupiga kampeni za chama chenu Arumeru, lakini hafai kugombea urais kwa chama chenu, shame on all of you mnaomchukia bila sababu za msingi!

-Again, mimi simjui sana Zitto kwa karibu, ila nawaomba wale wote mnao-claim kumjua na kwamba hafai kuwa Rais kwa tiketi ya CDM, tupeni hoja nzito za kumchukia kwenu maana so far mnapwaya sana kwenye hoja za ku-back up chuki zenu, tunaojali Taifa kwanza tunafurihishwa na uamuzi wa Zitto kwa sababu unafungua njia kwa Vijana wote wanaotaka kugombea nafasi kubwa za taifa, otherwise tusiwe part of the problem kwa kulilia mambo ya zamani tu!

Es!
 
Mmmmmh, labda.

Ngoja nikaperuzi alichofanya pale DARUSO!
 
Guys

the whole political circus in our country is dirty, hasnt been clean since the circus was built by JKN and his allies.... it will remain that way, and the Zitto just shared his dream, anyone is allowed to dream and share his dream

Nonetheless, we dont need to share any dream if e think the timing is wrong... and for that case i think Zitto is just a continuation of dirty games within the circus!!!

where was his focus on during this political melee in CDM and Arumeru mashariki?? kuota urais.... huh
 
Hatimaye sasa nimejiridhisha pasipo na shaka ni kwa nini zitto Kabwe ni swahiba mkubwa wa Deputy Director wa Usalama wa Taifa ndugu Jacky Nzoka, Zitto aje hapa kuuelezea umma wa JF ni sababu zipi za msingi zilizokuwa zinamfanya awe na mawasiliano ya mara kwa mara wakati chama chake kiko katika uchaguzi mkuu na Idara ya usalama wa Taifa ndiyo ilikuwa inaihujumu CHADEMA? hapa sitalajii jibu rahisi kwa swali gumu.

Pili Ben Saanane nimekuwa nikifuatilia mabandiko yako kwa makini sana na kuna kipindi nilidhani huwa unaonewa, kumbe nilikuwa najidanganya, humu jamvini umejipambanuwa kwamba wewe ndio unayejuwa siasa na yeyote ambaye atakuwa kinyume na mtazamo wako basi wewe utambatiza kila aina ya jina mara mnafki mara hivi mara vile, kumbe sasa nimejiridhisha ni kweli chama chako kiliposema huna maadili hakuna walipokuwa wamekosea, kwa nini unatetea Alliance ndani ya chama? narudia kukwambia tena jifunze kwa John Mnyika, yule kijana anaaminika machoni pa watu kwa sababu he is humbled,......jiulize ni kwa nini kijana mmoja Mnyika alundikiwe vyeo na nyinyi wasomi mpo? endelea na Alliance. zako.

Huyo jamaa ni mbishi aliyepitiliza. Ma-radicals kama huyu hawatakiwi kupewa mamlaka makubwa sana.unaongelea maadili?huyu kama alijibizana na balozi kwenye kikao kama vile anajibizana na kimada wake mbele ya jumuiya ya watanzania atashindwa kufanya nini?kama aliweza kupotosha mdahalo chuoni na kugawa darasa profesa akagomea darasa hadi likafikia kwenye seneti ya chuo na ubalozi wa tanzania unategemea nini?kama aliweza kutembea na profesa wake unategemea awe na maadili gani aidi? kama aliweza kusababisha vurugu alipokuwa angombea chuo kikafungwa badala ya kujutia yeye akawa anawahi mahakamani kupinga amri ya chuo kumzuia kugombea unategemea nini?damu ya watu ilimwagika lakini alijifaragua tu kwenye kampeni zake kusimama dakika moja kabla ya kampeni ili kuvuta kura.Hii ndiyo aina ya akina Ghaddafi,kagame au huyu wa syria?

nilishamwambia tanzania haiko tayari kuongozwa na mujahidini au ma-ayattolaah.kama wanataka wahamie Iran kwa maradicals wenzao.waroho wakubwa wa madaraka hawa.Huu mtandao wao sasa ni mkubwa kuliko mnavyofikiria wakuu.Hili ni kundi ambalo litaleta vita kali dhidi ya wazee naona hadi vijana wa CCM akina Nape,Makamba na akina Bashe wako kundi hili.aliposimama Bashe na kuwaambia wazee ni tatizo haikuwa kwa bahati mbaya.huyu dogo Ben Saanane ana kisirani kibaya sana. ila ninachoona ni kwamba kama Zitto huko baadae atakuwa mwenyekiti wa chama chao au Rais na kwa jinsi ninavyoona anaungwa mkono na hawa vijana itakuja kutokea kama ya Zuma na Malema.

Maskini Freeman Mbowe watetezi wake wanazidiwa nguvu.kiboko ya hawa ni kutafuta wasomi nguli kuliko wao wanaojua kujenga hoja kwa umahiri ili kukabiliana nao.Nimesoma andiko la zitto nimegundua anaweza kujenga hoja na kuhamisha hata mawazo ya watu.hawa ni mabingwa wa propaganda. Saanane,ana uwezo mkubwa ni msomi aliyebobea na anajiamini isipokuwa akitumia taaluma yake vizuri na kujiamini kwake anaweza kukisaidia chama.Hizi raslimali anazoelekeza kwa kundi la Zitto zitaleta athari kwa vijana.Angesaidiana na John Heche kuisuka Bavicha naamini hali ya jumuiya hiyo ingekuwa imebadilika.Huyu dogo huwezi kumshauri hilo sana sana atakujibu kwa kukudhalilisha na watu watamuamini. Bavicha imegawanyika,makamu mwenyekiti girlfriend wa saanane yupo kundi la akina zitto.je kwa staili hii huko mbele si kuna mpasuko mkubwa?wiki mbili tu nilitabiri kama zitto atagombea uenyekiti wa chama au urais tutarajie mpasuko huko chadema kwa kuwa najua vijana alio nao kundi moja mbowe hataweza kuhimili vishindo vyao.hili ndilo linalotokea sasa


hawa wako tayari kuua ili wapate wanachotaka
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom