Zitto: Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema "Hatutetereki"

Zitto: Nashambuliwa, tunashambuliwa! PAC tunasema "Hatutetereki"

Kitendo cha wewe ku quote kilichoongelewa nikajua una akili na kwamba umeelewa jema lenye manufaa kwenye mustakabali wa Taifa ila baada ya kujibu mnikagundua wewe ni punguani ambaye inabidi uswekwe rumande kwa kukebehi hoja ya msingi.
Jambo gani la kitaifa kaandika hapo huyu mnafiki.
 
Bwana Zitto Ruyagwa Kabwe kwa nini usivuke daraja ukilifikia??? unachofanya sasa ni sawa na kuvuka daraja ukingali mbali na kingo za mto...Na hii inadhihirisha wazi kuwa siku zote mtoto mchokozi ndiye huwa wa kwanza kukimbilia kwa wazazi kushtaki...Bwana Ruyagwa kwanza ulikosea sana tena sana na umejishushia hadhi yako sana pale ulipotamka ati viongozi wa TPDC wapelekwe Polisi, lakini pili pamoja na kupelekwa Polisi wewe kama mlalamikaji (mtetezi wa unachokiita rasilmali za umma) ulipaswa kwenda kituoni na kufungua shauri pale..kwa kuwa ulikuwa unajua wazi kuwa unajaribu kujijengea umaarufu wa rejareja ndio maana hukuthubutu kwenda na wakaachiwa na baadaye tukapata taarifa kuwa umekiuka taratibu za kibunge...Nikija kwenye utetezi wako wote huu naona ni yale yale ya kuvuka mto kabla..Mmekwishakubaliana bungeni CAG na Dr.Hosea wafanye uchunguzi...wamefanya na kabla hawajamaliza mnakuwa watu wa mwanzo kubwatuka bungeni kwa kuwa tu mna kinga za kibunge ili muudanganye umma wa Tanzania kuwa kweli kuna ufisadi.

Kama mnao uhakika wa ufisadi huo tulieni tuliii..subirini ripoti itakuja kamati yako itapewa na bungeni itasomwa, hapo ndipo pa kuanzia kwani mbivu na mbichi zitakuwa tayari zimejulikana...Mimi nawaona wewe na Kafulila kama mnatumiwa na mna maslahi binafsi na ndio maana hamuachi vyombo vilivyopewa kazi hii vikamilishe kazi yake...Zile zama za Mbunge kuropoka na serikali kumwajibisha waziri zimepitwa na wakati kwani mawaziri wa sasa sio wale unaowadhani wapenda mshiko..hawa ni wazalendo kuliko wewe na wanafanya kazi kwa uadilifu wa hali ya juu...historia yao na yako zinaweza kulinganishwa ukaona wazi kuwa wewe umeibuka haraka katika kipindi kifupi tu

Bwana Zitto na Kafulila wacheni kupiga mayowe...tuachieni sisi tuone wenyewe. Zitto
 
Last edited by a moderator:
Kwa hilo la ESCROW watu walishajipanga kupiga mahela ya Wadanganyika ndio maana "wazee" wa bodi wako radhi kwenda rumande kuliko kuweka wazi mikataba ya gesi! wanajua lililo nyuma ya pazia na nani walioshikilia "remote control".
 
Ni jambo la kijinga kabisa baadhi ya mafisadi wanaojiita Upinzani kuungana na mafisadi kutunga tuhuma

Juzi nilisema tuhuma zinazohatarisha hadi diplomasia yetu na Kenya na Uingereza ni za kijinga sana sana

Tumeanzisha Kampeni na tumeionya IMF ikae mbali iachane na kuulea ufisadi wa Serikali ya Tanzania

"IPTL-Bring Back Our Money"

Yupo katibu Mkuu wa wizara moja kazi yake ni kufanya spinning na kutumia magazeti ya serikali kupotosha kuhusu ufisadi wa ESCROW

Nawapongeza wabunge wote vijana kwa kazi nzuri wiki iliyopita

Kila mtu amtumie mbunge wake ujumbe atoe sapoti bungeni kuhusu kashfa hii.

Nimeziona nyaraka zote ,ni aibu sana sana
 
Pole Ndugu ZITO! Natamani nikusaidie ila sijui nianzie wapi! Ila kama unavyosema watanzania sio Mabwege na pili Umesemea uzalendo kwa nchi/taifa lako. Haya ndio makubwa.

Unawezzaje mtu mzima kama waziri au katibu mkuu mwenye dhamana kubwa kuhatarisha maisha ya wananchi(kwa kupokonya fursa za uchumi) ili kutajirisha mataifa mengine na wewe pekee! Hivi yule Prof wa Wabongo ni Wafanyabiashara Juisi ameishia wapi? au ndio yuko jikoni anapika majungu haya.

GO GO Mbele Mbele kwa mbele Zitto- Natamani ungekuwa umerejesha mahusiano yako vizuri kule CDM - mapigano haya yangekuwa rahisi zaid- tuko pamoja TULIANZA NA MUNGU NA TUTAMALIZA NA MUNGU
 
Haujajibu tuhuma hata moja hspo,unapiga kelele tu na unadhihirisha u shalo wako.

Kwanza kwa nini unamjibia huyo ceo wa shell? kwamba sio aliyevujisha mkataba wa statoil balu ni waandishi wa habari?

Na unaizungumzia shell, wewe kana nani shell?

Nilitegemea kama umekuja hapa kujibu tuhuma ujibu tuhuma zako.

Kwa mfano,ungeeleza kwamba matibabu ya marehemu mama yako uliyagharamia kwa pesa zako mwenyewe n.k na haujawahi kuomba pesa directly au in directly kutoka PAP. Na sio kutishia watu na vyombo vya dola.
Mkuu umeongea jambo jema zitto ni msanii anachofanya hapa ni siasa kumisafisha baada ya kuchuja kisiasa anatafuta jambo la kutoka nalo ameshindwa kumibu hela aliyopewa kwenda kumtibu mama yake alipewa kwa misingi gani halafu anasema eti kamupini ile haifanyi biashara tangu lini kampuni inaanzishwa isifanye biashara halafu kawa msemaji wa shell jamni zitto kaharibika siyo yule wa kipindi kile amekuwa mla rushwa tu.
 
Zito, hukuwa na sababu ya kujustify hapa mtandaoni. Watanzania tuna ufahamu na tunaweza kusema ukweli isipokuwa mafisadi na wanafiki.
Wewe unaweza kuwa kiongozi mzuri kama tu utaacha tabia zako za ubinafsi, undumila kuwili, dharau na kiburi cha kutokutaka kusikiliza wenzako na kufanya kazi kwa ethics. Nina mifano mingi sana inayoweza kuthibitisha uwepo wa tabia hizi juu katika wewe.

Umeshindwa kukaa na wenzio kwenye chama mlichokitoa mbali kwa sababu ya kiburi, maringo na kutokukubali kuongozwa na maadili ya chama. Hakuna kiongozi makini duniani ambaye kila inapotokea kutokuelewana kwenye hoja ndani ya vikao, yeye anakimbilia media kujisafisha na kuwasaliti wenziye. Hakuna kiongozi hata mmoja mzuri ambaye asipokubaliwa hoja yake kwenye jumuia, anasusa na kuanza kuishi kwa kuwawinda wenziye ili wadharirike.

Hakuna mzalendo yeyote anayeweza kuficha taarifa muhimu ili azitumie kwa maslahi yake(popularity) na huwezi kuaminika na jamii yoyote kama wewe ni ndumila kuwili. Unakwenda unauma na kupuliza kote kote. Kwa tabia hizi zito jiandae kupotea katika medani za siasa unless ujirekebishe. Tatizo la kigoma ni wabishi wasiokubali kugeuka hata pale anapoonyeshwa kabisa kwamba kuna tatizo ama yuko wrong. Lakini wewe umepata exposure na unapotentials nyingi ambazo hazijawa exploited, acha jeuri na tabia hizo ili ulitumikie taifa at your full capacity.

Back to your points,
Sis tulioko huku tunaona na kutathmini. Kwa habari ya kile kijikaratasi kimechongwa chongwa kuku implicate kukopa 6m za matibabu ya familia, ni cha kughushi na malengo yake yamejieleza mule mule. Ukikiangalia tu na ukaoma contents zilivyokuwa framed, kwa mtu anayejua sheria tayari unaki nullify. Mimi personal nimshaki declare ni NULL AND VOID.

Huna sababu wala ya kukiongelea hapa kwa sababu hata kabla yako, wapenda haki tumeshakutetea kwamba katika hicho unaonewa. Unaweza ku sue na kupata millions of money kama una muda.

Lakini , msichanganye hesabu. endeleeni mbele katika hili la kutetea faida wala msitetereke kama ulivyosema. Mwenye tuhuma na vielelezo vya otherwise, afungue shauri tofauti na wala si kuunganisha na kazi mnayoifanya kama tume. Kama mmefisidi, mmefisidi individuals na mnastahili kuchukuliwa hatua kama individuala na wala si PAC.Pa

PAC fanyeni kazi, makosa yenu binafsi yachukuliwa hatua binafsi kwa sabbu ni ya kibinafsi.

Ccm rest in pieces.
 
Zitto nakushukuru kwa niaba ya wale wote wasioweza kuona inayoyafanya kamati yako hasa raia wa kijijini kama mama yangu na bibi yangu.

Napenda kukusihi uwe mvumilivu kwa haya yanayotokea sasa manake kama ni wizi haijalishi kaiba nani wote wanatakiwa wawajibike ipasavyo. Najua hata huku kwenye mitandao ya kijamii tupo vijana ambao hatukupendezwa na yale uliyoyafanya CHADEMA hadi hali ikawa kama ilivyo sasa.

Lakini kwa kuwa suala hili ni la maslahi kwa watanzania hasa wa kipato cha chini kama mama yangu na bibi yangu kule kijijini, lazima tufike mahali vijana wote na watanzania wote tuseme hapana kwa wizi hata kama aliyeiba ni baba yangu mzazi.

Mimi na baadhi ya watu tulipopata taarifa kuwa kamati imewafikisha polisi waliogomea mikataba, hatukuwaza juu ya uhalali wala isivyo halali kwa sababu hata sheria,bunge na mahakama kamazikishindwa kusimamia maslahi ya nchi basi ni sawa na hazipo.

Nasisitiza ahsanteni, poleni na Mwenyenzi Mungu ninayemtumikia awaongoze ili watanzania tushinde.
 
Usichoke kupambana Zitto katika hili, pia angalizo kuwa makini sana na hao mafisadi unaopambana nao maana hawakawii kukulimboka, mtangulize Mungu thenly yote utayashinda.

Lastl, ufisadi umekuwa sugu nchini hasa kwa hawa watawala wenye ukoma masikioni, how comes mtu uibe bilion 200? Jamani wananchi tusipojitambua ipo siku watauza hadi wake zetu.

TANZANIA STAND UP.
 
Last edited by a moderator:
Zitto kabwe,
kwanza umefanya vema kujitokeza kujibu tuhuma zinazokukabili lakini unaonekana kutumia akili pana sana kujibu tuhuma zako hasa kwa kutumia maneno ya kulaghai badala ya kumibu hoja asilia,ninashaka na maneno yako hasa kwenye maeneo haya,

kwanza,umesema kampuni ya shell haifanyi biashara hivi kunakampuni ambayo inaweza kuanzishwa siyo kufanya biashara? Kama haifanyi biashara inafanya kazi gani sasa.

Pili utakumbuka kwenye tuhuma zako unatuhumiwa kuazimwa au kukopeshwa kiasi cha milioni sita na kampuni moja wapo hapa nchini pesa hiyo ilitumika kwenda kumtibia mama yako kwanini hujasema hiyo pesa ulipewa kwa makubaliano gani au ulipewa kama msaada au kama mikopo mingine ili urudishe.

suala lako la kupewa hela na ubarozi wa uingeleza siyo jipya hata wakili wako ambaye sote tunamjua anayetokea mkoa wa kaskazini unamtumia sana kwenda kuchukua pesa zako za madili kutoka kwenye makampuni kadhaa unachofanya pesa nyingi huchukui wewe unatuma watu kwaniaba yako.

zipo sehemu mbili ambazo wakili wako amechukua pesa kwa maelekezo yako na amesainishwa siku moja hiyo document utawekewa hapa ila mnamuaibisha sana wakili wako japo hapendi unavyofanya lakini wewe unasema huwezi kuacha kuwasaidia waingeleza umetoka nao mbali.

jambo lingine ni wewe kutumiwa na nimrod mkono kiukweli hili unavyokataa binafsi mimi nakuona kituko mkono hajaanza leo kukutumia mpaka anakununulia ile gari ambayo kwasasa umeikodisha ni katika makubaliano yenu ya baadhi ya kazi unazomfanyia za kutumika kiukweli zitto nilikuwa shabiki wako sana tangu nijue kuwa wewe mla rushwa nakuweka kundi moja na wachumia tumbo wengine na hii tabia ya rushwa na wizi sasa umemfundisha hata deo filikunjombe.

ushauri wangu kwako fanyeni yote mnayofanya

Brabrabraaaaaaa abragdabagaaaaa hii ndio nini? Simiyu lete hoja sio ngonjera zako zilizopitwa na wakati,,Fedha ya Escrow ni mali ya watanzania na tunaomba irudishwe tu
 
Hongera sana bw. Zito na kamati yako kwa kuyaweka wazi haya mambo...bigup bro.

Vilevile nisikitike kwa baadhi ya wadau humu kuanza kuleta mizaha na kutaka kukukatisha tamaa...hilo lisikupe shida wazalendo wakweli tupo nanyi...

Mnyonge mnyongeni lakini haki mnayostahili lazima tuwape. Watanzania wengi walikuwa hawaujui uchafu huu lakini kwa uzalendo wenu kila mtu amejua na kupigwa bumbuazi.

Nadhani wanaobeza ni wale wenye ukoo wa panya.
 
Mkuu kaza buti,tupo pamoja,mpaka kieleweke,hayo majizi lazima tuyapige suna kwa kipande cha chupa,
Usitishike kaka,Mungu akiwa upande wetu,nani atakuwa juu yetu,mtumainie Mungu,maana amtumainiaye ni kama mlima sayuni,

ALUTA CONTINUA
 
Zitto,

Kwanza Karibu tena JF, binafsi nashukuru kwa Maelezo yako Maridhawa, usiishie hapa tu, umekuwa kimya sana tokea Saga lako na CHADEMA, kuanzishwa ACT na Matamshi yako ya hapa na pale juu ya uanzishwaji wa UKAWA.

Back to the Main topic, Naomba kutoa comments zangu kama ifuatavyo based on your response dhidi ya kutuhumiwa Kwako kwenye issue ya escraw account

Tuhuma #1 :

Zitto anaye rafiki yake Mkenya aitwae Rapahel Ongangi ambao kwa pamoja wameanzisha Gombe Advisors Co. Ltd (registered on 24 November 2011, Certificate No 87387) kwa ajili ya kufanya biashara na Makampuni ya Gesi na Mafuta yanayofanya kazi nchini hapa.

Majibu:

Gombe Advisors ni kampuni binafsi isiyofanya faida yaani ‘Company Limited by Guarantee'. Haina kazi na kampuni yoyote ya Gesi na Mafuta na wala yenyewe haijuhusishi na biashara hiyo. Gombe advisors haijafanya kazi yoyote ile na kampuni nyingine zaidi ya kusaidia wasanii wa kundi la Kigoma All stars. Upotoshaji hapa unalenga kupindisha mjadala.

Kuna Madai kuwa unaitumia Gombe Advisors kuchota fedha kwenye mifuko ya akiba ya Jamii sio tu kwa Maslahi ya Wasanii kutoka Kigoma, bali ni kwa Manufaa ya kwako binafsi, Pia wadadisi wa Masuala ya Conflict of interest wanakosoa Kampuni hiyo kwenda kukopa kwenye Mifuko ya Hifadhi ikiwa wewe mmiliki wake unaiwajibisha hiyo Mifuko kupitia Kofia yako ya ueneyekiti wa PAC, some sort of kutumia Madaraka vibaya kunaweza kutafsiriwa hapa, hizi shutuma hujazijibu Mpaka Leo.
Bottom Line, Hapa hujakanusha kuwa huyo Bwana Rapahel Ongangi kuwa unafahamiana nae kwa namna yoyote


Tuhuma #2 :

Zitto amemsaidia Ongangi kupata uraia wa Tanzania na kwa sasa ni raia wa pasipoti. Zitto na Ongangi walimtafutia CEO wa Shell aitwae Axel Knospe nyumba na gari ya kukodi.

Majibu:

Raphael ni mtu binafsi ambaye anafanya shughuli zake hapa nchini, amesoma hapa nchini na ameoa na ana mtoto. Tuhuma hizi hazina msingi wowote ule maana ni uwongo. Wanaotoa tuhuma hizi waonyeshe hiyo pasipoti ya Bwana Ongangi kuthibitisha madai yao.

Hapa unaonesha kuwa unamfahamu huyu mtu vyema sana.
Lakini kwanini Bwana Raphael asikanushe hayo yeye Mwenyewe?, je, wewe ni Msemaji wake, siku akijitokeza yeye Mwenyewe ama ama watu wakileta huo ushahidi utauweka wapi uso wako ?
Reffer to China wakiwanyonga some of their officials kwa kubeba Ivory kwenye their Diplomatic Bags, Membe wetu atauweka wapi uso wake ???


Tuhuma #3 :

Mikataba ya STATOIL iliyokuwa inarushwa kwenye mitandao ya jamii na kuchapishwa kwenye magazeti ya Kenya ya hapa nchini (The Citizen na Mwananchi) mwandishi mkuu alikuwa huyo CEO wa Shell.

Majibu:

Mkataba uliovujishwa wa StatOil ulivujishwa na waandishi wa habari wa Norway. Uchambuzi wa mkataba huo nimeufanya mwenyewe kwa kutumia utaalamu wangu niliosomea wa kuchambua mifumo ya kodi kwenye sekta ya mafuta na gesi. Kwa namna yoyote ile, huyo anayetajwa kuwa CEO wa kampuni ya Shell hahusiki. Tuhuma hii wanaoitoa watoe ushahidi usio na chembe ya mashaka.

Ikumbukwe kuwa mkataba wa StatOil utaipotezea Tanzania mapato ya dola za Marekani bilioni 12 (takribani Tshs 20,400,000,000,000/=) katika kipindi cha miaka 15 baada ya gesi kuanza kuchimbwa. Uamuzi wa Kamati ya PAC kutaka mikataba yote ya Gesi kuwa wazi una lengo la kuchambua kuona kama mikataba yote nchini haipotezi mapato kwa nchi. Uamuzi huo umewakasirisha sana baadhi ya waliohusika kuingia mikataba Serikalini maana wanajua kuna madudu kwenye mikataba na wanataka umma wa watanzania usijue!

Tutajuaje kama wewe ndo ulichambua ???, we need Facts, tuletee uchambuzi wako na wa Norwaay tupembue wenyewe.
Siamini kuwa wa Noorway walivujisha tu bila kuchambua

Tuhuma #4 :

Kampuni ya SHELL imechukizwa sana kucheleweshwa kwa kupata kibali cha kutafuta gesi na mafuta kule Pemba. Vilevile SHELL haina uwekezaji mkubwa Tanzania Bara kwani ilishindwa kwenye tenda zenye vitalu vyenye gesi nyingi upande wa Bara.

Majibu:

Ukweli ni kuwa Kampuni ya Shell ina vitalu 4 huko Zanzibar na tayari ina makubaliano na Serikali ya Zanzibar kuhusu utafutaji mafuta huko katika vitalu namba 9,10,11 na 12. Shell inafanya kazi na kampuni ya Petrobras ya Brazil kwenye kitalu namba 6 na namba 8. Taarifa hizi zipo wazi kwenye tovuti ya TPDC. Tuhuma nyepesi namna hii dhidi ya kampuni kubwa kama Shell zinaonyesha dharau na kiburi kinachotokana na uelewa mdogo wa mambo wa watu wanaotuhumu.

Hapa unarudia Makosa ya hapo Juu ya kuwa Msemaji wa Bwana Raphael.
Hapa unajipachika usemaji wa Kampuni ya SHELL

Tuhuma 5:

Ongangi anapokea maelekezo kutoka Serikali ya Kenya kuhujumu uwekezaji nchini mwetu.

Majibu:

Nazifahamu mbinu nyingi zinazotumika kufanya propaganda, lakini mbinu hii imeshindwa ikiwa mapema sana. Ni vema wanaotoa tuhuma hizi wazithibitishe vinginevyo ni mwendelezo wa propaganda zisozingatia diplomasia ndani yake dhidi ya jirani zetu wa Kenya. Hizi ni propaganda hatari ambazo hata hao wanaotuhumiwa wakisikia watatudharau sana.

Hapa tena unajipa Kazi ya usemaji wa Serikali ya Kenya katika kuisafisha na Kumsafisha Bwana Raphael.

Tuhuma #6 (juu ya Uingereza):

Uingereza imekuwa inamfadhili Zitto kwa miaka mingi kwa mambo yake ya kisiasa kwa hiyo sasa hivi Ubalozi wa Uingereza unamlipa Zitto na Kafulila kuhakikisha kwamba Standard Chartered ya Uingereza inalipwa deni lake lisilotambulika kisheria nchini mwetu.

Majibu:

Nimetangulia kusema hapo awali kuwa kuna propaganda ambazo haziangalii hata diplomasia; nyingine ni hii. Pamoja na kukanusha uzushi huu, ni vizuri wanaotoa tuhuma za namna hii kuthibitisha. Mimi binafsi sijawahi kufadhiliwa kisiasa na Taifa lolote lile. Inaelekea kuna wanasiasa wanaofadhiliwa na mataifa mengine ambao kwakuwa kwao ndiyo maisha wanaamini na wengine tupo kama walivyo. Kwangu itikadi yangu ni ‘Uzalendo kwa nchi yangu', ni jambo ambalo halina mbadala wake. Siku zote nasema "Right or wrong, my country first". Kurudia kurusha tuhuma kwa Ubalozi wa Uingereza nchini ni kudhihirisha kwa mara nyingine kiburi cha kuwa na mamlaka (arrogance of power) walicho nacho wanaotuma tuhuma hizi.

Aidha, wanatuhumu kuwa "Kafulila na Zitto wamehaidiwa 15% ya USD 150 million kama deni likilipwa"

Mtanzania anayeweza propaganda dhaifu kama hizi basi anatakiwa ajitafakari. Hata hivyo ni vema wanaotoa tuhuma hizi wathibitishe bila chembe ya mashaka.

Hapo kwenye RED and BOLD, inaelekea kuna unachojua dhidi ya hao wana Siasa, huenda nao kuna wanachojua dhidi yako.
Waarabu wa Pemba wajuana kwa Vilemba

Tuhuma #7 :

Mbunge Mkono nae ameshikwa hasira kupoteza kazi ya uwakili pale TANESCO. Kafulila na Zitto wanalipwa na Mkono kuvuruga Serikali kwa hasira za kukosa fedha za kitapeli za TANESCO.

Majibu:

Hizi ni tuhuma ambazo sasa tumezizoea kutolewa. Mambo mepesi hayawezi kujibu mambo ya msingi kama tuhuma za wizi wa fedha zaidi ya Tshs bilioni 200 kutoka Benki kuu ya Tanzania. Kukusanya kila propaganda ili kuuhamisha umma ni kupungukiwa hekima na busara.


Aidha, wanaotuhumu wanadokeza kuwa "Naomba tuwe macho na Wabunge wetu achananeni na madai ya Zitto ya wizi. Huyu mtu anafanya biashara na Kampuni ya SHELL na inasemekana analipwa na Ubalozi wa Uingereza. Serikali ya Kenya na tapeli mkubwa Mbunge Mkono nae anawalipa Zitto na Kafulila".

Watanzania, haya ni maneno ya hasira ya watu wanaokaribia kukamatwa kwa kushiriki wizi wa fedha katika Benki kuu ya Tanzania. Kamwe tuhuma kama hizi haziwezi kutukatisha tamaa katika kupambana ili ukweli ujulikane. Sisi tutapigana kwa ajili ya Taifa, kwa ajili ya mtanzania na tunachotaka ni umma uujue ukweli wa mambo.

Intentionally left Blank

Hasira hizi zinatokana na mambo mawili:

Moja ni uamuzi wa kamati ya PAC kuwasweka ndani baadhi ya watendaji wa TPDC kwa kushindwa kutekeleza maamuzi ya Kamati yanayohusu uwazi wa mikataba ya Gesi na Mafuta.

Then what happened baada ya hawa jamaa kusekwa ndani ??
Je, kuna ambaye amajiuzulu ?, je wakishinda hii kesi wewe na Kamati yako mko tayari kuwajibika ???
Naoma hili tuliweke kwenye kumbu kumbu Tutahitaji Mrejesho kutoka kwenye kamati yako regarding this.
.
Harbinder Singh Seth aliiangusha Serikali ya KANU nchini Kenya, sasa anachotaka kukifanya kinaweza kuiangusha Serikali ya CCM wakiende

Hapa unaonekana kuihurumia CCM na Serikali yake kwa kuipa anaglizo.
WTF !!!!!!!!!!! ????????????????


===============================
Nachelea Kusema Pia maelezo yako mengi ni ya Jumla jumla sana na hayana facts akama ambazo umetaka kupewa na unaodai wana kuchafua.
Pia, na wewe Kama msomi, akili Kubwa kama unavyojinadi / nadiwa, umerudia Makosa yale yale aliyoyfanya MFA jana kwa kujigeuza Msemaji wa China bila facts kwa kukanusa tuhumua za EIA kuwa Kwenye Dimplomatic Bags az Msafara wa Rais, Pembe za Ndovu zilibebwa.
 
Hasira sana kamanda, ipo siku Mungu wa Eliya ajibuye kwa moto atawaumbua wadhalimu wote wanaolitafuna taifa.
Hajaweka ushahidi wowote unaonesha anachikisema zitto zaidi ya ulaghai wa maneno ya kisiasa.
 
Binafsi nitafurahi kama jambo hili la Escrow litashughulikiwa kwa mujibu wa taratibu na sheria za nchi.

Kinachokera hivi sasa ni kutafuta umaarufu wa kisiasa. Kwamba baada ya Zitto kugaragazwa vibaya kisiasa na Chadema kiasi cha kuishi ubungeni kwa msaada wa mahakama na kupoteza mashabiki wengi aliokuwa nao, sasa anataka kuwa-retain waliobaki na kupata popularity upya kupitia matukio.

Wakati Zitto ana deni letu la majina ya walioficha fedha uswisi, anakuja na mbwembwe za kutishiwa maisha bila ushahidi.

Fedha za uswis sisi hatukumtuma aziseme. Ni yeye mwenyewe aliyesema anajua majina ya watu walioficha hizo fedha huko. Akafanya safari mbili tatu akapotea kimyaa lakini ilikuwa ni baada ya mbwembwe kama hizi. Maana ilikuwa kila siku ni Zitto na fedha za uswisi. Ikaja tena hekaya kama ya leo kuwa kutokana na fedha ya uswis kubumbuliwa na yeye eti wanataka kumuua. Fedha za uswis hazijaja na majina hatujayapata na kwenye tume ya Werema Zitto kakanusha kuyajua majina.

Hili la Escrow ni dana dana nyingine ya 'nitoke vipi' Ni mwendelezo ule ule wa Zitto kutaka kujiinua tena kwa visibgizio na mbinu za kizamani tena bila ushahidi.
Asubihi leo, zimepandishwa threads tatu za kumsifia Zitto toka kwa mtu mmoja. Thread zenyewe ukiziona ni kama takataka tu lakini kwakuwa ni mkakati maalum zikaanzishwa. Mara eti Zitto ni Mbunge bora wa November. Wapi walianza kutoa hizo tuzo? Kama Zitto ni mbunge bora wa November, wa February ni nani? Mbunge bora kwa Parameters zipi? Zimekubaliwa na nani hizo parameters hadi tukubali Zitto ni mbunge bora wa November? Wenye akili tulipoona thread zinazomsifia Zitto zimeanzishwa tukajua tu kuna kitu kitaibuliwa.

Sasa Zitto amekuja na hadithi njoo utamu kolea. Sisi hatutaki kujua nani katishiwa nani hajatishiwa. Tunataka fedha za Escrow zirudi kwa watanzania wanaokosa dawa, wanaochangishwa michango ya kishenzi ilhali fedha ipo mifukoni mwa wajanja. Hii move pamoja na Kafulila Mnyika aliwahi kuishikia bango. Sasa PAC mnayo, fanyeni kazi zenu mje na matokeo acheni longolongo kama za fedha za uswis. Na mkome kutaka kupata umaarufu binafsi kwenye ishu yenye national interest.
 
"Nasapoti" sana jitihada za ZZK lakini ni vema pia awe anatufikisha mwisho wa alichokipigania , kwa mfano suala la Pesa zilizo nje ya nchi (Uswisi na kwingineko).

Suala lile hakutujulisha limefikia wapi, samahani kama labda alitoa maelezo, kumbukumbu zangu ni kuwa liliishia hewani tu.

Ningependa apiganie hoja hizi hadi paa ling'oke kama alivyosema Wenje.

Otherwise, hongera sana zito kwa kazi unayofanya na jitihada zako zinazidi kuwafumbua macho Watanzania wenzako. Haiwezekani wote tukawa na mawazo kama ya ZZK lakini umeonyesha njia na sasa wengi wa wabunge huko mjengoni wanapaswa wakupe "sapoti" kwa kuchangia hoja na wawe wazalendo wa kweli na wakali katika hili.

Mungu akujaalie katika harakati hizi.
Kuna wengine watakuwa na mawazo tofauti na ya kwako lakini wote wapokee, utafika muda wataelewa japo itawachukua muda. Hata leo kule DRC kuna watu ndio wanaanza kumuelewa Pat Lumumba.
 
Back
Top Bottom