Zitto: Ndio ninautaka urais

Zitto: Ndio ninautaka urais

Status
Not open for further replies.
Mkuu ikiwa tutajadili suala la taasisi ya urais kuona kama kuna umuhimu wa kupunguza umri au la outside Zitto na wengine wengi mimi ni miongoni mwa watu wanaounga mkono suala la kupunguza umri kabisa tena ikiwezekana mtu mwenye umri wa miaka 30 kama anafikia sifa zingine za Kikatiba basi aruhusiwe kugombea urais. Ikiwa tunasema life spam yetu sasa ni 47 why kugombea urais wa nchi iwe 40?? A young person can be a great president of the country. Point yangu hapa hatuwezi kujadili taasisi ya urais kwa kuwa tu Zitto au January wanataka kugombea bali tujadili kwa kuwa tu vijana wana uwezo wa uongozi.

@Hassan J. Mosoka, sina tatizo na umri wa rais, anaweza kuwa miaka 18, 20, 35, 50 na hata 80 na kuendelea PROVIDED tuna mfumo mzuri wa kiuongozi. Kwa miaka 50 tangu Tanzania ipate uhuru, tumekuwa chini ya urais (presidency) wa kifalme. Rais amekuwa na mamlaka makubwa sana na yuko almost every where kwenye chain ya utawala. Na rais anaonekana kuwa juu ya sheria. Rais anateuwa mpaka mkurenzi mkuu wa gazeti na hakuna wa kumhoji! Awe ni mtu mwenye uwezo au la hakuna wa kumzuia. Huu ndio utaratibu tuliokuwa nao kwa miaka yote 50.

Yote hiyo inaweza isiwe tatizo lakini shida inakuja pale inapotokea mtu anayekalia hicho kiti cha urais (urais wa kifalme) akawa ni dhaifu. Hapa ndipo nchi inaweza kwenda mrama. Wananchi wanabaki kuwa kama mateka, wanajikuta hawana nguvu hata kidogo ya kurekebisha mambo kwa sababu mfumo hautoi nafasi.

Sasa hivi tuko kwenye mchakato wa kupata katiba mpya, hatuna uhakika itakuwaje maana politics inaweza kuingiza vitu tusivyotaka (tuombe mungu isiwe hivyo). Na kwa hakika rais ajae atakuwa na challenge kubwa sana maana ataanza uongozi chini ya katiba mpya, lakini kama taifa bado tutakuwa kwenye 'transition period' kutoka kwenye urais wa kifalme kwenda kwenye urais ulio na ukomo kimamlaka (tafsiri yangu).

Je, ni mtu wa aina gani anayeweza kubeba mzigo huu mzito wa kuongoza nchi toka kwenye urais wa kifalme kwenye kwenye urais wa ukomo kimamlaka? Jibu la haraka haraka ni mtu mwenye uelewa, nia dhamira uzoefu/tested (nasisitiza) na anayeweza kufanya maamuzi magumu, kwa kifupi aliyekomaa. Na je, mtu aliyekomaa anakuwa na umri gani? 18? 20? 35? 60? 80? 120? Hapa ndipo kuna kasheshe.

Jambo jingine muhimu sana watanzania wote tunatakiwa tukumbuke ni kwamba tuko kwenye wakati wa majiribio makubwa, nchi hii ina madini mengi sana, diamond, gold, tanzanite, URANIUM. Na sasa tuna gas. Ukishakuwa na hivi vitu viwili URANIUM na GAS inabidi uwe tayari kwa michezo ya kuigiza toka kwa big boys wa nchi za magharibi. Sasa hivi tunaona jinsi gani Marekani iko kila mahali, kuanzia malaria no more hadi Symbion. Wakati huo huo Urusi kila kukicha kuna 'special messanger' toka kwa rais wao anakuja kuleta ujumbe. Haujakaa vizuri China wanatuandalia Chinese New Year. Ukigeuka kule France inakuambia 'nakufutia madeni! (unafuta madeni wakati credit rating yako imekuwa down-graded?). Unafuta madeni halafu inakuwaje? Kila mtu anaenda nyumbani and live happily ever after?

Ninasema yote haya ili kama taifa tujue challenge tuliyonayo katika kusuka mfumo wa uongozi kuanzia rais hadi serikali za mitaa. Kama ni kushudha umri wa urais basi tuwe na hakika tuna vijana wa Tanzania wanaoweza kumkatalia special envoy wa rais wa nchi yeyote kuhusu rasimali za nchi hii. Tuwe na hakika kwamba tuna vijana 'tested' wanaoweza kuhimili mikikiki ya kununiliana suti. Lakini kubwa tushushe umri wa urais tukiwa na hakika tuna 'system' ambayo itainusuru nchi pale udhaifu wa kiongozi huyo utakapotekea. Tusijaribishe kwenye hili. 50 yrs is enough. tuwe na uhakika na tunalofanya.
 
nimekuwa nikifuatilia kwa kina kunani kati ya zitto zuberi Kabwe na Dr. Slaa hapa pamenistua, nimepitia tamko la zitto juu ya urais kwa vijana, amerudia historia yoote ya chadema lakini anamtaja Freeman Mbowe kama mtu aliye shiriki nae kujenga chama na si Slaa, katika macho ya zitto k. slaa hana lolote ndani ya chadema, lakini kuna watu tunaujua weledi wa slaa, anasema walikubaliana na mbowe 2005 agombee urais lengo likiwa kujenga chama. na 2010 haiongelei kabisa ambayo slaa alivuta kura nyingi, je zitto amekuwa na mtazamo gani kwa slaa? kwani mara chache anamrecognise, naye slaa anafanya nini ndani ya chadema, coz ni kama antumiwa tu?

pia zitto ana mwongelea mdee tuuu, na mnyika tuuuu. what about vijana watz wasio kati ya hao? je ni kweli alishiriki kuvuruga uchaguzi 2010 kwa mawasiliano yake na wakubwa wa TISS? je chadema ya wapenda pesa kama mbowe, zitto na wengine wataweza kweli kusimamia maslahi ya nchi yetu mbele ya wageni? alijichanganya alipoingia tume ya madini, je amejichomoa huko? usafi aliopoteza mbele yetu vijana tulio makini ana hakika gani kama tumemuelewa tofauti? ajitoze katika midhara ya wazi ya vijana walio makini na ayajibu haya basi?
mustakabali wa chadema uko mashakani

Kwanza labda inakupasa ujue nini maana ya demokrasia.
Hivyo mi sioni shida kwa zito kueleza mawazo yake hiyo ndo demokrasia ya kweli,
Na kwa viongozi makini kama wa chadema hiyo sio issue kabisa.
 
ilikuwa Zitto vs Mbowe
sasa hivi Zitto vs Slaa
Kesho itakuaje??
 
Jamani jamani jamani..mbona mnakosa point? CDM Ilishapita huko kitaaambo... Ilishajipanga miaka 10 iliyopita. Muyaonayo leo c mapya bali ni mikakati iliyojiwekea wakati nyie (magamba)mnawaza kujisafisha wenzenu tayari wamesha maliza..
Rais tayari yupp mnamjua..
na baraza lake la mawaziri nalo lipo (kivuli) na linafanya kazi vizuri tu.. Ndoto zenu kwishney ..
 
CDM lazima wakubali challange za Zito, huko ndio kujenga democracy ndani ya chama, safi sanaa Zito endelea nakuunga mkono asilimia mia wewe ndio mkombozi wa watanzania sio kulindana chamani na baadae tusione tofauti na CCM tukiwapa ridhaa
 
nimekuwa nikifuatilia kwa kina kunani kati ya zitto zuberi Kabwe na Dr. Slaa hapa pamenistua, nimepitia tamko la zitto juu ya urais kwa vijana, amerudia historia yoote ya chadema lakini anamtaja Freeman Mbowe kama mtu aliye shiriki nae kujenga chama na si Slaa, katika macho ya zitto k. slaa hana lolote ndani ya chadema, lakini kuna watu tunaujua weledi wa slaa, anasema walikubaliana na mbowe 2005 agombee urais lengo likiwa kujenga chama. na 2010 haiongelei kabisa ambayo slaa alivuta kura nyingi, je zitto amekuwa na mtazamo gani kwa slaa? kwani mara chache anamrecognise, naye slaa anafanya nini ndani ya chadema, coz ni kama antumiwa tu?

pia zitto ana mwongelea mdee tuuu, na mnyika tuuuu. what about vijana watz wasio kati ya hao? je ni kweli alishiriki kuvuruga uchaguzi 2010 kwa mawasiliano yake na wakubwa wa TISS? je chadema ya wapenda pesa kama mbowe, zitto na wengine wataweza kweli kusimamia maslahi ya nchi yetu mbele ya wageni? alijichanganya alipoingia tume ya madini, je amejichomoa huko? usafi aliopoteza mbele yetu vijana tulio makini ana hakika gani kama tumemuelewa tofauti? ajitoze katika midhara ya wazi ya vijana walio makini na ayajibu haya basi?
mustakabali wa chadema uko mashakani

wewe hauna akili Zito amejibu hoja ambayo imeletwa na muandishi wa gazeti fulani sasa ulitaka atajemajina ya wanachama wote wa chadema ,ameonesha ni jinsi gani chadema inavyolea vijana kuja kuwa viongozi Ficha ujinga wako zito kaeleweka vizuri mno
 
Tatizo wagonjwa ndo wanautamani urais, matokea wakiupata wanapoteza muda mwingi kujitibu badala ya kufanya yale waliyoyahidi e.g Mkwe.re

So what is your point Mkuu?
 
Kama mnamaanisha Zitto ninayemfahamu mimi yaani huyu anayeitwa Kabwe basi urais sasa umegeuzwa kuwa nguo ya mtumba inayorushwarushwa na wateja na kutupwa huko na huko bila kununuliwa.
 
Wewe unafaa sana, nashangaa kwa nini JK hakukuteua!

Yani we ndio hufai kabisa sababu unatumia mas.. i yako kusoma. Na kwa taarifa yako sio wote ambao hatumsupport zitto ni CCM. mi CDM pure. Lakini kwa uongozi wa juu au uwakilishi wa juu katika chama mi binafsi nasema zitto ni BIG NO!!.
 
IMG_5154.jpg


Hivi huyu jamaa anaitakia Chadema mema kweli? Mara nyingi wakati wa kampeni amekuwa anakuja na kauli kutatanisha.

Mtakumbuka uchaguzi wa 2010 wakati Dkt Slaa anazunguka Tanzania nzima kuomba kura Zitto nae alikuwa anajipigia kampeni za 2015 na kusifia Kikwete kaleta maendeleo Kigoma.

Kungekuwa na tatizo gani kama angesubiri mpaka Kampeni za Arumeru zimekwisha ndio atangaze nia yake?
 
Hivi huyu jamaa anaitakia Chadema mema kweli? Mara nyingi wakati wa kampeni amekuwa anakuja na kauli kutatanisha.

Mtakumbuka uchaguzi wa 2010 wakati Dkt Slaa anazunguka Tanzania nzima kuomba kura Zitto nae alikuwa anajipigia kampeni za 2015 na kusifia Kikwete kaleta maendeleo Kigoma.

Kungekuwa na tatizo gani kama angesubiri mpaka Kampeni za Arumeru zimekwisha ndio atangaze nia yake?

We uko mbali sana na kinachoendelea sasa, huu mjadala ni wa siku nyingi sana na zitto alijibu hoja iliyojengwa na mwandishi mmoja, hapa kuetwa JF ni post tu imetokea. kuwa makini usome mada husika usichangie kwa kusoma kichwa cha habari.
 
Hii taarifa bado haitatosheza kukufanya upate malipo maziri kwa Dogo Nape kwa kukishambulia vema CHADEMA - hebu ongeza dozi kidooogo mkuu.

Hapo ametumia resources kibao. Sidhani kama ataweza kuongeza. Most likely ataharibu.
 
..kuna kitu kinaitwa TIMING.

..huu haukuwa wakati wa Zitto kutoa makala kama hii.

..wengine tunasema, angekuwa mtu mzima kidogo[40+] asingeweza kufanya mambo kwa kuhemkwa kiasi hiki.

..matendo na mwenendo wa Zitto ni utetezi tosha kwamba mgombea wa Uraisi awe na umri wa miaka 40 au zaidi.

NB:

..kwa mtizamo wangu mgombea Uraisi mwenye umri wa miaka chini ya 40 has to be really exceptional.
 
Wadau ,Mimi nina swali;

Kwa nini adui wa CDM yaani CCM wengi Wanampigia sana upatu Zitto agombee Urais 2015 kupitia CDM?,wanamponda sana Dr Slaa kwamba hafai.Nina wasiwasi pale ambapo adui yako anakusifia.
 
Kikwete alikuja kwa sera ya kwamba tumchague yeye ni kijana kwani ametufanyia nn cha maana?

Msiwe wavivu wa kufikiri. Zitto hajasema anataka urais kwa kuwa yeye ni kijana,bali anataka urais kwa kuwa ana uwezo. Na ameweka clear kabisa,atafanya hivyo(kugombea) endapo chama chake kitampa ridhaa ya kupeperusha bendera ya CDM,na endapo wananchi watakubali kuwa anafaa. Kipi hamjaelewa? Wakati mwingine tujaribu kushirikisha ubongo kufikiri kidogo!..
 
binafsi nakuunga mkono,umefanya makubwa kwa chama na taifa kwa ujumla. Binafsi nakupitisha kwani naamini unaweza na najua hutaniangusha.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom