Suley2019
JF-Expert Member
- Oct 7, 2019
- 1,817
- 4,566
Salaam Wakuu,
Ile Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo Ushahidi unaendelea kutolewa.
Fuatilia uzi huu ili kujua kinachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 28/10/2021
====
Mawakili upande wa utetezi tayari wameshafika mahakamani na kuketi katika nafasi zao, tayari kuanza kwa kesi.
Mawakili upande wa utetezi tayari wameshafika mahakamani na kuketi katika nafasi zao, tayari kuanza kwa kesi.
Shahidi akiwasili mahakamani, akiwa ameambatana na wakili wa Serikali, ambapo leo atakutana na wakili Peter Kibatala anayeongoza jopo la mawakili wa utetezi.
Upande wa utetezi ameongezeka Wakili Niyikiza Seth Jacob, ametokea Bukoba mkoa wa Kagera Kuja kuongeza nguvu katika kesi ya Mbowe na wenzake.
- Jaji ameingia Mahakamani, Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando anawatambulisha wenzake
1.Abdallah Chavula,
2. Jenitreza Kitali,
3. Nasorro Katuga,
4. Esther Martin,
5. Ignasi Mwinuka
6. Tulimanywa Majige
Wakili Kibatala anawatambilisha wenzake
1. Peter Kibatala
2. Bonifasia Mapunda
3. Seleman Matauka
4. Sisty Aloyce
5. Dickson Matata
6. Michael Mwangasa
7. Jonathan Mndeme
8. Hadija Aron
9. Evaresta Kisanga
10. Maria Mushi
11. Idd Msawanga
12. John Malya
Wakili wa Serikali: Shauri linalopaswa limekuja kwa a ajili ya Ushahidi na Shahidi namba mbili anaendelea
Jaji: Jana tuliishia kwa Mawakili wa Mshitakiwa wa Kwanza wa Pili, Naomba tuendelee na Wakili wa tatu Mshitakiwa na nakukumbusha Shahidi upo chini ya Kiapo, Naomba sasa.
MATATA: Kwa Niaba ya Mshtakiwa watatu sisi hatuna Maswali
JAJI: Wakili wa Mshtakiwa wa Nne
Kibatala: kwa Ruhusa yako Mheshimiwa Jaji naomba Kuuliza Maswali yakibakia nitaomba Michael Mwangasa amalizie.
Kibatala: Shahidi unakumbuka Jana wakati wa Ushahidi wako ulitaja namba zako za Simu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaweza kunitajia
Shahidi: 0693006700 na 0754916666
Kibatala: Unajua kuwa Umekuja Kutoa Ushahidi Kwenye kesi Nzito?
Shahidi: sijui Kesi Nzito, Najua Nimekuja kutoa Ushahidi tu
Kibatala: Unakumbuka wakati Unaandika Maelezo yako kwa Inspector Swila ulitoa namba zako za Simu
Shahidi: Hapana sikutoa
Kibatala: kwa Ruhusa ya Mahakama Unaweza Kusoma Hapa
Shahidi: 0754 216170
Kibatala: Je unasemaje kuhusu hizo namba
Shahidi: sijui sasa
Kibatala: Je iambie Mahakama chini ya Kiapo hizi namba Inspector Swila kazitoa wapi
Shahidi: Sijui
Kibatala: Shahidi unaweza kutuambia aliyethibitisha Maelezo ya Inspector Swila kuwa Maelezo ni sahihi ni nani?
Shahidi: Ni mimi
Kibatala: ni Mmoja wa aliyekuwa anawalinda Mahakamani wakati wa kesi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: tutarudi hapo baadae
Shahidi: Jana wakati Unatoa Ushahidi ulisema hujawahi kuwa Mwanachama wa Chama chochote cha siasa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hujawahi Kushiriki Kura za Maoni kata ya Pili?
Shahidi: Sijawahi
Kibatala: Kama Nikileta Ushahidi ulishiriki
Shahidi: walete Mahakamani
Kibatala: Nimesikia umesema kuwa Umeishi na Sabaya na Ukasema ulikuwa unaishi naye akiwa na Mke wake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je ulitutajia Jina la Mke wa Sabaya
Shahidi: Nilitaja Jina Moja la Jesca
Kibatala: Je Uliishi na Sabaya Kwa Muda gani akiwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Miezi Mitatu
Kibatala: Unafahamu Mahala anapoishi Mkuu wa Wilaya ni Mahala Nyeti
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Unafahamu Makazi ya Mkuu wa Wilaya ni Ikuku Ndogo ya Hilo eneo
Shahidi: sahihi
Kibatala: Unafahamu Kuwa kuna Baadhi ya Vikao Vya Kiusalama vinafanyika kwa Mkuu wa Wilaya
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Je, wewe ulifanyiwa Vetting na Tasisi yoyote?
Shahidi: Hapana
Kibatala: na Ulikuwa na Access ya Kuachiwa Nyumba na kuingia popote kwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Nimeona pia una jina lingine la Power Kaaya, umelitoa wapi
Shahidi: Tangu nikiwa Nyumbani
Kibatala: nitakuwa sahihi nikisema Umepewa hilo Jina baada ya Kufanya uhalifu sana Maeneo ya Longido na Arusha..?
Shahidi: Hapana si Kweli
Kibatala: nitarudi eneo hilo baadae
Kibatala: Je, unafahamu wakati Unakutana na Freeman Mbowe ulikuwa unafahamu ni Mwalifu
Shahidi: Sijui
Kibatala: Wakati Unakutana na Mbowe ulikuwa unajisikia Amani Kukutana naye peke yako?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati unampa Majina ulitambua kuwa yanakwenda kutendewa Uhalifu
Shahidi: Ndiyo nilijua kuwa kuna harufu ya uhalifu
Kibatala: Una Elimu gani Shahidi: Kidato cha Nne
Kibatala: Kwa hiyo ukiona Uhalifu wa Madawa ya Kulevya unatolea Taarifa wapi
Shahidi: Polisi
Kibatala: Ukiona uhalifu wa Wizi unatolea Taarifa wapi
Shahidi: Polisi
Kibatala: Je, Wakati Mbowe anakupatia pesa TSh Laki Mbili ulijua ilikuwa kwa ajili ya Uhalifu?
Shahidi: Hapana alisema ilikuwa ni ya Usumbufu
Kibatala: we Uliamini kuwa ni ya usumbufu?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisema baada ya Kukutana na Mbowe ulimpigia simu Mbunge na Sabaya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Je uliriport polisi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, Kazi ya Mbunge ni Kushughulika na uhalifu
Shahidi: Ndiyo wao ni watunga Sheria
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya kutoa Taarifa kwa Mbunge ulifuatilia kama amefanyia kazi Taarifa hiyo
Shahidi: Hapana sikufuatilia
Kibatala: Shika Maelezo yako haya Kielelezo D1 uliyoyatoa kwa Inspector Swila kama Ulimwambia Mambo ya Kihalifu aliyokwambia Mbowe
Shahidi: Haipo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa ulitolea Maelezo kwa Tasisi yoyote ya Kiuchunguzi kuhusu uhalifu wa Mbowe
Shahidi: Hakuna
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa ulimpigia Sabaya Simu, Je ulitaja namba za Simu za Sabaya
Shahidi: Sikuzitaja
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kuwa Baada ya Kumkosa Sabaya Ulifanya Jitihada za kumtafuta Sabaya
Shahidi: sikumwambia
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Baada ya kumkosa Sabaya ulimtafuta Mke wa Sabaya huyo Jesca kwamba Kuna Taarifa Mbaya ya Sabaya
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Uliowataja Jana ni Walinzi wa Sabaya?
Shahidi: Hapana ni Marafiki zake
Kibatala: hao uliokuwa umewataja Jana ulikuwa umefahamiana nao kwa muda mrefu au Mfupi
Shahidi: Muda Mfupi
Kibatala: Je, uliwataarifu hao Marafiki wa Sabaya
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Unakutana na Freeman Mbowe ulihisi uhalifu gani unataka kufanyika
Shahidi: Sikuwa nafahamu
Kibatala: Mkutano wa kwanza unaosema mlikutana na Mbowe, Kama Kweli ilikuwa Lini
Shahidi: mwaka 2020 Mwezi wa Kumi, sikumbuki tarehe.
Kibatala: nilisikia kuwa Umesema walikufuata na Gari, Je ilikuwa gari ya KUB?
Shahidi: ilikuwa gari ya Kiraia
Kibatala: ulisema alikuwa anaendesha Mwanamke?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Angalia Maelezo yako hapo, Je umeeleza kuhusu huyo Mwanamke
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuna Mahala yoyote ulitoa Taarifa, kama Polisi hivi, ndiyo ukaenda Kukutana naye
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Ulipokamatwa 20/08/2020 ulihifadhiwa Gereza gani..?
Shahidi: Ukonga
kibatala: Lakini Ulikutana na Mbowe Longido 0ctober 2020, Okeeeey Kazi yangu Kuuliza Maswali.
Kibatala: haya Mara ya Pili Mlikutana na Mbowe Wapi na lini
Shahidi: Mwanzoni Mwaka 2020
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi katika Statement ataona Khalfani Bwire alikwepo Katika Kikao Moshi
Shahidi: Khalfani Bwire alikuwa katika Kikao cha tatu
Kibatala: Sawa Mwambie sasa Katika hayo Maelezo yako, ni wapi ulimwambia Inspector Swila kuwa Khalfani Bwire alikwepo?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nini kilitangulia kati ya Maelezo yako na Ushahidi wako Mahakamani
Shahidi: Kilitangulia Maelezo
Kibatala: Je wewe ulimtambua Bwire wapi?
Shahidi: Kabla ya Mahakamani
Kibatala: kwa hiyo kumtambua Bwire umefanya Jana Hapa Mahakamani
Shahidi: Nilimtambua Kabla
Kibatala: kwa Hapo Kwenye maelezo ipo sehemu Umemtaja Bwire.?
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo sisi tunaona umefanya hivyo kwa mara ya kwanza Jana, uliwahi Kuwa nao Pamoja jela
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: mliongea nini
Shahidi: wao ndiyo walikuwa wananielezea walivyokuwa wanamtafuta Sabaya, Wakakurupushwa, wakahisi ni mimi.
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Mambo mazito kama hayo katika Statement hiyo atayaona Ukurasa wa ngapi
Shahidi: Hayapo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Mambo Mazito kama hayo kama uliriport kwa Mkuu wa Gereza
Shahidi: Sikusema
Kibatala: inawezekana wewe na Inspector Swila Mlipitiwa sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji kama uliriport Matukio kama hayo popote
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Ulizungumzia kuwa Ulikamatiwa wakati unapelekea pesa benki
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ukasema ulikuwa na Dollar na Euro
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ukasema ulikuwa unafanya Biashara na Hotel na Hotel gani
Shahidi: Mount Meru
Kibatala: Je, ulitoa kielelezo Chochote kama Ulilipwa fedha hizo
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji kwamba Ulibadili pesa kwa Euro na Dollar kwenda fedha za kitanzania
Shahidi: Nilifafanua Jana Kuwa nilipewa pesa mbalimbali
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Ulitoa Nyaraka za Malipo za Mount Meru
Shahidi: Sikutoa Kibatala: ulitaja Jina la Afisa aliyekulipa hizo pesa
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Mount Meru hawanunui papo kwa papo wanafanya kazi kwa mkataba na Mzabuni, Je ulitoa Mkataba kwa Jaji
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Ulitoa Risiti za TRA na Zingine, kwamba Biashara ni halali
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Je, unataka Mount Meru Hotel Leo wasikie wanapo fuatilia kesi hii wasikie luxury walikulipa Dollar 1000 cash
Shahidi: Siyo Mount Meru Bali Mtu wa Mount Meru
Kibatala: ooohooo Uliyasema hayo Jana
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Karoti za fedha hizo Nyingi sana, Je ulitoa Maelezo kuhusu Namna ulivyozipeleka, kwa usafiri gani na Risiti zake?
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Polisi walipokukamata Unawakumbuka?
Shahidi: Siwakumbuki
Kibatala: unasema ulihojiwa na Inspector Mahita
Shahidi: Ndiyo Kuhusu tuhuma zote
Kibatala: Mahojiano uliyafanyia wapi
Shahidi: Central Dar es Salaam
Kibatala: Mashitaka yalifutwa na Ukakabidhiwa fedha zako
Shahidi: Ndiyo nilirudishiwa
Kibatala: Walichukua hivi hivi au walikuandikisha na kukupa Karatasi
Shahidi: Walinipa Karatasi
Kibatala: Je jana Wakati Mawakili wa Serikali wakikuongoza walikuonyesha hapa Mahakamani hiyo karatasi
Shahidi: Hapana hawakunionyesha
Kibatala: swala la pesa ni kubwa sana, Je ulionyesha Karatasi kwamba sasa wamenirudishia
Shahidi: Sikuonyesha
Kibatala: Unaweza Kutuambia huyo Wakili wa Serikali ambaye badala ya kukwambia uende kwa DPP badala yake akakawambia uende Central
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: Sisi tunasema kuwa hizo Euro au Dollar hujarudishiwa
Shahidi: Wamenirudishia Kibatala: Sisi tutaamini Vipi
Shahidi: nimesema Chini ya kiapo
Kibatala: Ingekuwa hivyo usingekuwa unahojiwa hapa
Kibatala: haya niambie sasa kuhusu Kukutana na Freeman Mbowe, Je ulitoa Taarifa hapa Mahakamani kuwa Mlinzi wake sikuwa namfahamu Vizuri
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya Kuombwa Majina mara ya Pili Ulichukua tahadhari za Kwenda polisi
Shahidi: Sikusema
Kibatala: zile fedha ulizopokea ulizionaje za Kihalifu au fedha safi
Shahidi: Niliona Fedha safi
Kibatala: baada ya Kuona Siyo pesa Mbaya ndiyo Maana hukumuMwambia Sabaya, Mke wa Sabaya, wala Marafiki zake
Shahidi: Hapana, si kweli
Kibatala: Mwambie sasa Mheshimiwa Jaji hayo Majina Yamo katika Statement?
Shahidi: Hayamo
Kibatala: Kibatala Namba zao za Simu?
Shahidi: Hazimo
Kibatala: hilo gari la KUB uliona lini
Shahidi: January 2020
Kibatala: unataka Mahakama ikuchukulie wewe ni shahidi Muhimu na Umetoka kwa Chumbani wako kuja Kutoa Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu January 2020 Freeman Mbowe alikuwa Gerezani Segerea baada ya kufutiwa Dhamana Mahakama ya Kisutu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Mtu akiwa Gerezani Segerea anaweza Kukutana na wewe Longido
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: umezungumzia Joyce Mukya Jana, Nieleze kwenye Statement hiyo Umeandika Wapi
Shahidi: Hakuna mahala nilipoandika
Kibatala: kwetu Muhimu sana sijui Kwa Mahakama
Kibatala: Je kuna Karatasi Umetoa hapa Mhakamani inayoonyesha Ushahidi wa kwamba Namba hii ilimpigia namba hii, Je ulitoa Karatasi hiyo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana sikutoa
Kibatala: Ni kweli Freeman Mbowe ni Mtu Maarufu
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa hiyo hata mtu wa kawaida anaweza Kumfahamu Freeman Mbowe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sawa
Kibatala: Shahidi Jana Ulizungumzia kuwa wewe ni Mkulima, Je Mkulima analipa kodi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa wewe Ulitoa Karatasi yoyote hapa Mahakamani Kwamba unalipa Kodi
Shahidi: sikutoa kibatala: Jana Ulimtajia Majina ya Kina japhet na wenzake kwamba Je ni Viongozi wa Serikali
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je unafahamu Kuwa Sabaya kwa Mujibu wa sheria ni Muhalifu hapa tunavyoongea
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: ila Unajua kuwa amefungwa Miaka 30
Shahidi: Ndiyo nimesikia
Kibatala: Umesikia kafungwa ila hujui kama ni Muhalifu na alifanya uhalifu Miaka ya 2018 Mpaka 2020
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Bila shaka hufahamu pia kwamba Freeman Mbowe aliwasiliana na IGP SIRRO Kumfahamisha Matendo ya Kihalifu aliyokuwa anatenda Sabaya
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: bila Shaka hufahamu pia kuwa ni Wajibu wa Raia Mwema Kukusanya Taarifa na Kuzifikisha kwa Mamlaka husika
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Mwanzoni ulisema kuwa Mbunge kazi yake ni Kushughulika na Uhalifu
Shahidi: Nilisema Kuwa Mbunge kazi yake ni Kutunga Sheria na anaweza Kushughulika na uhalifu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa kuwa Wakati Mbowe anakuomba Taarifa alikuwa Mbunge
Shahidi: Alikuwa Mbunge wa Hai
Kibatala: Je, unafahamu Mtu uliye mtajia Jina lake Sylvester Nyegu amehukuliwa Kifungu cha Miaka 30 na Sabaya Kwa Makosa ya Ujambazi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Huyo ndiyo uliyempatia Freeman Mbowe Taarifa zake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Umesema hujui kuwa Mbowe alikuomba Taarifa zao
Shahidi: Ndiyo sikuwa nafahamu
Kibatala: hufahamu kuwa Hizo Taarifa alizishughulikia
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kama nakumbuka baada ya Kumpatia Mbowe Majina na Namba nimekunukuu Mbowe alisema "Wewe niache Mimi nafahamu nitashughulika nao Vipi"
Shahidi: Ndiyo alisema hivyo
Kibatala: Na Hukusema kama Mbowe alikwambia kuwa anataka kumdhuru Sabaya wala Wenzie
Shahidi: Hakusema
Kibatala: Jana Katika Statement Yako umeeleza kuwa ulimtongoza Helga Mchomvu
Shahidi: Ndiyo ni sahihi
Kibatala: unafahamu Helga Mchomvu Aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Ya Hai kuwa anamiaka Mingapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mimi Nakwambia Sasa Ana miaka 60,wewe Unamiaka Mingapi
Shahidi: Miaka 31
Kibatala: na Ulimtongoza
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jana Katika ushahidi wako ulisema palikuwa na Diwani wa kiboriloni
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama ulitaja Jina lake
Shahidi: Sikutaja Jina lake
Kibatala: Je unafahamu Kuwa Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Hai alitekwa na kumizwa Vibaya
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo unafahamu kuwa Mbowe kama Mbunge alikuwa anafuatilia Taarifa za Uhalifu wa watu waliomdhuru Kiongozi wake
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Jana ulitaja Majina ya SG hotel na Gold Crest Hotel
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu sehemu zote hizo Sabaya alikuwa hawezi Kufika kwa sababu ya madeni Makubwa ambayo alikuwa halipi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umesema pia ulilala Aishi Hotel
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulitaja Jina la Chumba Ulicho Lala..?
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulitaja Aina Ya Chakula Ulicho kura pale
Shahidi: Hapana
Kibatala: Nilisikia mara zote ulikuwa unasafiri kwa kutumia public transport
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Na ni sahihi Hukutoa risiti/Ticket yoyote ya Magari uliyokuwa unasafiria
Shahidi: ni sahihi
Kibatala: ni sahihi kwamba Ulikuwa unaendelea kuwasiliana na hao Marafiki wa Sabaya Mpaka Muda Unakutana na Mbowe Mara ya Mwisho
Shahidi: Sahihi Kibatala: na hukumwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa mlikuwa mnawasiliana kwa Mambo Mema au Mabaya
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji labda kama Mwenzangu atakuwa na Maswali
Michael Mwangasa: unatamani Mahakama Iamini kuwa Ushahidi wako ni wa kweli
Shahidi: Ndiyo natamani
Michael: Je Kuna Mahala yoyote Umesema Mbowe alishiriki Vikao Vya ugaidi
Shahidi: Hapana, Sikusema
Michael: Je kuna sehemu yoyote Umesema kuwa uliwahi kushiriki Vikao Vya Ugaidi na Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Sikusema
Michael: Je uliiambia Mahakama Kwamba ulishiriki Vikao Vya ugaidi
Shahidi: Nilieleza Vikao tu
Michael: Kweli kuwa ulikuwa unafanya Vikao na Mbowe na kushitakiwa, kisha Kuachiwa huru
Shahidi: Nilisema nilishitakiwa nikaachiwa huru
Michael: Ulisema ulimpatia Mbowe namba za akina Japhet, Je ulitaja hizo namba hapa Mahakamani
Shahidi: Sikutaja
Michael: Ulisema Ulimpa Taarifa Mbunge wa Longido Taarifa za Kiuhalifu?
Shahidi: Hazikuwa Taarifa za Kiuhalifu, nilimwambia kuna mtu Mkubwa amekuja Longido kunifuata sikutegemea
Michael: ni sahihi hukusema hapa Mahakamani kuwa walikupa Mrejesho gani?
Shahidi: ndiyo
Michael: nitakuwa sahihi nikisema walikupuuza?
Shahidi: Sijui
Michael: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
---
Jaji: Re examination?
Wakili wa Serikali: tutaendelea na Re Examination na ataanza Abdallah Chavula kwa Ruhusa yako Mheshimiwa Jaji tungeomba tupatiwe Kielelezo E1
Principal State attorney, Akitaka aweke hayo kwenye final submission.
Wakili wa Serikali: Shahidi Umeulizwa Maswala Mengi sana kuhusiana na Karatasi ya Maelezo uliyoyatoa Polisi dhidi ya Maelezo uliyoyatoa hapa Mahakamani, Wakiwa wanataka Kuonyesha
Kibatala: OBJECTION aende Straight kwenye Re examination, anajua kuwa hairuhusiwi na ni...
Jaji: Wakili wa Serikali Unasemaje
Wakili wa Serikali: Sawa
Wakili wa Serikali: kwanini Kwenye Statement yako uliyotoa Polisi haina Maelezo uliyoyatoa Jana Mahakamani
Shahidi: Kwa sababu Jana ilikuwa naeleza kwa urefu Nilichoandika kwenye Statement yangu polisi.
Wakili wa Serikali: NitaKukabidhi sasa hii Karatasi ufafanue
Shahidi: hapa Nimeona Nimeeleza Kuhusu Kilimo, Nilikuwa nalima Viazi na Karoti. Jambo Lingine ni Mwandishi amekosea Mwaka nilioacha kazi kwa Sabaya. Ambaye Mheshimiwa alinitambulisha kuwa ni Kiongozi wa Ulinzi Kanda ya kaskazini.
Jaji: hapo sasa Mnafanya nini Wakili wa Serikali
Shahidi: anafafanua kilichopo
Jaji: afafanue Sasa
Wakili wa Serikali: Sawa
Shahidi: Swala lingine nilimtaja yule Diwani
Wakili wa Serikali: Kwenye Ushahidi wako ulitaja Diwani wa wapi ?
Shahidi: Diwani wa Kiboboroni
Mallya: OBJECTION hiyo ni fact Mpya kuhusu ni Kiongozi wa ulinzi Kanda ya kaskazini
Jaji: Mimi nilirekodi hivyo
Mallya: kama Mahakama ili Rekodi sina tatizo
Wakili wa Serikali: Kuhusiana na huyo Diwani ulisema nini?
Shahidi: Sikutaja Jina la Diwani
Wakili wa Serikali: sasa Uliambia Mahakama Huyo anaitwa nani
Kibatala: Sasa Ndiyo tunafanya nini, Shahidi ameshasema hakutaja Jina, yeye anataka Shahidi ajibu nini cha ziada.
Jaji: Ngoja tuone swali lake Maana hata Mimi nimerekodi kuwa Hakutaja Jina la Diwani
Wakili wa Serikali: Tueleze kuhusu Majina na Maeneo uliyoyatoa Jana hukutaja.? Shahidi: Sikutaja
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa kwanini sasa Katika Maelezo yako Polisi hukutaja na Jana hukataja
Shahidi: Nilichofanya nilifanya ufafanuzi kwa kutaja hayo Majina niliyomtajia Mheshimiwa Mbowe bowe ..wakawa wananichanganya baadae nikakumbuka.
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kuhusu Kukutana na Bwana Mbowe Ukasema ni Mwanzoni mwa October 2020 longido na Baadae Ukasema ni October 2018 fafanunua Mkanganyiko huo
Shahidi: kwa sababu Mawakili wa Upande wa Utetezi walikuwa wananiuliza kwa njia Isiyo sahihi...
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Naomba nimkaribishe Mwenzangu
Shahidi: Ninachofahamu yeye alinitafuta akiwa na Mikutano ya Jimbo
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kuhusu Vikao kama Vilikuwa Vya kigaidi Ukasema Hapana Sasa hoja ilikuwa ni nini
Shahidi: Hoja ilikuwa ni Kuomba Majina ya wale Vijana wanaotembea na Sabaya na Namba zao za Simu
Wakili wa Serikali: Ukaulizwa na Wakili Kibatala Kwamba, Kama ulikuwa na hofu ya kiuhalifu Ukasema Hapana hebu fafanua
Shahidi: nilipata hofu kwa sababu Yeye alikuwa Mbunge na Sabaya alikuwa Mkuu wa Wilaya, nikajiuliza kwanini asitafuti kwa Kiongozi Mwenzie
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusu Kule Longido baada ya Kumtafuta Sabaya ukampigia Mbunge na Hukuriport hata Polisi
Shahidi: ni Kwa sababu nilihisi wote ni Viongozi na atamwambia mwenzie nikawa nimeshafikisha ujumbe
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwamba Neno Bwire ni Msiri na Mlinzi wa mbowe, Elezea Sasa Kule Polisi Ulimtaja kwa namna gani?
Shahidi: Nilitaja kuwa alikuwa na Mlinzi, hapa nikajakutoa ufafanuzi
Wakili wa Serikali: Hebu fafanua kuhusu Biashara yako na mount meru ilikuwa je hukuleta nyaraka za Malipo hapa Mahakamani
Shahidi: Kwa sababu nilikwepo Muda mrefu Gerezani na Nyaraka hizo ni za Muda Mrefu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama Ulileta Nyaraka za Mount Meru Ukasema hujaileta, kwa sababu Ulifanya na mtu wao hebu tufafanulie
Shahidi: ni Kwa sababu Kuna watu wanakuja kwa wakulima kwa ajili ya Kupeleka Mazao Mount meru.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana kutotaja watu wa Sabaya Pale Polisi
Shahidi: niliulizwa Majina ya watu hao hapa Mahakamani, Hapo kwenye maelezo Siku ya orodhesha
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana na Jina Power Kaaya kwamba linatokana na Matendo ya Kihalifu, tufafanulie kwanini unaitwa Power Kaaya
Shahidi: ni Jina langu Ndiyo Maana naitwa Power Kaaya hata kwenye Charge Sheet lipo, tangu kwenye ubatizo niliitwa Power
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba Ulipewa Laki 2 ndiyo Maana Hukutoa Taarifa polisi
Shahidi: OBJECTION, Sikuwa nimesema Kitu hicho
Jaji: Hata Mimi Siku Rekodi Jambo hilo
Wakili wa Serikali: Kuhusiana na namba hiyo kwenye Statement hukasema siyo Namba yako, kwanini sasa unasema siyo Namba yako
Shahidi: Sijui Sasa Mwandishi aliyeandika
Wakili wa Serikali: Na Ukaulizwa kuhusiana namba zako mbili za Simu na Ukaulizwa kama Ulileta Uthibitisho Mahakamani, elezea Sasa kwanini unasema namba hizo ni zako
Shahidi: kwa sababu Namba hizo ndiyo nazitumia
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Swali Kwamba Katika Dhamana ya Mbowe kuwa aliwahi kufutiwa Dhamana, je Ni kitu gani walichokuonyesha kuwa walikuwa na Kesi na ikafutwa Dhamana
Shahidi: Hawajanionyesha Kitu chochote
Wakili wa Serikali: Umeulizwa kuhusiana uhalifu wa Sylvester Nyegu na Ole Sabaya Ukasema Ufahamu, elezea kwanini ufahamu
Shahidi: Kwa sababu wakati wanakamatwa Mimi nilikuwa Gerezani
Wakili wa Serikali: Shahidi Mwingine tuliyekuwa tumemuita hajafika, hivyo tunaomba Hairisho hadi Kesho tarehe 29 Mwezi wa 10 ilituweze kuendelea na Shahidi Mwingine
Jaji: Shahidi Tunashukuru kwa Ushahidi wako, una eza kwenda sasa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji huyo ndiyo Shahidi tuliyekuwa naye kwa Leo
Jaji: Shauri linahairishwa mpka Kesho saa 3 Asubuhi
Ile Kesi inayomkabili Freeman Mbowe na wenzake itaendelea katika Mahakama Kuu, Divisheni ya Uhujumu Uchumi na Rushwa, ambapo Ushahidi unaendelea kutolewa.
Fuatilia uzi huu ili kujua kinachojiri katika mchakato mzima wa kesi hiyo kwa siku ya leo 28/10/2021
====
Mawakili upande wa utetezi tayari wameshafika mahakamani na kuketi katika nafasi zao, tayari kuanza kwa kesi.
Mawakili upande wa utetezi tayari wameshafika mahakamani na kuketi katika nafasi zao, tayari kuanza kwa kesi.
Shahidi akiwasili mahakamani, akiwa ameambatana na wakili wa Serikali, ambapo leo atakutana na wakili Peter Kibatala anayeongoza jopo la mawakili wa utetezi.
Upande wa utetezi ameongezeka Wakili Niyikiza Seth Jacob, ametokea Bukoba mkoa wa Kagera Kuja kuongeza nguvu katika kesi ya Mbowe na wenzake.
- Jaji ameingia Mahakamani, Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 inatajwa
Wakili wa Serikali Robert Kidando anawatambulisha wenzake
1.Abdallah Chavula,
2. Jenitreza Kitali,
3. Nasorro Katuga,
4. Esther Martin,
5. Ignasi Mwinuka
6. Tulimanywa Majige
Wakili Kibatala anawatambilisha wenzake
1. Peter Kibatala
2. Bonifasia Mapunda
3. Seleman Matauka
4. Sisty Aloyce
5. Dickson Matata
6. Michael Mwangasa
7. Jonathan Mndeme
8. Hadija Aron
9. Evaresta Kisanga
10. Maria Mushi
11. Idd Msawanga
12. John Malya
Wakili wa Serikali: Shauri linalopaswa limekuja kwa a ajili ya Ushahidi na Shahidi namba mbili anaendelea
Jaji: Jana tuliishia kwa Mawakili wa Mshitakiwa wa Kwanza wa Pili, Naomba tuendelee na Wakili wa tatu Mshitakiwa na nakukumbusha Shahidi upo chini ya Kiapo, Naomba sasa.
MATATA: Kwa Niaba ya Mshtakiwa watatu sisi hatuna Maswali
JAJI: Wakili wa Mshtakiwa wa Nne
Wakili Kibatala ameanza kumuuliza Shahidi maswali
Kibatala: kwa Ruhusa yako Mheshimiwa Jaji naomba Kuuliza Maswali yakibakia nitaomba Michael Mwangasa amalizie.
Kibatala: Shahidi unakumbuka Jana wakati wa Ushahidi wako ulitaja namba zako za Simu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unaweza kunitajia
Shahidi: 0693006700 na 0754916666
Kibatala: Unajua kuwa Umekuja Kutoa Ushahidi Kwenye kesi Nzito?
Shahidi: sijui Kesi Nzito, Najua Nimekuja kutoa Ushahidi tu
Kibatala: Unakumbuka wakati Unaandika Maelezo yako kwa Inspector Swila ulitoa namba zako za Simu
Shahidi: Hapana sikutoa
Kibatala: kwa Ruhusa ya Mahakama Unaweza Kusoma Hapa
Shahidi: 0754 216170
Kibatala: Je unasemaje kuhusu hizo namba
Shahidi: sijui sasa
Kibatala: Je iambie Mahakama chini ya Kiapo hizi namba Inspector Swila kazitoa wapi
Shahidi: Sijui
Kibatala: Shahidi unaweza kutuambia aliyethibitisha Maelezo ya Inspector Swila kuwa Maelezo ni sahihi ni nani?
Shahidi: Ni mimi
Kibatala: ni Mmoja wa aliyekuwa anawalinda Mahakamani wakati wa kesi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: tutarudi hapo baadae
Shahidi: Jana wakati Unatoa Ushahidi ulisema hujawahi kuwa Mwanachama wa Chama chochote cha siasa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: hujawahi Kushiriki Kura za Maoni kata ya Pili?
Shahidi: Sijawahi
Kibatala: Kama Nikileta Ushahidi ulishiriki
Shahidi: walete Mahakamani
Kibatala: Nimesikia umesema kuwa Umeishi na Sabaya na Ukasema ulikuwa unaishi naye akiwa na Mke wake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je ulitutajia Jina la Mke wa Sabaya
Shahidi: Nilitaja Jina Moja la Jesca
Kibatala: Je Uliishi na Sabaya Kwa Muda gani akiwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Miezi Mitatu
Kibatala: Unafahamu Mahala anapoishi Mkuu wa Wilaya ni Mahala Nyeti
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Unafahamu Makazi ya Mkuu wa Wilaya ni Ikuku Ndogo ya Hilo eneo
Shahidi: sahihi
Kibatala: Unafahamu Kuwa kuna Baadhi ya Vikao Vya Kiusalama vinafanyika kwa Mkuu wa Wilaya
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Je, wewe ulifanyiwa Vetting na Tasisi yoyote?
Shahidi: Hapana
Kibatala: na Ulikuwa na Access ya Kuachiwa Nyumba na kuingia popote kwa Mkuu wa wilaya
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Nimeona pia una jina lingine la Power Kaaya, umelitoa wapi
Shahidi: Tangu nikiwa Nyumbani
Kibatala: nitakuwa sahihi nikisema Umepewa hilo Jina baada ya Kufanya uhalifu sana Maeneo ya Longido na Arusha..?
Shahidi: Hapana si Kweli
Kibatala: nitarudi eneo hilo baadae
Kibatala: Je, unafahamu wakati Unakutana na Freeman Mbowe ulikuwa unafahamu ni Mwalifu
Shahidi: Sijui
Kibatala: Wakati Unakutana na Mbowe ulikuwa unajisikia Amani Kukutana naye peke yako?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Wakati unampa Majina ulitambua kuwa yanakwenda kutendewa Uhalifu
Shahidi: Ndiyo nilijua kuwa kuna harufu ya uhalifu
Kibatala: Una Elimu gani Shahidi: Kidato cha Nne
Kibatala: Kwa hiyo ukiona Uhalifu wa Madawa ya Kulevya unatolea Taarifa wapi
Shahidi: Polisi
Kibatala: Ukiona uhalifu wa Wizi unatolea Taarifa wapi
Shahidi: Polisi
Kibatala: Je, Wakati Mbowe anakupatia pesa TSh Laki Mbili ulijua ilikuwa kwa ajili ya Uhalifu?
Shahidi: Hapana alisema ilikuwa ni ya Usumbufu
Kibatala: we Uliamini kuwa ni ya usumbufu?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisema baada ya Kukutana na Mbowe ulimpigia simu Mbunge na Sabaya
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Je uliriport polisi?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, Kazi ya Mbunge ni Kushughulika na uhalifu
Shahidi: Ndiyo wao ni watunga Sheria
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya kutoa Taarifa kwa Mbunge ulifuatilia kama amefanyia kazi Taarifa hiyo
Shahidi: Hapana sikufuatilia
Kibatala: Shika Maelezo yako haya Kielelezo D1 uliyoyatoa kwa Inspector Swila kama Ulimwambia Mambo ya Kihalifu aliyokwambia Mbowe
Shahidi: Haipo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa ulitolea Maelezo kwa Tasisi yoyote ya Kiuchunguzi kuhusu uhalifu wa Mbowe
Shahidi: Hakuna
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa ulimpigia Sabaya Simu, Je ulitaja namba za Simu za Sabaya
Shahidi: Sikuzitaja
Kibatala: Ulimwambia Jaji Kuwa Baada ya Kumkosa Sabaya Ulifanya Jitihada za kumtafuta Sabaya
Shahidi: sikumwambia
Kibatala: ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa Baada ya kumkosa Sabaya ulimtafuta Mke wa Sabaya huyo Jesca kwamba Kuna Taarifa Mbaya ya Sabaya
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Uliowataja Jana ni Walinzi wa Sabaya?
Shahidi: Hapana ni Marafiki zake
Kibatala: hao uliokuwa umewataja Jana ulikuwa umefahamiana nao kwa muda mrefu au Mfupi
Shahidi: Muda Mfupi
Kibatala: Je, uliwataarifu hao Marafiki wa Sabaya
Shahidi: Hapana
Kibatala: Wakati Unakutana na Freeman Mbowe ulihisi uhalifu gani unataka kufanyika
Shahidi: Sikuwa nafahamu
Kibatala: Mkutano wa kwanza unaosema mlikutana na Mbowe, Kama Kweli ilikuwa Lini
Shahidi: mwaka 2020 Mwezi wa Kumi, sikumbuki tarehe.
Kibatala: nilisikia kuwa Umesema walikufuata na Gari, Je ilikuwa gari ya KUB?
Shahidi: ilikuwa gari ya Kiraia
Kibatala: ulisema alikuwa anaendesha Mwanamke?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Angalia Maelezo yako hapo, Je umeeleza kuhusu huyo Mwanamke
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kuna Mahala yoyote ulitoa Taarifa, kama Polisi hivi, ndiyo ukaenda Kukutana naye
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Ulipokamatwa 20/08/2020 ulihifadhiwa Gereza gani..?
Shahidi: Ukonga
kibatala: Lakini Ulikutana na Mbowe Longido 0ctober 2020, Okeeeey Kazi yangu Kuuliza Maswali.
Kibatala: haya Mara ya Pili Mlikutana na Mbowe Wapi na lini
Shahidi: Mwanzoni Mwaka 2020
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji ni wapi katika Statement ataona Khalfani Bwire alikwepo Katika Kikao Moshi
Shahidi: Khalfani Bwire alikuwa katika Kikao cha tatu
Kibatala: Sawa Mwambie sasa Katika hayo Maelezo yako, ni wapi ulimwambia Inspector Swila kuwa Khalfani Bwire alikwepo?
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Nini kilitangulia kati ya Maelezo yako na Ushahidi wako Mahakamani
Shahidi: Kilitangulia Maelezo
Kibatala: Je wewe ulimtambua Bwire wapi?
Shahidi: Kabla ya Mahakamani
Kibatala: kwa hiyo kumtambua Bwire umefanya Jana Hapa Mahakamani
Shahidi: Nilimtambua Kabla
Kibatala: kwa Hapo Kwenye maelezo ipo sehemu Umemtaja Bwire.?
Shahidi: Hapana
Kibatala: kwa hiyo sisi tunaona umefanya hivyo kwa mara ya kwanza Jana, uliwahi Kuwa nao Pamoja jela
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: mliongea nini
Shahidi: wao ndiyo walikuwa wananielezea walivyokuwa wanamtafuta Sabaya, Wakakurupushwa, wakahisi ni mimi.
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Mambo mazito kama hayo katika Statement hiyo atayaona Ukurasa wa ngapi
Shahidi: Hayapo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Mambo Mazito kama hayo kama uliriport kwa Mkuu wa Gereza
Shahidi: Sikusema
Kibatala: inawezekana wewe na Inspector Swila Mlipitiwa sasa Mwambie Mheshimiwa Jaji kama uliriport Matukio kama hayo popote
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Je Ulizungumzia kuwa Ulikamatiwa wakati unapelekea pesa benki
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ukasema ulikuwa na Dollar na Euro
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Ukasema ulikuwa unafanya Biashara na Hotel na Hotel gani
Shahidi: Mount Meru
Kibatala: Je, ulitoa kielelezo Chochote kama Ulilipwa fedha hizo
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: ulifafanua kwa Mheshimiwa Jaji kwamba Ulibadili pesa kwa Euro na Dollar kwenda fedha za kitanzania
Shahidi: Nilifafanua Jana Kuwa nilipewa pesa mbalimbali
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kuwa Ulitoa Nyaraka za Malipo za Mount Meru
Shahidi: Sikutoa Kibatala: ulitaja Jina la Afisa aliyekulipa hizo pesa
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Mount Meru hawanunui papo kwa papo wanafanya kazi kwa mkataba na Mzabuni, Je ulitoa Mkataba kwa Jaji
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Ulitoa Risiti za TRA na Zingine, kwamba Biashara ni halali
Shahidi: Sikutoa
Kibatala: Je, unataka Mount Meru Hotel Leo wasikie wanapo fuatilia kesi hii wasikie luxury walikulipa Dollar 1000 cash
Shahidi: Siyo Mount Meru Bali Mtu wa Mount Meru
Kibatala: ooohooo Uliyasema hayo Jana
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Karoti za fedha hizo Nyingi sana, Je ulitoa Maelezo kuhusu Namna ulivyozipeleka, kwa usafiri gani na Risiti zake?
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Polisi walipokukamata Unawakumbuka?
Shahidi: Siwakumbuki
Kibatala: unasema ulihojiwa na Inspector Mahita
Shahidi: Ndiyo Kuhusu tuhuma zote
Kibatala: Mahojiano uliyafanyia wapi
Shahidi: Central Dar es Salaam
Kibatala: Mashitaka yalifutwa na Ukakabidhiwa fedha zako
Shahidi: Ndiyo nilirudishiwa
Kibatala: Walichukua hivi hivi au walikuandikisha na kukupa Karatasi
Shahidi: Walinipa Karatasi
Kibatala: Je jana Wakati Mawakili wa Serikali wakikuongoza walikuonyesha hapa Mahakamani hiyo karatasi
Shahidi: Hapana hawakunionyesha
Kibatala: swala la pesa ni kubwa sana, Je ulionyesha Karatasi kwamba sasa wamenirudishia
Shahidi: Sikuonyesha
Kibatala: Unaweza Kutuambia huyo Wakili wa Serikali ambaye badala ya kukwambia uende kwa DPP badala yake akakawambia uende Central
Shahidi: Simkumbuki
Kibatala: Sisi tunasema kuwa hizo Euro au Dollar hujarudishiwa
Shahidi: Wamenirudishia Kibatala: Sisi tutaamini Vipi
Shahidi: nimesema Chini ya kiapo
Kibatala: Ingekuwa hivyo usingekuwa unahojiwa hapa
Kibatala: haya niambie sasa kuhusu Kukutana na Freeman Mbowe, Je ulitoa Taarifa hapa Mahakamani kuwa Mlinzi wake sikuwa namfahamu Vizuri
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je, Ulimwambia Mheshimiwa Jaji baada ya Kuombwa Majina mara ya Pili Ulichukua tahadhari za Kwenda polisi
Shahidi: Sikusema
Kibatala: zile fedha ulizopokea ulizionaje za Kihalifu au fedha safi
Shahidi: Niliona Fedha safi
Kibatala: baada ya Kuona Siyo pesa Mbaya ndiyo Maana hukumuMwambia Sabaya, Mke wa Sabaya, wala Marafiki zake
Shahidi: Hapana, si kweli
Kibatala: Mwambie sasa Mheshimiwa Jaji hayo Majina Yamo katika Statement?
Shahidi: Hayamo
Kibatala: Kibatala Namba zao za Simu?
Shahidi: Hazimo
Kibatala: hilo gari la KUB uliona lini
Shahidi: January 2020
Kibatala: unataka Mahakama ikuchukulie wewe ni shahidi Muhimu na Umetoka kwa Chumbani wako kuja Kutoa Ushahidi
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu January 2020 Freeman Mbowe alikuwa Gerezani Segerea baada ya kufutiwa Dhamana Mahakama ya Kisutu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je Mtu akiwa Gerezani Segerea anaweza Kukutana na wewe Longido
Shahidi: Hapana Sifahamu
Kibatala: umezungumzia Joyce Mukya Jana, Nieleze kwenye Statement hiyo Umeandika Wapi
Shahidi: Hakuna mahala nilipoandika
Kibatala: kwetu Muhimu sana sijui Kwa Mahakama
Kibatala: Je kuna Karatasi Umetoa hapa Mhakamani inayoonyesha Ushahidi wa kwamba Namba hii ilimpigia namba hii, Je ulitoa Karatasi hiyo hapa Mahakamani
Shahidi: Hapana sikutoa
Kibatala: Ni kweli Freeman Mbowe ni Mtu Maarufu
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: kwa hiyo hata mtu wa kawaida anaweza Kumfahamu Freeman Mbowe
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sawa
Kibatala: Shahidi Jana Ulizungumzia kuwa wewe ni Mkulima, Je Mkulima analipa kodi?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Sasa wewe Ulitoa Karatasi yoyote hapa Mahakamani Kwamba unalipa Kodi
Shahidi: sikutoa kibatala: Jana Ulimtajia Majina ya Kina japhet na wenzake kwamba Je ni Viongozi wa Serikali
Shahidi: Hapana
Kibatala: Je unafahamu Kuwa Sabaya kwa Mujibu wa sheria ni Muhalifu hapa tunavyoongea
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: ila Unajua kuwa amefungwa Miaka 30
Shahidi: Ndiyo nimesikia
Kibatala: Umesikia kafungwa ila hujui kama ni Muhalifu na alifanya uhalifu Miaka ya 2018 Mpaka 2020
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Bila shaka hufahamu pia kwamba Freeman Mbowe aliwasiliana na IGP SIRRO Kumfahamisha Matendo ya Kihalifu aliyokuwa anatenda Sabaya
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: bila Shaka hufahamu pia kuwa ni Wajibu wa Raia Mwema Kukusanya Taarifa na Kuzifikisha kwa Mamlaka husika
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Mwanzoni ulisema kuwa Mbunge kazi yake ni Kushughulika na Uhalifu
Shahidi: Nilisema Kuwa Mbunge kazi yake ni Kutunga Sheria na anaweza Kushughulika na uhalifu
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa kuwa Wakati Mbowe anakuomba Taarifa alikuwa Mbunge
Shahidi: Alikuwa Mbunge wa Hai
Kibatala: Je, unafahamu Mtu uliye mtajia Jina lake Sylvester Nyegu amehukuliwa Kifungu cha Miaka 30 na Sabaya Kwa Makosa ya Ujambazi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Huyo ndiyo uliyempatia Freeman Mbowe Taarifa zake
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: na Umesema hujui kuwa Mbowe alikuomba Taarifa zao
Shahidi: Ndiyo sikuwa nafahamu
Kibatala: hufahamu kuwa Hizo Taarifa alizishughulikia
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kama nakumbuka baada ya Kumpatia Mbowe Majina na Namba nimekunukuu Mbowe alisema "Wewe niache Mimi nafahamu nitashughulika nao Vipi"
Shahidi: Ndiyo alisema hivyo
Kibatala: Na Hukusema kama Mbowe alikwambia kuwa anataka kumdhuru Sabaya wala Wenzie
Shahidi: Hakusema
Kibatala: Jana Katika Statement Yako umeeleza kuwa ulimtongoza Helga Mchomvu
Shahidi: Ndiyo ni sahihi
Kibatala: unafahamu Helga Mchomvu Aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri Ya Hai kuwa anamiaka Mingapi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Mimi Nakwambia Sasa Ana miaka 60,wewe Unamiaka Mingapi
Shahidi: Miaka 31
Kibatala: na Ulimtongoza
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Jana Katika ushahidi wako ulisema palikuwa na Diwani wa kiboriloni
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama ulitaja Jina lake
Shahidi: Sikutaja Jina lake
Kibatala: Je unafahamu Kuwa Mwenyekiti wa Chadema jimbo la Hai alitekwa na kumizwa Vibaya
Shahidi: sifahamu
Kibatala: Kwa hiyo unafahamu kuwa Mbowe kama Mbunge alikuwa anafuatilia Taarifa za Uhalifu wa watu waliomdhuru Kiongozi wake
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Jana ulitaja Majina ya SG hotel na Gold Crest Hotel
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu sehemu zote hizo Sabaya alikuwa hawezi Kufika kwa sababu ya madeni Makubwa ambayo alikuwa halipi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umesema pia ulilala Aishi Hotel
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Ulitaja Jina la Chumba Ulicho Lala..?
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulitaja Aina Ya Chakula Ulicho kura pale
Shahidi: Hapana
Kibatala: Nilisikia mara zote ulikuwa unasafiri kwa kutumia public transport
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Na ni sahihi Hukutoa risiti/Ticket yoyote ya Magari uliyokuwa unasafiria
Shahidi: ni sahihi
Kibatala: ni sahihi kwamba Ulikuwa unaendelea kuwasiliana na hao Marafiki wa Sabaya Mpaka Muda Unakutana na Mbowe Mara ya Mwisho
Shahidi: Sahihi Kibatala: na hukumwambia Mheshimiwa Jaji Kuwa mlikuwa mnawasiliana kwa Mambo Mema au Mabaya
Shahidi: Sikusema
Kibatala: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji labda kama Mwenzangu atakuwa na Maswali
Wakili Michael Mwangasa ameanza kuuliza maswali
Michael Mwangasa: unatamani Mahakama Iamini kuwa Ushahidi wako ni wa kweli
Shahidi: Ndiyo natamani
Michael: Je Kuna Mahala yoyote Umesema Mbowe alishiriki Vikao Vya ugaidi
Shahidi: Hapana, Sikusema
Michael: Je kuna sehemu yoyote Umesema kuwa uliwahi kushiriki Vikao Vya Ugaidi na Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Sikusema
Michael: Je uliiambia Mahakama Kwamba ulishiriki Vikao Vya ugaidi
Shahidi: Nilieleza Vikao tu
Michael: Kweli kuwa ulikuwa unafanya Vikao na Mbowe na kushitakiwa, kisha Kuachiwa huru
Shahidi: Nilisema nilishitakiwa nikaachiwa huru
Michael: Ulisema ulimpatia Mbowe namba za akina Japhet, Je ulitaja hizo namba hapa Mahakamani
Shahidi: Sikutaja
Michael: Ulisema Ulimpa Taarifa Mbunge wa Longido Taarifa za Kiuhalifu?
Shahidi: Hazikuwa Taarifa za Kiuhalifu, nilimwambia kuna mtu Mkubwa amekuja Longido kunifuata sikutegemea
Michael: ni sahihi hukusema hapa Mahakamani kuwa walikupa Mrejesho gani?
Shahidi: ndiyo
Michael: nitakuwa sahihi nikisema walikupuuza?
Shahidi: Sijui
Michael: Ni hayo tu Mheshimiwa Jaji
---
Jaji: Re examination?
Wakili wa Serikali: tutaendelea na Re Examination na ataanza Abdallah Chavula kwa Ruhusa yako Mheshimiwa Jaji tungeomba tupatiwe Kielelezo E1
Principal State attorney, Akitaka aweke hayo kwenye final submission.
Wakili wa Serikali: Shahidi Umeulizwa Maswala Mengi sana kuhusiana na Karatasi ya Maelezo uliyoyatoa Polisi dhidi ya Maelezo uliyoyatoa hapa Mahakamani, Wakiwa wanataka Kuonyesha
Kibatala: OBJECTION aende Straight kwenye Re examination, anajua kuwa hairuhusiwi na ni...
Jaji: Wakili wa Serikali Unasemaje
Wakili wa Serikali: Sawa
Wakili wa Serikali: kwanini Kwenye Statement yako uliyotoa Polisi haina Maelezo uliyoyatoa Jana Mahakamani
Shahidi: Kwa sababu Jana ilikuwa naeleza kwa urefu Nilichoandika kwenye Statement yangu polisi.
Wakili wa Serikali: NitaKukabidhi sasa hii Karatasi ufafanue
Shahidi: hapa Nimeona Nimeeleza Kuhusu Kilimo, Nilikuwa nalima Viazi na Karoti. Jambo Lingine ni Mwandishi amekosea Mwaka nilioacha kazi kwa Sabaya. Ambaye Mheshimiwa alinitambulisha kuwa ni Kiongozi wa Ulinzi Kanda ya kaskazini.
Jaji: hapo sasa Mnafanya nini Wakili wa Serikali
Shahidi: anafafanua kilichopo
Jaji: afafanue Sasa
Wakili wa Serikali: Sawa
Shahidi: Swala lingine nilimtaja yule Diwani
Wakili wa Serikali: Kwenye Ushahidi wako ulitaja Diwani wa wapi ?
Shahidi: Diwani wa Kiboboroni
Mallya: OBJECTION hiyo ni fact Mpya kuhusu ni Kiongozi wa ulinzi Kanda ya kaskazini
Jaji: Mimi nilirekodi hivyo
Mallya: kama Mahakama ili Rekodi sina tatizo
Wakili wa Serikali: Kuhusiana na huyo Diwani ulisema nini?
Shahidi: Sikutaja Jina la Diwani
Wakili wa Serikali: sasa Uliambia Mahakama Huyo anaitwa nani
Kibatala: Sasa Ndiyo tunafanya nini, Shahidi ameshasema hakutaja Jina, yeye anataka Shahidi ajibu nini cha ziada.
Jaji: Ngoja tuone swali lake Maana hata Mimi nimerekodi kuwa Hakutaja Jina la Diwani
Wakili wa Serikali: Tueleze kuhusu Majina na Maeneo uliyoyatoa Jana hukutaja.? Shahidi: Sikutaja
Wakili wa Serikali: Tueleze sasa kwanini sasa Katika Maelezo yako Polisi hukutaja na Jana hukataja
Shahidi: Nilichofanya nilifanya ufafanuzi kwa kutaja hayo Majina niliyomtajia Mheshimiwa Mbowe bowe ..wakawa wananichanganya baadae nikakumbuka.
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kuhusu Kukutana na Bwana Mbowe Ukasema ni Mwanzoni mwa October 2020 longido na Baadae Ukasema ni October 2018 fafanunua Mkanganyiko huo
Shahidi: kwa sababu Mawakili wa Upande wa Utetezi walikuwa wananiuliza kwa njia Isiyo sahihi...
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Naomba nimkaribishe Mwenzangu
Wakili wa Serikali Robert Kidando anasimama
Wakili wa Serikali: kuna swali Uliulizwa na Wakili Kibatala Kwamba Mbowe alikuwa wapi kuanzia November 2019 Mpaka January 2020 Ukasema hufahamu hebu tuambieShahidi: Ninachofahamu yeye alinitafuta akiwa na Mikutano ya Jimbo
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Kuhusu Vikao kama Vilikuwa Vya kigaidi Ukasema Hapana Sasa hoja ilikuwa ni nini
Shahidi: Hoja ilikuwa ni Kuomba Majina ya wale Vijana wanaotembea na Sabaya na Namba zao za Simu
Wakili wa Serikali: Ukaulizwa na Wakili Kibatala Kwamba, Kama ulikuwa na hofu ya kiuhalifu Ukasema Hapana hebu fafanua
Shahidi: nilipata hofu kwa sababu Yeye alikuwa Mbunge na Sabaya alikuwa Mkuu wa Wilaya, nikajiuliza kwanini asitafuti kwa Kiongozi Mwenzie
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusu Kule Longido baada ya Kumtafuta Sabaya ukampigia Mbunge na Hukuriport hata Polisi
Shahidi: ni Kwa sababu nilihisi wote ni Viongozi na atamwambia mwenzie nikawa nimeshafikisha ujumbe
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kwamba Neno Bwire ni Msiri na Mlinzi wa mbowe, Elezea Sasa Kule Polisi Ulimtaja kwa namna gani?
Shahidi: Nilitaja kuwa alikuwa na Mlinzi, hapa nikajakutoa ufafanuzi
Wakili wa Serikali: Hebu fafanua kuhusu Biashara yako na mount meru ilikuwa je hukuleta nyaraka za Malipo hapa Mahakamani
Shahidi: Kwa sababu nilikwepo Muda mrefu Gerezani na Nyaraka hizo ni za Muda Mrefu
Wakili wa Serikali: Uliulizwa Kama Ulileta Nyaraka za Mount Meru Ukasema hujaileta, kwa sababu Ulifanya na mtu wao hebu tufafanulie
Shahidi: ni Kwa sababu Kuna watu wanakuja kwa wakulima kwa ajili ya Kupeleka Mazao Mount meru.
Wakili wa Serikali: Uliulizwa kuhusiana kutotaja watu wa Sabaya Pale Polisi
Shahidi: niliulizwa Majina ya watu hao hapa Mahakamani, Hapo kwenye maelezo Siku ya orodhesha
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kuhusiana na Jina Power Kaaya kwamba linatokana na Matendo ya Kihalifu, tufafanulie kwanini unaitwa Power Kaaya
Shahidi: ni Jina langu Ndiyo Maana naitwa Power Kaaya hata kwenye Charge Sheet lipo, tangu kwenye ubatizo niliitwa Power
Wakili wa Serikali: Uliulizwa swali kwamba Ulipewa Laki 2 ndiyo Maana Hukutoa Taarifa polisi
Shahidi: OBJECTION, Sikuwa nimesema Kitu hicho
Jaji: Hata Mimi Siku Rekodi Jambo hilo
Wakili wa Serikali: Kuhusiana na namba hiyo kwenye Statement hukasema siyo Namba yako, kwanini sasa unasema siyo Namba yako
Shahidi: Sijui Sasa Mwandishi aliyeandika
Wakili wa Serikali: Na Ukaulizwa kuhusiana namba zako mbili za Simu na Ukaulizwa kama Ulileta Uthibitisho Mahakamani, elezea Sasa kwanini unasema namba hizo ni zako
Shahidi: kwa sababu Namba hizo ndiyo nazitumia
Wakili wa Serikali: Umeulizwa Swali Kwamba Katika Dhamana ya Mbowe kuwa aliwahi kufutiwa Dhamana, je Ni kitu gani walichokuonyesha kuwa walikuwa na Kesi na ikafutwa Dhamana
Shahidi: Hawajanionyesha Kitu chochote
Wakili wa Serikali: Umeulizwa kuhusiana uhalifu wa Sylvester Nyegu na Ole Sabaya Ukasema Ufahamu, elezea kwanini ufahamu
Shahidi: Kwa sababu wakati wanakamatwa Mimi nilikuwa Gerezani
Wakili wa Serikali: Shahidi Mwingine tuliyekuwa tumemuita hajafika, hivyo tunaomba Hairisho hadi Kesho tarehe 29 Mwezi wa 10 ilituweze kuendelea na Shahidi Mwingine
Jaji: Shahidi Tunashukuru kwa Ushahidi wako, una eza kwenda sasa
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji huyo ndiyo Shahidi tuliyekuwa naye kwa Leo
Jaji: Shauri linahairishwa mpka Kesho saa 3 Asubuhi