Sasa akina mkandamizaji watajua kuwa 'kuna sheria' Tanzania.
Manji amewadanganya sasa wataula wa chuya.
hawa jamaa wa eatv inaonyesha kuwa walikuwa wanashibisha matumbo yao kwa kupitia ZE comedy kwa nn wamewang'ang'ania wasitumie vipaji vyao??
Nao hao COSOTA inabidi wamulikwe labda kuna mkono wa mtu.
Lakini tuangalie upende wa shilingi labda kitendo cha hawa jamaa kuomba ulezi kwa Manji utakuwa umewaletea matatizo....si mnajua fika eatv ni ya Mengi sasa Mengi na Manji paka na panya...wanakomoana wakubwa huku wadogo wakiumia sasa.
Sina undugu na Kajura wala Seikh Yahya, lakini haya niliyatabiri hapa...
varangati la ze comedy
KIKUNDI cha Sanaa za Maigizo ya Luninga nchini maarufu kama 'Ze Komedi' kimeulalamikia uongozi wa East Afrika Television (EATV) kwa kuwazuia kutumia majina na uhusika wa uigizaji waliokuwanao katika kituo kingine cha TV kwa madai kuwa ni hati miliki yao.
Akizungumza jana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa Ze Komedy Production, Isaya Mwakisyala alisema uamuzi wa Cosota kukubaliana na ombi la EATV kuwa Ze Komedy ni mali yao katika barua walioiandika Juni 9 na kujibiwa na Cosota Juni 10 kuwa ni mali yao si sawa kwa kuwa wao ni kikundi kinachojitegemea.
"Hatukuanzishwa na EATV bali tulikuwa ni waigizaji kipindi kirefu kabla hata hatujaonekana huko, kinatushangaza na kustaajabisha kitendo cha EATV kudai kuwa Ze Komedy ni mali yao, sisi tuanchosema tutaendelea kuwa huru na kubakia vile vile katika uigizaji huo kama kawaida," alisema Mwakisyala.
Alisema mkataba wa uhalali wa kumiliki kikundi cha Ze Komedy waliupata Julai Mosi mwaka 2007 kwa cheti halali baada ya kusajiliwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata) tofauti na EATV ambao wanadai kupewa umiliki wa Ze Komedy Juni 30 mwaka huu.
Alisema endapo kutatokea kutoelewana kokote baada ya uamuzi wao wa kuingia mkataba na Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC1) ambao uhamasishaji wa matangazo ulianza jana, watakwenda kumuona Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo na ikishindikana watafika kwa Waziri Mkuu na hatimae kwa Rais.
Hata hivyo kurushwa kwa vipindi vya kundi hilo TBC1 kutaanza baada ya wiki mbili zijazo kutokana na safari ya kundi hilo nchini Uingereza baada ya kuahirisha ya kwanza nchini Afrika Kusini kutokana na ghasia zilizokuwapo nchini humo.
Source:www.issamichuzi.blogspot
I love this story
Naona COSOTA wameamua kuwa MAFISADI.... Lets see na mwaka huu unga robo
Sheria Ifwate Mkondo Wake
Waziri Hana Jipya La Kufanya Hapo
Vijana Rudini Kaeni Chini Na Eatv..msidanganyike Na Waziri Yoyote
Mtaishia Porini Na Kusahaulika....
watanzania tumekuwa na kawaida ya kutothamini utaalamu au ushauri wa kitaalam in this case wanasheria.... utasikia wasanii wakilia hakimiliki hakimiliki...ukiwauliza maana yake nini..sidhani hata kama they have a clue... pamoja na ubutu huo..nadhani kama alivyosema mkuu hapo juu we need to help them ila in so helping we shouldnt mislead them kuwafanye waone it is that simple..katika kubadilisha majina inashawishi ku maintain majina yanayofanana..lakini mtu akitaka kuwabana kisheria bado wanaweza kuwa cornered....perhaps the only way out is to change the brand all together..wawe hata na new identity ...kwani kinachojalisha ni hayo majina ya joti,masanja au wakuvanga?.. i dont think so..nadhani wahusika wanapendwa tu..wasihofu kujibadili big tme... go on comrades!!siungi mkono EATV asilani!!!!! they could have done better; lakini tuangalie pia sheria za hakimiliki [ambazo wasanii huzipigania bila kuzijua vizuri]; vilevile nahisi kwamba EATV wametumia ile chachu ya "branding" kuwamaliza wavuja jasho.
Wazo: ili kuwaweza EATV, ningeshauri Ze Comedy wacheze mchezo huo huo wa EATV; how? badili jina kuwa Ze Komidy [with same pronouciation maana najua huzuiwi kutamka kitu kwa namna fulani, branding iko kwenye writings]; Joti anaweza kuitwa Jyoti [or Gyoti] lakini matamshi yaleyale ya zamani; Masanja akawa Masancha, Seki akawa Syeki; and then they make fun of EATV for the rest of their lives
Ni wazo tu...
Maskini wakandamizaji!inasikitisha sana Watanzania kufanyiana hivi!badala ya kuinuana tunapelekana chini!
Mtanzania anaewawekea vingingi the comedyMtanzania unayemzungumzia hapo ni Mengi au Manji?
Mtanzania anaewawekea vingingi the comedy
...ndio yale yale, mke anakukataa unamnyang'anya kanga, mpaka chupi ulizomnunulia, kisa weye ndio uliyemnunulia, hivyo aondoke mwenyewe kama alivyokuja!
mimi nawashauri ikiwezekana kina Seki na wenzake wawaachie EATV hilo jina na hizo characters, tuone kama EATV wataendeshaje ZE Comedy na actors wapya,
...au ndio itabakia 'kujifariji na harufu ya nguo', eti umemkomoa mtu!
Hizo sheria na hakimiliki zinakuwa 'valid' sababu Ze Comedy wameachana na EATV tu? kuna mangapi na wangapi Tanzania hii wanadhulumiwa hakimiliki zao hapa Tanzania kunakochangiwa na vituo 'kama' hivi vya radio na Tv,
...au ndio mnyonge hana haki, na kwakuwa EATV imeshika mpini, vijana wamekamata makali?
Acheni roho mbaya jamani,