Yanayotokea Muhimbili ni kweli?

Yanayotokea Muhimbili ni kweli?

The Boss

JF-Expert Member
Joined
Aug 18, 2009
Posts
49,320
Reaction score
117,654
Humu ndani tuna waandishi wa habari na watu wengine wafanyakazi wa Muhimbili ninaomba watueleze kama niliyosikia huko ni kweli.

Kuna taarifa huko Muhimbili sasa huduma zote ni za kulipia na gharama ni juu kupita hospitali za binafsi.

Mfano huduma ya wamama wajawazito ambayo ilikuwa bure kabisa sasa naambiwa lazima walipe laki tatu na ishirini..320,000/- na vipimo kama CT scan ni kulipa kuanzia laki sita.

Kuna vipimo ambavyo hospitali binafsi wana charge elfu 40 Muhimbili unalipa laki nne 400,000/ na kwamba mgonjwa akilazwa tu siku moja lazima alipe
na chakula ni kununua.

Nimejiuliza hizi taarifa ni za kweli au uzushi?

Kuna watu ambao mmekwenda Muhimbili hivi karibuni mtusaidie?

Pascal Mayalla Manyerere Jackton
Salary Slip

==================
Maoni ya wadau wengine

Huu ni ukweli kabisa,hii kitu sio ya Leo ni vile ulikua haijasemwa ama imesemwa ila haijawekwa public.sina hamu nao hao muhimbili nilipeleka mkewangu kujifungua ni kam miezi mitatu imepita kwa bahati mbaya mtoto Siku haikua kamilika vizuri so walimweka kwenye chumba cha joto,wife alikaa hospital kama Siku ,4 ila bill niliyopewa ni sh million 1.6 aisee niliwaza sana kuhusu watanzania wenzangu ni kwa jinsi gani hizi gharama watazimundu,bila kwa kweli pale muhimbili hali sio nzuri,hata nilivyokuwa kwenye foleni kwenda kulipa kila mtu analalamika ughali wa huduma..!![/QUOTE
Hii pia iko Hospitali ya Rufaa Bugando,kitanda kulaza mgonjwa siku tatu 400,000/,zikiisha siku tatu unalipa tena 400,000/=

operesheni ya uzazi 300,000/=
Hii ni nje ya vipimo,madawa,na huduma mbalimbali

kama huna huhudumiwi kabisa na unarudishwa

Na hii hospitali inahudumia rufaa za mikoa karibu 7
 
Sasa kama kila kona taarifa ni za kupika unategemea pesa ya itoke wapi?.........

Leo mtu anatoa taarifa kesho uyo uyo anaikanusha kwa maelekezo toka juu....

Kiufupi uchumi umekufa acha tuwakamue wananchi pesa waliobakiza huku tunasubiri sanda na kuosha tufanye mazishi.........
 
1. Hata mimi nasubiri jibu.
2. Akina Lizabon et. all tuweke siasa kando ili mtu anapojiandaa kwenda MNH ajiandae kiuchumi
 
Back
Top Bottom