Jidu La Mabambasi
JF-Expert Member
- Oct 20, 2014
- 17,547
- 28,493
Katika miaka ya karibuni , wizara hii ya Ujenzi imekuwa kichwa cha mwenda wazimu.
Kila anyejifunza kunyoa anapelekwa hapo, na nywele anajua anakozipeleka.
Siyo siri ,sasa Wizara , taasisi zake kama TANROADS, ni mufilisi.
Wadau wa ujenzi wanaikimbia wizara ya Ujenzi.
Yote tisa, kumi ni hii habari ya kutengwa Tshs milioni 10 kwa Wanafunzi wa chuo kikuu kutoa wazo la kumaliza foleni Dar!!!
Wizara Ina wahandisi waliobobea katika fani ya barabara, Kuna makampuni ya kihandisi kufanya feasibility studies za Traffic na Highway Engineering na Design.
Kwa watu wabobezi katika fani tungeweza kusema Waziri Ulega amekula maharage ya wapi?