Zitto nakupa wiki moja uondoke CHADEMA

Zitto nakupa wiki moja uondoke CHADEMA

Kifupi Zitto ana moyo mkubwa sana kubakia Chadema hadi leo hii na sielewi kwa nini maana Dr.Slaa aliondoka CCM na akapata Umaarufu zaidi Chadema, historia imetufundisha mengi sana. Kama ningekuwa mimi nisingesubiri hata siku moja maana chama hiki kimekuwa club ya Mpira na sii chama cha Siasa tena. Ujinga mkubwa unaendelea na sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu atakubali kupelekeshwa kiasi hiki..Najaribu kumwelewa Zitto, lakini sasa imefika mahala nadhani aijitoe mwenyewe na kujiunga rasmi ACT halafu mchezo uanze, sisi watazamaji tukanunue soda na Popcorn.
Hahahaha you wish....imechukua miaka,20,chadema kuwa chama kilichokomaa kama kilivyo...usitarajie,chama kilichoundwa,na wasaliti kwa ufadhili wa ccm kukishinda chadema kinachosimamia kanuni zake
 
Zitto Zuberi Kabwe aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini CHADEMA(sasa Mbunge wa Mahakama) nampa ‘‘grace period’’ ya wiki moja ya kufungaisha chochote alichobakisha katika ofisi yeyote ya CHADEMA(sijui kama vipo) na kuondoka. Upo CHADEMA ili iweje,hatukutaki!
Ulivyovimba kichwa ulidhani bila CHADEMA ungekuwa mwenyekiti wa PAC, ungekuwa mbunge wa Bunge la Katiba, ungejulikana kimataifa.
Tunazo sababu za kukulazimisha kuondoka CHADEMA kinguvu. Mbali na mikakati unayoifanya vichakani, lakini yapo haya ya wazi:-

1.Umehusishwa na njama za kutungua helkopta iliyotumiwa na katibu kipenzi chetu Dr.Slaa. Madiwani wa Shinyanga wamekuumbua. Hujakanusha ‘‘Silence means YES’’

2.Umehusishwa na mipango ya kubambikiza wanachama ugaidi. Kwa macho na masikio yangu nimekushuhudia Star TV ukiwa na Mwigulu Nchemba mkitangaza kuwa mna mkanda wa video ukionyesha vigogo wa CHADEMA wakipanga ugaidi. Nasema mkitangaza kwa kuwa yalipotamkwa haya na Mwigulu wewe ulikuwa pembeni yake, ukiwa kama Naibu Katibu Mkuu hukukanusha wala kuonyesha kukerwa na propaganda hizo zilizovuka mipaka. ‘‘Silence means YES’’

3.Katika mwendelezo wa kubambikiza kesi za Ugaidi ukaendeleza unafiki wako wakati Kamanda Lwakatare ‘‘Lwax’’ akiwa sero wewe ulikiandikia barua chama kwamba kijiweke mbali na kesi ya Lwakatare, bishaaa. Nikuulize wewe Msaliti Mkuu yupo wapi Lwakatare?

Kama hutaki kufungaisha virago tupe sababu za msingi kwa nini unaona ubaki kuwa mwana CHADEMA. Imebidi nifikishie ujumbe wangu kwa MM na ACT nzima
My Take:-Makamanda na wapenda mabadiliko wote niungeni mkono katika hili. Mods msifute, kama inawauma muiteni aje ajibu kwa nini tusimfurumushe

Acha kumtumia zitto kupaka umaarufu Wa
JF
 
Teh teh teh! ukimya wa Zitto unawatesa sana maboya! a.k.a akili ndogo. Zitto hawez kujibizana na mjinga kama wewe! angalau angekua Slaa! wewe ni kamdudu kadogo tu kanakohitaji kuuwawa kwa ukucha tu bila hata kutumia nguvu. Zitto ni level nyingine hata MAGAMBA wanajua hilo.
 
Kifupi Zitto ana moyo mkubwa sana kubakia Chadema hadi leo hii na sielewi kwa nini maana Dr.Slaa aliondoka CCM na akapata Umaarufu zaidi Chadema, historia imetufundisha mengi sana. Kama ningekuwa mimi nisingesubiri hata siku moja maana chama hiki kimekuwa club ya Mpira na sii chama cha Siasa tena. Ujinga mkubwa unaendelea na sidhani kama kuna mtu mwenye akili timamu atakubali kupelekeshwa kiasi hiki..Najaribu kumwelewa Zitto, lakini sasa imefika mahala nadhani aijitoe mwenyewe na kujiunga rasmi ACT halafu mchezo uanze, sisi watazamaji tukanunue soda na Popcorn.

mkuu Mkandara unaweza kunikumba how long umeanza kuiombea cdm mabaya?kitambo sana,unasogeza tarehe tu
 
Zitto ni mzito siyo mwepesi kama mnavyodhani jipangeni sawa sawa mkishindwa kujipanga ipo siku mtajibeba mapema kabisa.
 
Zitto hayuko CHADEMA yuko mahakamani kusubiria kiinua mgongo cha ubunge.

Eti kanajidai hakataki posho! Nyooooo, mbona uliililia mahakama ikusaidie kubaki na ubunge! Umaarufu kuujenga ni kazi lakini kuporomoka ni kugusa tu, jamaa hana bao tena!!!
 
mkuu Mkandara unaweza kunikumba how long umeanza kuiombea cdm mabaya?kitambo sana,unasogeza tarehe tu
Mkuu kwanza nikupe pole kwa kujaa upepo juu ya zitto ukitaka kujua ukomavu wa mtu ni pamoja na kumeza mambo kama anavyofanya zitto mmemchokoza mkashindwa kila mnalofanya yupo kimya nadhani mnawaza sana juu yake huyu ndiyo zitto bwana poleni sana.
 
Wamepanga kuondoka kwa awamu, katika mkakati mahususi wa kudhoofisha chama, kwa hiyo anasubiri wakati muafaka ili akiondoka na hao aliowarubuni, chama kitikisike. Zinaitwa POLITICAL MACHINATIONS.
 
Haya mnayafanya kwa lengo gani hasa, kwa kufikiria nini, kwa ajili ya nini au nani?????
Mbona mnafanya chama kizidi kuonekana cha ovyoovyo tu????
Watu ''wa maana'' wanaondoka na kuacha uanachama/ufuasi/ushabiki na kadhalika lakini ninyi mnapongezana kwa kelele zenu wenyewe na kuendelea kuamini mnazidi kukua. Wakati fulani kijana alikuwa anajisikia proud kusema yeye yuko CHADEMA, leo hii ni wangapi wanajisikia fahari tena??? Kimekuwa chama chenye sifa nyingi za ovyoovyo!

From the far corner!
 
Haya mambo kama huyajui ni bora ukajikalia kimya tu , zitto hana uwezo wa kushindana na cdm ,kama unabisha muulize wasira au zoka .
Hata kama hana uwezo mmezidi sana mdomo kiasi kwamba sasa mnachosha. Ni sawa na mtu alolewa pombe anaongea hovyo usiku kucha.
Na nawaambieni kabisa kwamba Zitto akijiondoa rasmi Chadema na kuingia ACT, moto wa kisiasa utaripuka na utaona jinsi Chadema itakavyosambaratika maana sasa imefikia kuwa Chadema ina watu wake wanaoaminika - Chama cha Mpira, mnachosha sana hata kuwasikiliza!
 
Hata mimi najua Zitto ni mnafiki, lakini mijitu inakuja humu inaongea pumba, eti tunamuhofia, tutamuhofiaje msaliti? na ulitaka akae CDM kwa lipi wakati unajua anavuruga Zzk alishaharibu. alijijengea heshima kubwa kabla hajaanza kuwa ndumila kuwili lakini mara tulipomgundua kuwa natumika kiukweli tumemchoka ni bora aende akawe mwenyekiti taifa wa act. Nenda hatukuhitaji.
 
Zitto tupu kichwani,kweli hayawani,
Akili zipo kwapani,Zito punguani,
Sura kama nyani,haso na aibu usoni,
Zito toka chamani,cdm mfukuzeni

Zito cdm hatufai,kama mavi chooni,
Sasa chadema bai,we kwako jalalani,
Sura kama kalai,afadhali hata nyani,
chadema hutufai,msaliti ewe mfitini,

Fuata akina stela,binti mwampumbu,
Mwezio Yule taila,cdm sio mbumbu,
Zito tena ----,cdm usitujazie mbu,
Zito hufai kanisani,hufai ata msikitini


Na malenga wenu. MANGUNGO

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums
 
Kuna nyakati unaweza ukamsema mtu vibaya na kuzusha kila aina ya uovu juu yake ila watu wasiamini hata moja na kumwona mzushi kama punguani
 
Zitto tupu kichwani,kweli hayawani,
Akili zipo kwapani,Zito punguani,
Sura kama nyani,haso na aibu usoni,
Zito toka chamani,cdm mfukuzeni

Zito cdm hatufai,kama mavi chooni,
Sasa chadema bai,we kwako jalalani,
Sura kama kalai,afadhali hata nyani,
chadema hutufai,msaliti ewe mfitini,

Fuata akina stela,binti mwampumbu,
Mwezio Yule taila,cdm sio mbumbu,
Zito tena ----,cdm usitujazie mbu,
Zito hufai kanisani,hufai ata msikitini


Na malenga wenu. MANGUNGO

Sent from my BlackBerry 9900 using JamiiForums

hivi kuna chama gani cha siasa kina mchukia mtu namna hii?

you guys you are after money!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom