Zitto Kabwe, ndani ya Addis na JK

Hakubaliki kwa sababu aligombea uenyekiti wa chadema taifa2009 na kumpinga mkurugenzi wa chagga development manifestal na pia anahoji kwa nini chama kinaendeshwa kikampuni zaidi mpaka uwe mchaga ndo unatapa nafasi

Acha ukabila wewe! Jina zuri mawazo ya ki-ukabila. ZZK ni makamu, je ni mchaga? Silaa ni Mchaga?
 

Kaka tumbili hapo chini ni cv au vitu gani?
 

Nakubaliana na wewe Radhia huyu jamaa ni MOLE [ Ndumila kuwili au kwa jina limgine KIKULACHO!!] wa ccm humo Chadema, the sooner he is flushed out the better!!
 
tatizo la zuberi zitto ndani ya chadema ni hilo jina lake.

Akaanzishe chama chake na mgoma mwenzie Kafulila ama sivyo atafulia kama mgoma mwingine aitwae Kaborou WALID ambae ccm ilimghilibu akili na sasa imemtosa!!
 
Tatizo la wachangiaji wengi wa Jamii forums wako biased na Zitto. Hamuangalii uhusiano wake na hao mnaowaita CCM ni wakati gani. Mbowe Sugu, lema wote wako nje ya nchi. Kaenda Zitto msibani mnahoji kutokuwepo kwakwe kwenye M4C. Mbona hamuwahoji hao wengine? Nyie ndio mnaofanya watu waone CDM ni chama cha Ukanda. Zitto angekuwa mnafiki angeichachafya serikali bungeni? Mnazungumzia unafiki kuhudhuria misiba? Nani atabisha kwamba unaposema wabunge wawili wanaoisumbua serikali ktk CDM lazima zitto yumo? Zitto ndio aliyeleta hamasa ndani ya CDM na kukipa umaarufu. Ana mchango mkubwa sana. Mlitaka aende Mnyika ndio muone amewakilisha CDM? Kweli waswahii husema 'kunyata anyate kinyonga, akinyata kicheche anavizia kuku'. Je mkijua kuwa chama ndio kimemteua kuwakilisha mtasemaje? Mwacheni kijana afanye anachofanya mnatakiwa kumuunga mkono. Je wale wabunge wa CCM walioenda na zitto Kigoma kwenye Leka Tutigite waliisaliti CCM? Kwani CCM haikujua kuwa wameenda na organiser ni CDM? Inamaana kwakuwa zitto ni CDM wangesusa? Hapa angalieni ushiriki wa mtu kwa jambo husika. By the way, siasa sio uadui. Nawakilisha.
 
Kichuguu,
Sijakuelewa rafiki yangu. Unamaanisha nini kuwa JK alishupalia makampuni ya madini? Si yeye aliyewaingiza akina Sinclair bongo?
 
Hivi yule "Zoka" ni wa ikulu?ama ni Ghondi?anyways RIP Zenawi.

Zoka ndo yupi kati ya hao kwenye picha? Kwani hawa watu hupenda kuficha sana nyuso zao hadharni, hapo alijianika wajanja wenzake wakamwahi.
 
Sizani kama ni sahihi kukandia kila jambo linalofanywa na Zitto. Kufanya hivyo tutakuwa hatumjengi ,ana mabaya yake na mazuri pia.Ameenda kutuwakilisha hivyo ni vyema tukapunguza hisia na chuki zenye mtazamo hasi.

are you sure MWAKALINGA Y.R
 
Last edited by a moderator:

Ni msaliti anajulikana wala hakuna wa kushangaa!!! Ananyemelea ukwe!!! Subiri tuone!!!
 

Mkwe mtarajiwa!!! Sasa niseme nini kama kweli mtu unajifanya eti hufungamani na upande wowote, Non-Alignment Movement (NAM). Is he a family member!!! kwa mtizamo wa Extendede family? To be revealed soon or later!!
 
Hujui kama Mhe. Zitto ni waziri wa Serikali kivuli. Yuko kwenye msafara wa Mhe Raisi kwa baraka za wananchi kama mbunge na waziri kivuli kupitia mihimili ya nchi.

Tatizo ni kuwa, kila jambo mnafikilia siasa siasa tu.

 
M4C movement for chaga na yeye ni muha wa kigoma sasa unataka akafanye nini huko?

Wewe hujui unalolisema kazi yako kuu ni ukabila usiokuwa na msingi! Kwa hiyo serikali ya sasa ya CCM ni ya wakwere? Pole sana kwa ujinga. Dr.Slaa, na wengine wengi ni wachaga?
 
wasiomfahamu zitto waendelee kumjadili ili kiukweli hapa hatuna mwanamapinduzi bali mwanaharakati ambaye urais unamtesa kuliko Mugonjwa wa tumbo la ku-drive
 
acheni majungu watoto wa mtei. mbona hamsemi ni kosa gani kafanya kwa kuhudhuria mazishi?

Siyo watoto wa Mtei ni watanzania PLEASE. Kuuliza si ujinga je kuna protocol labda au mwaliko rasmi? Pengine viongozi wa CDM wangetueleza kwa sababu katika hali ya kawaida viongozi wa upinzani hawaambatani na rais kwenye ziara zake za nje.
Hii ni mpya!
 

TUMBIRI (PhD in Progress at HULL, CPA(T), MBA(UDSM), Bcom(UDSM), PCM(Mzumbe High School - 2[SUP]nd[/SUP] Overall Best Student in Form Six National Exams)

tumbiri@jamiiforums.com


Mkuu TUMBIRI, nashukuru kwa kutufahamisha protocols kuhusu uwakilishi wa upinzani.

Quote yangu hiyo hapo juu inahusu hiyo signecha yako; mbona hukuweka Form 4, na darasa la saba? Nimejaribu kuona ambavyo signecha yangu ingekuwa iwapo ningefuata format yako, nikaona watu wasingeweza kunielewa.

Kichuguu

Executive MBA (in progress, expected in May 2013); P.E; MIEEE; MIET: Ph.D (Physics); Ph.D.(Engineering); M.S. (Math), M.Eng.Sc; B.Sc(Eng); Certificate of Service (JKT); Advanced Certificate of Secondary Education (PCM-Form 6); Certificate of Secondary Education (Form 4); Primary School Leaving Certificate (Std 7);
 
Sizani kama ni sahihi kukandia kila jambo linalofanywa na Zitto. Kufanya hivyo tutakuwa hatumjengi ,ana mabaya yake na mazuri pia.Ameenda kutuwakilisha hivyo ni vyema tukapunguza hisia na chuki zenye mtazamo hasi.

Siyo lazima chiki na mtazamo hasi bali hii inasababishwa na lack of transparency in our political and administrative systems. Kumbuka kuna wanaouliza kwa dhati kabisa ni katika misingi ipi Zitto anajumuika katika ziara hii ya rais. Hii ni kutokana na watu kukosa kueleweshwa kama taratibu za kiprotocol katika utawala wa CCM zinajumuisha vyama vya upinzani kwenye ziara za rais anaposafiri nje. There is clearly no framework to referred to concerning this issue.
 
ni nani huko CHADEMA asiyependa kuandamana na Rais KIKWETE? mbona hao wakubwa wake wa CHADEMA walimfata ikulu wakaambulia kupiga nae picha tuu!.. acheni wivu
 
Nilikuwa najiuliza. Sawa siasa sio uadui, lakni kwa vitendo CCM imefanya kwa wananchi Sidhani au siamini mtu mwenye kutaka mabadiliko anaweza kukaa benchi moja na CCM.
Nilijiuliza hivi Zitto leo apewe uraisi chadema, je anaweza kumshitaki Kikwete au wale watu wote waliofilisi nchi na kutufikisha hapa tulipo? Sidhani.
Pia nimeshangazwa na Zitto kujifanya anamjua Melews kuliko mtu yeyote wakati hajui lolote kuhusu siasa za ethiopia.
Ni sawa na mtu burundi amsifie kikwete wakati hajawahi kujua kiundani siasa za tanzania na kikwete mwenye.
Kumwita melews hero, glorify melews Nathan its a sin. Wacha wafu wazike wafuu wenzao.
Ushauri;Zitto ni mtu hatari, mnafiki, Ibilisi na mwongo. Kuna haja kumtafuta kwa hali na mali na kummaliza kisiasa maana ni maafa na msiba wa tanzania.
Kingine nashauri vijana wenzangu, achaneni na ushabiki wa CDM. Tutumie CDM kutafuta mabadiliko tunayoyataka sisi na sio vile wanayotaka CDM kama chama. Pamoja sijamwongelea Mbowe,yeye na Zitto hawfa. Hamniamini tusubiri tuone.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…