Yes madam Speaker, We are stupid!

Hapa kuna tatizo kubwa, rais hajaaprove, wanalipana... je kuna kupoteza kazi?? kurudisha posho?? kufuja mali ya umma? fraud??? au ndio sisi wajinga tuliwao?

Under this govt and the current state of parliament and opposition, hii ishu itabaki kwenye magazeti na kuishia huko huko. Kwani leo imeongelewa huko bungeni?
 
Wao wajiongezee tu, kila kilicho na mwanzo kina mwisho, Maisha magumu Dodoma, kwani Dodoma sio parts ya Tanzania? au huo ugumu wa maisha ni kwa wao tu wabunge??

UMIMI umezidi kwa viongozi wetu, Yes mama Makinda we are stupid indeed
 
mimi janamani nijuzeni hivi posho za wabunge hzitakiwi ku observe budget. Yaani zinaweza kufanyiwa kazi anytime ?

Kama bunge liko juu ya bajeti wanaypitisha wenyewe kwa matumzi ya nchi na wao wakiwemo hizo za posho kati kati ya mwaa wa fedha wanazichota kutoka kwenye fuko gani ?
 
Brain power ya Mwenyekiti wa CCM/Rais wa TZ imegota tumsaidieni kwa kumtoa madarakani kama Misri au Libya. Eti wakati mchakato wa kutafuta Spika yeye akiwa Mwenyekiti ndani ya Chama walipitisha lazima awe mwanamke wakati mchezo umekwishaanza. Je, Sitta / Chenge walirejeshewa pesa za kuchukulia form???
 
huyo na mwanamke ambaye rais aliamua kubadili sheria za mchezo wakati mchezo uko katikati. Ukweli RAIS ndo anatuchezea waTZ sio huyo mama ambaye kapewa cheo/ushindi wakati mechi inaendelea.
 
Hawajalipwa,
Kama wamelipwa

  1. Nani kaidhinisha
  2. Kutoka badget ipi
  3. Kutoka fungu lipi
  4. Nani na nani wamelipwa
  5. Nani hajalipwa
Nadhani Mama Makinda anadhani wa-Tanzania ni wazungu nini?

na kama walishaanza kilipwa anayesema hajaindhinisha au kuruhusu alikuwa wapi na alisema nini? wanafikiri sisi ni watoto waambiwao usilie nitakupa pipi enheeeee
 
The whole government system is full of stupidity and foolishness......

..enheee niulize hivi Mawaziri na Manaibu nao si wabunge? wanalipwaje? wanapata mshahara wa ofisi zao kama kawaida na mshahara wa ubunge pia? na hizo posho pia wanapata?:A S confused:
 
Kesho Alhamis:
posho za waheshimiwa wabunge ("SERIKALI IMELIONA HILO NA KWAMBA WABUNGE WETU WANAISHI MAISHA MAGUMU SANA<HIVYO HATUNA BUDI KUWAONGEZEA SITTING ALLOWANCE") PM

posho za madaktari na walimu (PM >" SERIKALI HAINA HELA
 
Daaaaaaaaaaa! tumekwisha kama hizo posho wanapeana kimyakimya bila kusainiwa na RAIS. na huyo mtoto wa mkulima ndio anaziunga mkono kwa macho yote Eeeeeeeeeeeeeehe.
 
Tungekuwa tunaheshimu sheria tusingelikuwapo hapa tulipo. Sheria zipo kwenye makaratasi tu, kila jengine ni deal mwanzo mwisho

Hakika sheria zipo kwenye makaratasi na zinatumika chache tu kwenye maeneo machache tu. Mfano sheria za jinai zinatumika kama kibaka akikamatwa kaiba lakini fisadi akikamatwa anaambiwa arudishe kidogo kidogo pesa alizoiba. Daktari akiomba nyumba anaambiwa hastahili kupata nyumba kutokana na "Standing Orders" za sasa lakini mkubwa sio tu anapewa nyumba aishi akiwa mtumishi anauziwa kimojaa kwa bei chee!
 
Inasikitisha sana kuona kwamba Wadanganyika kwa kawaida yao leo tunajiita Stupid kwa kebehi wakati sisi ni stupid kweli!.. Tuwe stupid mara ngapi ikiwa wazungu husema Stupid is what stupid does (Forrest Gump). Sisi wote hapa ni reflection ya viongozi wetu na tumeonyesha u stupid wetu kwa kuwaunga mkono madaktari nao wapewe posho maadam wabunge wanapata..Hatujui kusema No is NO! kumbe ni ile NO ya kiswahili ukisema wakati mwingine ndio YES, kukubali mchezo.

Mwaka juzi kabla ya Uchaguzi TUCTA, walitaka kufanya maandamano ya mgomo ili kuongezewa mishahara kwa watumishi wa Umma hasa kima cha chini. Watu walisema sana hadi kiongozi wao akatafutiwa uchawi na kuitwa kibaraka na mchonganishi...akaachwa solemba ajkijiuma na kujificha huku na huku bila msaada. Baada ya hapo hakuna mtu hata mmoja aliyeinua kidole kukemea maamuzi ya serikali wala kuandaa Upinzani wa nguvu kutokana na maamuzi ya serikali na hasa hotuba ya JK kwa wazee wa Dar - es - Salaam... Ukwa ndio mwisho wa kila kitu.

Majuzi tu tumeshuhudia Katiba ikipatiwa sheria kinyemela na tukalazimishwa kuikubali kama ilivyo na kufuata masharti yaliyopitishwa na Bunge, tumafanya nini ? zaidi ya kuendeleza - Parapanda limelia parapanda na kumshukuru Mungu kuwa yeye ndiye mwamuzi! Ati Jk asingeweza kutoweka saini kwa sababu wanaCCM wenzake wasingemwelewa.. Mijitu ikatoka pale na furaha kwamba JK kasema anakubaliana nao ila....

Leo hii Madaktari wasiokuwa na hata na chembe ya Uzalendo wanaweka mgomo nchi nzima kuhatarisha maisha ya wananchi wanapewa support japokuwa mishahara ya watu wengine midogo sana, huduma za Hospital acha mbali kutowepo kwa vitendea kazi na madawa hizo huduma zenyewe haziridhishi lazima uhonge kiasi kukutana na daktari Tsh 5,000 hadi 10,000 kwa zahanati na Hospital ndogo, Tsh 40,00 hadi 50,000 kwa zile za Rufaa. haya hatuyaoni kama mzigo kwa wananchi lakini tupo radhi kuikosoa serikali kwa kutowalipa madaktari posho zao. Kama hakuna vitendea kazi kwa nini mnatutoza fedha za kuwaona?.

Hizi ndizo athari za UTUMWA. kwa wale waliopinga kwamba Kutawaliwa haikuwa athari kubwa ktk maendeleo yetu inabidi wafikirie upya maana tumezoea kuendeshwa kwa mabora na kukemewa. Hii ni mifano mizuri sana kuonyesha kwamba mtumwa akikemewa mara moja huacha kudai haki yake kwa hofu ile ile alorithi toka kwa mababu zake. Na tunapopewa Unyapala hujiona sisi miungu na wenye nafasi nzuri kuliko mtumwa shambani.. Wewe nyapala kupewa wadhifa huna lolote bado ni mtumwa tu.

Nitaendela kusema kwamba siasa za Bongo ni za kudanganyana tu hakuna mkombozi wala hakuna mtu mwenye uchungu na Taifa hili hivyo tukubali matokeo na kuishi ndani ya giza kama tulivyolelewa - Na ukweli utabakia kwamba UBEPARI hatuuwezi wala hatujui miiko na maadili yake zaidi ya ku copy na ku paste mifumo ya watu kama vazi la suti..Tunavaa ili nasi tuonekane kama wazungu japokuwa nje ni jua kali nyuzi 40 na kumcheka yule alovaa kanzu kwa sababu ni vazi la waarabu.
- Tunadai, ni Kudai, kudai, kudai tu...
 
Ndio wameamua kuongeza posho za wabunge! lakini madaktari big NO!. Da nchi yetu bwana sijui inakwenda wapi. Rais anasema kuwa watumie busara ila anafahamu kuwa kuna haja ya kuongeza posho. Swali ni je kama anafahamu kuna umuhimu wa kupanda kwa posho kwanini anagoma kusaini? wenye akili zetu tunajua ya kuwa ameshaidhinisha posho hizo zipande, ndio maana mama Makinda yupo mstari wa mbele kuzitetea. Naona sasa wakina Mkamia roho zenu kwatu!
 
Mbona Lissu alisema huwa hazipokei bali anazikuta kwenye akaunti yake?

Hii banana republic bana, kila mtu na lwake, hovyo sana hakuna namna ya kuutolea huu mkorogo maelezo.
 
Back
Top Bottom