Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

Western Propaganda Turns Mugabe into a Tyrant

watu Wenye Mtazamo Wa Wazungu Wanamuona Morgan Mshindi......!
Wenye Mtazamo Wa Kiafrika tunamuona mugabe Mshindi........!
mugabe Fight For Your Land....! Dont Let Vibaraka Wachukue Ardhi Huku Wewe Ukiangalia.....!
anachofanya Mugabe Sasa Ndicho Ilichofanya Tanzania Miaka Ya Nyuma.....! mugabe Uzi Huo Huo, Mpaka Kieleweke......!
Niliwaambia Hawakusikia!
Afrika Is For Afrika!
 
Hao wazungu tutawatumia kama fig leaf mpaka lini? Hili suala la Zimbabwe wametuachia sisi tulimalize tunavyojua lakini bado hatuwaachi. Hizo sanctions mnazozingumzia ni zipi? Kumkataza Mugabe na maswahiba wake kutembelea kwao ndiko kumesababisha njaa Zimbabwe? Zimbabwe si ya kwanza kuminywa na IMF. Wao wana vigezo vyao ambavyo kama nchi haitimizi wanajitoa. Sasa mlitegemea waendelee kutupa pesa kwenye shimo lisilo na mwisho? Tunawalaumu kwa kutoingilia Darfur. Sisi kama waafrika tumefanya nini. Somalia kuna waka moto na mpaka leo nani ameenda kumpiga taf methiopia? Badala yake tumeenda kuwashikisha adabu watu wa Anjuan! Huko DRC, tulijifanya (nchi za kiafrika) kusaidia kumbe tulienda kukwapua! Watu zaidi ya milioni tano wamekufa wakati waganda, wanyarwanda naam na wazimbabwe walienda kuchota almasi na mali nyingine. Huko Sierra Leone na Ivory Coast bila ya hao wazungu watu wangekuwa wanaendelea kutoana utumbo. Waafrika tulishindwa kufanya kitu. Kwa nini tunang'ang'ania u'victim' hata pale ambapo wenyewe tuna'missmanage'?

Huyu Mugabe tumemlea wenyewe tukidai ati tuna njia zetu wenyewe za kiafrika. Leo watu wake wanachomwa moto Afrika ya Kusini. Huko kwake kungekuwa peponi, wanafanya nini Msumbji, Botswana, Afrika Kusini na kwengineko? Kukua ni kukubali pale unapokosea. Solidarity yetu iwe wa wananchi wa Zimbabwe na sio huyo despot.
 
Hivi Kamuzu Banda si alikuwa baba wa Taifa la Malawi? Obote naye si alikuwa baba wa Taifa la Malawi? Leo hii Mandela ameamua kumtolea uvivu Mugabe.
 
Mkuu Kichuguu....

Ardhi siyo jambo la kupuuzia katika nchi iliyo huru.Wewe fikiria leo hii ungekuwa Tanzania halafu ardhi yote yenye rutuba iko kwa wahindi na wazungu wachache na wanaendelea kukuambia kuwa watu weusi hawawezi kumiliki ardhi kwa kuwa hawawezi kuzalisha wewe ndugu yangu ungelielewaje hilo???? na mbaya zaidi mkijadili suala hilo kwa kuwa linahusu wazungu wachache then UK na Marekani inaweka vikwazo vya kiuchumi na kukataa kulipa fidia kama mlivyokubaliana utalielewa hilo???..
Afadhali kama Zimbabwe ingekuwa ni nchi ya viwanda tungesema basi hawa ndugu zetu weusi wataenda viwandani lakini Zimbabwe ardhi ndiyo viwanda,ndiyo maisha,ndiyo utu sasa utafanyaje??? Hata Tsvangirai mwenyewe anaelewa kuwa akiigusa issue ya ardhi itakuwa ndiyo mwisho wa urafiki wake na UK na Marekani....upoo hapo mkuu

-Wembe.
Lakini sasa si Mugabe amechukua ardhi, mbona basi hali inazidi kuwa mbaya? Halafu hiyo ardhi iliyochukuliwa aligawiwa nani kama si wale wanaomzunguka Mugabe? Hapana, Mugabe ni dikteta tu. Kwa vitendo anavyowafanyia wananchi wake mwenyewe sasa hivi tunanvua ushujaa tuliompa wakati wa mapambano dhili ya ukoloni na mara baada ya uhuru wa Zimbabwe. Sasa hivi Mugabe si shujaa. Kinachoshangaza zaidi, kwa nini hataki kuachia madaraka kwa watu wengine ndani ya chama chake? Siamini kuwa Mugabe peke yake ndiye bora kuliko wanachama wengine wa chama chake. Kama asingekuwa ni dikteta, na kama angekuwa na busara, angelikuwa tayari ku-step down na awaachie wanachama wake wengine wagombee uongozi badala yake. Kulaumu wapinzani, UK, US ni visingizio tu. Kiongozi muungwana hawezi kusema kuwa hataachia madaraka hata kama atashindwa uchaguzi. Kama Mugabe hataki kuondoka madarakani ni kwa nini alikubali uchaguzi ufanyike, any way? Sina jina lingine la kumwita Mugabe isipokuwa la DIKTETA.
 
Tuwaachie Watu Wa Huko Kusini!
Hivi Hamuelewi Kikwete Hawezi Tena Kusema Kitu?
Rudini Bungeni Nyie!
Tupeni Taarifa Za Mafisadi Nyie Vijakazi Wa Mafisadi!
Wazalendo Taim Ni Sasa!
Zimbabwe Is Over!
Rudini Bungeni!
Tunataka Kumsikia Slaa!
 
Unajua Wadanganyika mnacheklesha sana...
Nyerere alipokuwa akitumia siasa za UJAMAA alitupeleka karibu kuwa taifa lisilojiweza kiuchumi..kwani sisi hatukua na hiyo ardhi! Hapo ni sisi tuliyefunga milango yetu kiuchumi kwa nchi za kibepari tena bila kushikwa mkono na tulifikia mahala karibu tuanze kula nyama za watu....Leo Mugabe kafungiwa yeye milango yua kiuchumi mnafikiri ataweza kufanya nini kama sisi ndani ya Ujamaa tulishindwa!..

Nitarudia kusema hivi hakuna kitu kinachoweza kuota Zimbabwe bila mbegu ya mzungu...ardhi imekwisha haribika kwa hizo mbegu za maabala..mbolea na vitu vingine vyote muhimu kwa kilimo siku hizi vinaagizwa toka nje.. maswala ya organic seeds Zimbabwe yalikwisha longtime..
Kisha ebu jaribuni kufikiria kitu kimoja, leo hii Tanzania tufungiwe kila kitu kutoka nje... nambie huko madukani kutakuwa na nini... Hata unga wa ngano tunaagiza, mchele,...chukueni muda mcchache sana kufkiria hali hii ya Tanzania bila mali kutoka nje kisha mrudi ktk swala la Zimbabwe.. Jamani siku hizi ktk kila chakula chetu kuna kitu kinatoka Ulaya hata mkate utahitaji amira kama huna mkate hauwezi kupikika..
Nitarudia kusema kwamba binafsi namlaani Mugabe kwa vitendo vyake lakini siwezi kusukumwa na mzungu kwa vigezo vyake!..
Swala la Zimbabwe ni kubwa kuliko Mugabe peke yake ingawa ni bora sana akitoweka lakini haiwezi kurudisha amani nchi hiyo hadi haki na ardhi ya mzungu imepatikana.

nachowaomba mnambie ni ushauri wenu kwa jinsi mnavyoiona Zimbabwe ya kesho... mathaln akitoka Mugabe mtazamo wenu ni nani atawale?...hapo nawaomba mzingatie tu ya kwamba Mugabe akiondolewa kwa mabavu, basi mjue Zimbabwe ni Somalia nyingine ambayo kwa miaka 17 haina serikali. Wamekwisha kufa watu zaidi la laki 5 toka Siad barre aondolewe kwa msukumo wa nchi za magharibi ambazo leo wamewaacha wananchi wa Somalia ktk mataa. Was Siad barre that bad? sijui lakini hali ya leo sSomalia siwezi kuiombea nchi yoyote ile itokee na hasa Zimbabwe.. Huu ndio mtazamo wangu.
Je, hii ndio Zimbabwe mnayoiombea?..Kama sio basi nambieni kile mnachokiona nyie na mimi sikioni..
Interest za mzungu zinajulikana, tuwaache nje tuzungumze sisi kama waafrika! nipeni solution ambayo hata Membe anaweza kuipendekeza kwa Mugabe na serikali yake..
Nachosema mimi suluhu ya swala la Zimbabwe ni kumwomba Mugabe akae pembeni tu na mtu mwingine ndani ya ZANU PF ashike madaraka hali wakijua kabisa kuwa vikwazo havitaondoka..nje ya hapo mauaji yataendelea na pengine kuhatarisha zaidi usalama wa nchi zote kusini mwa jangwa!
 
Unajua Wadanganyika mnacheklesha sana...
Nyerere alipokuwa akitumia siasa za UJAMAA alitupeleka karibu kuwa taifa lisilojiweza kiuchumi.. Hapo ni sisi tuliyefunga milango ya kiuchumi kwa nchi nyingine na tulifikia mahala tuanze kula nyama za watu....
Leo Mugabe kafungiwa yeye milango yua kiuchumi mnafikiri ataweza kufanya nini kama sisi ndani ya Ujamaa tulishindwa!..Nitarudia kusema hivi kila kitu kinachoweza kuota Zimbabwe bila mbegu ya mzungu...ardhi imekwisha haribika kwa hizo mbegu za maabala..
Kisha ebu jaribuni kufikiria kitu kimoja, leo hii Tanzania tufungiwe kila kitu kutoka nje... nambie huko madukani kutakuwa na nini... Hata unga wa ngano tunaagiza, mchele,... jamani siku hizi ktk kila chakula chetu kuna kitu kinatoka Ulaya hata mkate utahitaji amira kama huna mkate hauwezi kupikika..
Nitarudia kusema kwamba binafsi namlaani Mugabe kwa vitendo vyake lakini siwezi kusukumwa na mzungu kwa vigezo vyake!..
Swala la Zimbabwe ni kubwa kuliko Mugabe peke yake ingawa ni bora sana akitoweka lakini haiwezi kurudisha amani nchi hiyo hadi haki na ardhi ya mzungu imepatikana.

nachowaomba mnambie ni ushauri wenu kwa jinsi mnavyoiona Zimbabwe ya kesho... mathaln akitoka Mugabe mtazamo wenu ni nani atawale?...hapo nawaomba mzingatie tu ya kwamba Mugabe akiondolewa kwa mabavu, basi mjue Zimbabwe ni Somalia nyingine ambayo kwa miaka 17 haina serikali. Wamekwisha kufa watu zaidi la laki 5..
Je, hii ndio Zimbabwe mnayoiombea?..Kama sio basi nambieni kile mnachokiona nyie na mimi sikioni..
Interest za mzungu zinajulikana, tuwaache nje tuzungumze sisi kama waafrika! nipeni solution ambayo hata Membe anaweza kuipendekeza kwa Mugabe na serikali yake..
Nachosema mimi suluhu ya swala la Zimbabwe ni kumwomba Mugabe akae pembeni tu na mtu mwingine ndani ya ZANU PF ashike madaraka hali wakijua kabisa kuwa vikwazo havitaondoka..nje ya hapo mauaji yataendelea na pengine kuhatarisha zaidi usalama wa nchi zote kusini mwa jangwa!

Kafungiwa na nani? Hivyo vikwazo ni vipi mnavyovizungumzia? Mbona leo Anglo American inataka kufungua machimbo ya platinum Zimbabwe? Na hawa makao yao makuu yako uingereza?

Mteja mkuu wa Mugabe si Afrika Kusini? Mugabe ameifilisi nchi, hapo hakuna shaka.

Atakayemfuata Mugabe wanajua waZimbabwe wenyewe. Sisi hatuwezi kuwapangia kama vile tusivyoweza kuwaondolea Mugabe. Wala sidhani kama kuna nchi yenye nia hio. Sisi ni kuwapa moral support kwa kuonyesha kuwa kilio chao ni chetu. Kwa kuonyesha kuwa damu ya mwafrika inathaminiwa na atakayeimwagwa hataonewa aibu hata akiwa mwafrika mwenzetu!
 
Fundi Mchundo,
Mkuu tatizo lako huelewi siasa za nchi za magharibi.. hao Anglo American wapo South Africa siku nyinghi sana wakichimba Platinum na hawawezi kusimama kujipanua unless wakatazwe na serikali ya UK...Hata Cuba zipo kapuni za Kiamerika ambazo zinaendesha shughuli zake kwa kupitia Brazil...Hata Iran si imewekewa vikwazo unafikiri ni mashirika ya wapi wanayochim,ba mafuta huko? Hizi ni siasa za uchumi siku hizi mkuu.. Muhimu sana kueplewa mapana ya biashara..
Nitarudia kuuliza wewe unataka Zimbabwe iwe kama Somalia?... kumbuka tu kwamba Somalia ni nchi pekee duniani yenye wakimbizi wengi nje kuliko population ya nchi hiyo.. Nipe solution kisha tutaongea... Kuhusu vikwazo unaweza ku google ukapata kuelewa zaidi.
 
Mkuu Kichuguu....

Ardhi siyo jambo la kupuuzia katika nchi iliyo huru.Wewe fikiria leo hii ungekuwa Tanzania halafu ardhi yote yenye rutuba iko kwa wahindi na wazungu wachache na wanaendelea kukuambia kuwa watu weusi hawawezi kumiliki ardhi kwa kuwa hawawezi kuzalisha wewe ndugu yangu ungelielewaje hilo???? na mbaya zaidi mkijadili suala hilo kwa kuwa linahusu wazungu wachache then UK na Marekani inaweka vikwazo vya kiuchumi na kukataa kulipa fidia kama mlivyokubaliana utalielewa hilo???..
Afadhali kama Zimbabwe ingekuwa ni nchi ya viwanda tungesema basi hawa ndugu zetu weusi wataenda viwandani lakini Zimbabwe ardhi ndiyo viwanda,ndiyo maisha,ndiyo utu sasa utafanyaje??? Hata Tsvangirai mwenyewe anaelewa kuwa akiigusa issue ya ardhi itakuwa ndiyo mwisho wa urafiki wake na UK na Marekani....upoo hapo mkuu

-Wembe.

Mimi namsagia mzee Mugabe kwa sababu kadhaa:

  1. Niliwahi kuishi Zimbabwe mwaka 1989 na 1990, tulikuwa tukibadilisha dola moja ya Kimarekani kwa Zim$ 2 na in fact wazimbo walikuwa hawataki fedha za nje. Leo hii ukienda na US$1 inabidi uwe na toroli kwa vile utakuwa milionea mara moja. Hedbu angalia huyu kijana ombaomba alivyosheheneza manoti.

    1.jpg
  2. Mugabe huyu aliwagawanya Wazimbabwe kwa msingi wa ukabila kati ya Washona na Wandebele kwa kuwauwa Wandebele wengi sana katika operesheni aliyoiita Gukurahundi. Mauaji wa wandebele yalikuwa na nia ya kumnyamazisha hayati Dr. Joshua Nkomo ambaye pamoja na kuwa waliongoza mapambao pamoja, alikuwa anamwogopa kwa vile jamaa yule alikuwa na akili zaidi yake. Mugabe mwenyewe aliingia madarakani kwa kutumia trufu ya ukabila baada ya akina Abel Muzorewa na Ndabaningi Sithole kuboronga. Mugabe alifanya njama za kumwua Josiah Tongogara ambaye pamoja na kuwa mshona, alikuwa anasimama kuhakikisha kuwa Nkomo na wandebele wa ZAPU wana sauti kubwa kwenye serikali mpya baada ukombozi, jambo ambalo Mugabe aliliona kuwa ni tishio sana kwa usalama wake kisiasa.
  3. Kulikuwa na njia nyingi za kugawanya ardhi kwa usawa mara tu baada ya uhuru. Mugabe huyu alikuwa anakula nchi tu bila kushughulikia swala la ardhi hadi pale alipoona kuwa uchaguzi wa 2000 unamkaba koo ndipo akakurupuka na kete ya ardhi. Hiyo ilikuwa ni miaka 20 tangu wapate uhuru. Amekurupuka na kunyanganya ardhi bila mpangilio wala plani ya kutumia ardhi hiyo, ndiyo maana akakaribisha njaa nchini mwake. Huyu mzee mpumbavu sana kwa vile anaendelea kung'ang'ania madaraka pamoja na kuona kwa ameharibu maisha ya raia wake; hakujifunza kwa Nyerere wetu ambaye alipoona kuwa ameboa aliamua kuachia ngazi kwa amani.
  4. Huko USA ni watu wachache sana wanaomiliki ardhi ya kilimo; sidhani kama wanafikia hata asilimia 20. Lakini, je mbona USA ni taifa kubwa duniani hapa? Je Mugabe alidhani kuwa kunyanganya ardhi bila plani ndiko kutafanaya Zimbabwe iwe taifa kubwa? In fact Zimbabwe lilikuwa taifa kubwa kabla ya mwaka 1995, ni Mugabe yeye mwenyewe aliyeliharibu. Miaka ya themanini, sisi Tanzania tuliwahi kuletewa mahindi ya chakula kutoka Zimbabawe wakati tuna njaa. Leo hii wao wenyewe hawana hata punje moja ya kula: wanaombaomba tu.
 
Kichuguuu,
Mkuu nitasema moja tu rudia kusoma vizuri historia ya habari ulizoandika... utakuta mengi uliyosema umeyapamba kama wazungu wanvyofanya tofauti na msukumo halisi wa yale yalioajiri.. siwezi kurudia kila neno uloandika isipokuwa rudia kusoma vizuri kila ulichoandika.. yapo marekebisho mengi sana..as a fact karibu kila ibara yako ina makosa..
 
Fundi Mchundo,
Mkuu tatizo lako huelewi siasa za nchi za magharibi.. hao Anglo American wapo South Africa siku nyinghi sana wakichimba Platinum na hawawezi kusimama kujipanua unless wakatazwe na serikali ya UK...Hata Cuba zipo kapuni za Kiamerika ambazo zinaendesha shughuli zake kwa kupitia Brazil...Hata Iran si imewekewa vikwazo unafikiri ni mashirika ya wapi wanayochim,ba mafuta huko? Hizi ni siasa za uchumi siku hizi mkuu.. Muhimu sana kueplewa mapana ya biashara..
Nitarudia kuuliza wewe unataka Zimbabwe iwe kama Somalia?... kumbuka tu kwamba Somalia ni nchi pekee duniani yenye wakimbizi wengi nje kuliko population ya nchi hiyo.. Nipe solution kisha tutaongea... Kuhusu vikwazo unaweza ku google ukapata kuelewa zaidi.

Anglo American waliishahamisha makao yao makuu kutoka Afrika Kusini kitambo. Sasa kama hizo sanctions zipo, kampuni kubwa kama hii ingewezaje kutangaza hadharani kuwa ina mpango wa kuwekeza? Sanctions zilizopo zinahusu ununuzi wa silaha na kusafiri kwa hao wakubwa. Economic sanctions zinazungumziwa lakini hazijatekelezwa kwa kuogopa kuwa zitawaumiza wanachi wa kawaida zaidi.

Haya wewe unayewajua wazungu. Nitajie hayo makampuni ya kimarekani yanayofanya biashara Cuba? Au wamarekani hauwaelewi? Usizungumzie hivyo vi mom and pop businesses.

Somalia iliingia kwenye anarchy baada ya Siad Barre kukimbizwa na kutokea power vacuum. Kwa kumchelea Mugabe na kumruhusu achezee demokrasi with impunity ndiko kutatufikisha huko. Hii itatokana na mpuuzi mmoja katika hao cronies wake kuacha uzalendo na kumfanya waliyomfanya baba yake Kabila! Au a bunch of rogues watokee kama walivyotokea Haiti na kumfukuza. Tunachoombea wengine ni kuwa aondoke wakati bado kuna viable institutions na watu wanaoweza kum'replace' (io lazima awe Morgan). Ila kuondoka aondoke!
 
Watanzania wajue hili...Nilisha mshahuri kikwete amkubali OBAMA!
AMEKATAA!

Nilipojaribu kumuonyesha umuhimu wa OBAMA KUWA RAIS WA MAREKANI!NAFASI AMBAYO NI KAMA RAIS WA DUNIA!
AKAAMUA KUMKUMBATIA YOUNG ALIYEMTUKANA OBAMA PAMOJA NA BUSH ANAYEMSAPOTI SINCLAIR NA PIA CHUKI YA YOUNG AMBAYE ALIKUWA KARIBU SANA AMA MSAIDIZI MKUU WA MLK!

HUYU YOUNG NI KAMA MKAPA....!KAJIFANYA MFUWASI WA MLK KUMBE KIBARAKA!

KAMA MKAPA ALIVYOJIFANYA MFUASI WA NYERERE...KUMBE MTANDAO!

TUKISEMA MTANDAO WALIMWUA NYERERE NANI ATABISHA?

WABISHE BAADA YA UCHUNGUZI...BAADA YA WAZALENDO KUCHUKUA NCHI!

GOD WILLING...

FISADI LENYE KUJIDAI LINAPENDA WAAFRIKA KUMBE SIO!

FISADI KAMA CONDOLEEZA RICE AMBAYE ALIWEKWA MAKUSUDI NA BUSH KWANI MALENGO NI AFRIKA!

THANKS GOD FOR OBAMA!

ITS A DEFING MOMENT!
MUNGU ANAIPENDA AFRIKA!

HATA YESU MWENYEWE INASEMEKANA ALIKUWA MWEUSI!
PROPAGANDA SI NZURI!

Lakini...THIS IS GOD'S TIME...AND YES!
KIKWETE WAS GOD'S PLANS!
 
Mugabe is just another dictator,he must be defeated...why defend this stupid ambaye ameleta disaster kwenye nchi yake,28 yrs in power? what is he looking for kwani hakuna wengine,no excuse and he should go...i'll be more than happy to see this guy in the Hague akinyea debe for the rest of his life,sijui mnalitetea la nini wakati half of his countrymen end up refugees kutokana na policy zake mbovu.
 
sanctions Za Marekani Zinapatikana Hapa.[media]http://www.treas.gov/offices/enforcement/ofac/programs/zimbabwe/zimb.pdf[/media]

Please Note Kwamba Zinazungumzia Sanction Target Na Kuna List Ya Kuwa Hawa Ni Wakina Nani!

Mandela Anatosha!
Mugabe Atamsikiliza Kama Bush Asipoingilia!
Bush Na Blair Wanavuruga Jitihada Za Wazalendo Kwani Hawataki Tuwe Huru!
Just Like Vile Hawataki Kutangaza Mandela Ni Huru Licha Ya Kwamba Ameshaachiwa Kutoka Jela Baada Ya 27 Years In Prison...And still alive!

Ni martin Luther king wetu....cinco demayo wetu Indira gandhi wetu, kwame nkrumah wetu, lumumba wetu...Mwalimu wetu kabla ya ccm mtandao ya kina RA!

Shujaa Wa Afrika Ni Mandela Na Si Zitto Na Kikwete!
Ni Watu Waliomsikiliza Obasanjo Kama Mengi,slaa,sita ,Mwakembye,mwakasege,FMES Nk!
 
The United States is tightening financial sanctions against the government of Zimbabwe. President George W. Bush issued an executive order that will increase the number of individuals under sanctions, make it easier to target companies connected to government leaders; and give U.S. authorities the power to impose sanctions on the spouses and children of top Zimbabwean officials.

The sanctions are in response to clear signs that the government of President Robert Mugabe is not serious about restoring democratic freedoms. The blatant rigging of the March parliamentary elections showed that the government has contempt for democracy. The destruction of tens of thousands of low-income homes – the so-called Operation Murambatsvina showed that the government has contempt for Zimbabwe’s people.

U.S. sanctions are not aimed at the general economy and do not impose an economic “blockade” on Zimbabwe. Zimbabwean firms not connected to government leaders are free to do business with American firms; Americans firms are free to invest in and trade with Zimbabwe, so long as they avoid business deals with top officials. Moreover, the United States will still provide humanitarian aid and help Zimbabwe confront the HIV/AIDS pandemic. Since 2002, the U.S. has provided more than three-hundred-million dollars of food assistance to Zimbabwe. Zimbabweans should not suffer because of the crimes of their leadership.

Haya, Mandara! Ni sanctions zipi ambazo ziko targeted kwa wananchi wa Zimbabwe?
 
Fundi mchundo,
Issue hapa ni Zimbabwe usitake kudai kila nachosema na kuanzisha mada nyingine!..
Mkuu nimekwambia hizi ni siasa za kiuchumi lakini unaweza kuona mwenyewe ktk site hii kisha nipatie jibu wewe unavyofikiria hivi vitu vinapitia wapi..
http://www.msnbc.msn.com/id/18664571/
 
Fundi mchundo,
Issue hapa ni Zimbabwe usitake kudai kila nachosema na kuanzisha mada nyingine!..
Mkuu nimekwambia hizi ni siasa za kiuchumi lakini unaweza kuona mwenyewe ktk site hii kisha nipatie jibu wewe unavyofikiria hivi vitu vinapitia wapi..
http://www.msnbc.msn.com/id/18664571/

Mada gani nyingine niliyoianzisha? Si nyinyi ndio mnaodai sanctions ndizo zilizosababisha matatizo Zimbabwe.

Hivi kwa vile mimi ni Fundi unadhani kiingereza kigumu kinanishinda? Hiyo article yako inazungumzia bidhaa kama Nike n.k kuweko madukani lakini si kuwa makampuni yanafanya biashara na Cuba. Hakunakitu kinachomzuia mfanyabiashara wa Cuba au China kwenda dukani Brazil na kujinunulia idadi anayotaka ya viatu vya Nike. Sisi wakati tumefunga mpaka na Kenya, bidhaa zao kibao zilikuwa bado zinaingia. Sasa kama wangesema Nike wana kiwanda chao Brazil kinacho export Cuba hapo ningekuelewa. Lakini kwa hili? Bado.
 
Kama marekani wana nia nzuri!

Basi wamuondoe MANDELA KWENYE LISTI YA UGAIDI!

MANDELA AMBAYE HAWAKUTAKA AACHIWE HURU!

WAMUONDOE HUKO NA ANC KABLA HATUJAAMUA KUWA NI KWELI WANA NIA NZURI NA AFRIKA!

KIKWETE NA ZITTO MPIGIENI MANDELA SIMU NA AKIKUBALI VITA NA MIMI NITAWASAPOTI KWANI YEYE NDIYE SHUJAA ALIYEBAKI!

NDIYE KIONGOZI WA AFRIKA...SI BUSH,SI KIKWETE,SI SINCLAIR,SI ADREW YOUNG,SI DICK CHENNEY,SI TSIVANGARAI!

AFRIKA NEEDS TO BE FREE!

AFRIKA IS THE RICHEST CONTINENT IN THE WORLD!

AFRICA SHOULD LEAD THE WORLD!

AFRIKA SHOULD NEVER STARVE...SHOULD NEVER DIE WITH PREVENTED DISEASES!

LETS GET TOGETHER AND CHANGE THE WORLD!
 
mkandara & JMush hivi mnamtetea huyo jamaa(Stupid Mugabe) kwa lipi jema kwa wananchi wake ambao zaidi ya nusu wamegeuka kuwa wakimbizi kutokana na utawala wake,excuse excuse everyday ndio tabia za waafrica wengi hata kama wao ndio wakosaji...the good news his end is near na atakuwa na bahati sana asipoishia jela!
 
Back
Top Bottom