Hakuna anayesema wahusika wasingefaidika na jasho lao, hell no! Ninachosema ni wahusika kufaidika zaidi kuliko wasanii wenyewe! Nimetoa mfano wa show ambayo ilifanyika pale Billz... nikikutajia ambacho walilipwa majority ya wale washikaji unaweza kusema "am making it up!"
Na hoja hapa ni kwamba, hata kama na wenyewe wanatakiwa kula kutokana na jasho lao (coz' no free lunch as you said) lakini sio kula kwa staili ya simulizi ya ng'ombe wanaokamuliwa bila kupewa malisho!! Kabla TMK Wanaume haijakufa, nitajie msanii mmoja tu ambae alikuwa na cha kuonesha mbali na Nature aliyekuwa na Benz ya Mtumba na nyumba Mbagala!!
Kwamba, Fella kafanya kitu positively, sidhani kama kuna anayeweza kukataa hili! Kwanza, kuwaweka Masela pamoja sio jambo dogo!! Lakini ukweli mchungu mwingine ni kwamba, wengi waliokuwa top pale TMK tayari walishakuwa hivyo hata kabla ya Fella! GWM kwa mfano, tangia enzi hizo tuko pale NASACO, Kurasini tayari GWM walikuwa wanafahamika na shoo zao za kibabe, kipindi hata Saidi Fella hajaenda South na kurudi Fella mwingine!
Hata Nature tayari alishakuwa stori mjini kwa sababu, kama kumbukumbu zangu zipo sawa, nadhani hata pini kama Kigheto gheto zilitoka wakati Fella ama kabla hajaenda SA au wakati yupo uko! Na kama sikosei, nadhani hata Chege alishakuwa ameshafahamika kupitia Manyema!!! Hata Mzimu ingawaje hakuwa TMK Cream na yeye tayari alishafahamika!
Wasanii ambao walianza kufahamika exclusively kupitia management ya Fella ni watu kama akina Y-Dash, YP, Kakaman, Mheshimiwa Temba, Doro, na wengine kadhaa! Ukitoa Mheshimiwa Temba, wote hawa walikuwa wanagongea hadi fegi!!!
Na kuhusu wengine could do even worse than Fella, sikatai na ndio maana hata hapa JF nimeshasema mara nyingi, Entertainment Industry (world wide) generally imejaa dhuluma lakini kuna dhuluma zingine zinakuwa too much!