Hivi kwanini zitto hashiriki m4c? Yeye namuona yupo kivyake tu..
yeye ana m4allstars yake, yani movement for allstars (yani kufanya miziki ya kanda za tanzania) kama kigoma all stars, moro all stars nk zinakuja,
Hivi kwanini zitto hashiriki m4c? Yeye namuona yupo kivyake tu..
Sasa tatizo liko wapi mbona makubwajinga hayaishi majunguu kuwa mwanasiasa sio et ndo uchukie mtu wa chama kingine wote watz upande wangu hakuna tatizo. cdm m4c daima.
Haka kajamaa nika**** sana,kanategea kuimalisha chama,kina slaa wanahangaika na m4c then baadae kaje eti nataka kuwa raisi..hapo kamekwenda kuuza dili kwa mwislamu mwenzie,hatudanganyiki.
Hawamwezi Zitto watabaki kumwangalia tu,halafu watu bwana hawajiulizi kwanini wamechemka kumtimua? Aliyonayo Yao mnaweza kihama chadema bure ni hatariiii!!! Bora wakae kimya tu maana Kila mtu lazima atahama chadema!!!! So ni kweli watu waache ushabiki wa vyama humu!!!Ningefurahi (na kuamini) kama shutuma zote anazotupiwa Kabwe zingetoka au angalau kuthibtishwa kutoka safu ya uongozi wa CHADEMA.
Kama yote hayo ni kweli, kwa nini uongozi wa CDM unaendelea kuwa naye? Kama ni msaliti wa chama, kwa nini hawamtimui mara moja? Wanamng'ang'ania kwa faida ya nani? Tuacheni ushabiki na siasa za maji taka!
Ni kweli kabisa...sijui kwanini people trust this guy....i dont trust him a single bit
slaa amekuwa akiishi na mke wake wa ndoa mama rose kamili,slaa akiwa mbunge wa chadema na katibu mkuu wa chadema huku mke wake wa ndoa akiwa diwani wa ccm na wamekuwa wakilala pamoja na kula pamoja lakini hilo mashabiki wa cdm hawalioni bali wanaona tatizo zitto akiwa msibani na kikwete!
Mkuu KIM KARDASH karibu tena. Vipi ulikuwa Segerea ya JF manake ni muda! Hivi Zitto yupo kwenye ujumbe wa Rais au ni binafsi. Kama ni ujumbe wa Rais basi huenda anawakilisha bunge au vyama vya ulinzani. Hivyo basi ana baraka
Hivi amekwenda naye kama mshkaji tu ama ni kwamba amewakilisha upinzani?
Zito kawakilisha wapinzani, sio mbaya kwenda kwenye msiba, mbaya kama alipanda ndege ya Raisi ambayo tunalia inatumaliza walipa kodi.
Inawezekana amekwenda kama sehemu ya ujumbe wa Tanzania kutoka vyama vya upinzani. Nadhani wenzake huko CDM watakauwa na taarifa.
Mbowe na Sugu wako marekani wanafanya matamasha ya muziki sugu anaimba mbowe ni DJ wake.
Hawamwezi Zitto watabaki kumwangalia tu,halafu watu bwana hawajiulizi kwanini wamechemka kumtimua?
Mnatoa povu sana humu! Hata Mbowe anajua who is ZZK.. Go go goooo my president to be
Kwani kufanya kazi za kitaifa ni kosa. Kwa mawazo yako, kwa vile ni Mbunge wa CHADEMA basi hatakiwi afanye shughuli za kitaifa. Kwani hujui kama ni mwakilishi wa wananchi. Mawazo kama haya ni matokeo ya mbegu iliyopandikizwa ya chuki kwa tofauti ya kimawazo na kiitikadi. Kwani mpaka awepo kwenye M4C ndiyo uone kama anafanya kazi. Think bigger
Uko sahihi TUMBIRI Mkuu, hilo ndio tulipaswa kulielewa kabla ya kuanza mipasho na uchochezi ambao hauisaidii CDM! Kama Great Thinkers, ikiwa kweli ni Great Thinkers, tungepaswa kuwa na uhakika wa kila tunachokisema badala ya kuigeuza JF kuwa kijiwe cha mipasho.Wakuu heshima mbele,
Hoja ya Zitto kuwakilisha Upinzani ina mashiko lakini hoja nyingine inaibuka ni nani amemtua kuwakilisha upinzani? Maana tunavyojua ki Protocal ilipaswa Ikulu iiombe ofisi ya Spika Mbunge mmoja kutoka kambi ya Upinzani ashiriki kwenye msiba kwa niaba ya upinzani. Hata hivyo, Spika nae asingekuwa na mandate ya kuteua Mwakilishi kutoka kambi ya Upinzani. Ilipaswa ashushe dokezi chini hadi kwenye Ofisi ya Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani ndiye ateue Mbunge wa Kuwakilisha.
Sasa kama Jina la Zitto limetoka moja kwa moja kutoka Ikulu lazima watu wahoji. Kunani Zitto? Kwa nini asiwe Lissu au Nassari au Silinde au Wenje nk? Je uteuzi wa Zitto kwenda Ethiopia ulikuwa na baraka za Ofisi ya Spika na Kiongozi wa Upinzani? Haya ndiyo maswali ya kujiuliza, Mimi, wewe na wengine.
TUMBIRI (PhD in Progress at HULL, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(UDSM), PCM(Mzumbe High School - 2[SUP]nd[/SUP] Overall Best Student in Form Six National Exams)
tumbiri@jamiiforums.com
Hata kama amekwenda mwenyewe kama Zitto, bila ya hata kuwakilisha jimbo lake, kuna ubaya gani?Wakuu, nasikitika kusema kwamba wana JF wengi waliochangia uzi huu wamechangia kwa jazba, wengine kwa kuunga mkono na wengine hata kwa kupongeza.
Lakini mtoa mada amekuja kwa kutoa taarifa ya uwepo wa Mhe. Zitto katika msafara wa Mhe. Rais kuelekea katika mazishi ya Mhe. Zenawi, lakini pia ameongeza na swali, hii imekaaje?
Matarajio yangu yalikuwa, wana JF wangekuja na ushahidi wa aidha CDM imemruhusu akiwakilishe au kajiamulia mwenyewe nk.
Sasa majibu kama siasa si uadui, anafanya kazi ya kitaifa au anachukua uzoefu na mengine kama hayo yanatoka wapi?
Tafadhali mwenye taarifa kamili atujuze, amekwenda kwa baraka za nani? Bunge, Serikali, CDM, Jimbo lake au binafsi?
Hata kama amekwenda mwenyewe kama Zitto, bila ya hata kuwakilisha jimbo lake, kuna ubaya gani?
yaya, mimi sio msemaji wa CDM, nipo na maswali kama wewe. Nilichotaka kusema ni kuwa sioni ubaya wa Zitto kuhudhuria mazishi hata kama amejiendea kwa matakwa na/au mijisifa yake mwenyewe, kwani katiba yetu inamruhusu kila Mtanzania kwenda anakotaka na kukutana na anaotaka, halmuradi havunji sheria za nchi.Mkuu, bado hujajibu swali. Au ndivyo kama wanavyosema wajuaji kwamba m-Tz ukimwuliza swali atakujibu kwa swali badala ya jawabu!?
yaya, mimi sio msemaji wa CDM, nipo na maswali kama wewe. Nilichotaka kusema ni kuwa sioni ubaya wa Zitto kuhudhuria mazishi hata kama amejiendea kwa matakwa na/au mijisifa yake mwenyewe, kwani katiba yetu inamruhusu kila Mtanzania kwenda anakotaka na kukutana na anaotaka, halmuradi havunji sheria za nchi.