ZeMarcopolo
Platinum Member
- May 11, 2008
- 14,019
- 7,223
​​
Nianze tu kwa kusema Ukishakataliwa na Jammiforums umekataliwa na jamii nzima ya watanzania na lazima mtu husika uwe makini na idadi ndogo (minor proportion) ya watu wanaoweza kukuhadaa eti wanakuunga mkono hapa jamvini kuliko wale wanaokupinga.
Ujumbe wako nimeishia kusoma hapa. Jamiiforums kama umefuatilia hivi karibuni imedhihirika kuwa kuna watu wengi tu ambao wanaandika mawazo "fake" ili kuvipatia maslahi vikundi fulani. ID moja inaweza kutumiwa na watu zaidi ya watano kutoa maoni. Hivyo basi kuamini kuwa maoni ya JF yanareflect uhalisia wa fikra za jamii SI KWELI.
Kuna wakati JF ilikuwa inatoa picha halisi ya fikra za jamii lakini baada ya kuvamiwa na walafi wa kisiasa hali imekuwa tofauti. Sasa hivi JF unaweza kuandika point nzuri tu lakini kwa sababu mlengo wako ni wa upande fulani, basi litaibuka kundi kubwa kukupinga. Infact kundi hilo ni kundi la ID sio kundi la members kwa sababu anaweza kuwa ni mtu mmoja tu anayetumia ID mbalimbali.
Sisi wengine tunakuja JF kwa vile ni kijiwe chetu tulichokizoea na kimekuwa sehemu ya maisha yetu, lakini genuine nature ya JF haipo tena. Siku hizi JF imekuwa sehemu ya watu kuleta habari za uongo kama ile ya mwanamke wa kimarekani aliyesingiziwa kuwa ndiye aliyekuwa na RPC wa Mwanza wakati anauwawa!
Kimsingi kuna kitu kinatakiwa kufanyika ili JF irudi kwenye hali ya kuaminiwa na kuwa sehemu ambayo akili zinapimana nguvu siyo kijiwe cha kumezeshana itikadi.