Yussuf Manji, Omba Toba

Yussuf Manji, Omba Toba

Yussuf Manji ni Muislam na aliwakosea Waislam na ni wajibu wetu kukumbushana.Toba ni kwa yeyote.
Hamuwezi kumsamehe Muislam mwenzenu juu kwa juu ..au mpaka yeye ndo awapigie magoti kwanza? Sisi tunafundishwa kusamehe 7×70 na "kugeuza shavu upande wa pili unapowashwa kibao upande mmoja"

Music wa Sizonje tu umeshamuacha hoi. Sasa ukichanganya na mapigo yenu, si mtamuua mwenzenu?..
 
Udini uko wapi? Kumtaka Manji aombe toba kwa makosa yake ni udini?

Reference za JF za miaka hiyo zipo hapo, soma vizuri post namba moja, nazo si udini?

Au unafurahi unapoona mwenzako anateketea?
We haufurahii manji akiteketea ilhali mmemsemelea kwa huyo mungu wenu na sasa maombi yanajibiwa?
 
KWANINI UNAMSHAMBULIA MUISILAAM MWENZETU?HUONI KAMA UNAWAPA WAKRISTU NGUVU YA KUUZOOFISHA UISLAMU?KWANINI HUKUSEMA HAYA KULE FARAGHANI
Anashambuliwa au anashauriwa! Waislam tumeagizwa na dini yetu kuusiana mema na kukatazana mabaya. Allah amesema "hana atakachozidishiwa mwenye kudhulumu ila khasara!" Kuna viongozi wa BAKWATA waliamua kwa makusudi kuwadhulumu Waislam mali za Wakfu, Yusuf Manji alishiriki dhulma hiyo kwa kununua baadhi ya mali hizo huku akijua, kilio cha Waislam kilikuwa kikuu, wala hakikuwa faraghani, kisha wakashitakia kwa Mola wao, kisha wakamwachia Mola ahukumu, na wala Mola Subhanahu wa taala hana haraka katika kutekeleza hukumu zake! Viongozi waliofanya vile wengi walifikwa na makubwa na wengine hivi sasa wako mbele za haki, hapo Manji atanusurikaje! Manji hivi sasa anadhalilika big time, anapotokea Muislam mwenzake, akamkumbusha alikotoka, kisha akamshauri arudi kwa Mola wake kuomba maghfira, huyo ni Muislam mwenye imani ya kweli kwa dini yake na muumin mwenzake. Manji ana khiari ya kufuata ushauri au kuendelea kukaidi na kuendelea kukabiliana na Muumba wake kama alivyofanya Fir'aun. Nyie msio wa imani hii, au washirika wa waliodhulumu ni vyema mkanyamaza kuliko kuonesha udhaifu wenu.
 
Hayo maombi mabaya mlitakiwa kuyaelekeza bakwata sio kwa mtu aliyeuziwa kihalali
Wote pamoja na Manji, since Manji alijua fika alichokuwa anakifanya si sahihi,
Ila Allah amfanyie wepesi juu ya mitihani alyompa
 
Wewe mavi towa boriti kwanza kwenye jicho lako mnafki mkubwa wewe.
Mnafiki ni wewe mwenye mdomo unaotoa kinyesi, na una boriti kwenye macho yako yote mawili na masikioni, huwezi kusikia wala kuona, nadhani kuna nyingine imekuziba kule chini ndio maana unajisaidia haja kubwa kupitia mdomoni!
 
Hamuwezi kumsamehe Muislam mwenzenu juu kwa juu ..au mpaka yeye ndo awapigie magoti kwanza? Sisi tunafundishwa kusamehe 7×70 na "kugeuza shavu upande wa pili unapowashwa kibao upande mmoja"

Music wa Sizonje tu umeshamuacha hoi. Sasa ukichanganya na mapigo yenu, si mtamuua mwenzenu?..
Nadhani ushauri huu wa kugeuza shavu upande wa pili ungewapa kina Mbowe na Gwajima wasimshughulikie Mkristo mwenzao Paul Makonda, bali wamgeuzie tu mashavu ili awazabe tena mabao mengine!
 
Utajiataje muislamu wakati una ngozi nyeusi, huoni aibu kukumbatia dini za kitumwa{ Ukristo na Uislamu}, kabila lako ndiyo dini yako, hizo dini zililetwa kwa njia utumwa kutesa na kuwauza mababu na mabibi zetu weusi wakati waliwakuta na imani zao, jitambue
Bonge la point
 
Mohamed Said,tunaomba ukubaliane na F,au utufafanulie zaidi
Jackline,
Historia ya kuundwa kwa BAKWATA si ngeni katika ukumbi huu.

Historia hii inahusiana moja kwa moja na historia ya kupigania
uhuru wa Tanganyika uhuru ambao Waislam walikuwa na mchango
mkubwa usio na kifani.

Nguvu hii ya Waislam katika kupambana na dhulma za kikoloni
ilisababisha hofu kwa serikali huru ya Tanganyika iliyokuwa
inaongozwa na Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.

Nini kilisababisha hofu hii?

Baada ya uhuru kupatikana 1961 mwaka uliofatia 1962 Waislam
chini ya uongozi wa Mufti wa Tanganyika Sheikh Hassan bin Amir
waliitisha Muslim Congress wakiwa na agenda moja tu nayo ni suala
la elimu kwa Waislam ili na wao wanufaike na uhuru walioupigania
kwa kwa nguvu zao zote.

Hili ni kati ya vitendawili vikubwa katika utafiti na uandishi wa historia
ya TANU na uhuru wa Tanganyika.

Muslim Congress ya 1962 iliamua
kuwa Waislam wajenge shule za msingi na upili pamoja na Chuo Kikuu.

Shule zikaanza kujengwa na mipango ya ujenzi wa Chuo Kikuu kadhalika
ikaanza.

Hapa ndipo Kanisa likaingia hofu kuwa nini itakuwa hatma yake ikiwa
Waislam wataelimika.

Katika ukoloni Kanisa lilinufaika sana katika elimu wakati Waislam
walibinywa.

Elimu ilikuwa katika mikono ya serikali ya kikoloni na kwa Wamishionari.
Hii ilikuwa hofu ya kwanza.

Hofu ya pili na ndiyo ilikuwa hofu kuu ni mustakbali wa siasa katika
Tanganyika huru.

Kanisa lilikuwa mimeshuhudia nguvu ya Waislam katika kumng’oa
Muingereza na pia hata katika Vita Vya Maji Maji.

Ukifanya utafiti katika historia hizi mbili mtafiti hatashindwa kuona
mkono ulioshika kifutio ukijaribu kufuta mengi ya ukweli na kuingiza mengi
ya kughushi.

Ikawa sasa njama za chini kwa chini zinaanza kwa nia ya kuhakikisha kuwa
Chuo Kikuu hakijengwi na jumuia huru za Kiislam zinavunjwa pamoja na
mihimili mingine iliyokuwa ikitia nguvu Uislam Tanganyika.

Katika Muslim Congress ya mwaka wa 1963 katika moja ya ajenda iliyozungumzwa
ilikuwa njama za serikali iliyopo madarakani dhidi ya Uislam katika Tanganyika.

Nimekuwekeeni hapa huu mukhtasari uwe kama kifungua dimba.

Kisa kizima nimekieleza katika kitabu,’’The Life and Times of Abdulwahid Sykes
(1924 – 1968) The Untold Story of the Muslim Struggle Against British Colonialism
in Tanganyika (1998),'' Minerva Press London.

Lakini msomaji anaweza pia kusoma kuhusu BAKWATA kwa kuingia:

Mohamed Said: BAKWATA KIBARAKA KIPINDI MAALUM KILICHORUSHWA NA RADIO KHERI, RADIO QUIBLATAIN NA RADIO IMAAN 1 OKTOBA 2012
 
Utajiataje muislamu wakati una ngozi nyeusi, huoni aibu kukumbatia dini za kitumwa{ Ukristo na Uislamu}, kabila lako ndiyo dini yako, hizo dini zililetwa kwa njia utumwa kutesa na kuwauza mababu na mabibi zetu weusi wakati waliwakuta na imani zao, jitambue


Ngoja basi nijikoroge.
 
Yussuf Manji, ni matumaini yangu kuwa ujumbe huu utakufikia popote ulipo.

Binafsi kama Muislam mwenzako nnachukuwa fursa hii kukukumbusha kuwa hakuna kitu bora kama kukiri na kukubali makosa yako na kuomba toba.

Toba nnayokushauri kuiomba hapa, si kwa serikali wala kwa watawala. Toba nnayokukukumbusha mimi kuiomba ni kwa Mola wako Muumba mbingu na ardhi.

Manji uliwakosea sana Waislam kipindi cha nyuma kiasi, kwa kutumia fedha zako kununulia viwanja vya wakf vya Waislam, na kuwa mkaidi kila uliposemeshwa kuhusu hilo.

Viwanja hivyo ambavyo historia inaonyesha kuwa vilikuwa vijengwe chuo kikuu cha kwanza Tanganyika (hilo halikufanyika lakini hilo ni simulizi jingine kabisa ambalo Alama Mohamed Said anaweza kulisimulia vizuri zaidi).

Ulifatwa na Waislam wakikuomba kuwa mkataba ulioingia na BAKWATA ni wa kidhalimu na haufai lakini kwa ukaidi wako hukuwasikiliza na uliwatoa njiani na kuendelea na mkataba wako.

Sakata la viwanja hivyo lilipelekea Waislam kufungwa, kupigwa na kujeruhiwa mpaka walipoona kuwa hawakuwezi kwa ajili ya kutumia fedha zako na nguvu ya baadhi ya waliokuwa BAKWATA, Waislam wakafikia maamuzi makali ya kuwa sasa wanakushtaki kwa Mwenyeezi Mungu.

Miaka imepita ukidhani kuwa shtaka hilo halina meno kwako, lakini leo tunashuhudia ukigeukwa kila upande.

Aibu ya kushikwa na kuwekwa ndani pekee si ndogo kwa mtu wa "caliber" yako. Licha ya kupimwa na kukutwa kuwa u mlevi wa madawa, tumeona sakata la Oysterbay likikutia hasara kubwa sana, tumeona wafanyakazi wako wakifungiwa kuingia kwenye ofisi zao, tunasikia akaunti zako zinafungiwa kila kukicha.

Kama hiyo haitoshi, tunasikia umepatwa na matatizo ya moyo. Mwenyezi Mungu anasema katika Qur'an tukufu:

Qur'an 2:10. Nyoyoni mwao mna maradhi, na Mwenyezi Mungu amewazidishia maradhi. Basi watakuwa na adhabu chungu kwa sababu ya kusema kwao uwongo. Maelezo

Kwa yote hayo bado tu hujashtuka ni kwanini yakukute yote hayo? Nakusihi, zingine zote ni sababu lakini ukweli unabaki kuwa ukweli, Waislam wameitikiwa dua zao dhidi yako.

Yussuf Manji tunakutaka usiwe katika wale ambao:

Qur'an 2:7. Mwenyezi Mungu amepiga muhuri juu ya nyoyo zao na juu ya masikio yao, na juu ya macho yao pana kifuniko. Basi watapata adhabu kubwa. Maelezo

Kwa kuwa Mwenyezi Mungu ni wingi wa kusamehe na hachoki kusamehe, tunakutaka uombe toba kwa mola wako, umtake radhi, uwatake radhi na Waislam na uwarudishie viwanja vyao na mali zao, tena usithubutu kuvirudisha kwa wale wale waliokuuzia, itakuwa haina maana kabisa. Virudishe kwenye taasisi za Kiislam zenye kumuogopa Mwenyezi Mungu au tumia viwanja hivyo hivyo kuanzisha Manji Islamic Trust Fund na uiendeshe mwenyewe kwa manufaa ya Waislam.

Fata nasaha hizo uone mambo yatavyokunyookea.

Jikumbushe:

Maimamu kumsomea Manji Ahla-badri

Mjue Sheikh Ponda Issa Ponda na Kundecha

Waislamu wataka jengo lao toka Quality Group | Bongo5.com

MKATAMBUGA: WAISLAMU WAMELOGWA NA NANI?

Manji hakuna wakukuokoa katika haya na hayatokwisha ukifanya dharau isipokuwa wewe mwenyewe, anza kwa kumrudia Allah na kumuomba toba.

Na Mwenyeezi Mungu ndiye ajuwae zaidi.


Sasa nimejua kwa nn unamtetea sana Bashite...mwanzoni ulikuwa upande wa Manji sijui Hili la VIWANJA vya Bakwata ulikuwa umelisahau???
 
Hamuwezi kumsamehe Muislam mwenzenu juu kwa juu ..au mpaka yeye ndo awapigie magoti kwanza? Sisi tunafundishwa kusamehe 7×70 na "kugeuza shavu upande wa pili unapowashwa kibao upande mmoja"

Music wa Sizonje tu umeshamuacha hoi. Sasa ukichanganya na mapigo yenu, si mtamuua mwenzenu?..


Mbowe niliona kaenda mahakamani kushitaki. Vipi, hajuwi kugeuza shavu?

Gwajima vipi, umemsikia leo? Au yeye nae si Mkristo na hajuwi kugeuza shavu? Kwanini usiwape ushauri huo?

Sisi tunashauri Manji aombe toba.
 
Back
Top Bottom