Wivu!!

Wivu ni kidonda ukishiriki utakondaa
kuna wimbo tulivyokuwa watoto tulikuwa tunaimba :lol::lol::lol::lol:
 
Mimi naona siku zote WIVU sio mzuri.. Unaweza chukiwa bure, eti kwa saabu umemshinda rafiki yako class! au umependeza siku ya sikukuu, au kwenu kuna video (Enzi za Mwalimu)

Naona mzee DC ameshakujibu.Wivu mbaya ni ule unaokusukuma kufanya mambo ya ajabu!Unaojenga ruksa!
 
Hii Riwaya ni nzuri sana na ina mfunzo
Asante sana Lizzy kwa hii useful sread

Asante na karibu mama wa kwanza!Ngoja niitafute nijikumbushe maana nahisi kama nimewahi kuisoma sema siikumbuki!
 
Lizzy,

Mtu wa namna hiyo ni looser...Ameshakubali kwaba hawezi kufanya lolote la maana na kwa hiyo anaishia kucheza na mdomo..umbeya mtupu. Shida yetu Watanzania ni kwamba kuna watu wanapenda hizo hadithi za kishenzi na ndio maana watu wanaosema hovyo namna hiyo wanayo hadhira ya kutosha!
Hehehe unadhani wataacha kufurahia?Imagine wa2 wa3 wenye chuki na mtu mmoja au kundi la watu..kusikia kila mmoja akiongelea vibaya kuhusu wanaemchukia itafanya siku yao nzuri
 
Hehehe unadhani wataacha kufurahia?Imagine wa2 wa3 wenye chuki na mtu mmoja au kundi la watu..kusikia kila mmoja akiongelea vibaya kuhusu wanaemchukia itafanya siku yao nzuri

LIzzy,

Binafsi hapo ndipo ninapopataka!! Yaani dakika moja wanayotumia kunizumngumza mimi naitumia kutegeneza mwafweza...Kwa hiyo kesho yake itabid waongeze dakika zaidi ili kumaliza yote wanayotaka kuongea...Mwisho wa siku mimi nasonga mbele.

Halafu watu kama hao pia wanamsaidia mtu asifanye makosa katika mambo yake kwa kuwa anaamini kuna wachawi fulani wanafuatilia nyendo zake. Ndo maana wakenya wanatupenda sana kwa kuzungusha domo na kutenda less! Bila kubadilika tutaishia kukaaa vijiweni na kusifia gari/nyumba za wenzetu!
 
WIVU!!
Wivu uko kila mahali...kwenye mapenzi...kati ya marafiki...kati ya wafanyakazi na wanafunzi wenza...ndugu na hata maadui.

''Wivu ni kidonda ukizidisha utakonda.'' Ndivyo tulivyokua tukiambiana wakati tunakua...na huo ndio ukweli wenyewe.Maana kama vitu vingine vingi wivu ni mzuri ila ukizidi kipimo unageuka sumu.

Kwenye mapenzi: Wivu kati ya wawili ndani ya mahusiano unaweza kua kirutubisho au chachu ya mapenzi.Ukionyesha kwa kiasi utamfanya mwenzi wako ahisi kwamba unampenda na kumjali...sisemi kwamba ni kitu pekee kinachofanya hivyo bali ni kichocheo kizuri iwapo hakitazidishwa na kusababisha kero.Wivu unapozidi unaonyesha mapungufu yako kanakwamba hujiamini kitu ambacho kinaweza kupelekea mwenzako nae ahisi kwamba HUMUAMINI.

Kati ya wanafunzi/wafanyakazi: Unapomuonea wivu mwenzako kwa maendeleo yako ikiwa utaupangilia vizuri itakusukuma wewe kujitahidi kufika alipo yeye au hata zaidi.Ila ukikosea tu ukazidisha kiasi itasababisha chuki dhidi ya mwenzako huyo.Na kama mnavyojua chuki ni sumu.....sumu inayomuumiza aliyenayo na sio anayepelekewa hiyo chuki.Ukiwa na chuki utaishia kuchukia maendeleo ya mwenzako badala ya kujiboresha wewe hivyo hautafaidika.

Wivu kati ya ndugu na marafiki: Kwanza jiulize kwanini umuonee wivu ndugu au rafiki yako??Kwanini usifurahie mafanikio yake huku ukijaribu kufikia pale alipo yeye???Katika watu ambao unatakiwa ujitahidi kutowaonea wivu ni ndugu au rafiki wa karibu....maana ukizidi unaweza kuzaa chuki.Ikiwa unawaonea utumie kama msukumo wa kuelekea kwenye ubora badala ya kuonyesha udhaifu wako na kupelekea kumchukia mwenzako kwa kua na kitu ambacho huna.

Wivu dhidi ya adui: Jua kabisa kama humpendi mtu tayari kitendo cha kumuonea wivu kitakuumiza zaidi wewe binafsi zaidi ya kukusaidia.Japo ukiweza kuuendesha wivu wako badala ya wivu kukuendesha unaweza ukafaidika!

Kwahiyo wivu ni mzuri maana huleta maendeleo na hudumisha mapenzi pale unapotumiwa vizuri.....ila wivu huo huo huweza kugeuka kero au kuzaa chuki ambayo matokeo yake yaweza kua ufitini..umbea..kutojiridhisha/kutojitosheleza...na hata kufikia hatua ya kuumizana.

Hivyo basi....usiache kumuonyesha mpenzi wako wivu angalau kidogo wala usiache kuwa na wivu wa maendeleo....hayo mengine achana nayo maana maisha mafupi haya usitumie muda wako kuchukia na kuharibu....utumie kukunufaisha wewe na uwapendao.

Nawatakia jumatatu na wiki njema kwa ujumla.
Last edited by Lizzy; Today at 01:35 AM. Reason: napendezesha!

Huwezi amini, pamoja na maelezo yoooooooooooote hayo, mi nimepapenda zaidi hapo kwenye red.

:focus:
Ila sometimes kuridhika nako kunasaidia kuondokana na wivu usio wa lazima.
Utakuta mtu anaona wivu mwenzake kuwa mfanyakazi bora kazin, huku tukifahamu ufanyakazi bora hautafutwi wala hausomewi darasani.
Mtu anaona wivu mwenzake kushinda bahati nasibu fulani huku ikifahamika hiyo zawadi pia haitafutwi.
 
Mzee unayosema ni kweli tupu!Sawa na wazungu wanavyotuona...maneno mengi matendo zero.Watu wanajirudisha nyuma wenyewe...ikitokea siku watu wakaacha kupiga domo na kuhangaika na mambo yao kila mtu ataendelea kwa kiasi chake.Ila ndo hivyo tena wapo na watazidi kuwepo ili wanaojitahiti waongeze bidii.
 
Dah! Mi niliwahi kushikwa na wivu mkali nilipokuwa O level, kuna dogo huyo A zote alikuwa anapata yeye. Hata kutuachia na wenzie!
Advance tukachaguliwa tena shule moja, uzuri yeye alichagua kombi tofauti na yangu. Nilishukuru kweli maana dogo alizidi!!!
Miakili kama kachanjiwa....Hahaha!
 
Back
Top Bottom