Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Zitto Kabwe: Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela

Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Rais Magufuli kusamehe wafungwa ambao ni wanamuziki mashuhuri, Nguza Viking (Babu Seya) na mwanaye 'Papii Kocha'.

Tangu utangazwe msamaha huo, Zitto amekuwa akiandika na kutoa kauli zinazoonesha kupingana na jambo hilo licha ya Rais kuwa na mamlaka kikatiba kumsamehe mfungwa yeyote akiona inafaa..

Miongoni mwa kauli zake huko Twitter;

"I have read judgement that convicted Babu Seya and son. And judgements at the high court appeal, appeal at court of appeal and petition at African Court. I am appalled by decision to pardon convicted rapists. Devastated by statements to congratulate such a decision" ZZk.

"Waliozomea na kuzodoa ahadi ile walikuwa sahihi. Wanaomzomea Rais kwa kutoa msamaha wapo sahihi pia. Hakuna sababu kuzodoana. Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela" ZZK.
zito pambana n hali ya chama chako kinakufa....uanishia kupiga makelele yasiyo na faida
 
Hivi Mwenyekiti wa ACT kwasasa ni nani? Manake nasikia mara "mwenyekiti" ambaye ni tofauti na "Kiongozi Mkuu wa Chama".... Hata sielewi!!!! [HASHTAG]#Zittojengachamachako[/HASHTAG]!
 
Kwani huyo Zito yeye aliwaona kipindi wanabaka, inawezekanaje familia nzima wawe wabakaji, ina maana familia yote wanafanana tabia na hakuna hata mwenye busara.
Yeye apambane na hali ya chama chake na aache kudandia matukio.
Umekoment vizuri.......ila najaribu kutafuta comment yako katika Uzi wa tarehe 11/01/2017 uliopostiwa na technically wenye kichwa "he babu seya haweI kusamehewa?''
 
Everyday comes with a new scene. I love Tanzania my BEST POLITICAL ARENA in the world.
 
Zitto anako elekea ni kufungwa kamba maana kila muda unapoenda anazidi kuyeyuka
 
Katika j amii zinazojali utu wa mtu na zaidi, usalama wa watoto, kama hawa walivyoachiwa, wangewekwa katika mazingira ya kufuatiliwa nyendo zao, na jamii inayowazunguka kutahadharishwa uwepo wao ili wawachunge watoto wao wasiwe wahanga wa watu hawa.
 
Mbunge wa Kigoma Mjini kupitia ACT Wazalendo, Zitto Kabwe ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Rais Magufuli kusamehe wafungwa ambao ni wanamuziki mashuhuri, Nguza Viking (Babu Seya) na mwanaye 'Papii Kocha'.

Tangu utangazwe msamaha huo, Zitto amekuwa akiandika na kutoa kauli zinazoonesha kupingana na jambo hilo licha ya Rais kuwa na mamlaka kikatiba kumsamehe mfungwa yeyote akiona inafaa..

Miongoni mwa kauli zake huko Twitter;

"I have read judgement that convicted Babu Seya and son. And judgements at the high court appeal, appeal at court of appeal and petition at African Court. I am appalled by decision to pardon convicted rapists. Devastated by statements to congratulate such a decision" ZZk.

"Waliozomea na kuzodoa ahadi ile walikuwa sahihi. Wanaomzomea Rais kwa kutoa msamaha wapo sahihi pia. Hakuna sababu kuzodoana. Tukemee wabakaji kusamehewa kiholela" ZZK.

Mahakama inaweza kutoa hukumu sawa ila yawezekana kulikuwa na hila..duuuh yani familia nzima baba na watoto wote wanabaka watoto mmmmh
 
Nawahurumia Sana watoto
Waliobakwa na hao mabaradhuri
Magu kataka spate political support ambayo anaipoteza kila siku
 
Hii awamu ya tano wanaopeta ni type ya mheshimiwa Manenepa, Zitto anasomeshwa namba ile kinoma.

Wamesamehewa wauaji ambao hukumu zao zilisomwa na majaji wa mahakama hiyo hiyo iliyowatia hatiani Nguza na mwanae, nini cha ajabu kilichopo kwenye msamaha wa rais?.
 
Siwezi kumwamini Zito wa sasa.Zito alikuwa zamani.
Tatizo analopata Zito ni kuwa, wale walokuwa wa karibu wake walikuwa mapandikizi chama cha majuha. Ushauri walokuwa wakimpa kumbe ulikuwa uchochezi. Kagombanishwa na wenzie katika mapambano, walokuwa wapambe wake walikuwa nuksi tupu na sasa karibu wote wesharudia magamba yao.
Kwa sasa kapoteza "bearing" hana hakika kama yuko mbinguni au duniani. Anachohitaji ni pumziko la kujitafakari. Ninaamini kuwa Zito bado ni Kijana mzuri na akitulia anaweza akarudi njia kuu na imara katika upinzani. Amen
 
badala ya kumjadili zitto tujadili hoja aliyotoa siku zote tumekuwa tukipiga kelele wabakaji wapewe adhabu kali lakini inapoonekana wanaofanya hivyo ni watu wenye infuluence kwa jamii tunabadilika sasa tujiulize ni kweli tunachukia ubakaji au tunataka watu wa aina fulani ndio waadhibiwe kwa ubakaji
 
Samehe mara 7 -70...mwisho wa siku muhukumu wa kweli ni Mungu mwenyewe.

Ukiniuliza adhabu ya mbakaji iweje ningekwambia na yeye abakwe lakini sheria ikaweka adhabu ya kifungo.
JPM hakubakwa na hao kina babu seya, hiyo samehe 7*70 hai apply, laiti kama wale waathiriwa wangesema tumewasamehe hapo sawa. There is no place for sex predators and pedophiles in the society, they belong behind bars.
 
Hawa watu (Babu Seya na mwanaye) tayari walikuwa wameshatumikia sehemu kubwa ya adhabu yao. Sehemu ndogo tu ndiyo ilikuwa imebaki ambayo kwa Babu Seya ni takribani 3 years na kwa Matonya 1 year as per expert medical assesment. Hivyo rais kwa maombi ya majority including minority chadema, na kwa mjibu wa mamlaka aliyopewa na katiba amewasamehe hiyo sehemu ndogo ya adhabu iliyokuwa imebakia. Of course Zitto ambaye anatapatapa kutafuta dawa ya kuponyesha kachama kake kaliko ICU, anafikiri kapata dawa. Ukiwa na mgonjwa ICU lakima uchanganyikiwe akili. Pole sana Zitto, endelea kutafuta dawa. Hii uliyoipata siyo dawa na inaweza kuwa sumu.
 
Miaka 14 waliyokaa jela kama kuna watoto waliobakwa sasa watakuwa wamezidi miaka 18. Kama ni hivyo je haitakuwa jambo jema sasa wajitokeze watuambie kama kweli au magumashi? Maana sijawahi kumwona hata mmoja ambaye amejitokeza kusema Babu Seya na wanawe walimbaka. Maana huu ni wakati muafaka tuwaone ili tuwe na cha kuzungumza, vinginevyo kesi ilikuwa fake.
Halafu hili swala la kubakwa na kulawitiwa tena watoto wengine class 1. Najaribu kuwaza kwamba ikiwa MTU mzima hawezi kuhimili the first time, hivi mtoto si anakufa kabisa? Kweli maumbile Yale yaweze kuhimli MTU mzima halafu azoee kabisa? Najaribu tu kuwaza huko kubakwa na kulawitiwa. Ingekuwa kunajisiwa hapo ningeweza sema inawezekana. Sijui lakini ILA omba sana wewe mwanaume yasikukute haya maana ni mazito mno. Mimi nshawahi kusingiziwa na vibinti kuwa nilivitaka kimapenzi kisa vilinikosea. Vilinidhalilisha sana na kidogo yanipate yakunipata maana watu walishalishikikila kidedea lakini Mungu alisimama upande wangu.
 
Yaani wajitokeze waseme ni KWELI TULIFIRrWA?? SAHAU.

Kinachovuta na kuchanganya watu ni kesi yenyewe kuwa kama ilikuwa shinikizo tuko nyuma ya pazia kiasi kwamba hata ushahidi ulikuwa wenye utata. Kwa ujumla ninachoona hapa ni uhuru wa mahakama kuingiliwa, kesi hii ilijenga hisia kwamba mahakama ilipewa maelekezo jinsi ya kuhukumu hiyo kesi. Hii kelele unayoona sasa ya kwamba rais kafanya sawa ama la ni matokeo ya kesi yenyewe kuwa katika hisia za kisiasa.
 
Zee la DRAMA/MASIFA na MAKIKI limekaa muda bila KUSIFIWA, Likaona liyasake MASIFA. Nchi imeangukia kwa JITU SHAMBA, LIMBUKENI, PENDA SIFA, AKILI NDOGO ila linajifanya MUCH KNOW. Ni Mungu tu atusaidie
 
Huu yamkini ni ushahidi tosha kuwa ile kesi jamaa walibambikwa tu,wakuu wanajua na walikuwa kimya maana yamkini aliyembambika alikuwa mkuu mwenzao,wamekuwa wanaumia mioyoni,maana km kweli alitenda unyama ule kwa watoto aisee alipaswa siyo kufungwa ni kunyongwa,mnasameheje mbakaji,anachoongea zitto wenye akili ndogo hawawezi kujua anamaanisha mini,hilo ni dongo kwa double standard ya matendo ya serikali na ni kuwaambia waache udhalimu,unauaminisha umma kuwa jamaa mbakaji sugu unamfunga halafu unakuja kumuachia mbakaji
 
Back
Top Bottom