Wiki moja kabla ya Machozi... Zitto???

Wiki moja kabla ya Machozi... Zitto???

niliandika huko nyuma na hapa narudia, atakayeitumbukiza nchi kwenye mauaji, kiburi, umwagaji damu siyo mwingine bali ni rostam aziz, nilisoma mahojiano yake kuhusu mtikila, mtu nuyu ana dharau kali, anaamini kuwa pesa zake zimemweka mbali sana, anajiona yuko mawinguni na sisi tupo huku chini tukinyoosha mikono na kuomba toba kwake. ni mbaguzi rejea maelezo yake kuhusu mtikila kuwa haweza kumjibu kwa kuwa ananuka, yaani mtikila nanuka kwa kuwa ni mweusi tii.

mtu huyu na wote wanaombaba ni iterwhamwe kama rwanda, naomba kama mna nafasi someni makala ya padri privatus karugendo kwenye gazeti la mwanahalisi la jana, ROSTAM AZIZI NI NANI?
Watanzania tuna tabia moja mbaya kabisa! KULALAMIKA sisi ni hodari wa kulalamika na kusifia! na wengi hapa jf ni walalamishi tu, lakin tungejua vita tuliyo nayo mbele yetu hasa ss vijana ni kubwa na ya hatari mno, kwa sababu wale ambao tumewaamin hasa naongelea watu wa idara ya USALAMA WA TAIFA wamegeuka kuwa maadui wakubwa wa sis wapenda haki na usawa, kodi yetu inayotumika kuwalipia wao na wake zao na watoto kula, kunywa na kunya wanaitumia kutuwinda ili wakatishe uhai wetu!! sis hatuwezi na hatuna uwezo kulipa kisasi kwa yote wanayopanga kutufanyia, LAKINI MUNGU wetu tunayemwamini atawalipa wao na uzao wao wote kwa yote wanayotenda!!!!!!!!!!!!!!

Lakini lipo jambo moja pia, wasifikiri wao wako salama sana!! hata hapo wanapoishi ie makumbusho, si gharama kuwamaliza kwa bomu dogo tu litalowapa fundisho kwamba, hata wao wanaweza kuuawa wakati wowote tena na familia zao!!!

Zipo dalili zote tunakoelekea ni maisha ya kuwindana tu!! hakuna ulinzi wowote wa maana hapa tz, hata hao viongozi ni rahis sana kuwafikia, tena kwa gharama kdg tu, kwa vile wanataka tuishi hivyo, tuko tayari kwa hilo, na uzuri mmoja ni kwamba haijawahi kutokea usalama wa taifa ukawa loose na watu incopetent kama ilivyo sasa.

Wamesema kitendawili, ss tunasema TEGA!!!!
 
Heshima Mbele

Mimi ningependa ieleweke wabunge tulionao hasa hawa vijana ni watu muhimu kwetu na tunawahitaji kwa miaka mingi na siku zijazo hivyo ni muhimu wakalindwa kwa gharama yeyote na tusipende kudharau hata jambo dogo.

Tena leo nimependezwa na michango ya Mbunge Halima Mdee sijui siku nyingi hakuwepo alikuwa wapi Big up Halima wachemshe hao wazee hasa huyo fisadi Londa

Maneno mazito sana haya mkuu, hapa tupo ukurasa mmoja,

Unajua wananchi wengi wanashindwa kuelewa one thing, kama haya maneno ya Zitto, na huko Mombasa ni uongo, hivi uwt ambao wapo hapa 24 hours, yaani 24/7 wangekuwa hawajajibu? Serikali ingekuwa haijajibu? Wanajibu maneno low ya kina Deus Mallya, wataacha makubwa kama haya?

Hivi ni bin-adam gani mwenye akili timamu anayeweza kuamka na ku-create maneno mazito kama haya knowing kwamba yana one alternative, nayo ni kwenda jela kama ni uongo?

Hebu tufike mahali wakuu tuongelee the context ya this topic na rmifications zake kwa taifa letu na sisi wananchi kwa ujumla, badala ya kupoteza muda na our imaginations!
 
"Wajanja" watakwambia hao Rai Mwema wametunga tu hiyo habari! Natamani kujua "uchawi" waliotumia CCM hadi kuwafanya watu wawe "limbwende" kiasi hiki!
 
Hii habari ni ya kweli na kama mtakumbuka barua ya CHADEMA kwa IGP baada ya kifo cha wangwe hilo lilitajwa na pia polisi pamoja na usalama wa taifa walipewa taarifa hizo.

Kulikuwa na mkakati mbaya dhidi yake na pia sms hizo zilisambaa sana .
 
Inaelekea Zitto na yeye alikuwa na ulinzi wake binafsi ama vinginevyo na ndio maana aliweza kujuwa kuna wanaomfuatilia.
Sasa kama wote walikuwa wabunge..Then kwanini huyo Wangwe na yeye hakujuwa kama anafuatiliwa?
Ama Zitto yeye ni chale zilimcheza?
Maana Marehemu na yeye kusema ukweli nadhani alijuwa kuna hatari na maisha yake na kutokana na hilo basi...Huyo mtu aliyekuwa akutane naye...Huyo aliemfanya akahidi na kutokusikiliza ushauri wa kila mtu...Huyo LAZIMA ANA INFLUENCE KUBWA SANA NA MAISHA YA MAREHEMU..Huyo ndiye aliyemtuma Deus Mallya...Kwani Deus Mallya kama Dereva asiyekuwa na leseni...Hakuwa na nguvu za kumwamsha marehemu kama hakutumwa na mtu ambaye marehemu alimwamini SANA.
Na hicho kizungu zungu na usingizi mzito..Labda ni mbinu ili kijana aachiwe gari na aliendeshe yeye..Maana inasemekana kuwa marehemu allikuwa akipenda kuendesha mwenyewe...Sasa walipoona hivyo..Wakaandaa mtu mwenye kujidai kuwa hana leseni na hawezi kuendesha...Tatizo ni kuwa marehemu hakuweza kuendesha kabisa gari na ULAZIMA WA SAFARI ULIKUWEPO na ndio maana Deus alishindwa kujitetea kuwa hakuwa mwendeshaji..Kwani dalili zinaonyesha mbinu ilikuwa ni marehemu aendeshe at least kutoka nyumbani ili kufuta ile dhana ya kuwa deus ndio mwendeshaji.
Tatizo ni kwamba walimu OVERDOSE na hakuweza hata kuliondoa gari lake hadi hata nje ya nyumbani kwake.
Ni wazi kuwa mitego iko mingi na ni wazi kuwa hata Mh Zitto na wengineo wako hatarini..Je...Serikali imechukuwa hatua gani.
Kwasababu kama inafiki watu ambao ni viongozi wa Taifa wanatembea na maji yao na chakula..Then HAKUNA TENA UONGOZI.
 
Mpaka Kieleweke... Wangwe alikuwa na bodyguard wake mwenye silaha na mara nyingi amekuwa naye; hivi tunajua yuko wapi huyo bwana na kwanini hakuweza kuambatana na bosi wake siku ile?

na Pili, Ni nani aliyediagnose kuwa Wangwe alikuwa mgonjwa wa Malaria na alitumia dawa gani?
 
Haijulikani yuko wapi huyo jamaa ila alikuwa anaitwa Joel.

Kuhusu malaria walisema watoto wake kuwa alitumia dawa mseto za kutibu malaria .
 
Haijulikani yuko wapi huyo jamaa ila alikuwa anaitwa Joel.

Yaani aliyekuwa bodyguard wake hajulikani alipo? kuna mtu amejaribu kumtafuta? Vipi wakiambiwa kuna "mwili umeokotwa"?

Kuhusu malaria walisema watoto wake kuwa alitumia dawa mseto za kutibu malaria .

Una maana hakuna tabibu ambaye alithibitisha kuwa anaumwa Malaria?
 
Si mnaona mambo hayo...Mimi nakwambia tukiamuwa kuzungumzia hii issue kweli inaweza ikaendelea hadi mwaka 2010...Sasa kumbe ni kweli lazima huyo aliyemtuma Kijana atajwe kwasababu huyu marehemu alikuwa na IMANI KUBWA SANA NA HUYO MTU amabye kijana Deus alikuwa akimwakilisha...Mimi nakwambia hii mambo si mzuri kabisa na kama this is the case kuna vituko vingi sana tu expect in a near future..Inawezekana kuna yale tutakayoyasikia na hatutaamini masikio yetu.
Kwasabau kweli...WAPI BODYGUARD?
Na stori za kuumwa malaria nazo ni kama nilivyosema inawezekana ni USANII tu..Huyu walishamlegeza na madawa ya kulevya ama sumu flani ili asiweze kughairisha safari yake na pia kutokana na umuhimu wa safari hiyo...Ni wazi kuendesha angeshindwa na kwasababu kijana yuko Trained kupindua magari na ndio maana hana leseni..Basi hapo....
 
i) pamoja na kupata vielimu vya darasani, inaonekana baadhi yetu bado tu wa jinga kwa kiwango cha kutisha kuhusu elimu ya siasa, kiasi kwamba hata kazi za msingi za serikali hatuzijui!

ii) Baadhi ya watu humu wana wivu na chuki ya kutisha kwa mafanikio ya baadhi ya wanasiasa wetu. Inaonekana watu wakipata mafanikio huwa wanahuzunika sana, na wakikosea kidogo wanafurahi mno. Na sijui nani aliwaambia kwamba ukifanya vizuri na ukawa shujaa basi huwezi hata siku moja kukosea. Na nani aliwaambia kwamba ukikosea mara moja basi inafuta mazuri yote uliyoyafanya nyuma na unayoweza kuyafanya huko mbele? Watu wengine kaputi kabisa katika fikra!

Thanks Kitila: Coz hizi discussion za Rostam Aziz, Usalama wa taifa, TBC1, whatever & whatever, hazisaidii chochote hapa. Action is What's is needed now.

1: Ingekuwa vema kama tungetumia muda huu tunaopoteza hapa (kupiga kelele zisizo zaa matuda) ku-mobilize wapiga kura ktk njia ambayo ni more direct and effective. Kumbukeni kuwa, wapiga kura watakaoirudisha CCM madarani 2010 wengi wao wanaishi vijijini na hawana fursa kama tuliyonayo sisi ya kuingia humu JF every now and then ( I mean, access ya internet).

2: Hivi kweli mnadhani hao mafisadi wanatishika/kosa usingizi kila wanaposoma thread(s) zinazowahusu humu JF? Hapana, hawatishiki. Ila kama wangejua kuwa kuna organization/movement fulani(yenye mwelekeo na sio maneno matupu) inayowa-target/fuatilia nyendo zao vilivyo, wangekosa usingizi. Wangebadilika. Na nchi ingenufaika.

Neno la mwisho: to its credit, JF imekuwa tochi muhimu ambayo imeangaza nuru [iliyokuwa inahitajika sana!] kuhusu hili suala zima la ufisadi: ila sasa nadhani imefikia wakati tukafikiria strategy mpya ya vitendo badala ya kukalia maneno peke yake ambayo so far, sidhani kama yame-yield significant changes.
 
Hamjajua tu hata mlio jf mnawindwa vile vile, so mzee mkjj kaa chonjo!

Hili liko wazi..Mafioso wameshajaribu kweli na wataendelea kujaribu...Na ndio maana maneno ya watu kama kina Zitto yasipuuziwe kabisa.
 
Thanks Kitila: Coz hizi discussion za Rostam Aziz, Usalama wa taifa, TBC1, whatever & whatever, hazisaidii chochote hapa. Action is What's is needed now.

Heshima mbele mkuu, ni jumamosi hii tu nilipata nafasi ya kukaa chini na serikali kwa karibu masaa matano, katika kujaribu kuwaelewesha maana ya topic niyngi sana hapa, ambazo zimewagusa sana na sio mara ya kwanza, kwa hiyo mkuu kama huna uhakika uliza kwanza, hatupo hapa kupoteza muda,

Beleive me kila serious ishu inayoandikwa hapa, ujue ipo huko kwa sababu nilionyeshwa wazi, sasa tuendelee kukata ishus mengine waachie wengine, wewe ni kutimiza mradi wako tu hapa ambao ni wa kujitolea na unaheshimika sana kwa wanaohusika, kama kuna strategy nyingine zinahitajika hakuna tatizo, lakini hapa pataendelea kama palivyo, hakijaharibika kitu.

Ahsante Mkuu!
 
Beleive me kila serious ishu inayoandikwa hapa, ujue ipo huko kwa sababu nilionyeshwa wazi, sasa tuendelee kukata ishus mengine waachie wengine, wewe ni kutimiza mradi wako tu hapa ambao ni wa kujitolea na unaheshimika sana kwa wanaohusika, kama kuna strategy nyingine zinahitajika hakuna tatizo, lakini hapa pataendelea kama palivyo, hakijaharibika kitu.Ahsante Mkuu!

Nakubaliana na wewe mkuu ila ukweli wa mambo ni kwamba: the state of affair in our coutry is so dire that immediate action is required, now. Plus, sio kwamba nataka hii forum ifungwe, no. Iendelee. Ila tubadili strategy za ku-attack haya yanayosibu taifa letu. Kwani kuna tatizo gani endapo kama tuta-employ method zote mbili (maneno & vitendo) kama kweli tuko serious kuhakikisha kuwa ufisadi is rooted out nchini.
 
Kitu cha kusikitisha ni kua
Watanzania wanaojiita wasomi wanadhani wapo ktk siasa ili kupata mafanikio yao binafsi .

Mimi nionavyo mwanasiasa makini hua haoni wala hana mpango na mafanikio yake kisiasa badala yake mwanasiasa hua makini kuwaletea wananchi na nchi kwa ujumla kitu wanachopenda kukipata kwa ajili ya maendeleo husika.

Ukiangalia viongozi wa mataifa ya magharibi wapo tayari kuharibiwa majina yao kisiasa lakini wakisimama kufanya kile wanachoonelea kitaleta tija na maendeleo kwa taifa lao,hawa watu wanaweza kuamua kuvamia nchi na kuchukua wapendacho hata kama wengine mtawaona bwege kivipi.
tatizo wa kwetu wapo kufanikiwa kisiasa.kazi kweli kweli
 
Kamundu... haijasemwa mahali popote kuwa ni CCM...
Mkuu ,CCM is very large & Dynamic in its own Measures.Sasa tunaposema CCM twaweza kuwa tunazungumzia Wanachama,Mweka Hazina,Katibu Mkuu,Makamu Mwenyekiti,Mwenyekiti wa shina/tawi,inategemeana na Mtazamo wa 'Ka-Nzi',Is it TOP-DOWN or DOWN-TOP??
**Tunaelewa kuwa 'Ka-Nzi' hakana mbawa za Kupea hadi huko Matawi ya Juu,ila kanajua kuwa rangi ya Mti na Matawi yake ni ya KIJANI.
 
Mkuu ,CCM is very large & Dynamic in its own Measures.Sasa tunaposema CCM twaweza kuwa tunazungumzia Wanachama,Mweka Hazina,Katibu Mkuu,Makamu Mwenyekiti,Mwenyekiti wa shina/tawi,inategemeana na Mtazamo wa 'Ka-Nzi',Is it TOP-DOWN or DOWN-TOP??
**Tunaelewa kuwa 'Ka-Nzi' hakana mbawa za Kupea hadi huko Matawi ya Juu,ila kanajua kuwa rangi ya Mti na Matawi yake ni ya KIJANI.

Hauxtable usinivunje mbavu..Hayo matawi ya juu juu ni ya kijani sana na manjano tu.....Yani unasema eti kanzi ka MKJJ hakawezi kwenda matawi ya juu?
Yani matawi ya juu kabisa kule kileleni ama ni matawi ya kati kati?
 
Kitu cha kusikitisha ni kua
Watanzania wanaojiita wasomi wanadhani wapo ktk siasa ili kupata mafanikio yao binafsi.

It's true Mkamap. Hata hawa akina Zitto, Slaa, Anne-Kilango Malecela, wanaoimbwa hapa JF wote ni walewale. Wasioaminika. Kama ni grade,basi ningewapatia "C-" (tena hapo nimewapendelea, maana wanastahili "D+").

Kelele zote zile (list of shame/whatever) zilikuwa ni kujizolea umarufu tu.

Ukweli ni kwamba, kama wangekuwa na nia ya kuleta real changes, basi wangeendeleza hizo kelele zao hadi leo. It's sad kwamba when I look at Slaa, or Zitto, or mama Malecela (today) I don't see an ounce of courageousness or bravery in them. what I see, rather, is fear, vulnerability, fragility, and defeatism.
 
I don't see an ounce of courageousness or bravery in them. what I see, rather, is fear, vulnerability, fragility, and defeatism.

Wooow! Unaona nini kwenye sisi wananchi wa Tanzania mkuu? Halafu unaona nini kwa wabunge kama Serukamba na Chintalilo?

Haya mawazo ni haki yaki kisheria kuwa nayo, lakini ni misguided mkuu, bongo sio majuu hapa mambo yaliyokwisha fanywa na hao wabunge uliowataja ni mara ya kwanza yanatokea bongo, ambako mpaka leo bado wananchi wengi waanaamini kuwa mpinzani wa serikali ya CCM ni usaliti,

Mkuu Rome haikujengwa kwa siku moja, na ndio hasa unachojaribu ku-advocate hapa, hao viongozi wamejaribu kufanya something sasa ni zamu ya wengine pia kujaribu kuendeleza walichoanzisha, unajua unanikumbusha kijiji cha ujamaa cha Chamwino, Mwalimu alipokianzisha alipeleleka machine za kulima na kila kitu, ilipofikia wakati wa kuvuna wananchi wa kule wakagoma kuvuna wakisema wanasubiri iletwe machine ya kuvuna kwa sababu haiwezekani kuwa wana machine zote hizi lakini hawana ya kuvuna?

Hili taifa tumetoka mbali sana na bado safari ni ndefu sana, mliokata tamaa tuachieni sisi ambao bado tunaamini in uvumilivu na kwamba mabadiliko hayawezi kuletwa na Zitto, Dr. Slaa na Mama Kilango peke yao, bali ni lazima wananchi wote millioni 40 lazima tuwe involved!
 
Back
Top Bottom