Wiki moja kabla ya Machozi... Zitto???

Wiki moja kabla ya Machozi... Zitto???

Kumbuka hata ile ajali ya Salome Mbatia ilikuwa imemlenga Zitto, maana siku hiyo Zitto alisimama sehemu kukata kiu kidogo na kwa bahati mbaya/nzuri salome akawa anapita kuelekea uelekeo huohuo na kwa vile magari yao yalifanana basi jamaa wakammaliza Salome wakidhani ni Zitto. Ndo maana Zitto akawa miongoni mwa watu wa kwanza kuona ile ajali.

Hoja hiyo hapo juu ni NZITO sana tu...Na kusema ukweli kama hayo hapo juu ni kweli...Basi pamoja na yote yaliyokwisha tokea...Something gotta be done.
Na kweli kama nilivyosema hapo awali...Usalama wa Taifa nao umegawanayika...Na wale wanaomlaumumu Zitto pale anapotembea na chakula na maji yake..Basi wana wivu kuwa hawawezi kumwua kirahisi...Na badala ya hao viongozi wakuu wa nchi kuchukulia hii ni PORORJO...Basi wananchi WAANDAMANE mpaka HAKI itakapopatikana na UMAFIOSO HU KUWEKWA BAYANA.
 
Heshima Mbele

Mimi ningependa ieleweke wabunge tulionao hasa hawa vijana ni watu muhimu kwetu na tunawahitaji kwa miaka mingi na siku zijazo hivyo ni muhimu wakalindwa kwa gharama yeyote na tusipende kudharau hata jambo dogo.

Tena leo nimependezwa na michango ya Mbunge Halima Mdee sijui siku nyingi hakuwepo alikuwa wapi Big up Halima wachemshe hao wazee hasa huyo fisadi Londa
 
Serikali inaonekana imeshikwa pabaya..Sasa baada a issue waliyotaka iwe ya kisiasa kugeuka na kuwa ya kitaalam kwa wana jf wasioyumbishwa..Naona wamemtumia MKURUGENZI WA MASHTAKA KUWAPIGA WAZALENDO STPOP wasizungumzie kuhusu mambo ambayo karibia yawakute wengine ambao wako hai kama kina Zitto...Kina Zitto nawaonea HURUMA SANA..Ila Mungu yuko na nyie kwani kama ni KUFA basi wangeshawaua kitambo..Lakini wakati wa Mungu kamwe hauwezi kuzuiliwa ukishafika!

Habari za Wangwe sasa zapigwa `stop`

2008-08-07 09:56:26
Na Romana Mallya


Vyombo vya habari pamoja na taasisi nyingine, vimepigwa marufuku kufanya upelelezi kuhusu ajali liliyomuua aliyekuwa Mbunge wa Tarime kwa tiketi ya CHADEMA, marehemu Chacha Wangwe.

Badala yake, vyombo hivyo vimetakiwa kuacha kazi hiyo ya upelelezi ifanywe na Jeshi la Polisi.

Onyo hilo lilitolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Bw. Eliezer Mbuki.
Aidha, Bw. Mbuki amevitahadharisha vyombo vya habari na taasisi kuwa, kama vitaendelea kuandika habari hizo, vitawajibishwa.

Akizungumza na Nipashe kwa njia ya simu jana, Bw. Mbuki alisema habari zinazoendelea kuzungumzwa na kuripotiwa katika vyombo vya habari kuhusu tukio hilo, zinaweza kuleta madhara baada ya upelelezi wa polisi.

Marehemu Wangwe, alifariki dunia kwa ajali ya gari Julai 28, mwaka huu wakati akiwa safarini kutoka mjini Dodoma kuja jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, Deus Mallya aliyekuwa pamoja na marehemu Wangwe, tayari amefikishwa katika Mahakama ya Mkoa wa Dodoma akikabiliwa na mashtaka ya kuendesha gari la marehemu akiwa hana leseni na kwa mwendo wa kasi na hivyo kusababisha gari hilo kupinduka na kumuua Mbunge huyo.

``Endapo vyombo vya habari vitaendelea kuandika habari hiyo na baadaye kuonekana kuwa vilipotosha ukweli, itasababisha vyombo hivyo kuwajibishwa,`` alisisitiza.

Alisema kutokana na madhara hayo, wahusika wanaweza kuwajibishwa kwa kuvuruga upelelezi na kuingilia uhuru wa Mahakama.

Hivi karibuni, baadhi ya vyombo vya habari na wanasiasa, wameripotiwa kumtuhumu Mallya kuwa ni jasusi aliyewahi kupata mafunzo hayo nchini Libya.

Mkurugenzi huyo wa Mashtaka, aliyasema hayo alipotakiwa na Nipashe kutoa msimamo wake kuhusu habari zinazoendelea kuandikwa na kuibua mambo mbalimbali wakati kesi hiyo ikiwa tayari imefikishwa mahakamani na polisi wanaendelea na uchunguzi wao.

``Mimi nadhani tuliachie Jeshi la Polisi lifanye kazi yake ya kupeleleza tukio zima la ajali na vyombo vingine navyo visubiri upelelezi huo, kwani kwa kuendelea kuibua mambo na baadaye kuonekana ni uongo yanaweza kuleta madhara na kuwajibishwa`` alionya.

Aidha, Bw. Mbuki alisema Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri, Bi. Sakina Dotoo alitoa maelezo mazuri kwa vyombo vya habari, hivyo hakuna haja ya kurudia kwani maelezo yake yanajitosheleza.

Alisema Bi. Sakina alisema kuwa, lengo la jukwaa hilo ni kuleta usawa wa habari na kwa kila mtu na jukwaa hilo halifungamani na upende wo wote wa chama cha siasa na aliahidi kuwa watasimama katika msimamo huo.

SOURCE: Nipashe
 
Mi nashangaa sana..mbona wanamuandama zitto wa watu.....wakati kuna mtu anaitwa Slaa anatamka kabisa hadharani kua ana habari nyeti za nzito za wwatu wazito lakini sisikii wakimfuatilia kama Zitto...au wanamuogopa???
 
Kwa hali hii ya kuanza kuvizia kuua viongozi mi naona Tanzania tupo mbioni kuingia vutani...! Majirani zetu Rwanda walianza hivi hivi....!

War, start by unlawful killing of one person, followed by revenge of killing another person causing anger then killing tens, provoking infuriation then killing hundreds, ending up with Genocide, the act of errasing a particular sect.

Mzee umefika mbali, punguza munkari mzee, taifa hili ni letu wote tukianza kuwanyonga da! hapo si tutazua kitimtim?
 
.....wakati kuna mtu anaitwa Slaa anatamka kabisa hadharani kua ana habari nyeti za nzito za wwatu wazito lakini sisikii wakimfuatilia kama Zitto...au wanamuogopa???
__________________
Mkuu huyu Slaa ni mteule wa Mungu au kwa kifupi ni Nabii ambaye hata upange vp huwezi ukamfikia mbinu zako zinayeyuka.Angalia vizuri ile list of shame ya Mwembe Yanga alimtaja na Muungwana lakini hakuna kesi yeyote waliyo mfungulia huyu Mtikila kasema Muungwana Gaidi tayari wamesha mfungulia kesi.Huyu mkuu hawawezi kumfanya lolote lile alisha pewa upako.
 
niliandika huko nyuma na hapa narudia, atakayeitumbukiza nchi kwenye mauaji, kiburi, umwagaji damu siyo mwingine bali ni rostam aziz, nilisoma mahojiano yake kuhusu mtikila, mtu nuyu ana dharau kali, anaamini kuwa pesa zake zimemweka mbali sana, anajiona yuko mawinguni na sisi tupo huku chini tukinyoosha mikono na kuomba toba kwake. ni mbaguzi rejea maelezo yake kuhusu mtikila kuwa haweza kumjibu kwa kuwa ananuka, yaani mtikila nanuka kwa kuwa ni mweusi tii.

mtu huyu na wote wanaombaba ni iterwhamwe kama rwanda, naomba kama mna nafasi someni makala ya padri privatus karugendo kwenye gazeti la mwanahalisi la jana, ROSTAM AZIZI NI NANI?
 
Tujue kwanza maadui wa ZITTO ni akina nani???????ndo hapo tuanze kuchambua hoja moja baada ya nyingine..je Adui wa ZITTO ni Karamagi?au RA?au EL?lazima tuwafahamu ndo itakuwa rahisi kuwamulika lakini tukiendelea na bla bla za labda tutakuja kushtuka tumempoteza hivi hivi kiutani utani.

Maadui wa zito ni
miundo mbinu mibovu inayoelekea kigoma,barabara hazipitiki,reli nayo ndiyo hiyo hadi inabidi upande juu ya dari.
Wananchi masikini kule hawewezi nunua hata kandambili FUNZA ZINAWAMALIZA vidole kule kigoma .Hao ndio maadui wakubwa wa zito

Hakuna adui mwingine labda kama ameonekana kwa sijui ramli ama lamuli akipaa masafa mafupi.
 
Maadui wa zito ni
miundo mbinu mibovu inayoelekea kigoma,barabara hazipitiki,reli nayo ndiyo hiyo hadi inabidi upande juu ya dari.
Wananchi masikini kule hawewezi nunua hata kandambili FUNZA ZINAWAMALIZA vidole kule kigoma .Hao ndio maadui wakubwa wa zito

Hakuna adui mwingine labda kama ameonekana kwa sijui ramli ama lamuli akipaa masafa mafupi.

na wananchi wengine hawakabiliwi na maadui hao isipokuwa Zitto tu?
 
Mimi ningependa sana kuona
1.Ahadi za Zitto aliwaahidi nini wananchi wake wakati wa uchaguzi na nini amefanikisha kati ya ahadi zake.Naamini suala la buzwag halikuwamo ktk ahadi zake za direct kwa wananchi
2.Pia vivyo hivyo kwa DR SLAA.

Nitashukuru sana DR SLAA na ZITTo mkinipa ahadi zenu wakati wa uchagunzi mkuu kwa wananchi ili na mafanikio yenu hadi sasa ili UMMA uwaelewe bayana nini kwanini, wapi lini.ASANTE.
 
na wananchi wengine hawakabiliwi na maadui hao isipokuwa Zitto tu?


wao ndio tumewakabidhi B52 ,ndio maana wanaposema bungeni wanalindwa na sheria na mkao mmoja tu ni zaidi ya mshahara wa polisi wa mwezi mnaowataka wafanye uchunguzi makini.
 
Hii nayo VIPI? Au hamjasoma magazeti?

Makachero wamfuatilia Zitto hadi Kenya

Mwandishi Wetu
Agosti 6, 2008

WIKI moja kabla ya Mbunge wa Tarime (CHADEMA), Chacha Zakayo Wangwe kufariki, Mbunge kijana wa Kigoma Kaskazini kupitia chama hicho, Zitto Zuberi Kabwe, alizushiwa kifo huku akifwatiliwa na watu wasiojulikana hadi nchini Kenya alikokwenda kikazi, Raia Mwema imeambiwa.

Uchunguzi wa Raia Mwema umethibitisha kuwepo kwa taarifa kadhaa za uvumi wa kifo cha Zitto, sambamba na taarifa ya kufuatwa kwake na watu watatu kutokea Dar es Salaam, Nairobi na hatimaye Mombasa.

Wangwe alifariki kwa ajali ya gari iliyotokea Julai 28, 2008 katika eneo la Pandambili, Kongwa mkoani Dodoma akiwa njiani kuelekea Dar es Salaam, ajali ambayo hadi sasa imezidi kugubikwa na utata na malumbano ya kila aina kila kukicha ikiwa ni pamoja na mgawanyiko miongoni mwa viongozi wa vyama vya upinzani.

Viongozi wa CHADEMA waliithibitisha Raia Mwema kupokea taarifa za uvumi wa kifo cha Zitto Kabwe, kabla ya kufanikiwa kumpata kwa simu akiwa Mombasa, alikoenda kwa shughuli za kibunge.

Zitto mwenyewe alilithibitishia Raia Mwema kuwapo kwa taarifa hizo ambazo alisema alishindwa kufahamu chanzo na sababu za kuwapo kwake, na alikataa kueleza kwa undani kuhusu suala la watu waliomfwatilia hadi nchini Kenya kwa maelezo kwamba “suala hili nimeliacha mikononi mwa mamlaka zinazohusika.”

“Ni kweli nilifuatwa na watu watatu, wakati ambao naelezwa nilikuwa nimevumishiwa kuwa nimekufa na kwa kuwa sikuwa naelewa sababu ya uvumi huo, niliziarifu mamlaka zinazohusika za Tanzania na Kenya na nilitakiwa niendelee na shughuli zangu bila wasiwasi wowote,” alisema Zitto.

Hata hivyo, haikuweza kufahamika mara moja watu hao watatu walioonekana Dar es Salaam, Nairobi na Mombasa walikua raia wa nchi gani na walikuwa na malengo gani baada ya kutokuwapo taarifa zozote za walikopelekwa na vyombo vya Serikali nchini Kenya baada ya kukamatwa na kuhojiwa katika uwanja wa ndege wa Mombasa.

Barua ya CHADEMA kwenda kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) nchini ilirejea, kwa ufupi, tishio hilo kwa viongozi wa CHADEMA na vyama vya siasa na kuomba ulinzi kwa viongozi wake ambao wamekua wakitishiwa maisha na hata kuzushiwa vifo bila kuingia undani wa suala hilo.

“Hivi karibuni wabunge wa CHADEMA wamekuwa wakipata taarifa za vitisho pamoja na kuzushiwa vifo kwa njia ya ujumbe mfupi wa simu za mikononi na ujumbe huo kusambazwa sana kama ilivyoripotiwa kwako na Mheshimiwa Zitto Kabwe. Tunaomba wabunge wetu wapatiwe ulinzi na pia taarifa hizo zifanyiwe kazi kwa kina,” imeeleza sehemu ya barua hiyo ya CHADEMA.

Hii si mara ya kwanza kwa viongozi wa CHADEMA kutajwa kutishiwa maisha baada ya taarifa za awali za Dk. Slaa mwenyewe kutishiwa maisha mara kadhaa baada ya kutolewa kwa kile kilichofahamika kuwa orodha ya aibu ya watu wanaotuhumiwa kujihusisha na ufisadi. Wengi wao katika orodha hiyo ni viongozi wenye madaraka ndani ya Serikali, baadhi yao wakiwa tayari wamekwisha kujiuzulu nafasi zao.

Baada ya kifo cha Wangwe, hali ya wasiwasi sasa imezidi kuingia miongoni mwa viongozi wa vyama vya siasa wakiwemo wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ambao nao wamejikuta wakiwa katika wakati mgumu kutokana na vitisho na hata kuvumishiwa vifo.

Miongoni mwa waliowahi kuvumishiwa kifo, yumo pia aliyekuwa Mwenyekiti wa Kamati iliyopitia mkataba wa mradi tata wa umeme wa dharura uliokabidhiwa kampuni ya Richmond Development LLC ya Marekani, Dk. Harrison Mwakyembe ambaye wakati uvumi huo ukiendelea alikua mgonjwa.

Dk. Mwakyembe ambaye ni Mbunge wa Kyela kupitia CCM alivumishiwa kifo siku chache baada ya kuugua ghalfa akiwa ndani ya Bunge na kutakiwa kupumzika akiendelea na matibabu, ugonjwa uliotaka kuhusishwa na kitu kilichodaiwa kumwagwa ndani ya ukumbi wa Bunge. Uchunguzi wa kitaalamu, hata hivyo, ulibaini kutokuwapo kwa aina yoyote ya sumu au kemikali yenye madhara yoyote.

Pamoja na kuwapo vitisho na hofu kubwa miongoni mwa wabunge na wanasiasa machachari, kifo cha Wangwe kimezidisha hofu miongoni mwa wanasiasa, hususan baada ya kuendeelea kuwapo kwa utata kuhusiana na kifo cha mbunge huyo machachari ambaye hata ndani ya chama chake cha CHADEMA alikuwa akiwachachafya mno.

Wakati huo huo, kifo cha Wangwe kimezidi kugubikwa na utata, na sasa inaelezwa kwamba kampeni za kisiasa kutafuta mrithi wake, zilianza kabla hata ya mwili wa mbunge huyo kuzikwa wilayani Tarime. Kampeni hizo zimeelezwa kuendelea hadi sasa kwa makundi mbalimbali ya kijamii kujaribu kutafuta mtu wa kugombea kiti hicho.

Habari kutoka Tarime zinaeleza kwamba, viongozi wa CUF, NCCR-Mageuzi na TLP waliokuwapo Tarime, walifanya mazungumzo na mwanasiasa mmoja wa Tarime wanayemgombea awanie ubunge kupitia vyama vyao, mazungumzo yaliyofanyika ndani ya chumba alipokua amelazwa marehemu Wangwe kabla ya mazishi.

Kwa mujibu wa habari hizo, hata malumbano yasiyo rasmi yaliyoibuka sasa miongoni mwa viongozi wa vyama hivyo na wale wa CHADEMA, yanaelezwa ya kuwa ni sehemu ya kampeni hizo za kuelekea uchaguzi mdogo wa jimbo la Tarime, ambao kila chama kinatajwa kutaka kusimamisha mgombea kwa imani ya kulitwaa jimbo hilo.

Viongozi wa CUF, Ibrahim Lipumba, Augustine Mrema wa TLP na James Mbatia wa NCCR-Mageuzi walikutana na waandishi wa habari siku moja tu baada ya Zitto kukutana na Jukwaa la Wahariri, akilalamikia taarifa za baadhi ya vyombo vya habari kuhusiana na matukio ya vurugu wakati wa msiba wa Wangwe, wilayani Tarime.

Lipumba alikwenda mbali zaidi na kusema kwamba kichwa cha Wangwe kilipondeka na kwamba kijana Deus Francis Mallya aliyekuwapo katika ajali hiyo na Wangwe ni jasusi ambaye alichukua mafunzo nchini Libya, tuhuma ambazo zimeelezwa kuwa nzito zikihusisha nchi nyingine yenye uhusiano na Tanzania.

“Lipumba ni kiongozi hatari. Kusema Mallya ni jasusi ni kumhukumu na je, ikigundulika sio? Kusema Wangwe kichwa kimepondeka pia ni hatari kwa kuwa familia na waliokuwamo katika uchunguzi wa daktari wametoa taarifa tofauti. Siasa za Tanzania sasa zimekua chafu sana,” anasema mwanasiasa mmoja ndani ya upinzani.

Tayari imeripotiwa kwamba Mallya alikwenda Libya katika mkutano, akiongozana na vijana wengine wa vyama vya upinzani na CCM pamoja na viongozi wa dini, safari ambayo Serikali ya Tanzania na Libya zilikuwa na taarifa nayo tofauti na taarifa za kuwa kijana huyo alikwenda kuchukua mafunzo ya kijasusi ama ya kijeshi.

Baba wa Mallya, Mzee Francis amenukuliwa na gazeti moja la kila siku akilalamikia kauli ya Lipumba akisema ni kumhukumu kabla ya uchunguzi wa vyombo vya dola kukamilika na kuthibitisha tuhuma hizo.

Katika safari ya Libya, Mallya anaelezwa kuwa pamoja na watu mbalimbali akiwamo Mbunge wa Iramba Magharibi (CCM), Juma Hassan Kilimbah, Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mamuya na Makongoro Nyerere ambaye sasa ni Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Mara.

Wengine katika safari hiyo anatajwa Sheikh Mkuu wa Tanzania, Mufti Shaaban Issa Simba, Shehe Seleman Kilemile na Hebron Mwakagenda, ambaye ni kutoka Leadership Forum.

Tayari Mallya amefikishwa mahakani akifunguliwa kesi ya usalama barabarani namba TR 103/08 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Dodoma, akidaiwa kuendesha gari kwa mwendo kasi na kusababisha kifo cha Wangwe na kuendesha gari bila leseni.

Wakati Chama cha Mapinduzi nacho kikituhumiwa kuchochea mtafaruku ndani ya vyama vya upinzani kwa kuhofia wabunge wake kuhamia vyama hivyo kutokana na kuyumba kwa chama hicho, Wangwe anatajwa kuwa mmoja wa wanasiasa ambaye angetumika kwa kazi hiyo.

Mbali ya ushahidi wa nyaraka ulionukuliwa katika gazeti la Mwananchi la jana, maelezo ya watu mbalimbali yanaeleza wazi kuwapo kwa taarifa za mbunge huyo kuweza kukivuruga chama chake na kukihama kujiunga na CCM.

Kwa nyakati tofauti, maofisa kadhaa wa CCM, ngazi za mikoa na Makao Makuu, wameiambia Raia Mwema wiki hii kwamba maandalizi ya Wangwe kuhamia CCM yalikwisha kukamilika kutokana na yeye kudai alikuwa hatendewi haki ndani ya CHADEMA.

“Maandalizi ya kuja CCM yalikwisha kukamilika. Sisi uongozi wa CCM wa Mkoa wa Mara ambako ndiko anakatoka Chacha Wangwe tulikuwa kama waratibu wa suala hilo,” anasema kiongozi mwandamizi mmoja wa CCM Mkoa wa Mara, aliyezungumza na Raia Mwema, wiki hii mjini Dodoma.

Anaongeza kiongozi huyo: “ Alikuwa (Wangwe) akienda Dar es Salaam ambako baada ya kushiriki mazishi ya Mzee Bhoke Munanka, na kusikiliza maendeleo ya kesi yake dhidi ya uongozi wa CHADEMA, angekutana na waandishi wa habari kusema kile alichokuwa akiamini kuwa hakiendi sawa ndani ya chama chake na baada ya hapo angekuja CCM.

Alipanga kuanika hadharani kile alichokiita yeye “uozo ndani ya CHADEMA wa ufujaji wa fedha za ruzuku na upendeleo katika kuteua wabunge wa viti maalumu ambao amekuwa akidai ulifuata zaidi ukabila badala ya sifa.”

Madai mengine ya Wangwe ambayo amekuwa akiyatoa mara kwa mara ni pamoja na kwamba majimbo, kama la kwake hayakuwa yakifaidika na fedha za ruzuku ambazo kimsingi zinatolewa kutokana na idadi ya viti vya ubunge ambavyo chama kinavyo na kwamba badala ya kwenda majimboni fedha hizo zilikuwa zikineemesha walioko Makao Makuu.

Raia Mwema haikufanikiwa kuzungumza na Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba wiki hii, lakini habari za walio karibu naye zimekuwa zikisema kwamba alikuwa na mawasiliano ya karibu na Wangwe kwa ajili ya yeye kuhamia CCM.

“Yamekuwapo mawasilino na Ofisi ya Katibu Mkuu na nadhani mambo yalikuwa yakienda sawa, kilichokuwa kinasubiriwa tu ni kwa Wangwe mwenyewe kukamilisha mambo yake CHADEMA ili isionekane kwamba CCM ilikuwa imemrubuni.

Wachunguzi wanasema hata hivyo kwamba suala hilo la kurubuniwa kwa Wangwe, kama hatimaye angehamia CCM, lazima lingeibuka kwa kuwa tayari kuna madai kutoka CHADEMA ya kwamba yeye alikuwa akitoa siri za chama hicho kwa CCM, madai ambayo yanaelezwa kuwa yalikuwa yakimkera sana mbunge huyo na ambayo yalichangia yeye kusimamishwa asiendelee na nafasi yake kama Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA.

Wachunguzi wanasema kifo cha Wangwe kitaendelea kwa muda kuibua mambo mengi kutokana na kuwa katika kipindi cha karibu mwaka mzima uliopita Wangwe mwenyewe alikuwa katika simulizi za mara kwa mara katika vyombo vya habari nchini.

http://www.raiamwema.co.tz/08/08/06/1.php
 
Back
Top Bottom