Zitto Zuberi Kabwe aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini CHADEMA(sasa Mbunge wa Mahakama) nampa grace period ya wiki moja ya kufungaisha chochote alichobakisha katika ofisi yeyote ya CHADEMA(sijui kama vipo) na kuondoka. Upo CHADEMA ili iweje,hatukutaki!
Ulivyovimba kichwa ulidhani bila CHADEMA ungekuwa mwenyekiti wa PAC, ungekuwa mbunge wa Bunge la Katiba, ungejulikana kimataifa.
Tunazo sababu za kukulazimisha kuondoka CHADEMA kinguvu. Mbali na mikakati unayoifanya vichakani, lakini yapo haya ya wazi:-
1.Umehusishwa na njama za kutungua helkopta iliyotumiwa na katibu kipenzi chetu Dr.Slaa. Madiwani wa Shinyanga wamekuumbua. Hujakanusha Silence means YES
2.Umehusishwa na mipango ya kubambikiza wanachama ugaidi. Kwa macho na masikio yangu nimekushuhudia Star TV ukiwa na Mwigulu Nchemba mkitangaza kuwa mna mkanda wa video ukionyesha vigogo wa CHADEMA wakipanga ugaidi. Nasema mkitangaza kwa kuwa yalipotamkwa haya na Mwigulu wewe ulikuwa pembeni yake, ukiwa kama Naibu Katibu Mkuu hukukanusha wala kuonyesha kukerwa na propaganda hizo zilizovuka mipaka. Silence means YES
3.Katika mwendelezo wa kubambikiza kesi za Ugaidi ukaendeleza unafiki wako wakati Kamanda Lwakatare Lwax akiwa sero wewe ulikiandikia barua chama kwamba kijiweke mbali na kesi ya Lwakatare, bishaaa. Nikuulize wewe Msaliti Mkuu yupo wapi Lwakatare?
Kama hutaki kufungaisha virago tupe sababu za msingi kwa nini unaona ubaki kuwa mwana CHADEMA. Imebidi nifikishie ujumbe wangu kwa MM na ACT nzima
My Take:-Makamanda na wapenda mabadiliko wote niungeni mkono katika hili. Mods msifute, kama inawauma muiteni aje ajibu kwa nini tusimfurumushe