Tatizo lako kubwa ni kuwa umejazwa ujinga ndani ya kichwa chako na wewe umeupokea mzima-mzima.
Ni vigumu sana kuanza kukusomesha historia ya uhakika, lakini hapa umefika, utalipata somo hilo.
Kwanza, elewa kuwa umedanganywa kuwa Waarabu "walifikia", napenda kukujuza kuwa Waarabu hawakufikia pahala, Waarabu hii Afrika ni yao na hata jina la Afrika linatokana na Kiarabu na Uarabu si nchi, Uarabu ni lugha, hapa Afrika lugha inayoongewa na wengi kuliko wowote ni Kiarabu na Waarabu wako wengi Afrika kuliko kwingine kokote. Na nna-kuhakikishia hawakuja kama ulivyodanganywa.
Isitoshe, hivi wewe katika akili yako, aje Mwaarabu asafiri kwa miguu kutoka Bwagamoyo mpaka Kigoma na Kongo, akamate watumwa njiani kote huko, vijikaka vya kibantu vilivyojaa vigimbi kwa kumbizana na ndezi, wawakamate tu wawapeleke kama mizoga? inakuingia akilini? wakati hao hao wanaoambiwa walikuwa wakikamatwa utumwa tunasoma kuwa walifanya "resistance" walipokuja wazungu (soma visa vya Mkwawa, Kimweri, Majimaji, Mirambo na wengineo). Sasa jiulize, hivi vipi hawakufanya "resistance" kwa Waarabu wafanye ressistance kwa wazungu?
Ukipata jibu, njoo, tuendelee na darsa.