Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,252
- 113,645
Kama kichwa cha mada kinavyobainisha, hizi ni hisia zangu tu.
Sijafanya utafiti ulio rasmi. Sina uwezo wa kiakili wala wa kiutaalamu kuweza kufanya utafiti wowote ule ulio wa kisayansi.
Ni hisia zangu kama mtu na raia mwenye busara za kawaida tu [common sense] ambaye hupenda kuangalia na kutazama mambo yajiriyo kwenye jamii na kuyachanganua kwa kadri ya uwezo wangu.
Sasa kilichonisukuma kuanzisha mada hii ni uteuzi wa aliyekuwa ‘Governor🤣’ wa Dar es Salaam enzi za utawala wa Rais John Pombe Joseph Magufuli [najua alikuwa ni Dokta pia ila nimeliacha tu hilo kwa makusudi 😉].
Siku si nyingi zilizopita, Paul Makonda aliteuliwa [au alichaguliwa?] kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM.
Sijui aliteuliwa kwa sifa zipi hasa maana jamaa ni kiwanda cha pumba tupu kila afunguapo domo lake.
Katika kumfuatilia kwangu kwa ukaribu tokea aanze utumishi wa umma, sijawahi kumsikia akiongea jambo lolote lile ambalo lilinifanya nimkubali. Akifungua domo lake huwa ni pumba tu mwanzo, katikati, mpaka mwisho. Pumba.com. Undisputed, undefeated PumbaMaker champion of the world.
Kilichonistua zaidi kuhusu uteuzi wake huo, ni yale mapokeo ya taarifa za yeye kuteuliwa kushika hiyo nafasi, hususan hapa JF ila pia hata kwingineko.
Majumuisho ya uangalizi [observation] wangu huo ni kwamba, idadi ya watu waliofurahia Makonda kurudi kwenye safi za juu za kiuongozi kwenye chama chake, ni kubwa.
Nilitegemea kuwepo mapokeo yaliyo hasi. Nilitegemea uteuzi wake huo ubezwe. Nilitegemea watu watapuuzia mbali huo uteuzi.
Lakini haikuwa hivyo. Watu walionyeshwa kufurahishwa na kurudishwa kwake. Wapo waliosema kuwa yeye ndiye mtu sahihi kwenye hiyo nafasi.
Baadhi ya walioonyesha furaha ya yeye kurudi ni wale ambao wamejitanabaisha kama ni watu walio pinzani na CCM.
Hali hiyo ya mapokeo ya watu juu ya taarifa za Makonda kuteuliwa kuwa katibu mwenezi zimenifanya nijiulize endapo labda Watanzania kwa uwingi wao wanasumbuliwa na Stockholm Syndrome baada ya kushikwa mateka na utawala wa chama kimoja tokea tupate uhuru zaidi ya miaka 60 iliyopita!
Manake haiingii akilini kabisa! Iweje mtu kama Paul Makonda mwenye kashfa nyingi zihusuzo uvunjwaji na ukiukaji wa haki za kibinadamu na makandokando mengine mengi kurudishwa kwake kwenye uongozi wa chama chake kufurahiwe namna hiyo na watu?
Ni kama vile CCM imeziteka akili na hisia za watu mpaka watu hao kuona kana kwamba bila hicho chama basi hata nchi nayo haipo.
Duniani kwa kawaida, kwa mtazamo wangu, idadi ya wapumbavu na wajinga huwa ni kubwa zaidi kuliko ile ya walio werevu.
Ila kwa Tanzania, nadhani idadi ya wapumbavu inaizidi idadi ya wajinga. Na ukijumlisha idadi ya wapumbavu na wajinga, kwa makisio yangu, inafika hata kwenye 99% ya idadi yote ya watu.
Sijafanya utafiti ulio rasmi. Sina uwezo wa kiakili wala wa kiutaalamu kuweza kufanya utafiti wowote ule ulio wa kisayansi.
Ni hisia zangu kama mtu na raia mwenye busara za kawaida tu [common sense] ambaye hupenda kuangalia na kutazama mambo yajiriyo kwenye jamii na kuyachanganua kwa kadri ya uwezo wangu.
Sasa kilichonisukuma kuanzisha mada hii ni uteuzi wa aliyekuwa ‘Governor🤣’ wa Dar es Salaam enzi za utawala wa Rais John Pombe Joseph Magufuli [najua alikuwa ni Dokta pia ila nimeliacha tu hilo kwa makusudi 😉].
Siku si nyingi zilizopita, Paul Makonda aliteuliwa [au alichaguliwa?] kuwa katibu wa itikadi na uenezi wa CCM.
Sijui aliteuliwa kwa sifa zipi hasa maana jamaa ni kiwanda cha pumba tupu kila afunguapo domo lake.
Katika kumfuatilia kwangu kwa ukaribu tokea aanze utumishi wa umma, sijawahi kumsikia akiongea jambo lolote lile ambalo lilinifanya nimkubali. Akifungua domo lake huwa ni pumba tu mwanzo, katikati, mpaka mwisho. Pumba.com. Undisputed, undefeated PumbaMaker champion of the world.
Kilichonistua zaidi kuhusu uteuzi wake huo, ni yale mapokeo ya taarifa za yeye kuteuliwa kushika hiyo nafasi, hususan hapa JF ila pia hata kwingineko.
Majumuisho ya uangalizi [observation] wangu huo ni kwamba, idadi ya watu waliofurahia Makonda kurudi kwenye safi za juu za kiuongozi kwenye chama chake, ni kubwa.
Nilitegemea kuwepo mapokeo yaliyo hasi. Nilitegemea uteuzi wake huo ubezwe. Nilitegemea watu watapuuzia mbali huo uteuzi.
Lakini haikuwa hivyo. Watu walionyeshwa kufurahishwa na kurudishwa kwake. Wapo waliosema kuwa yeye ndiye mtu sahihi kwenye hiyo nafasi.
Baadhi ya walioonyesha furaha ya yeye kurudi ni wale ambao wamejitanabaisha kama ni watu walio pinzani na CCM.
Hali hiyo ya mapokeo ya watu juu ya taarifa za Makonda kuteuliwa kuwa katibu mwenezi zimenifanya nijiulize endapo labda Watanzania kwa uwingi wao wanasumbuliwa na Stockholm Syndrome baada ya kushikwa mateka na utawala wa chama kimoja tokea tupate uhuru zaidi ya miaka 60 iliyopita!
Manake haiingii akilini kabisa! Iweje mtu kama Paul Makonda mwenye kashfa nyingi zihusuzo uvunjwaji na ukiukaji wa haki za kibinadamu na makandokando mengine mengi kurudishwa kwake kwenye uongozi wa chama chake kufurahiwe namna hiyo na watu?
Ni kama vile CCM imeziteka akili na hisia za watu mpaka watu hao kuona kana kwamba bila hicho chama basi hata nchi nayo haipo.
Duniani kwa kawaida, kwa mtazamo wangu, idadi ya wapumbavu na wajinga huwa ni kubwa zaidi kuliko ile ya walio werevu.
Ila kwa Tanzania, nadhani idadi ya wapumbavu inaizidi idadi ya wajinga. Na ukijumlisha idadi ya wapumbavu na wajinga, kwa makisio yangu, inafika hata kwenye 99% ya idadi yote ya watu.