Zijue sababu za Benjamin Mkapa kumuunga mkono Lowassa

Zijue sababu za Benjamin Mkapa kumuunga mkono Lowassa

hakuna jipya ktk uliyo yaandka, mi nilidhan ntaona very unique reasons kama ni hzo hata walevi wa gongo wanazijua
 
Mimi siipendi kabisa CCM lakini kama ni lazima kutawaliwaliwa na CCM basi katika wote wanaotaka kugombea kupitia CCM, afadhali ya Lowas.

Tunajua CCM wote ni wevi, ni wala rushwa na ni mafisadi. Kwa hiyo ndani ya CCM hatutafuti msafi, hatutampata maana ufisadi, rushwa na wizi ndani ya CCM upo ndani ya mfumo wa uendeshaji wa siasa za chama.

Tukija kwenye akili binafsi, Lowasa ana akili na uwezo wa kuelewa kuliko wagombea wote wa CCM. Hata wakati wanasoma pale chuo kikuu Lowasa, Kikwete na Ditopile, Lowasa alikuwa far ahead ya Kikwete na Ditopile, na ndiye pekee yake pale UDSM kwenye kundi lao aliyefauli. Kikwete na Ditopile hawakufaulu, Ikulu iliomba Kikwete na Ditopile wapewe minimum pass maana wana majukumu ya TANU Youth Legue.

Uwezo wa kufanya maamuzi, Lowasa yupo juu ya Kikwete na wagombea wengine wote wa CCM.

Uwezo kusimamia, kujiamini, na upeo yupo juu sana kuliko wale wote waliosema wanataka kugombea kupitia CCM. Ukimwacha Lowasa, wagombea wengine wote walioonesha nia kupitia CCM ni takataka.
 
mimi siipendi kabisa ccm lakini kama ni lazima kutawaliwaliwa na ccm basi katika wote wanaotaka kugombea kupitia ccm, afadhali ya lowas.

Tunajua ccm wote ni wevi, ni wala rushwa na ni mafisadi. Kwa hiyo ndani ya ccm hatutafuti msafi, hatutampata maana ufisadi, rushwa na wizi ndani ya ccm upo ndani ya mfumo wa uendeshaji wa siasa za chama.

Tukija kwenye akili binafsi, lowasa ana akili na uwezo wa kuelewa kuliko wagombea wote wa ccm. Hata wakati wanasoma pale chuo kikuu lowasa, kikwete na ditopile, lowasa alikuwa far ahead ya kikwete na ditopile, na ndiye pekee yake pale udsm kwenye kundi lao aliyefauli. Kikwete na ditopile hawakufaulu, ikulu iliomba kikwete na ditopile wapewe minimum pass maana wana majukumu ya tanu youth legue.

Uwezo wa kufanya maamuzi, lowasa yupo juu ya kikwete na wagombea wengine wote wa ccm.

Uwezo kusimamia, kujiamini, na upeo yupo juu sana kuliko wale wote waliosema wanataka kugombea kupitia ccm. Ukimwacha lowasa, wagombea wengine wote walioonesha nia kupitia ccm ni takataka.

waeleze wanaopishana na ukweli....
 
u

Acha wivi wa kike! Mkapa haitaji ulinzi hata kidogo kazi aliyoifanyia nchi hii inatosha kumlinda. Hizo hoja zako hafifu zipeleke kwenye mradi ule wenu usiyo uzika.
Kwa kuuza nyumba za serikali. Wizi wa Kiwira na ubinafsishaji wa NBC na viwanda vingine vilivyojengwa kwa jasho la walipa kodi upinzani ukichukua nchi atakuwa matatani. Na yeye pia analijua hilo ndio maana anapinga upinzani kwa nguvu zake zote. CCM wote ni wezi na wana tabia ya kulindana. Sidhani hilo ni wivu wa kike. Labda wivu wa kiume.
 
Acha porojo Baba,chaguo la Mkapa ni Magufuli.Fuatilia ni waziri gani pekee aliyekabidhiwa vitabu vya hotuba za Mkapa baada ya JK.

simuelewi okello hii taarifa kaitoa wapi? kama ni magazetini haya yanayotakwa kununuliwa basi pole yake

mkapa ana m support magufuli
 
Hakuna wa kushindana na lowasa ndani ya ccm na hata nje ya ccm kamwe! Huyo anauweza wa kuwahonga watanzania wote na hata wapinzani wakahongeka.
 
Lowassa anawatesa sana roho,subirn tu kidogo ni suala la muda ataingia uwanjani
 
Ikiwa Dunia imesimama kwa mshutuko wa kumpoteza kiongozi shupavu Rais wa Zambia Marehemu Michael Chilufya Satta kilichotokea London mapema wiki hii , Rais Mstaafu Benjamin Mkapa amekaririwa na kituo cha lunginga CITIZEN nchini Kenya kwa njia ya simu akihojiwa maswali mbali mbali baada ya kifo cha Satta, Katika mahojiano yake siku sita OKELLO kupata tafakuri ya Zaidi ya masaa 30 hadi sasa na kudhubutu kusema Lowassa ameungwa Mkono na Mkapa kwa maslahi ya Taifa , chama na Serikali. Zijue sababu za Mkapa kumuunga mkono Lowassa katika Tafsiri ya mahojiano yake na kituo tajwa.

1.EDWARD LOWASSA ANAUZIKA KWA WANANCHI.
Rais Mkapa aliangazia wasifu wa Lowassa bila shaka na kukiri ndie anaeuzika akiangalia utendaji na uchapakazi wa Lowassa na ndioa maana alinukuliwa aisema,"Chama kama chama lazima muwe na mtu anayeuzika na kukubalika katika jamii kwa utendaji wake, haiba yake, wasifu wake (ndani ya Chama na Serikali) lakini vile vile ushawishi wake.." ambae bila shaka ni Lowassa.

2. VIJANA WAJITOKEZE ILA NI WAKATI WA LOWASSA.
Hapa Mheshimiwa rais Mstaafu alionyesha kuwa chama kina kuza demokrasia pia na hivyo hazina ya vijana haipaswi kupuuzwa ila huu ni wa kati wa Lowassa na ndio maana hakusita kumtaja Lowassa pale alipo jitokeza 1995 na sasa ni wakati wake. Hivyo alisema "...Haya mambo ya umri na kadhalika sisi hatukutazama wakati huo ila si dhambi vijana KUJITOKEZA manake hata wakati wangu Rais wa sasa Mhe. Kikwete na kina Lowassa walijitokeza na LEO unaona Kikwete ndiye Rais" akimaanisha vijana wajitokeze ila Lowassa ndie Rais AJAE.

3.AKIRI LOWASSA HAKUNA WA KUMZUIA NDANI YA CHAMA
"...nikuhakikishie hata kama mimi Benjamin Mkapa siko na Kikwete mwisho wa siku wanachama ndio watakaosema wewe hutaki ila sisi tuachie huyo huyo...Na hayo yalijitokeza mwaka 2005 watu walimtaka Mhe Kikwete sasa mimi kuwa Mwenyekiti wa Chama hakunipi Mandate ya kushindana na walio wengi na mliona alishinda kwa asilimia kubwa kweli kweli.." HIVYO ni wazi hata Rais Jakaya hayuko kwa ajili ya kumzuia Lowassa bali kutimiza Demokrasia.

4.AONYA MAKUNDI YA URAIS NDANI YA CHAMA YANAYO MCHAFUA BILA SABABU.
Mheshimiwa Mkapa alirejea kauli ya Edward Lowassa February 7 ,2008 alipoonya wanasiasa kupakaziana siasa chafu hivyo nae alionya kwa kusema "Hivyo CCM Ina taratibu zake na wanajua nani anafaa manake siasa hizi...tuhuma zingine za kipuuzi kweli kweli...sasa mkiendekeza tuhuma mwishowe mnakuta mnabaki bila chama na kwenye siasa mkianza kushutumiana hakuna wa kusimama"

5.LOWASSA NI TUMAINI LA WENGI NA CHAGUO LA WENGI.
Amekishauri chama kuwa Lowassa ni tumaini la wengi hivyo cha kama chama wao watawekeza kwake na ndipo alipo yanena haya "Hakuna chama duniani ambacho kinaona kabisa fulani atatusaidia halafu kimwache -hakuna. Manake huko ni kukiua Chama...Naamini ndivyo ilivyo hata mpaka sasa tafiti zimefanyika na naamini wamesikia watu wakisema wanamtaka nani…wakati wangu mimi mgombea alikuwa amesha tungiwa nyimbo na watu mbali mbali wenye mapenzi nae. Hivyo labda hata sasa yawezekana kuwa hivyo…washwahili walisema nyota njema huonekana asubuhi"

MUNGU IBARIKI AFRIKA , MUNGU IBARIKI TANZANIA ,….SAFARI YA MATUMAINI KUELEKEA 2015.

Upumbavu!
 
hujui kama Lowasa alitajwa kwenye mkataba wa kifisadi wa richmond akiwa PM?
Hujui kama Mkapa alitajwa kuununua mgodi wa kiwira kwa bei ya chini sana?
uzushi unaoungea ni upi?
au hukusudii kuwa mkweli?
siamini kama huoni aibu kuiga majibu ya Lundenga kuhusu Siti.


Mkuu, mpotezee kwani watanzania wengi huwa ni wasaulifu na hawapendi kusikia ukweli. hapo ukimuuliza huyo jamaa Mkapa alikuwa rais wa tanzania mwaka gani atakuuliza Mkapa alikuwa rais wa nchi hii, lini....acha uwongo bwana! watu kama hawa ni kuwapotezea tu, na usikute pengine ni mpambe wa Lowassa kaja hapa kupotosha watu na kupinga ukweli wowote dhidi yake. Lowassa aligawa sana ardhi alipokuwa waziri wa ardhi hapa Tanzania. Marafiki zangu wa gazeti fulani ambao walikuwa wanampamba back in 1995 aiiwapa mashamba ya hajabu Morogoro, Tanga tena kiholela. Sasa utasema mtu makini huyu? labda alibadirika jana kwa sababu uchaguzi unakaribia.
 
Unavyodhani wasomi ndo walio na uwezo wa kufanya utafiti! Nakuonya tena Edward hakubaliki kwa watanzania na hata hao alionao wanajua kuwa kumuuza kwa wananchi itakuwa tabu sana, kwani kashfa alizo nazo hajawahi kujisafisha hata siku moja.

upeo mfupi wa kueleza tamaa zako mbele ya jamii za watafiti.....na wasomi utachekwa....
 
Back
Top Bottom