Yanini kusherehekea siku ambayo maelfu ya watu wasio na silaha wala hatia waliuliwa Zanzibar (12/01/1964)

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,200
10,938
Historia huwa inapitia msururu mrefu wa matukio.Yapo matukio ambayo mwanzoni huenekana ni sehemu ya historia nzuri lakini kadri muda unavyokwenda watu hujutia historia hiyo na hatimae kuamua kubadili hisia.
Matukio ya aina hiyo ni kama yale ya utumwa barani Amerika na ukoloni uliofanywa na baadhi ya mataifa kwa mataifa mengine hasa Afrika.Ipo pia historia ya ubaguzi wa rangi kwa Afrika kusini.
Matokeo ya kuzingatia hisroria hizo hatimae hupelelekea baadhi ya jamii na mataifa kuombana msamaha ili maisha yaende kama kawaida.
Jambo la kushangaza mpaka leo Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wanasherehekea siku ambapo maelfu ya watu waliuliwa Zanzibar.
Wasimulizi wa historia hizo wanaeleza kwamba lilikuwa ni tukio la kushtukiza na kwamba karibu wote waliouliwa walifanyiwa hivyo hawakuwa na silaha na waliuliwa wakiwa majumbani mwao.Na kwamba kwa ujumla hakukuwa na uhasama baina yao na wale waliokwenda kuwaua.
Mzee Muhammed Said naamini anajua habari hizi kwa undani.
 
Pongezi za dhati ziende kwa yule mla kitimoto John Okello aliyewanasua weusi wenzake toka kwa wadhalimu wa Omani.
 
Kobazi walitamani kumuondoa muomani ila kwakuwa aliwatawala kimwili na kiroho kupitia dini wakashindwa movements,hadi alipo kuja John Okello shujaa toka Uganda,akamtimua Muomani,hakika Shujaa John Okello ndio baba wa mapinduzi haya matukufu tunayo adhimisha leo.
 
Historia huwa inapitia msururu mrefu wa matukio.Yapo matukio ambayo mwanzoni huenekana ni sehemu ya historia nzuri lakini kadri muda unavyokwenda watu hujutia historia hiyo na hatimae kuamua kubadili hisia.
Matukio ya aina hiyo ni kama yale ya utumwa barani Amerika na ukoloni uliofanywa na baadhi ya mataifa kwa mataifa mengine hasa Afrika.Ipo pia historia ya ubaguzi wa rangi kwa Afrika kusini.
Matokeo ya kuzingatia hisroria hizo hatimae hupelelekea baadhi ya jamii na mataifa kuombana msamaha ili maisha yaende kama kawaida.
Jambo la kushangaza mpaka leo Zanzibar na Tanzania kwa ujumla wanasherehekea siku ambapo maelfu ya watu waliuliwa Zanzibar.
Wasimulizi wa historia hizo wanaeleza kwamba lilikuwa ni tukio la kushtukiza na kwamba karibu wote waliouliwa walifanyiwa hivyo hawakuwa na silaha na waliuliwa wakiwa majumbani mwao.Na kwamba kwa ujumla hakukuwa na uhasama baina yao na wale waliokwenda kuwaua.
Mzee Muhammed Said naamini anajua habari hizi kwa undani.
Kinacho shereherekewa ni matokeo ya Mapinduzi Matukufu yale, na sio yale matendo ya mauaji ya kimbari!.

Ni kama sisi Wakristu, Bwana wetu Yesu Kristo alikufa kifo kibaya cha kusulubiwa msalabani, hatusherehekei kifo chake, ni tunaadhimisha tuu, na kusherehekea matokeo ya kifo chake, kwa kupigwa kwake na kifo msalabani, sisi tumeponywa, tumekombolewa!.
P
 
Pongezi za dhati ziende kwa yule mla kitimoto John Okello aliyewanasua weusi wenzake toka kwa wadhalimu wa Omani.
Zanzibar hakukuwa na ubaguzi wa rangi kulingana na historia tunayoisoma
 
Kobazi walitamani kumuondoa muomani ila kwakuwa aliwatawala kimwili na kiroho kupitia dini wakashindwa movements,hadi alipo kuja John Okello shujaa toka Uganda,akamtimua Muomani,hakika Shujaa John Okello ndio baba wa mapinduzi haya matukufu tunayo adhimisha leo.
John Okello kuna watu waliomtuma halafu alipomaliza kazi wakamuondoa.
Hakuwa mwanasiasa
 
Kinacho shereherekewa ni matokeo ya Mapinduzi Matukufu yale, na sio yale matendo ya mauaji ya kimbari!.

Ni kama sisi Wakristu, Bwana wetu Yesu Kristo alikufa kifo kibaya cha kusulubiwa msalabani, hatusherehekei kifo chake, ni tunaadhimisha tuu, na kusherehekea matokeo ya kifo chake, kwa kupigwa kwake na kifo msalabani, sisi tumeponywa, tumekombolewa!.
P
Inashangaza sana.
Hayo matokeo ya mapinduzi ni yapi?
 
Zanzibar hakukuwa na ubaguzi wa rangi kulingana na historia tunayoisoma
Utawala dhalimu wa waarabu wa Oman chini ya Sultan ulihitimishwa na shujaa John Okello.

Wewe unasoma historia ipi ambayo wengine hawaisomi?
 
Kama muungano ni muhimu unadhani bila kufanyika mapinduzi usingekuwepo.
Kulikuwa na umuhimu gani wa kuua watu ili ufanyike muungano
Kuna baadhi ya vitu ili vitokee lazima viwe prompted na vitu vingine!. Kuna baadhi ya watu, kabla hujanunua gari, lazima ufanye test drive, u try, upendezewe ndipo ununue!. Hivyo ni yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yame prompt huu muungano wetu adhimu.
P
 
Kuna baadhi ya vitu ili vitokee lazima viwe prompted na vitu vingine!. Kuna baadhi ya watu, kabla hujanunua gari, lazima ufanye test drive, u try, upendezewe ndipo ununue!. Hivyo ni yale Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, yame prompt huu muungano wetu adhimu.
P
Ilitakiwa ifunguliwe kesi kwenye mahakama ya kimataifa kuhusu mauwaji ya mwaka 1964.sio kusherehekea
 
Nina uhakika mengi huyajui. Au unajaribu kuwapamba waoman kwa kujaribu kuziba kile walichokuwa wanafanyiwa wazanzibar chini ya utawala wa waoman.
Muhimu ukumbuke waoman walikuja kuikalia Zanzibar kimabavu. Tukisema kabavu maana yake si kwa hiari ya wazanzibar. Kwa vyovyote mtawaliwa! Zanzibar) atalazimishwa kufuata sheria zozote ziwe mbaya au za kikandamizi toka kwa mtawala (Oman). Ni sawa na kijani ya sasa
Kwa vyovyote mtawaliwa lazima aishi kwa unyonge chini ya sheria inayomnyima haki na Uhuru wa kufanya mambo yake kama mwenye nchi.
Kwa vyovyote kuuondoa huo utawala wa kimabavu uliowadumaza kwa miaka mingi,lazima kusherehekea.
 
Ilitakiwa ifunguliwe kesi kwenye mahakama ya kimataifa kuhusu mauwaji ya mwaka 1964.sio kusherehekea
Hatua ya kwanza kabla ya kufungua kesi yoyote ni kuripoti hayo mauaji!. Kwenye hayo mauaji ya Zanzibar, yakiripotiwa popote?.
P
 
Back
Top Bottom