Zawadi ya ngono

Zawadi ya ngono

Jamii nzima inatafunwa na ugonjwa wa upungufu wa maadili ambao binafsi nauona kama ni mbaya kuliko hata hata hili gonjwa la ukimwi. Mtu anapofikia kutoa thamani ya utu wake (penzi) ili tu kupata kazi, ama kupandishwa cheo,ama kufaulu katika mtihani flani huyu si mpiganaji ni mwoga wa maisha na hafai hata kwa mchuzi.

Mpiganaji wa kweli hawezi kukipimbia mapambano regardless yapi amekumbana nayo. Tabia ya kupenda kupita shortcut inatugharimu kama taifa. Watu hawataki kuhangaisha akili zao ili kuweza kujikwamua na maisha ila tunapenda kutimiza ndoto zetu pasina kuamka toka usingizini na kuanza kufanya kazi ili ndoto ziwe reality. Wengi wa binadamu ni waoga hata wa kujaribu ila tunataka tuamke asubuhi na kukuta kila kitu kimefanyika sasa ili iwe hivyo inagharimu maadili na utu wetu.

Tabia hii imekuwa na inaendelea kukua hasa kwa upande wa mabinti na wanawake kwa ujumla. Hatukatai ugumu wa maisha ila hawapaswi kujirahisisha kiivyo mie ninaamini kama bahati ni yako ipo itakuwepo tu. Wataalamu wananyimwa ajira kisa rushwa ya ngono imetolewa na baada ya muda taasisi ama kampuni inalalamika utendaji wake umeshuka huu ni wendawazimu ngoja niishie hapa naona hasira zimeanza kupanda nisije aandika vibaya nikala ban bure.

Acha tu!.kuna watu wamefukuzwa kazi kwa kulinda utu wao(kwangu mimi its worth it),.yani unahangaika na mavitabu afu mtu anakuja kutaka tena mengine!..wengi wamekua sexually abused and all naeza sema ni Mungu tu ndie mtetezi wa binadamu yeyote,.ni kuomba hekima tu.
 
On the other side of the coin Liizy naomba nikuulize:
Hivi kuna mwanaume haongi?
Hivi kuna mwanaume analazimishwa kuhonga?
 
Kuna watu wanapenda kuendesha farasi kama fun. Sasa kama mtu anaweza kumtumia farasi kwa starehe, kuna shda gn ktk starehe hyo akam2mia kujiwezesha kutoka sehem 1 kwenda nyingine? Lizzy, kufanya ngono ni starehe, na hata ucpoihongea, utaifanya tu. Sasa kama kuna chanc ya kui2mia kufanikisha mambo yako kuna ubaya gn?

Kwahiyo wewe unaona ni sahihi na haki kwa wale wanaokoseshwa hizo nafasi pamoja na kwamba wamezifanyia kazi?
Kaaazi kweli kweli.
 
On the other side of the coin Liizy naomba nikuulize:
Hivi kuna mwanaume haongi?
Hivi kuna mwanaume analazimishwa kuhonga?
Kuhonga sio ishu, wanapohonganiana ndio ishu.
Wahongane huko mitaani hamna anaejali, na sio sehemu za kazi kwa kupeana nafasi wasizostahili.
 
Kuhonga sio ishu, wanapohonganiana ndio ishu.
Wahongane huko mitaani hamna anaejali, na sio sehemu za kazi kwa kupeana nafasi wasizostahili.
kaaaaaaaaazi kweli kweli!!!!!!
 
Kwahiyo wewe unaona ni sahihi na haki kwa wale wanaokoseshwa hizo nafasi pamoja na kwamba wamezifanyia kazi?
Kaaazi kweli kweli.

Dunia msongamano Lizzy, walisema waungwana. Kila mtu lazima atumie silaha zake zote kupambana na maisha. Zubaa uchekwe.
 
Dunia msongamano Lizzy, walisema waungwana. Kila mtu lazima atumie silaha zake zote kupambana na maisha. Zubaa uchekwe.

Haya bana, usisahau tu kuwafahamisha ndugu na wanao wa kike kama umebahatika kuhusu hii mbinu ili wasije wakachekwa!!
 
Haya bana, usisahau tu kuwafahamisha ndugu na wanao wa kike kama umebahatika kuhusu hii mbinu ili wasije wakachekwa!!

Kama ntakuwa nimezaa wazembe hvo, ambao silaha yao kubwa ni kuhonga ngono, cna jinsi. Ila mi naamin bado zipo claha nyingine, na mjini shule.
 
Kama ntakuwa nimezaa wazembe hvo, ambao silaha yao kubwa ni kuhonga ngono, cna jinsi. Ila mi naamin bado zipo claha nyingine, na mjini shule.

Kila la kheri basi. . . .
 
Dunia msongamano Lizzy, walisema waungwana. Kila mtu lazima atumie silaha zake zote kupambana na maisha. Zubaa uchekwe.
Nikuulize kitu Tuko? nikitumia mawazo haya kwa kuhalalisha kukuua ili nipate gari lako nitakua nimekosea?
Kuna silaha mbali mbali ila sisi kama great thinkers (ngoja na mimi nijifagilie) tunatakiwa kujiuliza kama sikaha hizi ni halali, na kama sio ni kwa nini zinatumiwa, na tunawezaje kupunguza matumizi yake.
Kama wewe unaamini ni halali basi nambie, alafu nikuulize swali la pili.
 
Baada ya majadiliano na rafiki yangu kuhusiana na rushwa (zawadi) ya ngono mashuleni, vyuoni na maofisini nimejikuta najiuliza maswali mengi ambayo ningependa tusaidiane kuyajibu kwasababu kwa namna moja ama nyingine matokeo yake yanaathiri hata mahusiano, ndoa na malezi.

Kwanza ni wazi kabisa kwamba mtu akishaanza ni ngumu kuacha kutokana na ukweli kwamba anakua amejipa ulema wa aina fulani.Kwamba kama alifaulishwa sekondari kuna nafasi kubwa atahitaji kufaulishwa chuoni, na akifaulishwa chuoni kuna nafasi kubwa atahitaji kubebwa pale atakapokua kwenye mchakato wa kupata kazi na baadae kwenye kujiendeleza (kupandishwa cheo, kupata nafasi za masomo, kushirikishwa kwenye semina zinazolipa n.k).

Sasa je. . .
1. Mtu anapoanza kuhonga mwili wake ili afanyiwe kazi yake (kusoma, kuwa na CV kali, good work ethics, experience n.k) kwanini anafanya hivyo?Ni kutojiamini (mwenyewe siwezi) au ni kuzungukwa na watu wasio na imani nae (wazazi, ndugu na jamaa wasioisha kumwambia hatofika popote)???
2.Je kuna hatari gani mtu kutegemea mwili wake badala ya akili na uwezo unaohitajika kupata kazi,kufaulu n.k?
3.Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje?Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
4.Malezi yanachangia vipi kuwafanya ndugu zetu wawe hivyo?

Najua kwa kiasi kikubwa hata system yetu (kupeana kazi kwa kujuana bila kujali sana uwezo wa kazi ) inachangia kwa kiasi kikubwa, maana isingekua inaruhusu ingekua ngumu kutoa na kupokea rushwa ya aina hii ila napenda kuangalia kile kinachowasukuma wahusika zaidi.

Hapa Tanzania kwetu kwanza inategemea na kabila na familia. Kuna ambao wana utamaduni wa kuuza ubongo, yaani kutumia akili zao kwa njia halali na za ujanja ujanja kujitafutia maisha. Kuna wengine wanatumia nguvu yao (mitulinga) kujipatia riziki zao, na kuna wengine wanatumia nyuchi zao kujiafutia maisha. Sitaki kutaja ni makabila gani, lakini watanzania wengi wanajua.

Vilevile kuna wanaume wa makabila fulani ambao wakiona mwanamke kwao kitu cha kwanza ni kufikiri ngono tu, na wengine wanatafuta pesa na nyenzo nyingine mbalimbali katika maisha yao ili kusatisfy hilo. Kwa hiyo ukiangalia hilo ni swala la demand and supply, uwezo wa akili wa mtu, utamaduni, elimu etc. Kwa hiyo hizo ni factor zinazo-determine tabia hiyo.

Lakini kuna wengine hili halihusiano na rushwa, kuombwa au kutaka kutoa, ni nature yao na wanawashwa kila kukikcha, kwa hiyo nao ni demand inawafanya waigawe ovyo. Kuna swala la dini pia, unaweza kuona baadhi ya watu wenye imani fulani wanaongoza kwa hilo. [au kuwa wazi animists wao wanagawa ovyo tu]
 
Kuna haja ya kuweka policy HR wengi wawe wanawake sasa, kama imeonyesha wazi kuwa hii profession wanaume tunaitumia vibaya kuna haja ya kupunguza wanaume kawa waajiri. Ila hili haliwezekani kwa serikali reggae-reggae
 
Baada ya majadiliano na rafiki yangu kuhusiana na rushwa (zawadi) ya ngono mashuleni, vyuoni na maofisini nimejikuta najiuliza maswali mengi ambayo ningependa tusaidiane kuyajibu kwasababu kwa namna moja ama nyingine matokeo yake yanaathiri hata mahusiano, ndoa na malezi.

Kwanza ni wazi kabisa kwamba mtu akishaanza ni ngumu kuacha kutokana na ukweli kwamba anakua amejipa ulema wa aina fulani.Kwamba kama alifaulishwa sekondari kuna nafasi kubwa atahitaji kufaulishwa chuoni, na akifaulishwa chuoni kuna nafasi kubwa atahitaji kubebwa pale atakapokua kwenye mchakato wa kupata kazi na baadae kwenye kujiendeleza (kupandishwa cheo, kupata nafasi za masomo, kushirikishwa kwenye semina zinazolipa n.k).

Sasa je. . .
1. Mtu anapoanza kuhonga mwili wake ili afanyiwe kazi yake (kusoma, kuwa na CV kali, good work ethics, experience n.k) kwanini anafanya hivyo?Ni kutojiamini (mwenyewe siwezi) au ni kuzungukwa na watu wasio na imani nae (wazazi, ndugu na jamaa wasioisha kumwambia hatofika popote)???
2.Je kuna hatari gani mtu kutegemea mwili wake badala ya akili na uwezo unaohitajika kupata kazi,kufaulu n.k?
3.Mtu kama huyu akija kuwa mzazi atakuwaje?Ataweza kumfundisha mtoto wake kuwa tofauti na alivyo yeye?
4.Malezi yanachangia vipi kuwafanya ndugu zetu wawe hivyo?

Najua kwa kiasi kikubwa hata system yetu (kupeana kazi kwa kujuana bila kujali sana uwezo wa kazi ) inachangia kwa kiasi kikubwa, maana isingekua inaruhusu ingekua ngumu kutoa na kupokea rushwa ya aina hii ila napenda kuangalia kile kinachowasukuma wahusika zaidi.
kweli kabisa yan kuna mdada tulikuwa naye chuo acha kabisa, na kufwatilia alipotoka ndo alikuwa hvyo. ts a problem kwa kweli.
 
kuna uzi uliwai kuwekwa hapa jf.na ulikuwa unaelezea ukubwa la tatizo ili la gift ya....
Na ilikuwa inasema 75% kama sikosei ya wanawake walioajiriwa serikalini na sector binafsi walivuliwa sketi.
Nilikua nakazia tu uzi.
asilimia 75?:shock: duh! sijuwi kama tutafika, ila inawezekana, enzi zetu sie wa miaka 47 haya mabo hayakuwepo. hata mimi nangoja nione hapa ni nini kinachangia siku hizi rushwa ya ngono kupanda chati kulikoni ya fedha. mana tunasikia sehemu nyingi tu, hata kule kwenye umiss pia nako kunanuka ngono. mmmhh.
 
Kwenye uwanja wa vita wapiganaji hujitahidi kusoma mapungufu ya maadui zao ili washinde vita. Wanaume wengi hutumia mapungufu ya wanawake kuwini interest zao. Lakini pamoja na hilo katika suala la zawadi ya ngono kuna mambo mengi ambayo yanaweza kumsukuma mtoto wa kike kunasa katika mtego wa wanaume laghai, nitajaribu kutaja machache:
1.Kupenda mteremko, kutaka kitu kwa njia ya mkato.
2.Umaskini, mtu analaghaiwa kwa sababu ya shida alizonazo hivo anaona bora akubali ili yaishe.
3.Kutaka sifa, wengine huamini kuwa akitembea na bosi wk ataonekana yuko juu(high class).Ta
4.Shinikizo au ushawishi kutoka kwa watu wa karibu.
5.Tamaa ya umaarufu.
 
Ili kuondokana na tatizo hili inatubidi kufuata maadili ya kweli,kujikana, kufuata haki na kusimama imaara na kulinda heshima zetu. Vitabu vitakatifu vinasema mwili ni " Hekalu"
 
Mimi nafikiri 'kutumia ngono kujinufaisha kwa akina dada kunasababishwa na haya yafuatayo":
1. Tamaa ya urahisi wa maisha kuliko kujituma
2. Ufinyu wa nidhamu ya kimaadili (very low morality level)
3. Mfumo dume (yaani imani potofu ya kuridhia matakwa ya mwanaume pasipo pingamizi eti kwa sababu yeye ni mtu fulani, wa nafasi fulani au mahali fulani)

4. Kutojiamini na kukata tamaa haraka

Bado tuna safari ndefu ya kuelimisha mabinti kujikomboa, kwani japo wanasema eti "women empowerment" lakini hiyo kuwa empowered tuu mpaka uvue nguo now this is crap.
Akina dada tuweni majasiri kusema HAPANA. Kuwa tayari kulala njaa kuliko kudhalilishwa. I urge all you ladies, you are so beautiful why lowering yourself that much bwana.
Say NO to hypocricy, bureaucracy........say no!!
😛oa
 
Back
Top Bottom