2030 Bado Mbali: Acheni Mbwembwe, Watumikieni Wananchi

2030 Bado Mbali: Acheni Mbwembwe, Watumikieni Wananchi

Alloyce PR

JF-Expert Member
Joined
Nov 15, 2020
Posts
803
Reaction score
868
Viongozi, kumbukeni kwamba mwaka 2030 bado uko mbali. Kazi yenu kwa sasa ni kuwatumikia wananchi kwa uadilifu na kutekeleza wajibu wenu kwa matokeo yanayoonekana.

Mkianza mbwembwe za kisiasa mapema na kujenga taswira ya kutafuta umaarufu binafsi, mnaweza kujikuta mkirudia makosa yaliyowahi kuwagharimu wanasiasa wengine kama Edward Lowassa na Bernard Membe.

Tambueni kuwa CCM ni chama chenye mfumo mpana na wenye ushindani mkubwa wa ndani. Hivyo, badala ya kujitangaza kupitia mambo madogomadogo, elekezeni nguvu zenu katika utendaji, huduma kwa wananchi, na kujenga imani ya umma. Mwisho wa siku, matendo ndiyo yatakayowatambulisha kuliko kelele.​
 
Hakuna kiongozi aliyechaguliwa na wananchi wa Tanzania.
Hao wote waliopo lengo ni kutumikia matumbo yao.

Tunaongozwa na Mishanga na Mishungi
Manyani na Masokwe.
 
Uchaguzi wa 2030 utakuwa mgumu sana kama tutaendela na mazingira haya ya siasa tuliyonayo kwa sasa.

Kama 2025 raia hawakwenda kupiga kura hiyo 2030 watajifungia ndani siku 7 bila kutoka siku ya kupiga kura
 
Uchaguzi wa 2030 utakuwa mgumu sana kama tutaendela na mazingira haya ya siasa tuliyonayo kwa sasa.

Kama 2025 raia hawakwenda kupiga kura hiyo 2030 watajifungia ndani siku 7 bila kutoka siku ya kupiga kura
Duh! Noma sana.
 
Back
Top Bottom