Will the real Paul Makonda please stand up?

Will the real Paul Makonda please stand up?

Nyani ngabu assume ww ndio huyo Paulo makonda wanaedai vyeti vyake vinatumika na mtu mwingine, ungejitokeza hadharani ukizingatia uhalisia wa viongozi wa nchi za dunia ya tatu?
 
Hahaa Ngabu umenichekesha

tuendelee na mjadala

Sijasema unamsingizia...na binafsi naamini hana hivyo vyeti

Nninachokiona kwako kwa kuwa unaamini Gwajima ni mzushi na tapeli

kitu ambacho binafsi naweza kabisa kukubaliana na wewe.....
unataka kwa sababu hiyo
huyu Paul Makonda apewe benefits of the doubt au aachwe kuandamwa na tuhuma


Mimi ninachokipinga ni mtu kusema hizi tuhuma hazina maana ni uzushi simply sababu Gwajima
ndie front man wa hizi tuhuma.....

Ninachopingana na wewe ni kitu kimoja tu

wewe unataka Gwajima athibitishe

Mimi nataka Makonda himself ndo ajibu hizi tuhuma

kwangu Gwajima ni irrelevant kwenye tuhuma hizi....

point yangu ya wewe na Gwajima kuwa personal iko based na thread ulizomuanzishia kumkejeli
ikiwemo moja ya leo...

Ok, sawa tuendelee.

Nianze na suala la Gwajima.

Hakuna kitu kilicho personal. Simjui na hanijui kabisa. Na kusema ukweli nimemjulia humu humu JF kipindi kile cha Dkt. Slaa kuondoka CHADEMA. Hizo kejeli ziko based na kile ninachokijua juu yake hususan maneno yake mwenyewe...sikuamini masikio yangu alivyomtukana kadinali Pengo.

Na nadhani umenisoma vibaya. Mimi si dismiss kabisa tuhuma dhidi ya Makonda.

Lakini nachosema ni kwamba, kama Makonda mwenyewe anasuasua kuzijibu hizo tuhuma kwa nini basi [1] wasimburute mahakamani ambako huko atalazimishwa kuzijibu na [2] kwa nini yeye huyo Gwajima asitusaidie kwa kutuonyesha huo ushahidi aliosema anao?

Now tell me Bossman, what is so unreasonable about that?

All I want is to get to the bottom of it, one way or the other.
 
Ok, sawa tuendelee.

Nianze na suala la Gwajima.

Hakuna kitu kilicho personal. Simjui na hanijui kabisa. Na kusema ukweli nimemjulia humu humu JF kipindi kile cha Dkt. Slaa kuondoka CHADEMA. Hizo kejeli ziko based na kile ninachokijua juu yake hususan maneno yake mwenyewe...sikuamini masikio yangu alivyomtukana kadinali Pengo.

Na nadhani umenisoma vibaya. Mimi si dismiss kabisa tuhuma dhidi ya Makonda.

Lakini nachosema ni kwamba, kama Makonda mwenyewe anasuasua kuzijibu hizo tuhuma kwa nini basi [1] wasimburute mahakamani ambako huko atalazimishwa kuzijibu na [2] kwa nini yeye huyo Gwajima asitusaidie kwa kutuonyesha huo ushahidi aliosema anao?

Now tell me Bossman, what is so unreasonable about that?

All I want is to get to the bottom of it, one way or the other.


Kama unakubali kumburuta mahakamani ni second or third option sina shida
mradi tukubaliane kuna option ya kwanza ambayo ni yeye Makonda kuja clean
au ya serikali kutoa tamko na msimamo wa serikali....na kutueleza ukweli ni upi..

Binafsi naona Gwajima ni very very irrelevant kwenye hii issue ....
Wapo waliosema vyuo alivyosoma ndo vijitokeze na kuonesha vyeti alivyo wasilisha
naonna hiyo ni better option...

Lakini kwa nini yeye hajibu au kulazimishwa kujibu? hilo tu huoni kuwa ni ishara ya ukweli wa tuhuma?
Au kwa nini Magufuli yuko quick kufukuza na kutolea matamko mambo mbalimbali lakini hili yuko kiimya?
 
Kama unakubali kumburuta mahakamani ni second or third option sina shida
mradi tukubaliane kuna option ya kwanza ambayo ni yeye Makonda kuja clean
au ya serikali kutoa tamko na msimamo wa serikali....na kutueleza ukweli ni upi..

Ni kweli. Yeye Makonda ndo anaweza kufunga huu mjadala. Hilo siwezi kabisa kukataa.

Binafsi naona Gwajima ni very very irrelevant kwenye hii issue ....
Wapo waliosema vyuo alivyosoma ndo vijitokeze na kuonesha vyeti alivyo wasilisha
naonna hiyo ni better option...

Kwangu ni very relevant maana kasema anao ushahidi wa kilicho kiini katika tuhuma nzima.

Kwa sababu hiyo naamini he can do us all a big favor kwa kutuonyesha huo ushahidi alonao.

Kukiwa na kesi mahakamani yeye ndo atakuwa ni mmoja wa key witnesses. Naamini hivyo ingawa mimi siyo kaka msomi.

Lakini kwa nini yeye hajibu au kulazimishwa kujibu? hilo tu huoni kuwa ni ishara ya ukweli wa tuhuma?
Au kwa nini Magufuli yuko quick kufukuza na kutolea matamko mambo mbalimbali lakini hili yuko kiimya?

Hilo la yeye na Magufuli wake kuwa kimya hakika linatia shaka. Hapo napo siwezi kukataa.
 
Ni kweli. Yeye Makonda ndo anaweza kufunga huu mjadala. Hilo siwezi kabisa kukataa.



Kwangu ni very relevant maana kasema anao ushahidi wa kilicho kiini katika tuhuma nzima.

Kwa sababu hiyo naamini he can do us all a big favor kwa kutuonyesha huo ushahidi alonao.

Kukiwa na kesi mahakamani yeye ndo atakuwa ni mmoja wa key witnesses. Naamini hivyo ingawa mimi siyo kaka msomi.



Hilo la yeye na Magufuli wake kuwa kimya hakika linatia shaka. Hapo napo siwezi kukataa.


Na hili la watuhumiwa wa madawa kumnunulia magari je umelisikia?
umelionaje? hadi card za magari zimewekwa online
na picha akitumia hayo magari pia
 
In the interest of full disclosure, mimi sijui chochote kile cha ziada kuhusu hili sakata la vyeti vya mkuu wa mkoa wa Dar zaidi ya hiki ninachokisoma kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vinginevyo vya habari.

Lakini nikiwa mtu mwenye akili zangu timamu [well, naamini wapo wataobisha kuwa nina akili timamu, it's all good] nina maswali mepesi sana lakini ambayo naona kama vile hayana majibu kamili ya kueleweka.

Nimeshahoji juu ya uwezekano wa Makonda kufunguliwa mashitaka kwa manufaa ya umma. Hilo nimesikia kuna mtu au watu wanaolifanyia kazi.

Gwajima na Makonda wao naona wamegoma kabisa kutuonyesha vyeti walivyo navyo. Oh well...fine.

Sasa nije kwa huyo Paul Makonda halisi. Yaani Paul Makonda mwenyewe aliyeibiwa au aliyeuza [allegedly] huo utambulisho wake kwa Daudi Bashite.

Yeye huyo mtu yuko wapi?

Sasa hivi anatumia jina gani?

Anafanya shughuli gani?

Hivi huyo mtu hana ndugu, jamaa, na marafiki ambao wanaweza kutupa walau usuli [background] kidogo wa huyo mtu?

Naamini huyo Paul Makonda halisi haishi kwenye ombwe. Naamini anaishi miongoni mwa jamii.

Sasa kweli hao watu anaoishi nao na kukutana nao hakuna hata mmoja wao aliyejitokeza mpaka hivi sasa kusema lolote?

I'm getting so sick of this bullshit.

So will the real Paul Makonda please stand up...?

I repeat, will the real Paul Makonda please stand up...?
Tatizo lako mkuu una haraka mno. Mambo ya koromije huwa yanaenda polepole. Ukweli utajulikana tu na kuna mtu atakuja kuaibika hasa. Kila kitu kipo na nyaraka zote zipo na wahusika wote wapo.
 
Well, hata akili ya kawaida inahoji pia kuwa ni kweli huyo mtu yupo au hayupo?
Kaka, hakuna Paul Makonda halisi au feki....

Hapa kilichoibiwa na majina ya mwanzo...Paulo Christian Muyenge.
Huyo Muyenge ndio halisi sasa, ila Daud Albet Bashite, aliapa mahakamani, kuondoa Muyenge...iwe Makonda.

Pia posibility zilizopo (sina hakika), huu mkataba wa kuuziana cheti, ulifanywa baina ya Albert na Dada wa Paul Christian Muyenge.

So, yawezekana hata Paul halisi, kajua kipindi hiki kuwa cheti changu kiliwahi kutumika, na wakamuwahi kumzima.

Ila huyu Muyenge inasemekana yuko Tabora
 
Na hili la watuhumiwa wa madawa kumnunulia magari je umelisikia?
umelionaje? hadi card za magari zimewekwa online
na picha akitumia hayo magari pia

Yeah, hilo nalo nimeliona.

Ila sina taarifa za kutosha kuweza kulitolea maoni kikamilifu maana sasa hivi kuna hali ya chuki na visasi na kila aina ya mazagazaga.

Inahitaji utulivu wa akili kidogo na si kukurupuka tu.

Ila nakubali kuwa vitu havijakaa sawa kabisa na huyo bwana.

Anaonekana ana utoto utoto mwingine na ulimbukeni na hana kabisa busara.

Anaonekana ni mtu wa kujipendekeza sana.

Rejea tu jinsi yeye na Magufuli walivyomtendea yule mkurugenzi wa jiji Bw. Kabwe ile mwaka jana.

That was so beneath the offices they hold.
 
Mtu ambaye aliyetoa Cheti kwa Daudi Albert Bashite(Alias Paul C. Makonda) anaitwa Paul Christian Muyenge sasa Bwana Daudi Bashite Kuogopa ufanano wa Majina akaamua abadilishe Muyenge iwe Makonda na hilo Makonda ni kutokana na Kazi ya Ukonda aliyoifanya enzi za kutafuta maisha.
 
Unahongwa na wauza madawa ya kulevya kuja kumchafua shujaa wetu wa Dar??

Kila siku makonda makonda who are you??
Hivi atakuwa ni shujaa kweli? Nadhani angekuwa shujaa kama angethubutu kutoa gamba lake halisi!
 
Huwa ni jukumu la jeshi la polisi kusikiliza tuhuma, fununu au tetesi za uwepo wa jinai na kufungua jalada la uchunguzi, kama hawachunguzi basi wameamua kufumbia macho tu na labda hawataki, lakini kimsingi tulipaswa kusikia kuwa Jeshi la Polisi linamchunguza mkuu wa mkoa wa Dar es salaam kuhusu tuhuma za kutumia vyeti vya mtu mwingine kinyume cha sheria.
Mbona Benjamin Netanyahu kule Israel anachunguzwa tuhuma za rushwa?. Kwa nini polisi hapa Tanzania haifanyi hivyo juu ya Tuhuma za Makonda?
Jiulize kwa nini hawajafanya hivyo, au zua uzushi mwingine.

Wanaotaka kujua nani ni nani Tanzania waende RITA

Wanaotakakuona cheti cha elimu ya mtu waende shule/chuo alikosomea.

Mpumbavu na lofa hurukia mambo bila kufikiri.
 
Hoja ya kwamba Paul halisi atakuwa anaogopa kujitokeza haina mashiko.

Kama wameweza kuweka mpaka kadi za magari yanayodaiwa ya Makonda wanashindwaje kumuibua mtu huyo hata picha tu?
 
There you go again

Nakueleza kitu kimoja unajibu kingine

Nimekueleza tu jinsi ilivyo ngumu kwa mtu wa kawaida kupata haki zako
sijasema haiwezekani wala watu wasiende....

Suala la vyeti vya Makonda njia nyepesi na ya haraka ni serikali kutoa tamko
waseme tu wamechunguza nakukuta ni uongo mtupu
au waseme ni kweli wamtimue....

Sidhani kama inahitaji mtu wa kawaida a risk maisha yake aende mahakamani

Kuna risks nyingi mno kwa mtu wa kawaida kujaribu kumshtaki RC

Mifumo yetu ya sheria inafahamika kuwa kuna mapungufu mengi sana......hilo liko wazi kwa kuwa kwa namna moja au nyingine tulishawahi kuathiriwa na ukiritimba huo......

Lakini hilo halisababishi watu wasitafute haki kwenye vyombo vya sheria....na watu wanapata stahiki zao kwa mujibu wa sheria.......

Tulichokuwa tunakitaka ili kukata mzizi wa fitina....hilo shauri lifikishwe polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya Makonda aliyeghushi vyeti.....( kama kweli)......

Naamini ushahidi upo wa kutosha wa kumtia mtuhumiwa hatiani na hili suala likafikia mwisho......

Mbona mashauri mengi tu....wapinzani wanayapeleka mahakamani na kupata haki.....!!!
 
In the interest of full disclosure, mimi sijui chochote kile cha ziada kuhusu hili sakata la vyeti vya mkuu wa mkoa wa Dar zaidi ya hiki ninachokisoma kwenye mitandao ya kijamii na vyombo vinginevyo vya habari.

Lakini nikiwa mtu mwenye akili zangu timamu [well, naamini wapo wataobisha kuwa nina akili timamu, it's all good] nina maswali mepesi sana lakini ambayo naona kama vile hayana majibu kamili ya kueleweka.

Nimeshahoji juu ya uwezekano wa Makonda kufunguliwa mashitaka kwa manufaa ya umma. Hilo nimesikia kuna mtu au watu wanaolifanyia kazi.

Gwajima na Makonda wao naona wamegoma kabisa kutuonyesha vyeti walivyo navyo. Oh well...fine.

Sasa nije kwa huyo Paul Makonda halisi. Yaani Paul Makonda mwenyewe aliyeibiwa au aliyeuza [allegedly] huo utambulisho wake kwa Daudi Bashite.

Yeye huyo mtu yuko wapi?

Sasa hivi anatumia jina gani?

Anafanya shughuli gani?

Hivi huyo mtu hana ndugu, jamaa, na marafiki ambao wanaweza kutupa walau usuli [background] kidogo wa huyo mtu?

Naamini huyo Paul Makonda halisi haishi kwenye ombwe. Naamini anaishi miongoni mwa jamii.

Sasa kweli hao watu anaoishi nao na kukutana nao hakuna hata mmoja wao aliyejitokeza mpaka hivi sasa kusema lolote?

I'm getting so sick of this bullshit.

So will the real Paul Makonda please stand up...?

I repeat, will the real Paul Makonda please stand up...?
The Real Paul Makonda ndiye huyo Daudi Bashite.

Daudi Bashite( kwa masimulizi ya Gwajima) alisaidiwa na mpenzi wake ambaye alimuahidi kuwa wataoana baadae (Hilo halikutimia/ Daudi hakutimiza ahadi aliyompa Dada huyo) kupata kivuli cha cheti cha form 4 cha Paul M. Daudi alitumia kivuli hicho kuombea masomo. Paul M mwenyewe inawezekana hakujua kabisa kwamba Cheti chake kilitolewa kivuli na huyo ndugu yake wa kike.

Ili kuona utata na maelezo ya kina angalia hii

 
Jiulize kwa nini hawajafanya hivyo, au zua uzushi mwingine.

Wanaotaka kujua nani ni nani Tanzania waende RITA

Wanaotakakuona cheti cha elimu ya mtu waende shule/chuo alikosomea.

Mpumbavu na lofa hurukia mambo bila kufikiri.

Walituambiaga Lowasa ni fisadi na ushahidi wanao.....leo hii wanatuambia kuwa mwenye ushahidi aende polisi........

Ukistaajabu ya Mussa utayaona ya firauni......
 
Hoja ya kwamba Paul halisi atakuwa anaogopa kujitokeza haina mashiko.

Kama wameweza kuweka mpaka kadi za magari yanayodaiwa ya Makonda wanashindwaje kumuibua mtu huyo hata picha tu?

Hata Le Mutuz walimwibia passport yake wakaipiga picha wakairusha mtandaoni😀😀.

Kweli watu wana hila za fisi, si mchezo.

Nilicheka sana.
 
Makonda ana kinga ya Mkulu inayompa nguvu kubwa sana, ndiyo maana watu wanajiuliza kabla ya kumburuza mahakamani. Makonda na Guardian Angel wake wana nguvu ya ajabu. Makonda amelivimbia Bunge na mahakama muda si mrefu, na bado hakuna kilichotokea, nani leo ajitoe muhanga kupambana naye? Vyombo vyote vya kupambana naye kuhusu suala lake, viko chini 'yao'.

Swali la msingi ni; Kama kweli Makonda anasingiziwa ya Bashite, kwanini asiwashtaki hao kina Gwajima kwa kumchafua??
 
Unavoongea kama una muhim sana kwa jamii ya tanzania ati your getting sick ww kama nani? Issue ya makonda iko wazi na sasa anamambo makubwa kuliko hayo ya vyeti leo ujinga wake na uroho wake umebainishwa hadharan yaaan watu wanakwapua pesa yy anakwapua magari ya watu dah.
Ninachoshangaa mimi ni kitendo cha eti 'Mange' anaweza kupata copy ya kadi ya gari na kuipost mtandaini,,,, lakini eti anacho cheti cha 0 leo wiki ya tatu hajakitoa..... na kwa tunavyomfahamu mange alivyokuwa mmbea wa dunia, awe na cheti asikitume mtandaoni hadi leo, sio yeye. Hii kitu ni kelele tu, no one with undeniable evidence.
 
The real Paul Makonda is the one and only Paul Makonda, aliyesoma Moccobs, akateuliwa DC na sasa ni RC, mengine yote ni uongo mtupu!.

Ila huko nyuma kuna mtu aliitwa Daudi Albert Bashite, huyu alizaliwa Kolomije, akasoma Kolomije na kumalizia Nyanza. Akafeli la saba, lakini akafanya maarifa akasoma Pamba sekondari ya serekali, alipomaliza form IV alipata zero, na hadithi ya Daudi Bashite ikaishia hapo.

Kukatokea mtu anayeitwa Paul Christian M, ambaye alisoma Chuo cha Nyegezi, baadae Mbegani na mwisho Muccobs, kwenye hayo majina ya Paul Christian M, ndipo kwenye M, likaongezewa jina laMakonda, hivyo Paul Christian Makonda is one and only.

Paskali
😀😀😀😀😀😀😀😀
"Ila huko nyuma kuna mtu aliitwa Daudi Albert Bashite, huyu alizaliwa Kolomije, akasoma Kolomije na kumalizia Nyanza. Akafeli la saba, lakini akafanya maarifa akasoma Pamba sekondari ya serekali, alipomaliza form IV alipata zero, na hadithi ya Daudi Bashite ikaishia hapo."
 
Back
Top Bottom