Zanzibar tushakuwa tayari kujitenga

Zanzibar tushakuwa tayari kujitenga

mkuu...bidhaa za bakhresa zinanunuliwa sana na nani yaani...market.. na ipo wapi.?

Mkuu nenda katika record za TRA uhakikishe hilo na jiulize wewe kwa siku umenunua bidhaa ngapi za Bakhressa, Kama hujanunua maji ya kunywa umenunua mkate, kama sio mkate, ice cream, kama sio ice cream umepanga katika nyumba zake, kama sio kupanga umekula ugali wa unga wake, kama sio ugali chapati ulizokula zimetoka katika unga wake supu asubuhi, Jamaa anatisha
 
mkuu...bidhaa za bakhresa zinanunuliwa sana na nani yaani...market.. na ipo wapi.?


Mkuu nenda katika record za TRA uhakikishe hilo na jiulize wewe kwa siku umenunua bidhaa ngapi za Bakhressa, Kama hujanunua maji ya kunywa umenunua mkate, kama sio mkate, ice cream, kama sio ice cream umepanga katika nyumba zake, kama sio kupanga umekula ugali wa unga wake, kama sio ugali chapati ulizokula zimetoka katika unga wake supu asubuhi, Jamaa anatisha

mkuu... mbona haujajibu swali langu... ? lipo straignt
 
Ukweli ni kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Lakini kama watu tunaungana lakini upande mmoja unahisi kuonewa bora tutengane halafu baadaye tukishajiona tupo fit kuungana ndiyo tuungane tena. Hata sisi wabara huu muungano hatuuelewi yaani tupo tupo tu. Hapa kuna options 3:

1. Tutengane kila mtu atembee kivyake
2. Tuwe na serikali moja tu na au,
3. Tu na serikali ya Tanganyika, Zanzibar na ya Jamhuri ya muungano.

Vinginevyo huu muungano wa sasa ni kiini macho tu....
 
mkuu... mbona haujajibu swali langu... ? lipo straignt

Mkuu wangu nimekujibu,

Isome vizuri post iliyopita kwa kukurahisishia ni hivi ukitaka kujua market ya bakhressa toka nje ya ofisi yako zunguka mjini. Kwa siku mmoja jiulize umetumia bidhaa ngapi za Bakhressa. Ameshikilia kwa authority tena soko la unga ngano Tanzania nzima, Kenya, Uganda, Zambia na Misri. Huyu jamaa anameshikilia soko la ice cream mpaka lamba lamba zile walizokuwa wakifanya machinga na walalahoi amechukua yeye, amewekeza katika majengo, vitu vyengine vidogo vidogo, mtu mpaka ameikopesha serikali kwa kutumia Tbills cheki na BOT utaona. Ameshikilia pia soko la mafuta zanzibar (oil), boti za majini. Sasa anakimbizana na soko la unga wa sembe, madini , Jamaa anatisha ndugu.
 
Ukweli ni kuwa umoja ni nguvu na utengano ni udhaifu. Lakini kama watu tunaungana lakini upande mmoja unahisi kuonewa bora tutengane halafu baadaye tukishajiona tupo fit kuungana ndiyo tuungane tena. Hata sisi wabara huu muungano hatuuelewi yaani tupo tupo tu. Hapa kuna options 3:

1. Tutengane kila mtu atembee kivyake
2. Tuwe na serikali moja tu na au,
3. Tu na serikali ya Tanganyika, Zanzibar na ya Jamhuri ya muungano.

Vinginevyo huu muungano wa sasa ni kiini macho tu....
mkuu,

wewe jisaidie kwa kusoma hapa. bofya
http://www.kituochakatiba.org/index2.php?option=com_docman&task=doc_view&gid=1208&Itemid=27

vipo vyengine vingi, pia utauelewa tu kama una nia ya kuelewa.
 
baada ya marekebisho ya katiba ya mwaka jana yaliyofanyika tayari mlishajitenga kasoro jina ndio limebaki kuonyesha kuwa kuna muungano ila mmeng'ang'ania nafasi nyingi za ajira bara za kisiasa na za serikalini mmepora ardhi nyingi bara hata mashamba ya mipunga kyela kwa kuwapa hela kiduchu wakulima mmetengeneza uchochoro mkubwa wa bidhaa feki zilizopo bara na ndio chanzo cha ukosefu wa mapato bara ya TRA mmekuwa wasafirishaji wa mazao ya misitu kutoka bara kupitia bandari bubu kwa kweli hata sisi tunaona huu muungano ni biashara kichaa tumieni mwanya wa marekebisho ya katiba kubadilisha jina ili muitwe jamhuri ya zanzibar tuachane kabisa

Watakuwa na uhuru wa kuchagua kuwa raia wa sehemu yoyote ya iliyokuwa Jamhuri, na bila shaka wengi wao watabakia Tanganyika
 
tumeona watu wa sudani kusini wamepiga kura ya kujitenga na sudani kaskazini wadau mnafikiri zanzibar nayo itaanzisha mchakato wa kujitenga na tanzania bara.
 
watuachie tu visiwa vyetu halafu wahame kama wale wenzao wanaoishi Oman sasa
 
watuachie tu visiwa vyetu halafu wahame kama wale wenzao wanaoishi Oman sasa

Geza ulole nataka nikuulize suala la kizushi.

Mansour Yussuf Himid na Mahmoud Thabit Kombo ni wapinduzi au wapinduliwa?
 
tumeona watu wa sudani kusini wamepiga kura ya kujitenga na sudani kaskazini wadau mnafikiri zanzibar nayo itaanzisha mchakato wa kujitenga na tanzania bara.

and then Arusha, Kilimanjaro, Mwanza, Shinyanga, Tanga, Mara, Kagera :tongue:

tanzania-political-map.jpg
 
Mbona Zanzibar walishajitenga siku nyingi wakabadilisha hata katiba bila kushirikisha iliyokuwa katiba ya Muungano. Wajitenge mara ya ngapi? Hawa mawaziri waliopo kwenye serikali ya Tanganyika wapo kufanya vibarua tu kama exchanging Programm. Ndiyo maana Wanajeshi na Polisi Watanganyika wako Zanzibar.
 
Ha! ondokeni hata kesho, kwani nani kawakataza? mimi kama raia wa kawaida sipati faida yoyote ya uwepo wenu,sana sana hasara kwa sababu mnanizibia nafasi yangu mjengoni!
Utaonaje na kupataje faida wakati wakubwa zenu ndio wamekita mirija ,afu raia wakawaida wa Tanganyika hawezi kabisa kuhisi uonevu unaofanyiwa Zanzibar. Kwa mfano wakubwa zenu wamekula hela ya nchi na wanaendelea kula kwa mlango wa nyuma(Kulipwa kwa dowans ufahamu hela inaenda wapi) ,unahisi joto hilo kwa kupanda kwa bidhaa ukiwemo umeme maji kama mnayo na mambo mengi madogomadogo ambayo bei zinapaa ,yote hayo hutokana na wezi unaofanyika. Sasa Zanzibar nao kila wakipiga mahesabu wanaona wanaibiwa na kivuli cha Muungano hewa,wezi unaofanywa unaiathiri Zanzibar kwa sehemu kubwa sana ,ukiangalia njia za mapato zote zimebanwa na hayo mapato yakikusanywa yanavushwa bara ,huku bara haijulikani hela hiyo inaishia kwa nani.

Sasa huku mambo yeshaiva Raisi kivuli na Raisi original weshaweka gea ya kupandishia mlima na mambo yameanza kunoga ,ndio mkaambiwa mambu tayari ,hapa watu hawachezi kibereko.
 
Mkuu LAT,

Sijasahau na maji ya kunywa ya Uhai ambayo yapo mpaka ya shillingi 50 tehetehe ukisikia kiu wajipendelea tu. Jamaa amedominate sana biashara Tanzania kiasi anaua biashara za wenzie.
 
Baada ya hapo watagundua kumbe siyo wamoja."wataaza, hawa ni wapemba na wao ni wazanzibar" dhambi hii itawatafuna mpaka wabaki skeleton
 
Baada ya hapo watagundua kumbe siyo wamoja."wataaza, hawa ni wapemba na wao ni wazanzibar" dhambi hii itawatafuna mpaka wabaki skeleton
Hilo tatizo haliwahusu nyinyi ni la WaZanzibari wenyewe ,unajua jini likujualo halikuli likakumaliza au likakwisha ,sasa nyinyi hamtujui yaani wacha kutumaliza bali mnatuangamiza kabsaa ,Baba yenu wa Taifa si aliwambia kama angekuwa na uwezo angevisogeza visiwa vya Zanzibar mbali kabisa hata visionekane ,sababu kama mlikuwa hamuijui basi kuanzia sasa mtajua kuwa ni huu mwamko wa kisiasa ulioikumba Tanganyika na kutaka kukiondoa madarakani Chama cha Baba yenu wa Taifa.
 
Maswali ambayo nimekuwa nauliza na hakuna Mzanzibar aliyewahi kunijibu ni kuwa
1. Tanganyika itapoteza nini kwa Zanzibar kujitenga?
2. Kwanini Wazanzibar wasiondoke kwanza bara wakadai nchi yao wakiwa kwao?
3. Wazanzibar 400,000 wanafanya nini bara Vs Wabara 1000 walioko visiwani
4. Wazanzibar zaidi ya 50 wanafanya nini latika bunge la bara? mbona hawasusii bunge na kurudi kwenye baraza lao la uwakilishi.
5. Kwa uchumi wa bilioni 500, wabara wanafaidika nini kutoka Zanzibar? Hii ni sawa na bajeti ya wizara ya akina mama na watoto au mapato ya soko la kariakoo.
6. Zanzibar inachangia kiasi gani kuendesha serikali ya muungano.

Tujadiliane kwa haya

Justification ya muungano hapa si mapato bali usalama. Refer Cuba Vs USA. Hivyo ndivyo utakavyojibiwa na watawala
 
tumeona watu wa sudani kusini wamepiga kura ya kujitenga na sudani kaskazini wadau mnafikiri zanzibar nayo itaanzisha mchakato wa kujitenga na tanzania bara.

Kufuatilia marekebisho ya katiba ya 2010 Zanzibar ilishakuwa nchi hata kabla ya Sudan Kusini.

Itakayofuata sasa ni Tanganyika ambayo ilikuwa sii nchi itabidi sasa iwe nchi baada ya zanzibar kujitangaza kuwa nchi badala ya sehemu ya muungano.
 
Marais Wote wa Zanzibar wa Zamani wana Nyumba Bara na Watoto wao baadhi yao wanaishi Bara
Wafanya Biashara wengi wa Zanzibar wanaishi bara mkubwa akiwa Bahressa... Ina maana biashara itakufa akirudishwa Zanzibar
Kuna Wapemba Wengi Dar na wengi wao wafanya biashara hawafaidi na Biashara Zanzibar; kwahiyo inaonekana watachagua Bara
Matatizo ni Wazanzibari Wapemba wanajiona wako Karibu zaidi ya Bara kuliko Zanzibar angalia pia PEMBA itataka kura ya kujitoa ZANZIBAR
Matatizo sio CCM, kuna Matabaka Zanzibar hao weuzi wa Zanzibar sijui watawapenda Waarabu wa Zanzibar
Pemba ndio wanaonekana kuwa wana Mafuta zaidi ya Zanzibar wachunge Wazanzibar wanachotaka wakakosa kila kitu...

KURA NI ZANZIBAR na PEMBA --- Chungeni Wanzibar!!!!
 
Fanyeni fasta, mnatunyonya tu wavivu wakubwa nyie!!!!!!!!!!!!

Tawire mwana tumewadekeza saanaa!; sasa wanadeka unapo bebwa kunja miguu ubebwe vizuri wee ndio kwanza unanyoosha vimiguu vyako kivyao mwana! tumesha choka na ghilba zao!
 
Back
Top Bottom