Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania

Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania

Status
Not open for further replies.
Na hivi huu muungano una faida zipi kwa sote? bara na visiwani.
Hili swali nauliza kila siku hakuna anayetoa jibu. Why are we so busy na huo muungano? Kama Zanzibar wameshatengeneza katiba yao na kuitambua Zanzibar kama nchi, kwanini tuendelee kuwa na muungano? Tuvunje muungano, halafu tuungane na Zanzibar kwenye federation ya East Africa. Huu mwingine ni upuuzi tu. Na sielewi ni kwanini wabara ndiyo tunaonekana kuutaka sana huu muungano? Tunang'ang'ania muungano na kanchi kenye watu wasiozidi milioni mbili halafu kanataka tushare resources sawasawa kama zote ni nchi? Huu ni upuuzi kabisa. Either iwe mkoa wa Tanzania au tuvunje muungano. Huo ndiyo utabaki msimamo wangu through out.
 
Wanasahau kuwa Zanzibar ilikuwepo kabla ya Tanzania. Wanasahu kuwa hata Tanganyika ilikuwa part ya Zanzibar.

Mimi nauliza hivi huu muungano una faida zipi kwa wote hata ukae ujadiliwe miaka nenda miaka rudi?
Nakubaliana na wewe katika yaliyo mengi kuhusiana na muungano. Mimi pia sioni sababu ya kuwa na muungano. Lakini hoja ya kwamba eti Tanganyika ilikuwa ni sehemu ya Zanzibar hapa, umejidhalilisha. Maana hao wazanzibar unaowafahamu wewe walipelekwa hapo kisiwani na waarabu, wakitokea Tanganyika kama watumwa. Na hicho kilikuwa ni mmojawapo ya kiini cha hoja ya muungano, kwamba wazanzibar na watanganyika wana undugu wa damu. Sasa inashangaza unapotaka kutudanganya eti Tanganyika ilikuwa sehemu ya Zanzibar, lini, na ilikuwaje hadi ikawa sehemu ya Zanzibar. Tujenge hoja za kutusaidia kwa sasa.

Habari za muungano sijui wa serikali tatu, sijui mbili, hazitusaidii kwa sasa. Ama tufute muungano au tuunde nchi moja itakayoongozwa kwa mfumo wa majimbo. Kama mfumo wa marekani, ambako kila jimbo linakuwa na mamlaka kamili. Hiyo ndiyo njia pekee iliyobaki. Habari za serikali tatu au mbili ni kupotezeana muda na kutusababishia umasikini usio wa lazima.
 
Kwa hakika wewe kweli mbulula hivi Seychelles ina watu wangapi,Mauritius,Cape Varde,Kuwait hivi zote hizi zina watu wachachae kulikoni hata Zanzibar mbona zina Serikali zao,iweje uhoji kuhusu Zanzibar....Mutaiyona hivihivi na uchoyo wenu wa JOKA LA MDIMU


Sumbawanga.
BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, wametaka katika katiba ijayo kuwe na muundo wa Serikali moja, huku Zanzibar ikiwa ni moja ya mikoa ya nchi ya Tanzania na iwapo Wazanzibari watakataa, waruhusiwe kujitenga.

Mmoja wa wajumbe wa baraza hilo la Katiba Wilaya ya Kalambo, Afred Ntinda mkazi wa kata ya Mwazye kijiji cha Mpenje alisema hayo jana wakati akichangia maoni katika kikao cha baraza hilo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya mjini hapa.

Mpenje alisema kuwa mfumo wa sasa wa Serikali mbili una kasoro nyingi na umeshindwa kutatua kero za Muungano hivyo hautakiwi kuendelea kuwepo wakati ule wa Serikali tatu hawezi kulinda muungano huo kwa kuwa Serikali hizo zinaweza kuongozwa na marais kutoka vyama tofauti vya siasa na wenye mitizamo isiyolingana hivyo kuna hatari ya muungano kuvunjika.

“Sisi huku bara kuwa na Serikali moja si tatizo wengi wataridhia, nafikiri kuna tatizo katika upokeaji wa maoni kwa wenzetu wa Zanzibar.

Source: Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania - Habari Ya Ndani - mwananchi.co.tz

Binafsi naunga mkono hoja! Zanzibar ina watu wachache kuliko hata mkoa wa Mbeya, inatoa wapi sifa ya kuwa nchi. Iwe tu mkoa wa Tanzania.
 
Kwa hakika wewe kweli mbulula hivi Seychelles ina watu wangapi,Mauritius,Cape Varde,Kuwait hivi zote hizi zina watu wachachae kulikoni hata Zanzibar mbona zina Serikali zao,iweje uhoji kuhusu Zanzibar....Mutaiyona hivihivi na uchoyo wenu wa JOKA LA MDIMU
Nimejenga hoja in comparative to Tanganyika. Kwamba kama baadhi ya sehemu za Tanganyika zina watu milioni tatu hadi nne, na zinaitwa mikoa, ni kwa vipi upande mwingine wa Tanganyika hiyo hiyo, yenye watu wachache kuliko baadhi ya mikoa, iitwe nchi? Ni ama tuifanye hiyo sehemu ndogo ya nchi ambayo ina idadi chache kuliko baadhi ya mikoa kuwa ni mkoa pia, au tuiache ijitegemee. Lakini hakuna haja ya kuwa na li-nchi likubwa lenye wakazi milioni 45 halafu na kanchi kadogo kenye watu milioni moja na nusu halafu tukataka hizi zote zipate haki sawa kama nchi, huku kuna mikoa yenye watu wengi zaidi inakosa hiyo opportunity. Kwanini tuwajali zaidi watu milioni moja na nusu walioko Zanzibar, kiasi cha kuwapa mamlaka makubwa ya kujiamulia mambo yao, kuliko watu milioni tano waliopo Dar es salaam?
Either Zanzibar iwe ni mojawapo ya jimbo la Tanganyika au iondoke, ikajitegemee.
 
Nakubaliana na wewe katika yaliyo mengi kuhusiana na muungano. Mimi pia sioni sababu ya kuwa na muungano. Lakini hoja ya kwamba eti Tanganyika ilikuwa ni sehemu ya Zanzibar hapa, umejidhalilisha. Maana hao wazanzibar unaowafahamu wewe walipelekwa hapo kisiwani na waarabu, wakitokea Tanganyika kama watumwa. Na hicho kilikuwa ni mmojawapo ya kiini cha hoja ya muungano, kwamba wazanzibar na watanganyika wana undugu wa damu. Sasa inashangaza unapotaka kutudanganya eti Tanganyika ilikuwa sehemu ya Zanzibar, lini, na ilikuwaje hadi ikawa sehemu ya Zanzibar. Tujenge hoja za kutusaidia kwa sasa.

Habari za muungano sijui wa serikali tatu, sijui mbili, hazitusaidii kwa sasa. Ama tufute muungano au tuunde nchi moja itakayoongozwa kwa mfumo wa majimbo. Kama mfumo wa marekani, ambako kila jimbo linakuwa na mamlaka kamili. Hiyo ndiyo njia pekee iliyobaki. Habari za serikali tatu au mbili ni kupotezeana muda na kutusababishia umasikini usio wa lazima.

Waliowauzia watumwa Waarabu walikuwa ni wa nchi gani vile?
 
Waliowauzia watumwa Waarabu walikuwa ni wa nchi gani vile?
FaizaFoxy usijitoe ufahamu. Waarabu walifikia kwanza Zanzibar, ambako waliwachukua baadhi ya watu huko, na kwenda nao Tanganyika ambapo hao mburula wa Zanzibar walikubali kutumiwa na waarabu kufanya kazi ya kuwakamata watanganyika na kuwauzia waarabu. Hiyo haiifanyi Tanganyika kuwa sehemu ya Zanzibar.
 
Last edited by a moderator:
Duh kumbe kuna great thinker wengi Tanzania Alfred Ntindi anastahili pongezi kubwa kwa mchango wake wenye mashiko.



Sumbawanga.
BAADHI ya wajumbe wa Baraza la Katiba la Wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, wametaka katika katiba ijayo kuwe na muundo wa Serikali moja, huku Zanzibar ikiwa ni moja ya mikoa ya nchi ya Tanzania na iwapo Wazanzibari watakataa, waruhusiwe kujitenga.

Mmoja wa wajumbe wa baraza hilo la Katiba Wilaya ya Kalambo, Afred Ntinda mkazi wa kata ya Mwazye kijiji cha Mpenje alisema hayo jana wakati akichangia maoni katika kikao cha baraza hilo kilichofanyika kwenye Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya mjini hapa.

Mpenje alisema kuwa mfumo wa sasa wa Serikali mbili una kasoro nyingi na umeshindwa kutatua kero za Muungano hivyo hautakiwi kuendelea kuwepo wakati ule wa Serikali tatu hawezi kulinda muungano huo kwa kuwa Serikali hizo zinaweza kuongozwa na marais kutoka vyama tofauti vya siasa na wenye mitizamo isiyolingana hivyo kuna hatari ya muungano kuvunjika.

“Sisi huku bara kuwa na Serikali moja si tatizo wengi wataridhia, nafikiri kuna tatizo katika upokeaji wa maoni kwa wenzetu wa Zanzibar.

Source: Zanzibar iwe mkoa wa Tanzania - Habari Ya Ndani - mwananchi.co.tz

Binafsi naunga mkono hoja! Zanzibar ina watu wachache kuliko hata mkoa wa Mbeya, inatoa wapi sifa ya kuwa nchi. Iwe tu mkoa wa Tanzania.
 
...Pengine hata hawajui kama kuna katiba ya Zanzibar inayotambua Zanzibar kama nchi....
Mtoto hata akijitambulisha kwa watu kuwa yeye ni baba, bado haisaidii. Cha msingi hapa ni kuangalia katiba ya Muungano inasemaje, sio katiba ya Zanzibar inasemaje!
 
Hiyo sio hoja ya msingi kwani Zanzibar ilikuwepo kabla ya muungano na wala zanzibar haitegemei misaada kutoka bara kujiendesha kumbuka kama zanzibar inapata 4.5% hili ikiwa ni gawanyo la kodi ya VAT na misaada kutoka nje na mpaka wawakilishi wapige kelele ndio tupate.Hisa za Zanzibar 11% kuanzishwa kwa EAC ambazo baada ya kuvunjika zilitumika kuanzisha BOT mpaka muda huu Zanzibar haijapata gawanyo lake,sasa najiuliza Wazanzibar wao ndio wanaowanyonya watanganyika au watanganyika ndio wanaowanyonya wazanzibar ,maana tunaona leo makusanyo yote ya VAT na income tax yanaingizwa katika hazina kuu ya JMT na sio SMZ.
Sisi tunasema Wazanzibar kwa muungano huu bora basi,kwani ni muungano uliohodhi vyanzo vyote vya mapato ya nchi yetu mfano BOT,VAT,INCOME TAX,ANGA,BANDARI KUU, MISAADA KUTOKA NJE,KUJIUNGA NA MATAIFA YA NJE.Na kichekesho zaidi hakuna hata mzanzibar mmoja aliewahi kuongoza vitengo hivi
Nimejenga hoja in comparative to Tanganyika. Kwamba kama baadhi ya sehemu za Tanganyika zina watu milioni tatu hadi nne, na zinaitwa mikoa, ni kwa vipi upande mwingine wa Tanganyika hiyo hiyo, yenye watu wachache kuliko baadhi ya mikoa, iitwe nchi? Ni ama tuifanye hiyo sehemu ndogo ya nchi ambayo ina idadi chache kuliko baadhi ya mikoa kuwa ni mkoa pia, au tuiache ijitegemee. Lakini hakuna haja ya kuwa na li-nchi likubwa lenye wakazi milioni 45 halafu na kanchi kadogo kenye watu milioni moja na nusu halafu tukataka hizi zote zipate haki sawa kama nchi, huku kuna mikoa yenye watu wengi zaidi inakosa hiyo opportunity. Kwanini tuwajali zaidi watu milioni moja na nusu walioko Zanzibar, kiasi cha kuwapa mamlaka makubwa ya kujiamulia mambo yao, kuliko watu milioni tano waliopo Dar es salaam?
Either Zanzibar iwe ni mojawapo ya jimbo la Tanganyika au iondoke, ikajitegemee.
 
Zanzibar SI NI Nchi ? hayo mawazo yametoka wapi tena? Unataka kuchezea bakora nini? Au unataka kulia km naniii :Cry:
 
Kuna haiti ni ndogo kuliko zanzibar na nchi kamili na inamaendeleo kuliko hata tanzania kwa ujumla
 
Huu muungano hauna tija yoyote zaidi ya kutaka misifa tu kutoka kwa wakubwa. Hata ukivunjika hakuna cha kupoteza.
 
FaizaFoxy usijitoe ufahamu. Waarabu walifikia kwanza Zanzibar, ambako waliwachukua baadhi ya watu huko, na kwenda nao Tanganyika ambapo hao mburula wa Zanzibar walikubali kutumiwa na waarabu kufanya kazi ya kuwakamata watanganyika na kuwauzia waarabu. Hiyo haiifanyi Tanganyika kuwa sehemu ya Zanzibar.

Tatizo lako kubwa ni kuwa umejazwa ujinga ndani ya kichwa chako na wewe umeupokea mzima-mzima.

Ni vigumu sana kuanza kukusomesha historia ya uhakika, lakini hapa umefika, utalipata somo hilo.

Kwanza, elewa kuwa umedanganywa kuwa Waarabu "walifikia", napenda kukujuza kuwa Waarabu hawakufikia pahala, Waarabu hii Afrika ni yao na hata jina la Afrika linatokana na Kiarabu na Uarabu si nchi, Uarabu ni lugha, hapa Afrika lugha inayoongewa na wengi kuliko wowote ni Kiarabu na Waarabu wako wengi Afrika kuliko kwingine kokote. Na nna-kuhakikishia hawakuja kama ulivyodanganywa.

Isitoshe, hivi wewe katika akili yako, aje Mwaarabu asafiri kwa miguu kutoka Bwagamoyo mpaka Kigoma na Kongo, akamate watumwa njiani kote huko, vijikaka vya kibantu vilivyojaa vigimbi kwa kumbizana na ndezi, wawakamate tu wawapeleke kama mizoga? inakuingia akilini? wakati hao hao wanaoambiwa walikuwa wakikamatwa utumwa tunasoma kuwa walifanya "resistance" walipokuja wazungu (soma visa vya Mkwawa, Kimweri, Majimaji, Mirambo na wengineo). Sasa jiulize, hivi vipi hawakufanya "resistance" kwa Waarabu wafanye "resistance" kwa wazungu?

Ukipata jibu, njoo, tuendelee na darsa.
 
Hiyo sio hoja ya msingi kwani Zanzibar ilikuwepo kabla ya muungano na wala zanzibar haitegemei misaada kutoka bara kujiendesha kumbuka kama zanzibar inapata 4.5% hili ikiwa ni gawanyo la kodi ya VAT na misaada kutoka nje na mpaka wawakilishi wapige kelele ndio tupate.Hisa za Zanzibar 11% kuanzishwa kwa EAC ambazo baada ya kuvunjika zilitumika kuanzisha BOT mpaka muda huu Zanzibar haijapata gawanyo lake,sasa najiuliza Wazanzibar wao ndio wanaowanyonya watanganyika au watanganyika ndio wanaowanyonya wazanzibar ,maana tunaona leo makusanyo yote ya VAT na income tax yanaingizwa katika hazina kuu ya JMT na sio SMZ.
Sisi tunasema Wazanzibar kwa muungano huu bora basi,kwani ni muungano uliohodhi vyanzo vyote vya mapato ya nchi yetu mfano BOT,VAT,INCOME TAX,ANGA,BANDARI KUU, MISAADA KUTOKA NJE,KUJIUNGA NA MATAIFA YA NJE.Na kichekesho zaidi hakuna hata mzanzibar mmoja aliewahi kuongoza vitengo hivi
Pamoja na malalamiko haya yote, wakati tume ya katiba ikiwa Zanzibar, ilikuwa ni aghalabu kuwasikia wazanzibar wakipendekeza muungano uvunjwe. Wengi wao walikuwa wanaishia kutaka uboreshwe, akiwemo Seif. Sasa ninachojiuliza, kama hadi leo mnaona muungano unawaumiza mbona hamuamui kujitoa? Kwani kinachowazuia ni nini? Watanganyika wanalalamika usiku na mchana kwamba Zanzibar ni mzigo kwa Tanganyika na wanataka muuangano uvunjwe, mbona nyie hamuungi mkono kampeni hizo?
 
Naona mnataka kuwaharibia SWAUMU watu wa zanzbar,

M sure walivyosoma hiyo habari wametukana kimoyo moyo
 
Mbona UAMSHO mpaka leo wako ndani kwa kupinga muungano je dada yangu

unaweza kuniambia UAMSHO walikuwa kwenye ukweli?

Sina uzoefu na mambo ya uamsho lakini kwa kuwa umenipa changa moto InshaAllah ntawasoma na kupitia habari zao kisha ntakuja na jibu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom