Dr Lizzy
Platinum Member
- May 25, 2009
- 30,821
- 59,422
WIVU!!
Wivu uko kila mahali...kwenye mapenzi...kati ya marafiki...kati ya wafanyakazi na wanafunzi wenza...ndugu na hata maadui.
''Wivu ni kidonda ukizidisha utakonda.'' Ndivyo tulivyokua tukiambiana wakati tunakua...na huo ndio ukweli wenyewe.Maana kama vitu vingine vingi wivu ni mzuri ila ukizidi kipimo unageuka sumu.
Kwenye mapenzi: Wivu kati ya wawili ndani ya mahusiano unaweza kua kirutubisho au chachu ya mapenzi.Ukionyesha kwa kiasi utamfanya mwenzi wako ahisi kwamba unampenda na kumjali...sisemi kwamba ni kitu pekee kinachofanya hivyo bali ni kichocheo kizuri iwapo hakitazidishwa na kusababisha kero.Wivu unapozidi unaonyesha mapungufu yako kanakwamba hujiamini kitu ambacho kinaweza kupelekea mwenzako nae ahisi kwamba HUMUAMINI.
Kati ya wanafunzi/wafanyakazi: Unapomuonea wivu mwenzako kwa maendeleo yako ikiwa utaupangilia vizuri itakusukuma wewe kujitahidi kufika alipo yeye au hata zaidi.Ila ukikosea tu ukazidisha kiasi itasababisha chuki dhidi ya mwenzako huyo.Na kama mnavyojua chuki ni sumu.....sumu inayomuumiza aliyenayo na sio anayepelekewa hiyo chuki.Ukiwa na chuki utaishia kuchukia maendeleo ya mwenzako badala ya kujiboresha wewe hivyo hautafaidika.
Wivu kati ya ndugu na marafiki: Kwanza jiulize kwanini umuonee wivu ndugu au rafiki yako??Kwanini usifurahie mafanikio yake huku ukijaribu kufikia pale alipo yeye???Katika watu ambao unatakiwa ujitahidi kutowaonea wivu ni ndugu au rafiki wa karibu....maana ukizidi unaweza kuzaa chuki.Ikiwa unawaonea utumie kama msukumo wa kuelekea kwenye ubora badala ya kuonyesha udhaifu wako na kupelekea kumchukia mwenzako kwa kua na kitu ambacho huna.
Wivu dhidi ya adui: Jua kabisa kama humpendi mtu tayari kitendo cha kumuonea wivu kitakuumiza zaidi wewe binafsi zaidi ya kukusaidia.Japo ukiweza kuuendesha wivu wako badala ya wivu kukuendesha unaweza ukafaidika!
Kwahiyo wivu ni mzuri maana huleta maendeleo na hudumisha mapenzi pale unapotumiwa vizuri.....ila wivu huo huo huweza kugeuka kero au kuzaa chuki ambayo matokeo yake yaweza kua ufitini..umbea..kutojiridhisha/kutojitosheleza...na hata kufikia hatua ya kuumizana.
Hivyo basi....usiache kumuonyesha mpenzi wako wivu angalau kidogo wala usiache kuwa na wivu wa maendeleo....hayo mengine achana nayo maana maisha mafupi haya usitumie muda wako kuchukia na kuharibu....utumie kukunufaisha wewe na uwapendao.
Nawatakia jumatatu na wiki njema kwa ujumla.
Wivu uko kila mahali...kwenye mapenzi...kati ya marafiki...kati ya wafanyakazi na wanafunzi wenza...ndugu na hata maadui.
''Wivu ni kidonda ukizidisha utakonda.'' Ndivyo tulivyokua tukiambiana wakati tunakua...na huo ndio ukweli wenyewe.Maana kama vitu vingine vingi wivu ni mzuri ila ukizidi kipimo unageuka sumu.
Kwenye mapenzi: Wivu kati ya wawili ndani ya mahusiano unaweza kua kirutubisho au chachu ya mapenzi.Ukionyesha kwa kiasi utamfanya mwenzi wako ahisi kwamba unampenda na kumjali...sisemi kwamba ni kitu pekee kinachofanya hivyo bali ni kichocheo kizuri iwapo hakitazidishwa na kusababisha kero.Wivu unapozidi unaonyesha mapungufu yako kanakwamba hujiamini kitu ambacho kinaweza kupelekea mwenzako nae ahisi kwamba HUMUAMINI.
Kati ya wanafunzi/wafanyakazi: Unapomuonea wivu mwenzako kwa maendeleo yako ikiwa utaupangilia vizuri itakusukuma wewe kujitahidi kufika alipo yeye au hata zaidi.Ila ukikosea tu ukazidisha kiasi itasababisha chuki dhidi ya mwenzako huyo.Na kama mnavyojua chuki ni sumu.....sumu inayomuumiza aliyenayo na sio anayepelekewa hiyo chuki.Ukiwa na chuki utaishia kuchukia maendeleo ya mwenzako badala ya kujiboresha wewe hivyo hautafaidika.
Wivu kati ya ndugu na marafiki: Kwanza jiulize kwanini umuonee wivu ndugu au rafiki yako??Kwanini usifurahie mafanikio yake huku ukijaribu kufikia pale alipo yeye???Katika watu ambao unatakiwa ujitahidi kutowaonea wivu ni ndugu au rafiki wa karibu....maana ukizidi unaweza kuzaa chuki.Ikiwa unawaonea utumie kama msukumo wa kuelekea kwenye ubora badala ya kuonyesha udhaifu wako na kupelekea kumchukia mwenzako kwa kua na kitu ambacho huna.
Wivu dhidi ya adui: Jua kabisa kama humpendi mtu tayari kitendo cha kumuonea wivu kitakuumiza zaidi wewe binafsi zaidi ya kukusaidia.Japo ukiweza kuuendesha wivu wako badala ya wivu kukuendesha unaweza ukafaidika!
Kwahiyo wivu ni mzuri maana huleta maendeleo na hudumisha mapenzi pale unapotumiwa vizuri.....ila wivu huo huo huweza kugeuka kero au kuzaa chuki ambayo matokeo yake yaweza kua ufitini..umbea..kutojiridhisha/kutojitosheleza...na hata kufikia hatua ya kuumizana.
Hivyo basi....usiache kumuonyesha mpenzi wako wivu angalau kidogo wala usiache kuwa na wivu wa maendeleo....hayo mengine achana nayo maana maisha mafupi haya usitumie muda wako kuchukia na kuharibu....utumie kukunufaisha wewe na uwapendao.
Nawatakia jumatatu na wiki njema kwa ujumla.