Zitto Kabwe, ndani ya Addis na JK

Zitto Kabwe, ndani ya Addis na JK

Hivi kwanini zitto hashiriki m4c? Yeye namuona yupo kivyake tu..

Mi naona tatizo ni ninyi wala siyo Zitto. Kwa nini mnakua na wawazo hasi kila wakati? Hilo litakuja kuangamiza CDM siku za mbeleni coz tunakua na wanachama ambao hawataki kufikiri kwa mapana na kuwa na mawazo chanya. Kila wakati mawazo hasi tu. Mi sidhani kama Zitto atakua amekurupuka bila kuwaaga viongozi, na M4C haimtegemei Zitto. Bila Zitto M4C itakuwepo na matokeo tutayaona. Acheni kupandikiza chuzi binafsi, hizi hazijengi bali zinabomoa CDM. Kama unaleta hoja zako hapo, njoo na data kamili kwamba ameondoka bila kuaga na viongozi wake hawajui alipo na amegoma kuja Morogoro. kama ni fitna hatuzitaki na Mkome kukifuata fuata CDM, nyie mmetumwa kabisaaa wala sio Zitto!
 
amekutuma uje umtete,basi atakuwa mnafki kidoma ampigie kampeni dhaifu na yeye mwenyewe,ubungo ampigie kampeni mnyika.

ungetumia kiswahili tu ndugu yangu ningekuelewa kirahisi zaidi kuliko hiyo lugha unayotumia,husomeki,andika tena kwa kiswahili lakini sio kilugha.
 
Alijipigia kampeni mwenyewe za urais?ugombea binafsi?ama una maanisha alijipigia kampeni za ubunge?swali langu kama hukulielewa,lilihusu kampeni za ugombea urais,ni kweli alimkampenia JK?ama ni uzushi tu?
 
Last edited by a moderator:
wana forum tuwe na tafakuri za kina. viongozi wa vyama vya kisiasa ni viongozi wa kitaifa. licha ya tofauti za kisiasa, wanafaa kuheshimiwa na wanasiasa wote.

siasa siyo uadui. miezi miwili iliopita, lissu alikwenda na msafara wa spika ktk nchi za korea, japan........
prof kahigi alisafiri na jk pia. zitto kaenda na jk kwa mwaliko kutoka ikulu wakiwaandikia chdm kutoa muwakilishi atakae ungana na msafari wa rais kwenda ethiopia kuhudhuria maziko ya zanawi. zitto hajadandia msafara. ana baraka zote za chdm. msidhani mtu hujiunga na msafara bila ya mawasiliano ya awali kutoka ikulu na chama husika.

ukiangalia hiyo picha, utaona yupo pia haroun suleiman kutoka serikali ya znz, yupo lusinde wa ccm nk........

tuwe waungwana. zitto ninaemjua na uzalendo wa hali ya juu. sera yake ni TANZANIA KWANZA VYAMA BAADAYE. KWA WENGINE chama kwanza tanzania baadaye. hii ndiyo sababu inayomfanya zitto watu wengi wasimuelewe.

tutumie bongo zetu kujenga hoja siyo kufuata mkumbo!!!!!!!!!!!
 
Tatizo la wachangiaji wengi wa Jamii forums wako biased na Zitto. Hamuangalii uhusiano wake na hao mnaowaita CCM ni wakati gani. Mbowe Sugu, lema wote wako nje ya nchi. Kaenda Zitto msibani mnahoji kutokuwepo kwakwe kwenye M4C. Mbona hamuwahoji hao wengine? Nyie ndio mnaofanya watu waone CDM ni chama cha Ukanda. Zitto angekuwa mnafiki angeichachafya serikali bungeni? Mnazungumzia unafiki kuhudhuria misiba? Nani atabisha kwamba unaposema wabunge wawili wanaoisumbua serikali ktk CDM lazima zitto yumo? Zitto ndio aliyeleta hamasa ndani ya CDM na kukipa umaarufu. Ana mchango mkubwa sana. Mlitaka aende Mnyika ndio muone amewakilisha CDM? Kweli waswahii husema 'kunyata anyate kinyonga, akinyata kicheche anavizia kuku'. Je mkijua kuwa chama ndio kimemteua kuwakilisha mtasemaje? Mwacheni kijana afanye anachofanya mnatakiwa kumuunga mkono. Je wale wabunge wa CCM walioenda na zitto Kigoma kwenye Leka Tutigite waliisaliti CCM? Kwani CCM haikujua kuwa wameenda na organiser ni CDM? Inamaana kwakuwa zitto ni CDM wangesusa? Hapa angalieni ushiriki wa mtu kwa jambo husika. By the way, siasa sio uadui. Nawakilisha.

Mkuu waambie hao wasio jua/fahamu nini maana ya SIASA na MAHUSIANO MEMA ktk JAMII,na hata NCHI JIRANI.Si kila AINGIAE BAR MLEVI.ZZK ni TUNU na wala si MNAFIK na HANA SABABU YA KUWA MNAFIKI WA KISIASA!
 
WAKUU!

Namshangaa huyu Mh. Zitto Z. Kabwe. Wakati wa mkutano wa M4C Morogoro tuliambiwa angehudhuria. Baadae mawasiliano kati yake na Makamanda waliokuwa kwenye harakati za ukombozi yakapotea. Leo hii katia timu Addis na Mkulu.

Makamanda, hii ime kaa je? wakati Makamanda wengine wakiendeleza harakati za kuwakomboa waTanzania huyu Mh. mbona yupo beneti na Magogoni sana?

Ni kuuliza tu Makamanda.

Acha UZUSHI na SIASA za KI MEMKWA!
 
Umaskini mbaya kaliko wote ni umaskini wa mawazo. Zitto kaenda msibani kuwakilisha chama, hili nalo linahitaji uwe na degree kufikilia????????????
 
Mimi nathani ingekuwa vizuri kama ungefanya kauchunguzi kidogo ili kubaini kama aliondoka kwenda ADdis bila baraka ya viongozi wake. Aidha, ikumbukwe kuwa CDM nayo ilikuwa na haki ya kuwakilsishwa katika msiba huo. Huenda Zito katumwa na viongozi wake kuwakilisha chama chake katika msiba huo. Sasa kosa liko wapi kama atakuwa amepata idhini ya viongozi wake. Aidha, hata kama ameteuliwa na Serikali kufuatana na Rais, sio vizuri kupinga kila jambao linalofanywa na na Seikali hata kama ni zuri, Serikali ikifanya jambo zuri kama ambavyo majambazi wanashughulikiwa siku hizi, ipewe hongera zake, ikifanya vibaya, ikosolewe.
 
Atatumia njia kama ya JK huko chadema kwenye urais.
dr silaa angekuwa anatupigania uhuru kama nyerere, tunge upata lakini tunge mwaga damu, jamani chadema tuna hoja za msingi kweli kweli, lakini tusifikie hatua hii. tutambue kua uadui wa kisiasa sio uadui wa kushiriki katika mambo ya kijamii !
 
Zitto anaanza kujenga mazingira ya kurejea nyumbani kama mwenzake Kaboro. Hawa jamaa ni wa hovyo sana na wana tamaa ya madaraka hakuna mfano. Ukitaka kujua Zitto ni pandikizi jiulize ni kwanini hakukanusha vilivyo tuhuma za uhusiano wake na Zoka ambaye anadaiwa kumteka Ulimboka. Badala ya kujitetea serikali iliamua kulifungia gazeti la Mwanahalisi. Zitto na Kikwete wote ni wasanii na wapenda madaraka hata kama hawana uwezo na hayo madaraka.
wewe ni mwanaitikadi wala sio mwanasiasa ndo maana unamuungunisha Zitto na kikwete, Zitto amewakilisha cdm na wananchi wa tz, na sio itikadi, kwani kule hajaenda kuswali au kuongoza ibada, ameenda kwenye mazishi. kuwa mwelewa wewe ndg, vinginevyo watu watakushangaa sana tena sana. Pole.
 
dr silaa angekuwa anatupigania uhuru kama nyerere, tunge upata lakini tunge mwaga damu, jamani chadema tuna hoja za msingi kweli kweli, lakini tusifikie hatua hii. tutambue kua uadui wa kisiasa sio uadui wa kushiriki katika mambo ya kijamii !
ndo mkombozi mnayemfagilia kila kukicha, yaani hata akijisaidia njiani mtasema zoa kwa sababu anatoka kanda ya kasakzi. isitoshe Zitto ana busara hata ya kuyaendea mambo, watu wanaleta ushabiki tu wa kumusakama zitto eti kwa sababu ana dhamira ya kugombea urais hicho tu ndo kinachowatoa roho cdm na sio kingine, kwa sababu mnataka mchaga na familia yake yote watawale nchi ila sio kabila lingine kama zitto, kwa taarifa yenu kumjadili sana zito ndo mnampa chati zaid na nyie kujishushia hadhi.
 
Mi naona tatizo ni ninyi wala siyo Zitto. Kwa nini mnakua na wawazo hasi kila wakati? Hilo litakuja kuangamiza CDM siku za mbeleni coz tunakua na wanachama ambao hawataki kufikiri kwa mapana na kuwa na mawazo chanya. Kila wakati mawazo hasi tu. Mi sidhani kama Zitto atakua amekurupuka bila kuwaaga viongozi, na M4C haimtegemei Zitto. Bila Zitto M4C itakuwepo na matokeo tutayaona. Acheni kupandikiza chuzi binafsi, hizi hazijengi bali zinabomoa CDM. Kama unaleta hoja zako hapo, njoo na data kamili kwamba ameondoka bila kuaga na viongozi wake hawajui alipo na amegoma kuja Morogoro. kama ni fitna hatuzitaki na Mkome kukifuata fuata CDM, nyie mmetumwa kabisaaa wala sio Zitto!

Umesema sawa kabisa. Ili chama kiwe chama, lazima kijenge uwezo wa kujiendesha beyond powers of individuals.
 
napata wasiwasi kama majibu ya ngwilizi hayata chakachuka kumpa favour swahiba wa rais.
 
Mh!Hapo ni Ikulu kweli?Mbona inaonekana kama jengo ambalo hata halijaisha?
Naona hata wiring yake wire zimepita nje!Au walikaribishwa stoo ya ikulu?
 
Mh!Hapo ni Ikulu kweli?Mbona inaonekana kama jengo ambalo hata halijaisha?
Naona hata wiring yake wire zimepita nje!Au walikaribishwa stoo ya ikulu?
 
Zitto anataka kujimaliza mwenyewe kisiasa. Ni mtu intelligent lakini kwa mpango huu si vibaya kama Chadema watamtosa.:baby:
 
Jadilini kwa hoja na xio ghiriba na chuki,hayo mambo ya kuongozana na rais yapo kiprotocal na rais anaongozana na wapinzani na inategemea nafas ya mbunge huyo kuna shughuli gan inafanzika hayo maswali muulze MREMA anayeshughulika na masuala ya bunge atakupa majibu,na kwenda kwake ni baraka kutoka chama chake.Achen kuwa wabaguzi hivyo na ZITTO ni mwanachadema anayejali maslahi ya taifa na xio wengne wanajali chama chao kinachowaingizia pesa na xio watanzania na mkumbuke hakuna mwanachadema mwenye sura ya kitaifa kama ZITTO,POLEN SANA KWA KUTESWA NA UBAGUZI
 
Back
Top Bottom