Watanzania hivi karibuni tumeshuhudia makundi mawili makubwa yanayo utaka Urais ie Kundi la Mafisadi kwa upande mmoja na kundi la Wapinga ufisadi.
Kundi la mafisadi lilanonekana lilijipanga muda mrefu na lina fedha nyingi ambazo limekua likizitumia ili mgombea wao aweze kuibukaa mshindi wa kuiwakilisha CCM kama mgombea. Kundi la Wapinga ufisadi nalo limejikita katika kutetea uzalendo zaidi.
Sasa kwakua kuna kila dalili kwamba Chadema haitaweza kutwaa nchi, na kwakuwa kuna mkinzano mkubwa kati ya makundi haya mawili mimi nashauri kwamba Rais ajaye wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania atoke Zanzibar.
Hii itakuwa imeyakata kilimilimi makundi haya ambayo yameacha kufanya kazi za kujenga nchi kwa kuwaza Urais tu. Pia hii itafanya Zanzibar nayo itoe walau Rais wa pili wa Muungano maana zaidi ya Mwinyi hakuna mwingine aliyetoka Zanzibar.
Hii itakuwa safi kama vile Mtaange wa kugombea Uspika kati ya Chenge (akiwakilisha kundi la mafisadi) na Sitta aliyewakilisha kundi la kupinga ufisadi.
CCM ilitumia busara na kuyapiga chini makundi yote na kumchagua mwanamama. Naona CCM pia inaweza kumpata compromise candidate kwa kumtoa mgombea Zanzibar.
Hii imekaaje wadau?
Nyie wabara kila wakati mnataka mtu toka bara tu sasa huo ni muungano gani? Hata mwinyi ni mtu wa bara maana katokea bagamoyo so zanzibar actually haijawahi kutoa rais. 2015 zamu ya znz
Kwa nini tulinde Muungano?Tutafakari ili kuulinda muungano wetu.
Sitakutusi ila nitakuuliza ile katiba ya Zanzibar ya sasa umeisoma? Ndugu hatuko pamoja tena! Hata hao UAMSHO wanalijua hili. Ndugu muungano haupo! tusidanganyane!Ndugu wana bodi na wenye akili na iq ya kupambanua mambo ya kisiasa tujadili jambo hili bila jazba wala matusi. Mimi nikiwa mmoja wa vijana wanaotaka kuiona tanzania yetu ikisonga mbele kimaemdeleo na kiuchumi pamoja na afya ningefurahi kuona rais ajae either atoke chadema cuf tlp nccr mageuzi na hata hata sisiemu atoke upande wa pili wa muungano wetu nikimanisha atoke zanzibar due to tje fact that marais watatu wametoka tanzania bara hiyo haina uwiano wa kimadaraka. Kwa nini rais ajae asitokee zanzibar ama ndio nduguzetu hawana uwezo na iq ya kuongoza. Tutafakari ili kuulinda muungano wetu. Nawasilisha
Fahamu ya kwamba rais wa Tanzania 2015 ni LAZIMA AWE MKRISTO. Sasa jiulize je Wazanzibar mna mtu ambaye ni MKRISTO na anafaa kuwa rais 2015? Kama jibu ni hakuna basi kaeni kimya.
Kwa nini tulinde Muungano?
Muungano una faida gani kwa Mtanganyika?
Right, na wao siku hizi wamekataa jina la Tanzania Visiwani, wanaitwa Tanzania Zanzibar. Sisi tukanyimwa jina la Tanzania Tanganyika.siku hizi hawaiti tena tanganyika,eti wanaita tanzania bara.