Mkuu umenikumbusha siku ya kwanza naenda kuripoti kikosini nilifika Kabuku kama saa 11 jioni. Basi wenyeji wakaniambia subiri utapata lifti ya mkuu wa kikosi kaenda Korogwe. Nikajikuta niko na dada mmoja alikuwa na ulemavu wa mguu mmoja naye anaenda kuripoti.Baada ya kama saa moja akaja mkuu wakikosi ndani ya Landrover akitokea Korogwe. Huyo ndio Kanali Mtono,sijapata ona askari kama yule tena kwa maana ya mafunzo ya kujenga ujasiri.
Alichofanya ni kumchukua yule dada mwenye ulemavu na yeye kushuka kwenye gari na kunionyesha milima ya Gendagenda na kusema,mzalendo,kabla ya kufika milima ilee,kambi iko hapo,tembea utafika
Sasa wakati huo ndio na giza limeanza,huo ni msitu kwa wakati huo,njia siijui na hakukuwa na sababu kwa nini hakunipa lift. Hapo ndio nilianza kuona adha ya Jeshi.
Nilikomaa mpaka nikamaliza na mengine ni historia,but nilitoka nikiwa mtu tofauti kabisa. Zitto,naambiwa mnaenda wiki kadhaa,sidhani kama mtaiva kama wale ambao walihenya mwaka na ambao walivumilia machungu yooote lakini siku ya kutoka walikuwa na kicheko wao na wakufunzi wao.
Kila la kheri.