Acha Uvivu
JF-Expert Member
- Apr 28, 2011
- 524
- 131
​​Wanajamvi, sio kusudi langu kuingilia mtazamo wa mtu yeyote, ila kwa nia ya dhati na uelewa kuhusu uhuru wa kutoa maoni unaolenga kujenga na sio kubomoa, nimeona vema nitoe Ushauri kwa Mkuu Zitto na Kundi lake.
Nianze tu kwa kusema Ukishakataliwa na JammiForums umekataliwa na jamii nzima ya watanzania na lazima mtu husika uwe makini na idadi ndogo (minor proportion) ya watu wanaoweza kukuhadaa eti wanakuunga mkono hapa jamvini kuliko wale wanaokupinga. Na hasa ukijua kuwa wanachama wa JF ndo wapiga kampeni huko mitaani kuhusu Chama na mwanasiasa binafsi (kumbuka hofu ya Pinda-CCM) juu ya JF.
Kwa kutambua mchango wako (Zitto), achana na hao walala hoi wanaojipendekeza, wakiwemo CCM wanaotaka kukutumia kama tissue, ningeomba haya uyafanye kutoka kwangu kama Mtanzania mpenda mabadiliko na mchukia wanafiki:
KWANZA; Ujutie kile ulichokuwa unakifanya maana huenda ulikuwa hujui ulitendalo.
PILI; Jishushe tu tuombe radhi Watanzania ambao kwa idadi kubwa ni wakulima na wafanyakazi na ambao tunaomba usiku na mchana kuona nchi yetu imekombolewa toka mikononi mwa CCM. Haimanishi ufanye mkutano wa hadhara lakini JF inatosha tu kutupa jibu nasi tutakurudisha kundini, maana kama nilivyo sema hapo juu; UKIKUBALIWA NA JAMIIFORUMS UMEKUBALIWA NA WATZ WOTE. Na kwa kinachoendelea ndani ya chama chako, ambacho umewahi sema huna mpango wa kukihama, onyesha ushirikiano na baada ya kuyamaliza huko ndo uje kwetu.
TATU; Baada ya hayo hapo juu kufanyika, tufichulie wote walioficha mpunga (fedha) huko Uswisi kama ulivyoanza vema na usikate tamaa. Na lazima hili lifanyike baada ya hayo hapo juu kwa sababu hili likitangulia bado halitakurudisha kwenye level yako ya awali. Hakika ukiyafuata haya na ukatuambia wezi tulionao nguoni mwetu tutakurudisha kwenye form fasta.
Ni mtazamo wangu wanajamvi.
Nianze tu kwa kusema Ukishakataliwa na JammiForums umekataliwa na jamii nzima ya watanzania na lazima mtu husika uwe makini na idadi ndogo (minor proportion) ya watu wanaoweza kukuhadaa eti wanakuunga mkono hapa jamvini kuliko wale wanaokupinga. Na hasa ukijua kuwa wanachama wa JF ndo wapiga kampeni huko mitaani kuhusu Chama na mwanasiasa binafsi (kumbuka hofu ya Pinda-CCM) juu ya JF.
Kwa kutambua mchango wako (Zitto), achana na hao walala hoi wanaojipendekeza, wakiwemo CCM wanaotaka kukutumia kama tissue, ningeomba haya uyafanye kutoka kwangu kama Mtanzania mpenda mabadiliko na mchukia wanafiki:
KWANZA; Ujutie kile ulichokuwa unakifanya maana huenda ulikuwa hujui ulitendalo.
PILI; Jishushe tu tuombe radhi Watanzania ambao kwa idadi kubwa ni wakulima na wafanyakazi na ambao tunaomba usiku na mchana kuona nchi yetu imekombolewa toka mikononi mwa CCM. Haimanishi ufanye mkutano wa hadhara lakini JF inatosha tu kutupa jibu nasi tutakurudisha kundini, maana kama nilivyo sema hapo juu; UKIKUBALIWA NA JAMIIFORUMS UMEKUBALIWA NA WATZ WOTE. Na kwa kinachoendelea ndani ya chama chako, ambacho umewahi sema huna mpango wa kukihama, onyesha ushirikiano na baada ya kuyamaliza huko ndo uje kwetu.
TATU; Baada ya hayo hapo juu kufanyika, tufichulie wote walioficha mpunga (fedha) huko Uswisi kama ulivyoanza vema na usikate tamaa. Na lazima hili lifanyike baada ya hayo hapo juu kwa sababu hili likitangulia bado halitakurudisha kwenye level yako ya awali. Hakika ukiyafuata haya na ukatuambia wezi tulionao nguoni mwetu tutakurudisha kwenye form fasta.
Ni mtazamo wangu wanajamvi.