Yaliyojiri kwenye mazishi ya Sumari

CCM wafanya kampeni msibani,Lema ashangiliwa baada ya mazishi,Katibu CCM wilaya nusura achapwe makonde alipojaribu kumzuia watu wasimsalimie mbunge Lema, wana CCM wenzake washangaa.


Nimeshatabiri kimbembe kwenye hii byelection kama safu itakuwa hivi:Mgombea Joshua Nassary,Kampeni Meneja Godbless Lema na kiongozi wa ngome kama kawaida Mwita
 
RIP Mbunge mteuliwa.
naona hizi picha zinaonyesha kama RA na mh. 6 walikuwepo!?
 
CCM wafanya kampeni msibani,Lema ashangiliwa baada ya mazishi,Katibu CCM wilaya nusura achapwe makonde alipojaribu kumzuia watu wasimsalimie mbunge Lema, wana CCM wenzake washangaa.


aliponea chupu chupu.......basi tu kwa kuwa ni msibani ila ingekuwa kwingine angechezea kichapo
 
TOFAUTI KATI YA 'MTU WA WATU' NA 'WATU WA MTU' SIKU ZOTE HUDHIHIRIKA SIKU MAUTI UNAPOBISHA

Marehemu Mhe Regia alikua ni 'MTU WA WATU' tofauti kabisa na huyo Marehemu Sumari ambaye yeye alikua ni MIONGONI MWAO 'WATU WA MTU'.

Hakika ni muhimu tena sana watu tukaelewa kwamba wakati 'mtu wa watu' siku zote husononesha sana pindi wanapotutoka na kubaki mioyoni mwetu kwa miaka mingi mno, kwa upande mwingine ukweli wa mambo ni kwamba 'watu wa mtu' huondoka bila hata ya jamii kuhisi kama hayupo vile na historia yake nayo husahaulika pale pale anapozikwa tu.

Sasa tangu hapo kila kiongozi apaswa kujiuliza kwamba angependa aonekane vipi vile katika jamii yetu hii ya Tanzania hapo baadaye kidogo. Chaguo kama hilo tunalo tu wakati tukiwa hai na kuchagua kutetea umma na umma tu.


RIP Mhe Sumari lakini watu tusijisahau sana katika kumtumikia mtu badala ya kuwatumikia wananchi.

Naona habari zake hazijavutia jukwaa kama la Rejia!RIP SUMARI
 
Tujuze na tuletee picha zaidi, ninashawishika kama vile kulikuwa na zengwe jingi na wasiwasi wa usalama ukizingatia maeneo hayo yana kila dalili ya Upinzani. Wehu wa CCM sijui wanajifunza nini maana kwa sasa kwa kuwatenga wazee wakidanganywa na upepo wa CHADEMA ni uendawazimu hawatakaa wausahau utakapowadhihirishia ujinga wao. Ninawaheshimu viongozi wangu, ila hii homa ya CHADEMA ni aiubu kwelikweli kwa CCM inaonyesha jinsi gani walivyokosa ubunifu wameishiwa hata kutulia sembuse ubunifu wa mbinu za kisiasa? Mbaya zaidi hawana hata uratibu mzuri wa kauli kama tulivyozoea huko nyuma. Najua CCM ina Nguvu bado na ina uwezo wa kufanya mengi tu, ila kwa sasa ninaona mengi ya aibu tu, wana kila nafasi ya kufanya vema tena sana. Mfano sijui walikuwa na nia gani ila kuhudhuria mazinshi ya Rejia, that was stratergically good. Na hawakuzuiwa na mtu yeyote. sasa nina hamu ya kujua huko Meru kama uhuru ulikuwa vilevile kama kwa Rejia...

Mwenyekiti... usionee huruma mtu hataq kidogo, ukitoka acha harufu nzuri wakutafute kwa uzuri na acha jina zuri wakutafute kwa mema... ninajua una nia njema ingawa kwa bahati mbaya sana umejenga maadui weeengi, na unafanya vema kutokuwajadili. Toa kichapo Chairman, hichi chama hakiwezi kudhalilika hivihivi
 
Sijui kama Mhe Fredrick Sumaye watakua wamesalimiana na Dr Mary Nagu hapo msibani huko Arumeru? Je, kuna picha yoyote hadi sasa juu ya hilo???

amezikwa na sasa watu wancheza karata tu.....yule jamaa maarufu kwa kupanda juu makaburi na kupiga picha sijui yuko wapi!!!!
 
Toeni habari kwa kina hapa JF wale mliopata nafasi ya kuhudhuria mazishi ya Mh Sumari,maana sijajua kulikuwa na nini hasa,nimesikia muhutasari wa yaliyotokea kupitia WAPO redio wanasema kulitokea vurugu inasadikiwa ilisababishwa na vijana wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CDM.sasa niki-compare na uzi huu naona kama kulikuwa na kitu.
Tupasheni vizuri mliohudhuria mazishi hayo
 
Sijui kama Mhe Fredrick Sumaye watakua wamesalimiana na Dr Mary Nagu hapo msibani huko Arumeru? Je, kuna picha yoyote hadi sasa juu ya hilo???
Marry Nagu hakuwepo mkuu.... Mary nagu alikuwa kwenye matembezi yale wanayoita ya hisani ili kusaidia mama mjamzito ajifungue salama...hakuwepo kwenye mazishi...ngoja nikupe ka-evidence haka

PICHA%2B.%2BNO%2B1.JPG
 
Tumemsubiri sana JK Arusha baada ya mazishi, mpaka muda huu hatuamini kabisa kama anaweza akawa ameondoka mjini hapa bila hata ya salamu kwa Wana Arusha!
Mbona Morogoro alitembelea sehemu kadha, ikiwa ni pamoja na kuzindua madaraja akijiandaa kwenda kumzika mar.Regia?
 
Toeni habari kwa kina hapa JF wale mliopata nafasi ya kuhudhuria mazishi ya Mh Sumari,maana sijajua kulikuwa na nini hasa,nimesikia muhutasari wa yaliyotokea kupitia WAPO redio wanasema kulitokea vurugu inasadikiwa ilisababishwa na vijana wanaosadikiwa kuwa ni wafuasi wa CDM.sasa niki-compare na uzi huu naona kama kulikuwa na kitu.
Tupasheni vizuri mliohudhuria mazishi hayo
ni kwlei kulikukwa na kama kitu kama tafrani fulani.....

alipoingia mheshimiwa MANDELA..(Godbless Lema) watu wengi walienda wakitaka kumsalimia.....sasa kuna mwenyekiti wa ccm mmoja nadhani wa wilaya kama sikosei akawa anawazuia watu wasimsalimie Mhe.Lema...hapo kwa kweli yule mwenyekiti alitaka kupigwa....busara ya wazee na viongozi wengine wa ccm wakamzuia na kumuondoa huyu mwenyekiti wa ccm huku wakimlaumu kwa kuwazuia wananchi....kwa kifupi ni kwamba ni kama vle kampeni zimeanza....maana toka usa liver ni bendera za ccm hadi msibani pale....
 
Back
Top Bottom