Husika na kichwa cha habari hapo juu...
habari za jioni mabibi na mabwana, natumai kuwa mu wazima wa afya kabisa!
kama kichwa cha habari kinavyojieleza, naombeni kupewa knowledge hasa juu ya huyu kiumbe (sijui ni kiumbe ama ni roho? kiukweli sijui).
The so called jini mahaba, ni kiumbe wa aina gani? inakuwaje mpaka anamuingia binadamu na kuwa na mahusiano nae mpaka kuzaa nae na kujenga maisha?
kwanini jini mahaba akishamuingia mwanaume, basi mwanaume inakuwa ni vigumu sana kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mwanamke yeyote yule ama kutelekeza familia kabisa?
Hawa viumbe wanapendelea kuishi mazingira ya aina gani? wanapenda nini kiujumla na hawapendi nini katika maisha yao?
wakuu, naombeni tuelezane kila kitu kuhusiana na majini mahaba, kiukweli kuna kitu cha msingi sana nataka kufahamu kutoka kwenu, nimepitia maandiko mengi mtandaoni, lakini nimeona si mbaya kama tukijadili na hapa!
Mkuu Excel,
Sisi binadamu tuna sehemu kuu mbili, mwili na roho!. (physical body na spiritual body). Mwili ni hili umbo lililojengwa kwa udongo, na roho ni nafsi, uhai, iliyopuliziwa na Mungu. Mwili ulioumbwa kwa udongo, umetiwa uhai na nafsi, roho hivyo kuwa viumbe hai. Siku roho ikitoka (kufa) nafsi inaacha mwili na kuondoka zake, mwili ambao ni udongo, ni mavumbi, unazikwa unarudi mavumbini, na roho, inakwenda kwenye ulimwengu wa roho.
Dunia au ulimwengu nao unazo sehemu kuu mbili, ulimwengu wa miili, physical world na ulimwengu wa roho, the spiritual world. Ulimwengu wa milli ndio hii dunia tunayoishi yenye vitu viavyoonekana, na ulimwengu wa roho ni vile visivyo onekana, roho, malaika, liroho, shetani, majini, mizimu, wanga, wachawi, majini, mapepo, mbinguni, peponi, motoni, jehanum, toharani, kwenye nguvu na mwanga na nguvu za giza etc!.
Wanaoishi kwenye ulimwengu wa mwili ndio sisi binadamu, wanaoishi kwenye ulimwengu wa roho ndio viumbe hao wengine niliowataja wakiwemo majini!.
Hao majini wako wa aina nyingi, wako majini ya bahati, wanaokuletea bahati, wako majini wa majanga wanaokuletea majanga, na wako majini mahaba wao shida yao ni mapenzi tuu, uwapende, wakupende!. Mambo yoyote yanayohusiana na majini, ni mambo ya "liroho", shetani, ni mambo ya kishetani!.
Jini mahaba ni shetani la mapenzi, likikupenda, litakupa kila kitu isipokuwa mwenza!, litakuwa linafanya mapenzi na wewe ya kijini jini, au ukiwa usingizini kama ndoto. Tatizo la jini mahaba, huwezi kuwa na mahusiano na mpenzi wa kawaida wa kibinaadamu na akitokea mtu akakupenda, yatamkuta ya kumkuta!.
Majini yananunuliwa hadi e-bay.
Kitu kimoja amacho siku zote akisemwi kwenye mahusiano kati ya binadamu na majini, ni kitu kinachoitwa "bondage!", unakuwa ni mtumwa wa hilo jini na chochote litakachohitaji kutoka kwako lazima lipate!, litaanza na kuzitaka roho za wapendwa wako, wazazi, mke, watoto na mwisho wa siku ni roho yako mwenyewe!.
Haya ni mambo ya kishetani na mwisho wake siku zote ni kule kwenye jehenum ya moto wa milele.
Mambo yoyote ya ulimwengu wa giza, ni mambo ya kujiepusha nayo.
Pasco