Zitto anataka kusaliti CHADEMA?

Status
Not open for further replies.
Zitto anaagenda ya siri! Kama kweli anaamini katika demokrasia, basi baada ya kupiga kura na kushindwa angekaa kimya na badala yake awaunge mkono wale walioshinda (waliogomea hotuba ya raisi).

Napenda kuwaambia hapa wana JF, DOGO anajimaliza kisiasa!!! yuko wapi Amani Kaburu?? enzi zile alikuwa machachali sana kuliko zito, lakini leo kashakufa kabisa kisiasa amebaki kupiga magoti kwa CCM immpe chakula
 
jamani mbona hii ni thread ya tatu inahusu mada hiyohiyo??
 

ndiyo maana Nyerere aliwapuuza wakabaki nyuma hadi leo!!
 
Nyerereist,
Hivi watu kama hawa katika TANU na CCM Nyerere aliwafanyaje? Aliwafukuza. Therein lies a lesson for you.
 
Mwongo huna lolote hata huyo zitto anajua kabisa unasema uongo hii ni hali ya kawaida kabisa sio jambo la ajabu watu kutofautiana misimamo hakuna atakaye ondoka chadema propaganda zako zipelekee huko huko
 
Nyerereist,
Hivi watu kama hawa katika TANU na CCM Nyerere aliwafanyaje? Aliwafukuza. Therein lies a lesson for you.

- Mkuu kweli ninakusoma sawa sawa, eti kuwafukuza walio na mawazo tofauti na yako si ndio yamelifikisha hili taifa lilipo sasa, au?


William.
 
I have no comments,so zitto hataki katiba mpya? yeye alipendekeza nini kifanyike badala ya kuingia ndani na kutoka? au kaahidiwa uwaziri na aliona akiingia na kutoka atakuwa kapoteza nafasi yake kwa jk?

Am still watching this movie.
 
Kasyabone,
Hakuna cha kusambaratika kwa CHADEMA. Zitto katoa maoni yake kuwa hakuunga mkono uamuzi wa kumboycott Kikwete. Majority waliunga mkono na majority walishinda. Hakuna shida hapo. Kinachodhihirika ni kwamba CHADEMA is a democratic party na sijaona sababu zozote ambazo zimempelekea mheshimiwa Zitto kujiainisha na upinzani wa hatua hiyo isipokuwa kama alikuwa anajaribu kuwaridhisha marafiki zake on the other side.
 
Nyerereist,
Hivi watu kama hawa katika TANU na CCM Nyerere aliwafanyaje? Aliwafukuza. Therein lies a lesson for you.

Ndio maana nasema CHADEMA ni photocopy ya CCM 1970's to 1980's.. enzi za zidum fikra za mwenyekiti wa chama. Mbowe na Slaa wakisha sema basi wote mfuate. Thats BS. Wote ambao wamekua wakionyesha kutokubaliana na mitazamo yao wamekua wakiishia kufukuzwa (kama alivyokua anafanya nyerere na chama kimoja),, kwa mfano Kafulila, Dr Kaburu, Chacha wangwe (RIP) bado kidogo, na wengine wengi tu.. Acheni udictator
 

Nchi zilizoendelea na zenye mfumo wa demokrasia zinatumia njia kama hiyo aliyotumia Zitto. Hakuna mfarakano wowote kama Wabunge wakipingana kwa hoja ktk public level, hata kama wakiwa wanatoka chama kimoja.

Huu mfumo alioutumia Zitto ni mzuri especially kwa nchi changa ktk demokrasia. Kwa mfano angalia, Marekani, Democrats vs Democrats vs Obama, Or Republican vs Republican vs Bush. Hii ni demokrasia.

Zitto kabwe anajaribu kuelezea msimamo wake ktk public level, ni msimamo mzuri, lakini waTZ wanafikiri ni mfarakano. Kama Chadema itaendelea na kutumia system hii ya demokrasia ndani ya chama, basi Chadema kitakuwa ni chama bora TZ.
 
- Mkuu kweli ninakusoma sawa sawa, eti kuwafukuza walio na mawazo tofauti na yako si ndio yamelifikisha hili taifa lilipo sasa, au?


William.
Nilikuwa nampa Nyerereist somo hapo. Siyo kwamba naafiki hatua hiyo na pia natambua kuwa nyakati zilikuwa tofauti. Labda Nyerere angekuwepo kwenye siasa leo angetumia mbinu tofauti.
 
Wakuu zangu nataka kuuliza kitu..
Kuna utata gani haswa unawaumiza vichwa?...
Mbona nchi nyinginezo watu hutoka Bungeni na wengine kutohudhuria hata kama amekuja rais wao kulihutubia bunge na haiwi tatizo kubwa la kujenga chuki kama kwetu?
Hata UN wapo wawakilishi wa nchi huwa hawahudhurii hotuba za mairas kibao na wengine hutoka nje pindi akisimama rais fulani na sijasikia mfaragano kama wetu tena akilaumiwa aloondoka na sii msemaji mkuu.

Na ikisha basi mnataka kunambia Wabunge wetu hawajawahi kutohudhuria au kutoka bungeni wakati waziri mkuu au waziri akihutubia...mbona tunaifanya issue hii kuwa kubwa sana wakati Chadema wamekwisha eleza wazi kwa nini wamefanya hivyo na sidhani kama kuna sheria inayowakataza kutofanya hivyo. Au ndio Udikteta wenyewe unavyotumika kwa rangi ya demokrasia...
 
Hapana. You got it wrong. Zitto anazungumza na anaendelea kuwa na haki yake ya kuzunguza. Ni tofauti na enzi za Nyerere. Ndio maana nimekushauri ubadilishe jina.
Kenyattaist linakufaa zaidi.
 
I dont see an issue (hapa tuna make a mountain out of a mole hill) kutokukubaliana ni kawaida kura zikapigwa wengi wakashinda thats normal lakini i think Zitto angekaa kimya tu there is no need awaambie vyombo vya habari what went behind the scenes

Tunataka uwazi katika siasa za vyama vingi na kila mtu ana haki ya kutoa mawazo yake.

Hon Zito, we always believe that you are in a wrong camp - Tafakari juu ya uongozi wa chama chako!

Top leadership ni Wanasiasa uchwara!
 
Mhe Zitto tulikuamini tuka kupenda kama mpiganaji shupavu, lakini wewe ni mbayu wayu!!! ondoka chadema hamia nccr ili sisi wapambanaji wenye nia ya kumkomboa mtanzania tufanyekazi... Hawa wabakaji wa rasilimali za Tanzania tayari wamekwisha kuteka kirahisi sana kwa tamaa zako... nendaaaaa ... nendaaaaaa zitto zuberi kabwe kalawtweeee na hao mafisadi ... CHADEMA ni MOVEMENT na ni muda muwafaka wa mabadiliko watake wasitake.... Peoples POWER DAIMA
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…