Sidhani kama kuna watu wanabishia uningiliaji wa nchi za magharibi kwa interests zao lakini tusifumbie macho kwa jinsi naye Mugabe ambavyo anaiendesha Zimbabwe.
Hivi mugabe anataka kutuambia ni yeye peke yake ndio alipigania uhuru wa Zimbabwe au ni yeye peke yake ndio ana uchungu na Zimbabwe?
Tufanye hayo hapo juu ni kweli, basi ajifunze kurithisha wengine ambao anaona wana uchungu na hiyo nchi kama yeye, kwani naamini wapo. Urais miaka 28? Tangu hatujui mambo ya computer, internet, mobile phones, TV/Flat screen TVs na mengineyo mengi, yeye bado tu ni rais? Jamani hata akili yake imechoka na kama ni ufalme basi ni bora angesema na kama wazimbabwe wanakubali hakuna ambaye angemsumbua.
Lakini kama ni demokrasia basi yeye hayuko kabisa katika eneo hilo. Mugabe atalaumu nchi za magharibi na itaonekana sahihi na baadhi lakini hata yeye amekaa vibaya na kujisahau ambako kumepelekea watu wa Zimbabwe wawe katika hali mbaya mno.
Aondoke. Zimbabwe sio mali binafsi. Any Zimbabwean can make a good president kama ana uchungu na nchi yake. Of course sikubaliani na Tsivangarai anavyopelekesha mambo yake, lakini hao sio watu pekee waipendao na wenye uchungu na nchi yao.