Humu ndani tuna waandishi wa habari na watu wengine wafanyakazi wa Muhimbili ninaomba watueleze kama niliyosikia huko ni kweli.
Kuna taarifa huko Muhimbili sasa huduma zote ni za kulipia na gharama ni juu kupita hospitali za binafsi.
Mfano huduma ya wamama wajawazito ambayo ilikuwa bure kabisa sasa naambiwa lazima walipe laki tatu na ishirini..320,000/- na vipimo kama CT scan ni kulipa kuanzia laki sita.
Kuna vipimo ambavyo hospitali binafsi wana charge elfu 40 Muhimbili unalipa laki nne 400,000/ na kwamba mgonjwa akilazwa tu siku moja lazima alipe
na chakula ni kununua.
Nimejiuliza hizi taarifa ni za kweli au uzushi?
Kuna watu ambao mmekwenda Muhimbili hivi karibuni mtusaidie?
Pascal Mayalla Manyerere Jackton
Salary Slip