💥WAZO LA LEO💬:
Ukiona MTOTO unamtuma dukani halafu harudishi CHENJI ujue huyo ukubwani atakuwa MTAFUTAJI mzuri; Ni jambo jema mtie MOYO. Ukiona MTOTO anapiga wenzake ujue chuyo ni BONDIA wa baadae ni jambo jema usimpige. Ukiona MTOTO unampeleka shule za gharama lakini kichwani bado MBULULA! ujue huyo ukubwani atakuwa "MCHEZAJI WA TAIFA STARS" si mbaya sana. Ukiona mtoto anakuwa na tabia za "UONGO, WIZI WA MBOGA, MBISHI SANA" ujue huyo ukubwani atakuwa KADA wa CCM usimtie moyo CHARAZA VIBOKO maana watatuharibia Nchi yetu!!
Haya amka sasa, Kamata bakora yako(kalamu), nenda kituo cha kupigia kura, kamcharaze bakora zako mgombea wa CCM kwa kupeleka kura yako UKAWA!!
Nkutakie Uchaguzi Mwema!!
Wapi hukooo!!? Tujuze kamanda
Unaweza kusema CCM inalazimisha mapenzi kwa wananchi. Wananchi wameichoka. Wananchi hawaipendi CCM. Leo nimefika katika kituo changu nilichojiandikishia kupiga kura hapa jijini Mbeya, nikiwa na hamu kabisa ya kutumia haki ya msingi kumchagua kiongozi nimtakaye. Mbali na mimi niliwakuta pia wananchi wengine waliokuwa kituoni kwa lengo hilo hilo. Cha ajabu na cha kusikitisha tunaambiwa hakuna kupiga kura, kisa mgombea wa CCM amepita bila kupingwa. Kwamba mgombea wa UKAWA alienguliwa katika hatua za mwishoni kwa kutokutimiza taratibu za wagombea. Wananchi tukasema basi tumpigie kura huyo huyo wa CCM kuonesha kama tunamtaka yeye au la, wasimamizi wakasema kanuni haziruhusu kufanya hivyo! Tunajua hizo ni hila za CCM kuengua wagombea wa vyama vinavyounda ukawa kiujanja ujanja lakini naomba niwaambie kuwa kufanya hivyo ni sawa na kulazimisha mapenzi kwa wananchi! Kufanya hivyo ni sawa na mwanaume kulazimisha mapenzi kwa mwanamke ilihali hakutaki au kinyume chake! Naomba CCM wajue kuwa wakati wa kuongoza watapata shida kwani watakuwa wanaongoza wananchi wasiowapenda!
Alinacha=Mamayo.
Itakuwa Arusha ya Machame
Wakuu kumekucha, leo, Disemba 14, 2014 Watanzania wanapiga kura kuchagua viongozi wao wa Serikali za Mitaa. Viongozi wanaochaguliwa leo ni katika nafasi za Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa, Wenyeviti wa Vitongoji, Wajumbe 6 wa Serikali ya Mtaa (Halmashauri) na wajumbe wa Viti Maalum wa Mtaa/Kijiji.
Kama ilivyo ada JamiiForums itakuwa ikikujuza yanayojiri, katika uzi huu utapata/utaleta updates zinazohusiana na uchaguzi huu.
Karibuni sana
========
UPDATES MUHIMU:
- Eneo la Shariff Shamba, Ilala jijini Dar uchaguzi umeahirishwa mpaka Jumapili ijayo baada ya vifaa kutopatikana ndani ya muda. Vyama vyote vinavyoshiriki vimeafikiana
- Mgombea wa CHADEMA Kijiji cha Darajani huko Liwale, M. Manakwa amepigwa na watu wasiojulikana usiku wa kuamkia leo, amelazwa hospitali
Unazungumzia Arusha ipi?
Mgombea wa kitongoji cha Isandula juu kupitia CHADEMA ndugu Kasema amevamiwa usiku wa kuamkia leo tarehe 14/12/2014 na kukatwa katwa mapanga sehemu mbali mbali za mwili wake hali iliyompelekea kupoteza fahamu.
Ndugu Kasema anatarajiwa kushinda kitongoji hicho kutokana na nguvu kubwa aliyonayo, siku kadhaa zilizopita alifuatwa na viongozi wa ccm na kumtishia maisha iwapo ataendelea na msimamo wake wa kujitoa katika kinyang'anyiro hicho.
Hivi sasa amelazwa katika hospital ya Magu akiendelea kupatiwa matibabu. Tunamwombea kwa Mungu apone ili aendelee na harakati za ukombozi wa kitongoji chake