Mkuu Dega umoja ni nguvu, mwanzo tulikuwa wawili, mkubwa na mdogo, tukaungana tukawa kitu kimoja, mkubwa kawa mkubwa zaidi na mdogo kawa mkubwa. Hakuna anayetaka kuvitwaa hivyo visiwa bali tumekuwa kitu kimoja. Usiangalie changamoto tuu za muungano angalia faida na manufaa ya muungano, kiukweli kabisa anayefaidi zaidi huu muungano wetu adhimu ni visiwani!, angalia maduka ya Wapemba yalivyo tapakaa huku Bara. Zingeletwa takwimu za umiliki ardhi wenzetu mnamiliki ardhi ya bara kuliko ardhi yote ya visiwa vyenu. Karibu nusu kama sio yote ya yale maghorofa ya Kariakoo na Ilala ni ya Wapemba. Angalia ghorofa la Muzamil hapo Darajani Zanzibar ulinganishe na lile la Mtaa wa Kongo hapa Dar.
Angalia biashara za Bakhresa Zanzibar ulinganishe na huku Bara, kiukweli watu wanaofaidika zaidi na muungano huu ni wenzetu Wazanzibari tena baada ya yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, kama sio muungano saa hizi tungekuwa tunazungumza mengine.
P