Bwana Zitto Ruyagwa Kabwe kwa nini usivuke daraja ukilifikia??? unachofanya sasa ni sawa na kuvuka daraja ukingali mbali na kingo za mto...Na hii inadhihirisha wazi kuwa siku zote mtoto mchokozi ndiye huwa wa kwanza kukimbilia kwa wazazi kushtaki...Bwana Ruyagwa kwanza ulikosea sana tena sana na umejishushia hadhi yako sana pale ulipotamka ati viongozi wa TPDC wapelekwe Polisi, lakini pili pamoja na kupelekwa Polisi wewe kama mlalamikaji (mtetezi wa unachokiita rasilmali za umma) ulipaswa kwenda kituoni na kufungua shauri pale..kwa kuwa ulikuwa unajua wazi kuwa unajaribu kujijengea umaarufu wa rejareja ndio maana hukuthubutu kwenda na wakaachiwa na baadaye tukapata taarifa kuwa umekiuka taratibu za kibunge...Nikija kwenye utetezi wako wote huu naona ni yale yale ya kuvuka mto kabla..Mmekwishakubaliana bungeni CAG na Dr.Hosea wafanye uchunguzi...wamefanya na kabla hawajamaliza mnakuwa watu wa mwanzo kubwatuka bungeni kwa kuwa tu mna kinga za kibunge ili muudanganye umma wa Tanzania kuwa kweli kuna ufisadi.
Kama mnao uhakika wa ufisadi huo tulieni tuliii..subirini ripoti itakuja kamati yako itapewa na bungeni itasomwa, hapo ndipo pa kuanzia kwani mbivu na mbichi zitakuwa tayari zimejulikana...Mimi nawaona wewe na Kafulila kama mnatumiwa na mna maslahi binafsi na ndio maana hamuachi vyombo vilivyopewa kazi hii vikamilishe kazi yake...Zile zama za Mbunge kuropoka na serikali kumwajibisha waziri zimepitwa na wakati kwani mawaziri wa sasa sio wale unaowadhani wapenda mshiko..hawa ni wazalendo kuliko wewe na wanafanya kazi kwa uadilifu wa hali ya juu...historia yao na yako zinaweza kulinganishwa ukaona wazi kuwa wewe umeibuka haraka katika kipindi kifupi tu
Bwana Zitto na Kafulila wacheni kupiga mayowe...tuachieni sisi tuone wenyewe.
Zitto