CCM yashinda Udiwani Kata ya Kasingirima, ACT Wazalendo wadai kulikuwa na Kura Feki

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,376
8,118
Screenshot_2024-03-20-21-49-48-396_com.brave.browser-edit.jpg


Msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kata ya Kasingirima, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mwantumu Mgonja amemtangaza Mlekwa Kigeni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata kura 437 dhidi ya mshindani wake wa ACT-Wazalendo, Alumbula Khalidi aliyepata kura 233.

Ni katika uchaguzi mdogo uliofanyika leo Jumatano Machi 20, 2024.

Mwantumu amesema jumla ya vyama 12 vimeshiriki uchaguzi huo. Idadi ya walioandikishwa ni 1,960, idadi halisi ya waliopiga kura 713, kura halali 699 huku kura zilizoharibika ni 14.

Mgonja amesema katika uchaguzi huo vituo vya kupigia kura vilikuwa sita na wagombea wengine ni Salumu Hassani wa Chama cha Wananchi (CUF) ambaye alipata kura saba na mgombea wa UDP, Hassani Yungura amepata kura tano.

Mgombea wa Chaumma, Fikirini Selemani, Mussa Nkumila wa Ada Tadea na Hassani Rashidi wa Demokrasia Makini waliupata kura moja kila mmoja.

Diwani mteule, Kigeni mbali na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumpa ushindi, ameahidi kufanya kazi bega kwa bega na wananchi ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika kata hiyo.

Uchaguzi wa kata hiyo umefanyika kufutatia aliyekuwa Diwani wake, Abdallah Kiembe kuajiriwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.

Pia soma > ACT Wazalendo wakamata Kura Feki uchaguzi Mdogo Kata ya Kasingirima Kigoma, Zikiwa zimepigwa kwa Mgombea wa CCM
 
Kura feki kwani Jpm bado yupo hai?

Si wanasema sasa hivi wanaogelea kwenye demcrasia?
 
Visingizio Kwa Wapinzani Huwa ni kawaida kama kura feki mnazo Kwa ushahidi wahini mahakamani.
 
View attachment 2940362
Msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kata ya Kasingirima, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mwantumu Mgonja amemtangaza Mlekwa Kigeni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata kura 437 dhidi ya mshindani wake wa ACT-Wazalendo, Alumbula Khalidi aliyepata kura 233.

Ni katika uchaguzi mdogo uliofanyika leo Jumatano Machi 20, 2024.

Mwantumu amesema jumla ya vyama 12 vimeshiriki uchaguzi huo. Idadi ya walioandikishwa ni 1,960, idadi halisi ya waliopiga kura 713, kura halali 699 huku kura zilizoharibika ni 14.

Mgonja amesema katika uchaguzi huo vituo vya kupigia kura vilikuwa sita na wagombea wengine ni Salumu Hassani wa Chama cha Wananchi (CUF) ambaye alipata kura saba na mgombea wa UDP, Hassani Yungura amepata kura tano.

Mgombea wa Chaumma, Fikirini Selemani, Mussa Nkumila wa Ada Tadea na Hassani Rashidi wa Demokrasia Makini waliupata kura moja kila mmoja.

Diwani mteule, Kigeni mbali na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumpa ushindi, ameahidi kufanya kazi bega kwa bega na wananchi ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika kata hiyo.

Uchaguzi wa kata hiyo umefanyika kufutatia aliyekuwa Diwani wake, Abdallah Kiembe kuajiriwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.
kuiacha ccm au kususia uchaguzi ni kumwachia shamba nguruwe kuendelea kula mazao,je kutomwachia nguruwe imesaidia nini! si ameendelea kula mazao
 
View attachment 2940362
Msimamizi wa uchaguzi mdogo wa Kata ya Kasingirima, Halmashauri ya Manispaa ya Kigoma Ujiji, Mwantumu Mgonja amemtangaza Mlekwa Kigeni wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kuwa mshindi katika uchaguzi huo kwa kupata kura 437 dhidi ya mshindani wake wa ACT-Wazalendo, Alumbula Khalidi aliyepata kura 233.

Ni katika uchaguzi mdogo uliofanyika leo Jumatano Machi 20, 2024.

Mwantumu amesema jumla ya vyama 12 vimeshiriki uchaguzi huo. Idadi ya walioandikishwa ni 1,960, idadi halisi ya waliopiga kura 713, kura halali 699 huku kura zilizoharibika ni 14.

Mgonja amesema katika uchaguzi huo vituo vya kupigia kura vilikuwa sita na wagombea wengine ni Salumu Hassani wa Chama cha Wananchi (CUF) ambaye alipata kura saba na mgombea wa UDP, Hassani Yungura amepata kura tano.

Mgombea wa Chaumma, Fikirini Selemani, Mussa Nkumila wa Ada Tadea na Hassani Rashidi wa Demokrasia Makini waliupata kura moja kila mmoja.

Diwani mteule, Kigeni mbali na kuwashukuru wananchi wa kata hiyo kwa kumpa ushindi, ameahidi kufanya kazi bega kwa bega na wananchi ili kuhakikisha maendeleo yanapatikana katika kata hiyo.

Uchaguzi wa kata hiyo umefanyika kufutatia aliyekuwa Diwani wake, Abdallah Kiembe kuajiriwa kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Kondoa.
Mia4 kwa Mia2

ni vigumu kuikabili CCM pekeyako au hata mkiungana 🐒

Bado sana dah🐒
 
Asilimia 36 ya waliojiandikisha ndio wamepiga kura. Takriban watu 1000 hawakupiga kura! Kuna ujumbe hapo.

Amandla...
 
Back
Top Bottom