Zitto kabwe,
kwanza umefanya vema kujitokeza kujibu tuhuma zinazokukabili lakini unaonekana kutumia akili pana sana kujibu tuhuma zako hasa kwa kutumia maneno ya kulaghai badala ya kumibu hoja asilia,ninashaka na maneno yako hasa kwenye maeneo haya,
kwanza,umesema kampuni ya shell haifanyi biashara hivi kunakampuni ambayo inaweza kuanzishwa siyo kufanya biashara? Kama haifanyi biashara inafanya kazi gani sasa.
Pili utakumbuka kwenye tuhuma zako unatuhumiwa kuazimwa au kukopeshwa kiasi cha milioni sita na kampuni moja wapo hapa nchini pesa hiyo ilitumika kwenda kumtibia mama yako kwanini hujasema hiyo pesa ulipewa kwa makubaliano gani au ulipewa kama msaada au kama mikopo mingine ili urudishe.
suala lako la kupewa hela na ubarozi wa uingeleza siyo jipya hata wakili wako ambaye sote tunamjua anayetokea mkoa wa kaskazini unamtumia sana kwenda kuchukua pesa zako za madili kutoka kwenye makampuni kadhaa unachofanya pesa nyingi huchukui wewe unatuma watu kwaniaba yako.
zipo sehemu mbili ambazo wakili wako amechukua pesa kwa maelekezo yako na amesainishwa siku moja hiyo document utawekewa hapa ila mnamuaibisha sana wakili wako japo hapendi unavyofanya lakini wewe unasema huwezi kuacha kuwasaidia waingeleza umetoka nao mbali.
jambo lingine ni wewe kutumiwa na nimrod mkono kiukweli hili unavyokataa binafsi mimi nakuona kituko mkono hajaanza leo kukutumia mpaka anakununulia ile gari ambayo kwasasa umeikodisha ni katika makubaliano yenu ya baadhi ya kazi unazomfanyia za kutumika kiukweli zitto nilikuwa shabiki wako sana tangu nijue kuwa wewe mla rushwa nakuweka kundi moja na wachumia tumbo wengine na hii tabia ya rushwa na wizi sasa umemfundisha hata deo filikunjombe.
ushauri wangu kwako fanyeni yote mnayofanya watanzania wasije kuwajua lakini siku moja wakijua mtachomwa moto mchana kweupe.