Ze Utamu blogger under arrest?

Ze Utamu blogger under arrest?

Status
Not open for further replies.
hahhahahhaha sasa wakuuu naona badala ya ze utamu awe roho juuu na agonized imehamia kwenu maaana mnavyoshushuana? mhhhhhh now i too smell smthing fishyy ..... oh no smthing chickenyyyyy

Hapa kila kitu kitajulikana mwenye kucomment kupost pic n'k.Mkuu nipo kazini,jioni na peleka report,
 
Kuna mtandao mkubwa sana utakaoshtakiwa, watoa comments, wapiga picha, pamoja na waliokuwa wakii-visit ile blog najua kuna wana JF wengi tu watakao simamishwa kizimbani.

...wengi tuliobonyeza kitufe; "I understand and wish to continue" ...ngoja tu nijipe moyo, kifo cha wengi harusi!!! 😀

 
hahhahahhaha sasa wakuuu naona badala ya ze utamu awe roho juuu na agonized imehamia kwenu maaana mnavyoshushuana? mhhhhhh now i too smell smthing fishyy ..... oh no smthing chickenyyyyy

JOSM bora uendelee na JOSM maana....inaficha mengi
 
Ila watam charge na sheria ipi?

Alisema Shaaban Robert wa KUSADIKIKA, ni rahisi sana kubadilisha mifumo na sheria pale tu matendo makubwa yanapofanywa na kuwagusa Watawala. Usijekushangaa Notice za ile CEO Round Table (kutoka kwa FMES) zikapelekwa Bungeni haraka na kutungiwa sheria ili kijana aweze kusomewa mashtaka. Au watumie ‘Africa's-Own-Democracy" ambayo sasa inachukuliwa kuwa Katiba (Sheria Mama) ya Nchi za Afrika.
 
JOSM bora uendelee na JOSM maana....inaficha mengi
Na furahia sana kuwa mwana Jamii,kwenye jamii kuna watu wa aina mbali mbali wenye upeo wakufikiria na wasio na upeo kabisa.
 
the saga continues,mara he has been nabbed mara he has not,sasa which is which!!!!!!!!!!
 
Hapa kila kitu kitajulikana mwenye kucomment kupost pic n'k.Mkuu nipo kazini,jioni na peleka report,
poa mkuuu naona umekamia kuwatisha wenziooo,endelea bwana kujenga taifa wote tuko mkumbo huohuooo...............
 
poa mkuuu naona umekamia kuwatisha wenziooo,endelea bwana kujenga taifa wote tuko mkumbo huohuooo...............

...kuna wanaotamani hili sheshe lingekuwa mambo ya 'April fool' au uvumi tu kama wa 'popo-bawa', kwani inasemekana;

"Ipo ishara ya wazi kuwa wengi wataangamia na `Mzee wa Ze Utamu`, kwani amewataja wote waliokuwa wakimtumia picha na maelezo yaliyochafua watu pamoja na anuani zao. Vyote sasa vipo mikononi mwa polisi."

source; Mwananchi Read News
 
Na furahia sana kuwa mwana Jamii,kwenye jamii kuna watu wa aina mbali mbali wenye upeo wakufikiria na wasio na upeo kabisa.

Haya kaka nimegusa nyongo yako kidogo tu kidogo ujisahau!!! Yuko wapi ndugu yangu SHY akusaidie kukuonyesha ni jinsi gani ya kuelezea mambo ya ki ICT.. wewe unaposema kuwa web mbalimbali zinasema fulani anahusika na ZEUTAMU kwa nini sasa
 
Na furahia sana kuwa mwana Jamii,kwenye jamii kuna watu wa aina mbali mbali wenye upeo wakufikiria na wasio na upeo kabisa.

Haya kaka nimegusa nyongo yako kidogo tu kidogo ujisahau!!! Yuko wapi ndugu yangu SHY akusaidie kukuonyesha ni jinsi gani ya kuelezea mambo ya ki ICT.. wewe unaposema kuwa web mbalimbali zinasema fulani anahusika na ZEUTAMU kwa nini sasa usitupe link za hizo site.
 
Haya kaka nimegusa nyongo yako kidogo tu kidogo ujisahau!!! Yuko wapi ndugu yangu SHY akusaidie kukuonyesha ni jinsi gani ya kuelezea mambo ya ki ICT.. wewe unaposema kuwa web mbalimbali zinasema fulani anahusika na ZEUTAMU kwa nini sasa usitupe link za hizo site.

Ndugu unatuchafulia thread,futa post yako moja.Sitaki malumbano na wewe heshima mbele.
 
...kuna wanaotamani hili sheshe lingekuwa mambo ya 'April fool' au uvumi tu kama wa 'popo-bawa', kwani inasemekana;
Unaongelea habari hii?

Wengi kuunganishwa na Mzee wa Ze Utamu

Exuper Kachenje

KUKAMATWA kwa mtu anayetuhumiwa kumiliki mtandao wa zeutamu dot com ambao unawakashifu watu mbalimbali maarufu, wakiwemo vigogo wa serikali na wafanyabiashara, kunaweza kusababisha Watanzania wengi zaidi kutiwa mbaroni, Mwananchi imebaini.

Mtu huyo, ambaye anasadikiwa kuwa mtoto wa mmoja wa viongozi wa zamani wa serikali, amerejeshwa nchini baada ya kukamatwa nchini Uingereza mwishoni mwa wiki iliyopita.

Habari zilizolifikia gazeti hili jana zinasema kuwa mtu huyo tayari amewataja watu mbalimbali wa hapa nchini kuwa ndio waliokuwa wakimtumia picha za kuwakashifu watu mbalimbali, wakiwemo wanasiasa, wafanyabiashara, waandishi wa habari na wanafunzi wa vyuo mbalimbali.

Habari za uhakika kutoka vyanzo mbalimbali zinasema kuwa, baada ya kurejeshwa nchini, mtu huyo tayari amehojiwa na jeshi la polisi nchini na kwamba ameonyesha ushirikiano mkubwa.

Ingawa taarifa za kurejeshwa nchini kwa mtu huyo, raia wa Uingereza mwenye asili ya Tanzania, bado hazijathibitishwa na Jeshi la Polisi, habari za kiuchunguzi zinasema kuwa katika mahojiano na polisi, mtu huyo ameweka hadharani majina na anuani za watu wote kutoka Tanzania waliokuwa wakimtumia picha zilizotumika kwenye mtandao huo.

"Yule bwana tayari amerejeshwa nchini na tayari amehojiwa na polisi. Katika mahojiano ameonyesha ushirikiano mkubwa bila hofu," alisema mpashaji habari wetu.

"Ipo ishara ya wazi kuwa wengi wataangamia na `Mzee wa Ze Utamu`, kwani amewataja wote waliokuwa wakimtumia picha na maelezo yaliyochafua watu pamoja na anuani zao. Vyote sasa vipo mikononi mwa polisi."


Katika tovuti hiyo ya
zeutamu dot com iliyoanza kama ukurasa wa maoni binafsi (blog), mmiliki huiweka picha na kutoa maelezo machache na baadaye kuomba maoni. Baada ya hapo, watu wanaotembelea tovuti hiyo huchangia taarifa mbalimbali wanazojua kuhusu mtu huyo na hasa taarifa chafu.

Katika siku za mwishoni mwa tovuti hiyo, mmiliki alianza kuruhusu hata picha za kuunganisha ambazo zililenga kwa kuwachafua wahusika walio kwenye picha hizo, zikiwaonyesha kana kwamba walifanya uchafu.

Lakini mmiliki huyo, ambaye jina lake tunalihifadhi, anasemekana amejitetea kuwa picha hizo alitumiwa na watu ambao ana taarifa zao, hali inayoweza kusababisha watu wengi zaidi wakanaswa ili kusaidia upelelezi.

Habari zinasema kuwa katika orodha iliyotajwa na mmiliki huyo wa Ze Utamu, wamo watu mbalimbali maarufu nchini na kuwa jeshi la polisi lipo mbioni kuwasaka na kuwanasa watu hao tayari kuwachukulia hatua za kisheria.

Kwa mujibu wa vyanzo vyetu vya habari, katika maelezo yake mtu huyo amelieleza Jeshi la Polisi kuwa alianzisha mtandao huo kwa lengo la kufanya biashara, na si kukashifu watu na kuwa umepata usajili halali pamoja na hati zote za usajili nchini Uingereza.


Imeelezwa kuwa mtu huyo alilenga kupata fedha kupitia watu wanaotaka kutumia mtandao huo kwa kutuma picha na taarifa mbalimbali, lakini Watanzania wengi wamekuwa wakimtumia picha na taarifa zinazokashifu watu.

Hata hivyo, Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai, Robert Manumba jana alisema bado hana taarifa za kukamatwa kwa mtu huyo.

"Sina taarifa za mtu huyo, lakini nikipata taarifa zozote juu yake nitawaambia," alisema DCI Manumba.

Naye balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Mwanaidi Maajar aliendelea kudai kuwa hana taarifa za kukamatwa kwa mtu huyo.

Ijumaa iliyopita Mwananchi ilipata taarifa kwa njia ya mtandao na ambayo ilithibitishwa na afisa mmoja wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kuwa ni kweli mtu huyo amekamatwa.

Taarifa hizo zilisema kuwa mtu huyo alinaswa kutokana na juhudi za makachero wa Tanzania na polisi wa kimataifa (interpol) na alikuwa mbioni kurejeshwa nchini.

Habari zilidokeza zaidi kwamba wataalamu wa idara ya upelelezi kutoka Tanzania kwa pamoja na wenzao wa Uingereza, mbali na kumkamata mtuhumiwa huyo, wamepata ushahidi wa kutosha kumhusisha mtuhumiwa huyo na mtandao huo, uliokuwa kipenzi cha vijana.

Watu mbalimbali wamekuwa wakitembelea mtandao huo kwa lengo la kupata taarifa za aina mbalimbali, lakini zilizotamba sana zilikuwa za watu maarufu ambao walichafuliwa kwa kuhusishwa na vitendo vichafu.

Ilifikia wakati mtandao huo ulidiriki kumdhalilisha Rais Jakaya Kikwete, kitendo ambacho kinaonekana ndicho kilichochangia kufutwa kwake na baadaye kuanza kusakwa kwa mmiliki.

Katika ziara yake ya siku nane nchini Marekani, Rais Kikwete pia alitembelea ofisi za makao makuu ya kampuni ya Google, mtandao maarufu hasa kwa kusaidia kupatikana kwa taarifa mbalimbali duniani.

Kwa mujibu wa Sheria ya Kimataifa, mtu anayefanya kosa la uhalifu kama huo anaweza kushtakiwa kwenye nchi ambayo kosa hilo lina madhara.

Mbali na mtuhumiwa huyo, taarifa hizo zinaeleza kuwa Watanzania wengine wawili katika miji ya Wichita na San Diego nchini Marekani, wamehojiwa na polisi kwa kuhusishwa na mtandao huo wa Ze Utamu.

Source: Mwananchi
 
twist and turns at every corner,hii habari kuandikwa na the GUARDIAN on sunday la england gives us a new impetus,NINI kinafichwa?????trust me hili gazeti sio a mickey mouse publication-kuna jambo hapa
 
twist and turns at every corner,hii habari kuandikwa na the GUARDIAN on sunday la england gives us a new impetus,NINI kinafichwa?????trust me hili gazeti sio a mickey mouse publication-kuna jambo hapa

Weka link ya UK Guardian ku cover hiyo habari....
 
Last edited:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom