Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Hamjui kuja na strategy yenye kuleta uzito hadi imekuwa ni kama utoto sasa.
 
Magwanda yanapoanza kubana, inabidi kutafuta mapya.
 
wazinzi huku jf mko wengi.nahisi umekuwa too sensitive kwa hili kwa kuwa una maslahi nayo au ni tabia yako.sio utmie kigezo cha walioshindwa katika ndoa zao kuhalalisha ubazazi na uzinzi wenu.hatutaki kodi zetu zitumike kulipia mahawara.kuna wengine wanastahili kugombea u-big brother kwa kuwa hata kampeni zao kihistora tangu chuo ziliteka wanawake zaidi na kwa jinsi alivyo sidhani kama dada na wake zetu watasalimika.kuna watu wakishinda urais nchi hii tutahamisha wake na mabinti zetu

Mbona bado hamjawahamisha wake na mabinti zenu? Au wako salama? Ulipata habari za Igunga? na Morogoro je? Unafahamu fika kama kipimo cha usafi wa maisha binafsi kingetumika (bila unafiki) sasa hivi serikali yote ingeondoka madarakani. Kuanzia juu mpaka kwa kwa katibu tarafa. It is that bad!

Ndio maana sina interest hata kidogo na hoja kwamba Zitto hajaoa au ili uwe kiongozi (even ubunge) basi ni lazima uoe!
 
Zitto ndani ya chadema anacheza tu, hawezi kuivuruga. Kama ametumwa ataishia kubaya.
 
Tangu Nape amteue MUSIBA kuongoza kikosi cha waichafuao CDM mtandaoni imedhihirisha wazi kuwa Musiba amefeli kazi yake. Pole sana mkulima wa kisasa, kajipanga upya....
 
Kuna ubaya gani kwa Zitto au Mwana CDM yeyote kuwa na mawazo kama hayo hapo chini?:

Hata hivyo kazi hii hata kama naitaka ni lazima wenye nchi waamue kunipa kazi hii.Ni lazima kwanza Chama changu kiseme wewe ndio mwanachama unaestahili kuifanya kazi hii. Ni lazima Watanzania wengi waseme wewe ndio mwananchi mwenzetu unayeweza kuchukua jukumu hili. Kuitaka tu haitoshi. Ni lazima wananchi wakuamini na kukupa jukumu hili.

Sasa kama wananchi watasema huyu Zitto anapaswa kubeba jukumu hili mwaka 2015 tuache iwe. Kama watasema hapana wewe bado mpaka mwaka 2020 au hata 2025 tuache iwe hivyo. Pia Kama hawataki kabisa tuache iwe hivyo.

Kuna sehemu Zitto amesema mwaka 2015 lazima agombee uraisi, au hata kama CDM itakataa? Zitto ana ndoto zake, mwacheni aote, ni ndoto tu, mara nyengine ndoto hugeuka kuwa kweli, mara nyengine zinakuwa ndoto za mchana. Au hata kuota ni dhambi nchi hii? Zitto ni kama mtoto anayesema "Nikiwa mkubwa ninataka kuwa daktari", tafauti yeye kasema anataka kuwa raisi, kuna ubaya wowote? Katiba ya CDM inamkataza mwanachama yeyote kugombea nafasi yeyote? Tuacheni uhafidhina wa kimagamba na kikafu hapa na kuifanya nchi yetu Tanzania kuwa nchi ya fursa halmuradi tu mtu anafuata sheria na njia sahihi!
 
huu si muda wa kuiangalia CDM kwa jicho la usuda:

CDM imewatoa wa-tanzania walio wengi gizani, wamepata kujua upi ni mchele mzuri na upi si mchele mzuri, sasa uzushi na chokochoko zinazotolewa zidi ya CDM ni kuwarudisha wa-tanzania gizani.

Nani kakwambia kwamba Zito anamuona Slaa kwamba si chochote na wala si lolote???.
 
Kwa kusema kuwa changamoto za sasa za nchi zinahitaji kijana,ni wazi sasa zitto anataka rais ajae awe kijana!.na nadhani hata dr slaa akipendekezwa agombee tena huenda jambo hilo halitamfurahisha zitto.lkn kwangu naona bado slaa ana uwezo mkubwa sana wa kuongoza taifa hili.
 
na hawa wakipasuka hawataweza tena kujiunga hawa.

kumbe hawaja pasuka ...mwambie nape mjivue gamba kwanza ndio mjadili cdm viva slaa viva zito..umejiunga mwezi huu kwa ajili ya arumeru au kwa ajili ya slaa .
nakupa ushauri angalia nyuso za wapiga kampeni wa ccm ,kuna kitu inaitwa body language yaani wanacho ongea ni tofauti na sura zao

 
Hakuna jipya hapa, tupa kule afu mleta mada nenda kajipange upya!
 
kwanza alitaka uenyekiti,sasa urais,sio mbaya ni haki yake lakini ajifikirie kama anawezad kuongeza viti vingi vya ubunge kama slaa?nafikiri ccm wanajua slaa akigombea 2015 uwezekano wa kushinda ni mkubwa kama 2010 ndo maana hawalali kukushawishi ugombee..
 
ukishabikia ccm tu akili inaharibika kama walivyo hawajui wafanye nini wakati gani...cdm wala hawana mawazo ya urais kwa sasa mpaka june 2015
 
Adui muombee njaa cyo???
Ndugu yangu majiyamtungi!!!!! Yamwage hayo maji pengine machafu sana!!! Ndo utueleze la msingi
 
Mimi sioni ubaya upo wapi kama mtanzania mwenye haki ya kupiga na kupigiwa kura atakuwa na nia ya kugombea highest office in the land. Hata mimi binafsi ninautaka urais tena sana ili niweze kufanya yale ambayo ninaona waliopo wameshindwa hiyo ni haki ya kila Mtanzania mzalendo.

Ubaya unakuja pale mtu anautaka urais kwa 'VYOVYOTE' yaani ikibidi hata kuua wale anaoona ni tishio kwake katika kuufikia urais huyo. Tatizo hili mimi bado sijaliona kwa CDM kwani CDM wanajua kuwa the Ultimate decision yao kutoa rais ni wananchi (haki ambayo kwa sasa wananchi wamepokonywa na NEC) tofauti na CCM ambao huona kuwa the ultimate decision ya mtu kuwa rais ni Chama kwani wanajua kuwa ukiisha kuwa mgombea wa CCM wa urais basi wewe ni rais in waiting unachosubiri ni 'Abra ka dabra' za tume ya uchaguzi kukutangaza wewe hata kama wananchi wamekukataa. Hii ndiyo dhana ambayo inafanya CCM wenyewe kwa wenyewe kunyukana na kutishiana hata kujaribu kuuana ili tu kundi moja liibuke mshindi.

Zitto, Mnyika au yeyote yule ndani ya CDM anaweza kuwa na mawazo ya kuomba ridhaa ya kuwa rais lakini si kuutaka, maana unapoongelea kuutaka inamaanisha ni haki yako na wewe ndiyo unayefaa kwa vyovyote. Wanaoutaka urais ni lazima wawe wale wanaomini kuwa urais ni mali yao nao ni CCM. Anayesema kuwa kugombea urais CDM kunawafanya waparurane ni lazima atakuwa na matatizo ya ubongo na uwezo wa kufikiri. Tungekuwa na Tume huru ya Uchaguzi inayosimamia haki na kuheshimu matakwa ya wananchi kwa jinsi upepo sasa ulivyo ni dhahiri CHADEMA wana kura za urais, na hapo ningesema kuwa mtu kugombea kupitia CDM kunakufanya kuwa na uhakika wa kuwa rais kwa more than 70% ya kura za watanzania.

Lakini hali ilivyo kwa sasa ni kuwa CCM wana-urais ila hawana kura za wananchi za urais. Huo urais walio nao CCM ndiyo unawafanya kutoana macho na ngeu na kuwangiana usiku na mchana. Tukiurudisha urais kwa wananchi basi ni dhahiri hakuna chama kitakachokuwa na ugomvi wa ndani kwani urais unakuwa si mali yao tena na hivyo tungeshuhudia watu wanaoutaka urais kuwanyenyekea sana wenye urais (Wananchi).

So the whole notation of infighting for presidential candidacy within CDM is a fallace and a propaganda which can only work if its perpetrators are same as CDM which I think these two parties cannot form a tautology.
 
Zitto bana? acha hizo mkuu huwezi kuwa rais JMT kupitia CDM..NEVER!

Rais kupitia cdm ni Mbowe au Slaa au Mnyika etc..

Wewe endelea kubeba mabegi ya wakubwa wako..

Oh boy keep on crying..watakutumia kama toilet paper..soon wakikupatia watakutupa nje ya ulingo kwa hoja maalum..(siri yao)..

Acha hizo dream, msaidie Slaa na Mbowe period that is maximum we can offer kwenye chama chetu has kwa watu kama nyie..(kazi yenu ni kawawa type ok!)
inlalilahi wa inlailaihi rajiuun!
 
Huwezi kusafisha nguo yako kwa kuchukua uchafu na kuchafua ya mwenzako.Ccm imechafka mbaya mnachotaka kufanya ni kujaribu kujisafisha kwa kuwachafua wenzenu haiwezekani.Hadaa zenu pelekeni kwa watoto wa chekechea.Mlisema mbowe na zitto hawaivi leo mnakuja na stori nyingne pumbamfu!!
 
Wewe inakuhusu nini au wewe ni hawara ya ben.ninyi wadada mnapenda vibaya mno.

bahati nzuri Jf kuna rekodi bwana.chuki zake dhidi ya wazungu zinadhihirika angalia alivyokuwa anajibizana na waberoya hapa
Mbona sioni kama kuna tatizo lolote hapo?Tsivangarai ni traitor, hilo unapinga?
 
nami nawaambieni, zitto hafai hata kuwa waziri mkuu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom