Yanayotokea Muhimbili ni kweli?

Yanayotokea Muhimbili ni kweli?

Mkuu The Boss,

Sijajua vipimo vingine, lakini nataka nitoe ufafanuzi kwenye vile nilivyothibitisha.

Upande wa Ct Scan, ni uongo. Mdogo wangu alikuwa anatatizo moja hivi tukaenda kucheck pale, Gharama yake ni Tsh. 150.000 (Hiki kipimo kunakipindi niliona Ikonda ni Sh 270.000 sijui kwa sasa) Tena hapa alifanya Ct Scan ya kichwa.

Kwa upande wa M.R.I mimi mwenyewe nilikuwa (mpaka sasa) na tatizo moja hivi, Nimeenda kupima juzi kati hapo hata mwezi haujaisha. Gharama yake ni Tsh. 250.000. Hivyo ndivyo vipimo nilivyo na uthibitisho navyo.

Kinachokuza Gharama,

Pale Muhimbili panamsongamano mkubwa wa Wagonjwa na ukizingatia ukubwa wa Hosptitali yenyewe. So kwa wale wenye uwezo huwa hawataki kufuata utaratibu uliowekwa na hosptali hivyo huwatafuta "Madalali" Hawa ni wajuzi wa Hospitali hii, Madaktari na Vitengo vyake kulingana na Ugonjwa wa Mgonjwa mwenyewe.

Kwahiyo hawa usipokuwa makini ndio wanaokuza gharama pasipo wewe kujua... Unakuta kipimo fulani ni Shilingi 10.000 mf, Yeye anakwambia Laki moja..!! Wewe kwasababu hauelewi a wala be, na hautaki usumbufu unajikuta unalipa gharama hizo..!!

Halafu pia, Pale Muhimbili kuna huduma zinatolewa kama Private (kwa mahitaji ya mgonjwa mwenyewe) Gharama za Private haziringani na gharama za kawaida, ingawaje hazijapishana ile sana.

Hii ndiyo inawakuta watu wengine wanaopenda Wake zao wajifungue kwa huduma ya Private. Ninachojua, huduma ya Uzazi kwa kina mama ni bure, ingawaje kunagharama kidogo unachangia kama mkeo kafanyiwa Operation.

Hicho ndicho kidogo ninachojua..!!

BACK TANGANYIKA

asante kwa mchango wako
 
NDG WAPENDWA HUO NI UPOTOSHAJI WA HALI YA JUU LAKINI UKIJA MUHIMBILI KUPATA MATIBABU LAZIMA VIGEZO NA MASHARITI KUZINGATIWA KWA UFAFANUZI FIKA HOSPITALI UTAPATA IFAFANUZI WA KUTOSHA
 
Mpaka sasa hakuna ushahidi kuthibitisha madai yako!
 
Ni kweli kabisa mkuu! Leo nimeenda Muhimbili kufanya Medical check up, kwa vipimo nilivyopima, ukiacha CT Scan Kama sijakosea imegharimu zaidi ya 300,000 Na hapo bado matibabu, nikajiuliza hii ndo Hospital ya Serikali kweli??? Hata Kama kuchangia Huduma sio kiivyo!
 
Hizo garama ni kwa wagonjwa wote?(namaanisha wale wa self refferal na walokua reffered kutoka lower facilities)
 
Ni kweli kabisa mkuu! Leo nimeenda Muhimbili kufanya Medical check up, kwa vipimo nilivyopima, ukiacha CT Scan Kama sijakosea imegharimu zaidi ya 300,000 Na hapo bado matibabu, nikajiuliza hii ndo Hospital ya Serikali kweli??? Hata Kama kuchangia Huduma sio kiivyo!

Tuwekee risiti
 
Kadi ya kwenda kumuona Daktari. Kiongozi unatumia bima ya Afya nini?

kuna kadi nyingi sana hospitali na inategemea na setting ya hospitali, hata akina mama clinic wanatumia kadi, Care and treatment clinic wanatumia kadi nk
 
Kwa akili ya kawaida nadhani hili haliwekeni. Hiyo tofauti ni kubwa sana kuijustfy wa la watu kumudu. Ila uhakika ni kuwa baadhi ya huduma zilizokuwa zikitolewa zamani kwa misaada ya wahisani (waliojiondoa) au miradi kwisha inawezekana kukawa na tozo. Sasa ni za kiwango gani? hilo sijui.
Nilikuwa nawaza ni namna gani wanyama waliingia kwenye safina kipindi cha Nuhu, lakini nikayaona Tanzania twiga ndani ya bombadier angani na sio juu ya maji...hakuna lisilowezekana tz amini nakuambia
 
Kwa ninavyofahamu mimi mpaka sasa sera ile ya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano kutibiwa bure haijafutwa na bado wanatibiwa bure ila mjamzito ukienda na kadi ya bima unachajiwa kwa ile bima yako na si sera tena.
 
Back
Top Bottom