Zitto Kabwe amuomba Rais Samia amuachie Mbowe

Zitto Kabwe amuomba Rais Samia amuachie Mbowe

CDM ni lazima wajue strategies za kumaliza mambo sio kila wakati kuwa negative tuu.
Bora kuwa negative, kama ni kuwa upande wa haki, kuliko kuwa positive lakini ndio kuwa upande usi wa haki
 
Nawasalimu wanajukwaa.

Acha niende moja kwa moja kwenye hoja, nimemfuatilia kwa umakini Mh. Zitto jinsi ambavyo amekuwa akiendesha siasa zake na nikiri huyu Mh. hafanyi siasa kwa mihemko bali akili kubwa sana.

Wakati wengine wakisusia mkutano yeye amekwenda na alipopewa nafasi amemuomba Mh. Rais ikiwezekana kiongozi mwenzao mwenye changamoto za kisheria aachiwe, kwakweli ameonesha ukomavu wa kisiasa.

Pongezi kwako Zitto Kabwe.

Niwatakie kazi njema wanajukwaa.
Kwa hotuba ya Mh Rais na kurudia maneno ya kwamba kusamehe kupo naona kutakuwa na msamaha kwa Mbowe. Ila wakati gani msamaha utatoka ndio siwezi kujua; ima utatoka kabla ya hukumu kwa DPP kupiga Nolle ama baada ya Mbowe kukutwa na hatia na kupewa adhabu na Mh Rais kutumia mamlaka yake ya Kikatiba na Kisheria kumsamehe Mbowe. Yote kwa yote naona Mama amekuja na jani la mzeituni akitaka maridhiano; mwenye masikio na asikie.
 
Kwa hotuba ya Mh Rais na kurudia maneno ya kwamba kusamehe kupo naona kutakuwa na msamaha kwa Mbowe. Ila wakati gani msamaha utatoka ndio siwezi kujua; ima utatoka kabla ya hukumu kwa DPP kupiga Nolle ama baada ya Mbowe kukutwa na hatia na kupewa adhabu na Mh Rais kutumia mamlaka yake ya Kikatiba na Kisheria kumsamehe Mbowe. Yote kwa yote naona Mama amekuja na jani la mzeituni akitaka maridhiano; mwenye masikio na asikie.
Tunamshukuru tunaopenda siasa za nchi hii,hiki ndii kitu tulichokuwa tunakisubiria.
 
Nawasalimu wanajukwaa.

Acha niende moja kwa moja kwenye hoja, nimemfuatilia kwa umakini Mh. Zitto jinsi ambavyo amekuwa akiendesha siasa zake na nikiri huyu Mh. hafanyi siasa kwa mihemko bali akili kubwa sana.

Wakati wengine wakisusia mkutano yeye amekwenda na alipopewa nafasi amemuomba Mh. Rais ikiwezekana kiongozi mwenzao mwenye changamoto za kisheria aachiwe, kwakweli ameonesha ukomavu wa kisiasa.

Pongezi kwako Zitto Kabwe.

Niwatakie kazi njema wanajukwaa.
Yaani ukiamua kutotumia akili uliyopewa na Mungu ni ujinga wako.
Zitto anapomwomba rais kwa mujibu wa sheria amwachie mbowe ni sheria ipi inayomruhusu rais kumsamehe mtuhumiwa?
Huu ni mchongo wa kumfungulia njia rais ili atiririke kinyume na Mbowe.
Kilichopo kwenye kesi ya Mbowe ni siasa na wala sii sheria hivyo Zitto alipaswa kutambua hilo na kutochomeka neno kwa mujibu wa sheria.
 
Nawasalimu wanajukwaa.

Acha niende moja kwa moja kwenye hoja, nimemfuatilia kwa umakini Mh. Zitto jinsi ambavyo amekuwa akiendesha siasa zake na nikiri huyu Mh. hafanyi siasa kwa mihemko bali akili kubwa sana.

Wakati wengine wakisusia mkutano yeye amekwenda na alipopewa nafasi amemuomba Mh. Rais ikiwezekana kiongozi mwenzao mwenye changamoto za kisheria aachiwe, kwakweli ameonesha ukomavu wa kisiasa.

Pongezi kwako Zitto Kabwe.

Niwatakie kazi njema wanajukwaa.
Staged,
Zitto ni mwenzao na wanamtumia kutafuta gia ya namna ya kumuachia Mbowe
 
Zitto ameonyesha maturity na leaership na siyo kiburi Hicho ndicho kinakosekana kwa viongozi wa CDM kwa muda mrefu. Walimvamia Samia immediately baada ya kuchukua Serikali kufuatia kufa kwa DIKTETA Magufuli. Walipaswa wakae waone stly ya Samia then waweke mkakati unaoendana na haiba yake. Sielewi kama CDM ina Mbowe tu ndiye Mwenyekiti mwenyewe na ndiyo mshauri wa chama. Maana hata kutohudhuria mkutano huu ni ukosefu wa busara na hekima
 
Hakuna lolote huo ni mchorotu yani watu wamekaa wakaona kuwena kikao alafu iyoishu iwekwe mezani tuimalize kwa namna hiyo, anyway, kama mama akimuachia niheripia mahabusu sio kuzuri.
 
Muhimu Zitto ana busara sana ameenda na agenda ya kuomba muafaka Mbowe awe huru.

Nampongeza sana.
Muhimu ni kuacha uonevu na kubambika watu kesi,sio unafiki wa kumpaisha Zitto asiyostahili.

Sasa wamegeuka kuwa waigizaji,waache stages za kijinga ata watoto wa primary wanawazidi maigizo ya akili
 
Ili uwe na akili kubwa lazima ufuate kile CDM wanachotaka na kuamini...ukienda tofauti nao tu kidogo basi wewe ni akili ndogo, msaliti nk..
Uko sawa. Dawa ni kuwapuuza (ignore) tu wapotelee mbali. Kinachowavimbisha kichwa CHADEMA ni kuwa, pamoja na kufutwa kwenye ubunge na nafasi mbalimbali nchini, bado watu wengi hasa viongozi, wanachama na mashabiki wa CCM wanashindwa kuwa-ignore.

Katika kampeni za uchaguzi ambapo CHADEMA haina mgombea, mashambulizi makubwa ya CCM huwa dhidi ya CHADEMA kuliko hata wapinzani wenye wagombea. Wakizindua miradi ya serikali sehemu kubwa ya hotuba ni kushambulia CHADEMA kwa kutothamini juhudi. Hapa JF mwendo ni kuchambua na kupuuza misimamo ya CHADEMA. Hakika hicho chama kinapewa uhai na CCM na serikali.
 
Hahaaa... Kama mkakati wake huo wa kijinga ungekuwa unafanya kazi tangu 1995 tungekuwa na katiba mpya nchi hii. Hayo ni mawazo ya watu ambao wanakaa nyumbani na kusubiri wazazi ama mume walete chakula nyumbani.
We Dada una mambo yani CHADEMA wamnyenyekee SAMIA ili aruhusu mchakato wa Katiba Mpya?? uliwahi kuona wapi mtawala ambae Katiba ina mfeva aruhusu mabafikiko ya katiba.
 
Kwa hotuba ya Mh Rais na kurudia maneno ya kwamba kusamehe kupo naona kutakuwa na msamaha kwa Mbowe. Ila wakati gani msamaha utatoka ndio siwezi kujua; ima utatoka kabla ya hukumu kwa DPP kupiga Nolle ama baada ya Mbowe kukutwa na hatia na kupewa adhabu na Mh Rais kutumia mamlaka yake ya Kikatiba na Kisheria kumsamehe Mbowe. Yote kwa yote naona Mama amekuja na jani la mzeituni akitaka maridhiano; mwenye masikio na asikie.
Maridhiano at CHADEMA's grave expense. Kinachotafutwa tangu awamu ya nne, hasa ya tano, ni ama CHADEMA ife kabisa (literally) au ipoteze ushawishi (credibility) mbele ya Watanzania. Serikali ya CCM haitakaa ikubali uwepo wa chama aina ya CHADEMA nchini. Ni suala la kufa na kupona. CHADEMA and CCM are mutually exclusive. Hence, CHADEMA has to die for CCM to exist.

Hivyo, msamaha wa mama kwa mtuhumiwa wa ugaidi Mbowe ukipokelewa bila masharti yoyote litakuwa deni zito sana kwa CHADEMA ambalo litawakata makali ya kisiasa kisawasawa. Kwa bahati mbaya sana, hakuna maridhiano na CCM/serikali yenye heri kwa CHADEMA: There is only death and the (ongoing) fight to death for the party. - And, consequently, de-facto death to multiparty politics in Tanzania. Labda tutaishi kwa amani baada ya hapo.
 
Nawasalimu wanajukwaa.

Acha niende moja kwa moja kwenye hoja, nimemfuatilia kwa umakini Mh. Zitto jinsi ambavyo amekuwa akiendesha siasa zake na nikiri huyu Mh. hafanyi siasa kwa mihemko bali akili kubwa sana.

Wakati wengine wakisusia mkutano yeye amekwenda na alipopewa nafasi amemuomba Mh. Rais ikiwezekana kiongozi mwenzao mwenye changamoto za kisheria aachiwe, kwakweli ameonesha ukomavu wa kisiasa.

Pongezi kwako Zitto Kabwe.

Niwatakie kazi njema wanajukwaa.
Eti akili kubwa 😂😂😂ila wabongo daah, weng ni very dormant!!
 
Nyie sio mbowe tu waachiwr na wale mashekh waliobambikwa kesi ambayo haiishi ya ugaidi Ila wazanzibari wenzake kawatoa haraka hio ndio double standard nachukia awamu hii na ya tano hovyo kabisa
 
Chadema wamekuwa kama wamepoa sana,,, nafikiri sasa wanatafutiwa platform angalau waseme neno serikali ipate kujua wanawaza nn...

Mwanzoni waliweza kuwasikia bungeni lakini sasa hivi wengi wapo bize na shughuli zao
 
Back
Top Bottom