Ya Said Fella, Ruge na washindwa....

Ya Said Fella, Ruge na washindwa....

Pitieni Pitieni na uzi aloandika lady Jay dee pia maana watu wanataka kuaminisha wengne kuamarehemu hakua na mapungufu pia. Kiukweli wanaolalamika ukichunguza kinawaumiza ni kwamba Mr ruge licha ya kuofautiana na mtu bado alikua anapambana kw njia nyingne kukata mrija wa ridhki ya wengne kwa vikwazo kupitia wadau wengine
We are living in a very cruel world ndugu yangu.... Its a battle of win or lose.. Survival of the fittest.... Kuna vita ya kibiashara haikwepeki popote.... Na Ili ushinde unahitaji hata mbinu chafu... Sometimes kuwakanyaga wengine migongoni mwao kama kipandio chako.. No free lunch....

Jr[emoji769]
 
Dudu baya kajipambanua kwa kuwa muwazi ila kuna wengi wanalia kama samaki machozi yanaenda na maji. Rubi na wengine wengi kutoka THT walishalalamika sana juu ya mawingu media. Unaweza ukaona bifu kati ya WCB. Jide wengine walioachwa kwenye fiesta kisa waligomea ujira mdogo. Yanayofanywa na clouds media wanayajua wasanii. Sie wasikilizaji tutege masikio na macho.

Sent using Jamii Forums mobile app

My brother,

Ruge wasn't doing some charity work. He was not a Red Cross messiah or something. Alikuwa anatafuta kama wengine. Ndo kitu wengi tunaongelea humu. The story is the same kuanzia Makinikia ya Barrick mpaka machinga na kitambulisho cha JPM. Au house girl nyumbani kwako au kwangu anayelipwa 50k!!! Au mfanyakazi wa Bakhresa anayepewa laki mbili na nusu ingawa boss wake ndo richest man in the country!! Hakuna anayefanya kazi ya madhabahu. Kila mtu anataka kuchomoza. And in the process lazima wengine waumie. It is a cruel world. Kumlaumu Ruge au Masanja kwa hilo tunawakosea.

Are you aware kwamba nesi wa mshahara wa laki mbili au tatu analipa kodi.. Mbunge na mafao yake ya mamilioni au namba moja mwenyewe halipi kodi? Where's our rage? Au kwa sababu na sisi we are part of that crime pattern? Kwa sababu na sisi tukipata hizo nafasi we will do the same!

My aunt served the country for 40 years kama nesi. Amestaafu, mafao hata 20M hayakufika! Where is our rage.

Hapa sijaribu kumtetea marehemu au wengineo. Point yangu tuangalie wider social and economic dynamics za mifumo yetu.

Mwisho wa siku kwenye hizi debates tunasahau ukweli kwamba ubepari ni unyama. Unfortunately we are all in the tent. Wakati tunawanyoshea vidole wengine.... Tusisahau na sisi tunategemea mifumo hiyo hiyo kuendesha maisha yetu.

Masanja
 
Ni sawa lkn huwa sipendi kuzarau upande wa pili huenda wapo wengi lkn wanajifunga midomo na kustahi..kwakuwa hayo ndio maisha yetu
 
The Man is Gone, may his Soul Rest Supposedly Respectively. Nenda Ruge
 
Mapangufu madogo yanatoweka haraka Sana mtu afapo

Lakini ikiwa mpaka sasa watu wanazumza fifty-fifty_Basi Kuna shida sehemu kwa marehemu na alipaswa abadilike

Ila yote kwa yote apumzike kwa amani

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu Mshana Jr!!

Baada ya kutoka nje ya Daslam, hatimae nikarejea! Kama kawaida yangu, siku ya pili tu nikatimba Kiumeni kuonana na wana!! Mkubwa Fella hakuwepo na kwahiyo Washikaji walikuwa huru sana kuongea chochote!! Kuna baadhi walidhani ningeweza kuwa mkombozi wao huku wakishindwa kufahamu nilianza kufahamiana na Fella kabla ya wote hao collectively, au hata kabla ya wenyewe kwa wenyewe hawajafahamiana!!

In short, nisingeweza kufanya jambo la kumkwaza mshikaji wa siku nyingi haidhuru hata kama kuna wakati aliwahi kuninunia kwa kudhani nawashika masikio mabwana mdogo, kwa sababu miongoni mwao kuna wengine walikuwa jeuri kwa Mkuu wao; na Mkuu wao akaamini hakuna mwingine zaidi ya huyu jamaa!!!

Wiki chache baadae ukafanyika uzinduzi wa albamu ambayo nimeisahau jina lake lakini kulikuwa na ngoma kama Twende Zetu, Chai, n.k! Sijui ilikuwaje show kubwa kama ile ifanyike Billz!

Yaliyotokea kwenye ile show, ndugu yangu ningekuomba usijimalize sana kuhusu Fella!! Ni kweli Fella aliwafanya wengi sana wafahamike but trust me, majority hakuna walichokuwa wanapata... I repeat, ukitoa wachache kama akina Nature, Temba na Chege, majority hakuna walichokuwa wanapata! Majority ya hawa kama sio wote nilikuwa nawafahamu vema (except Chege ambae hakuwa mtoto wa Temeke) na sio kuwafahamu kupitia tv!

Hata huyo Nature mwenyewe alichokuwa anakipata huwezi kulinganisha na jina lake wakati ule!!

Baada ya siku zangu za kuwa Daslam kukamilika, nikasepa zangu lakini nikawaambia washikaji kwamba TMK iki-survive kwa mwaka mmoja zaidi, basi sio mimi!! And of course, ilichukua less than 4 months kabla TMK haijasambaratika!

Hata hivyo, nadhani pale Kiumeni wapo waliokuwa wananufaika zaidi kuliko hata huyo Fella mwenyewe!!! Ujue Fella ni mjanja mjanja tu wa mjini sasa juu yake kukawa na wajanja wajanja wengine lakini wenye elimu!! Ninachotaka kusema ni kwamba, ukisikia mtu anamlalamikia Fella wala usimbishie!!!

Mimi mwenyewe nilishawahi kuzunguka kwenye radio stations zote kusambaza kazi za mmoja wa wana-TMK! Hii ilikuwa ni awamu nyingine ya kuwapo Daslam! Jambo ambalo nakumbuka hadi leo, tumefika pale Magic, jamaa wakaonekana hawana furaha kabisa na ujio wetu! Yaani wakati wanachukua CD walionekana wazi waliichukua kutoa lawama!!

Hadi siku zangu za kuwapo Daslam zinaisha, sikuwahi kusikia ngoma yoyote ikipigwa, ingawaje tulishapata taarifa kabla kwamba Mkubwa Fella alishapita kabla yetu kufanya fitina!!!! And trust me, narudia, trust me, linapokuja suala la fitina kwenye Bongo Flavor, ile namba kaa nayo mbali!!!! Huyo Ruge inawezekana alikuwa juu ya Fella kwa sababu yeye alikuwa na nyenzo!!!

Tukija kwa upande wa marehemu, lazima niseme wazi mimi nimekuwa mtetezi mkubwa wa Ruge hapa jamvini kwa sababu nafahamu mchango wake! Lakini kingine, wengi waliokuwa wanamlalamikia Ruge ni wale ambao walikuwa wanalalamika baada ya kuwa wamesha-drop!! Na wengine ulalamishi wao ulikuwa wa kijinga; unaoonesha walikuwa hawafahamu vizuri biashara kati yao na Clouds!

Lakini habari za Ruge hata Juma Nature mwenyewe anazifahamu! Mchizi akalazimika kuweka usela na ustaa pembeni na kwenda kupiga goti kwa Ruge! Hapa nazungumzia enzi hata akina Diamond hawafahamiki!!!
 
Huyu sio yule aliyejitoa fiesta baada ya kusaini mkataba. Let's make this way... Unapewa mkataba unaosoma unaridhia pasi kulazimishwa na mtu unasaini. Unaenda Insta unapiga vigeregere yereeeeewi can't wait to be up on the stage. Halafu siku ya pili unaamka zako eti unajitoa na kuanza kelele eti mkataba wakinyonyaji. Tuiteje hii?!
Kuwaza kwa kutumia makalio.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
My brother,

Ruge wasn't doing some charity work. He was not a Red Cross messiah or something. Alikuwa anatafuta kama wengine. Ndo kitu wengi tunaongelea humu. The story is the same kuanzia Makinikia ya Barrick mpaka machinga na kitambulisho cha JPM. Au house girl nyumbani kwako au kwangu anayelipwa 50k!!! Au mfanyakazi wa Bakhresa anayepewa laki mbili na nusu ingawa boss wake ndo richest man in the country!! Hakuna anayefanya kazi ya madhabahu. Kila mtu anataka kuchomoza. And in the process lazima wengine waumie. It is a cruel world. Kumlaumu Ruge au Masanja kwa hilo tunawakosea.

Are you aware kwamba nesi wa mshahara wa laki mbili au tatu analipa kodi.. Mbunge na mafao yake ya mamilioni au namba moja mwenyewe halipi kodi? Where's our rage? Au kwa sababu na sisi we are part of that crime pattern? Kwa sababu na sisi tukipata hizo nafasi we will do the same!

My aunt served the country for 40 years kama nesi. Amestaafu, mafao hata 20M hayakufika! Where is our rage.

Hapa sijaribu kumtetea marehemu au wengineo. Point yangu tuangalie wider social and economic dynamics za mifumo yetu.

Mwisho wa siku kwenye hizi debates tunasahau ukweli kwamba ubepari ni unyama. Unfortunately we are all in the tent. Wakati tunawanyoshea vidole wengine.... Tusisahau na sisi tunategemea mifumo hiyo hiyo kuendesha maisha yetu.

Masanja
What a reply... Thinking great way.... [emoji123][emoji123][emoji123][emoji123][emoji123][emoji123][emoji123]

Jr[emoji769]
 
Nchi ya wanafiki hii


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom